Mkataba wa DP World unaweza kutufikisha kusikotakiwa

Daisam

JF-Expert Member
May 23, 2016
2,626
3,141
Hatuwezi kwenda Makanisani au Misikitini kupambana na shetani asiyeonekana badala ya kupambana na shetani anayeonekana kwanza(DP World)

Nitoe wito kwa wanaohusika na mkataba huu wa DP World kwamba wanatakiwa kujibu hoja za msingi kutoka kwa Watanzania na siyo tu kujificha kwenye udini, ujinsi na Uzanzibar. Hoja hizo ni kama vile:-

1. Kama mkataba huu una nia njema, kwa nini haujahusisha Bandari za Zanzibar?

2. Kwa nini mkataba huu unavunja Katiba yetu ya Nchi?

3. Kwa nini mkataba huu unavunja hata sheria za kimataifa?

4. Je, ni kweli kwamba Watanzania tumeshindwa kabisa kuendesha Bandari zetu?

Nawasilisha.
 
Mwenyezi MUNGU sikiliza kilio cha Watanganyika na utende miujiza katikati yetu.
 
  • Thanks
Reactions: YSK
Hatuwezi kwenda Makanisani au Misikitini kupambana na shetani asiyeonekana badala ya kupambana na shetani anayeonekana kwanza(DP World)

Nitoe wito kwa wanaohusika na mkataba huu wa DP World kwamba wanatakiwa kujibu hoja za msingi kutoka kwa Watanzania na siyo tu kujificha kwenye udini, ujinsi na Uzanzibar. Hoja hizo ni kama vile:-

1. Kama mkataba huu una nia njema, kwa nini haujahusisha Bandari za Zanzibar?

2. Kwa nini mkataba huu unavunja Katiba yetu ya Nchi?

3. Kwa nini mkataba huu unavunja hata sheria za kimataifa?

4. Je, ni kweli kwamba Watanzania tumeshindwa kabisa kuendesha Bandari zetu?

Nawasilisha.
Nchi ngapi zinaitegemea bandari ya Zanzibar ?
Yaani umlete DPW aje aendeshe bandari inayoingiza meli 3 kwa mwaka ? Huko sindio kujitukana ?
Unaujua msemo wa "Jino moja mswaki wa nini" maanake ?
 
Tumeshindwa kuendesha bandari yetu ndiyo , tunachojua Ni kuiibia serikali tu.
 
Nchi ngapi zinaitegemea bandari ya Zanzibar ?
Yaani umlete DPW aje aendeshe bandari inayoingiza meli 3 kwa mwaka ? Huko sindio kujitukana ?
Unaujua msemo wa "Jino moja mswaki wa nini" maanake ?
Unataka kusema hizo bandari za kwenye maziwa, ambazo zimeingizwa kwenye mkataba, zina meli nyingi kuliko bandari ya Zanzibar?
 
Influencers wapo bize kupiga pesa!
Screenshot_20230623-130707.png
 
Back
Top Bottom