Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,446
- 7,817
Salum Nkonja maarufu Emmanuel Nkonja, mkazi wa Maswa mkoani Simiyu, amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mkoani Dar es Salaam kujibu mashtaka 11 ikiwa ni pamoja na kukutwa na chuchu za binadamu, sehemu za siri tano za wanawake na mafuvu mawili ya kichwa cha binadamu.
Nkonja amefikishwa mahakamani hapo na kusomewa kesi ya uhujumu uchumi na wakili wa Serikali, Caroline Materu, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Ramadhani Rugemalira.
Mshtakiwa anadaiwa kutenda makosa hayo kati ya Oktoba 30 mwaka 2017 na Novemba 30 mwaka 2017 katika eneo la Ubungo.
CHANZO: TBC
Nkonja amefikishwa mahakamani hapo na kusomewa kesi ya uhujumu uchumi na wakili wa Serikali, Caroline Materu, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Ramadhani Rugemalira.
Mshtakiwa anadaiwa kutenda makosa hayo kati ya Oktoba 30 mwaka 2017 na Novemba 30 mwaka 2017 katika eneo la Ubungo.
CHANZO: TBC