#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

Duh! Weye mchawi nini Mkuu? nilikuwa kwenye uzi huu huu sekunde chache zilizopita mara napata notification yako. Nishazuka Mkuu.
Siku hizi hauko active sana. Mada zako nzito nilizisoma nikiwa sina akili sana, ulinishawishi kujiunga JF.
 
Nafurahi kusikia hivyo Mkuu kwamba mada zangu zilikuwa kichocheo cha wewe kujiunga hapa. Ahsante sana 🙏🏽

Zamani kulikuwa na uhuru mkubwa sana hapa wa FREEDOM OF EXPRESSION hata nukta au coma ilikuwa haibadilishwi. Siku hizi ukiandika wanaweza kubadili ulichoandika hata kupoteza ujumbe uliyoukusudia au hata kufuta kabisa ulichoandika.

Hali hii imesababisha hata mchecheto wa kuingia humu niliokuwa nao miaka ya nyuma kupungua sana.

Siku hizi hauko active sana. Mada zako nzito nilizisoma nikiwa sina akili sana, ulinishawishi kujiunga JF.
 
UPDATE NO 2: THURSDAY 14/05/2020

Kikao cha dharura cha wanaume kilichofanyika hivi karibuni kinaonekana kugongana sawia kabisa na mambo mawili makubwa

  • Kilifanyika J2 iliyofuatia ile ya mgogoro wa Sanitizer
  • Klilifanyika katika wiki ambayo J3 ya wiki hiyo, mhusika wa taarifa hizi aliamua kuanza kutoa rasmi taarifa za matendo anayofanyiwa yasiyomridhisha na mengine pia yanayoendelea Kanisani hapo, kupitia mtandao huu
Kwa hiyo ukizingatia mambo hayo mawili hapo juu, ukiunganisha na mood aliyokuwa nayo mwenyekiti wakati anafungua kikao, inaonyesha KAMA:

  • Mwenyekiti aliamua kutumia lugha ya ukali na kufoka sehemu ambayo haistahili, yaani kanisani, na kwa sababu ambazo hazikuwa za msingi, akiwa na lengo la kutafuta targets ambao alijua huwa hawawezi kuvumilia kusikiliza ujinga, mhusika wa taarifa hizi akiwa mmoja wao
  • kwa vile mhusika wa taarifa hizi alikuwa tayari ameshaazisha kitu ndani ya wiki hiyo, inaonyesha pia KAMA mojawapo ya potential targets zilizokuwa zimekusudiwa alikuwa ni yeye
Na kama ni kweli kwamba yeye alikuwa ni potential target:

  • haina shaka kuwa kulikuwa na kitu kikubwa kilikuwa kimeandaliwa kwa ajili yake nyuma ya pazia, ambacho yeye alikuwa hakijui, na ndiyo maana hata viongozi karibia wote walikuwepo, akiwemo kiongozi mkuu mwenyewe.
  • Kuna kitu kikubwa kilkuwa kimendaliwa nyuma ya pazia, yawezekana hata fujo ambazo zingelazimu hata vyombo vya dola kuwasili mahali pale kwa ajili ya kuja kuituliza ghasia
Kwa hiyo iwapo kungeweza kutokea fujo mahli pale, uwezekano mkubwa ni kwamba fujo hiyo ilikuwa imepangwa, na possibly kuna watu ambao tayari walikuwa wameandaliwa kwa ajili ya kuianzisha

Mhusika anadai kuwa hawa viongozi ni wa hatari mno na huko nyuma wameshawahi kupanga matukio mengi tu ya hatari kwake ambayo baadhi atayaleta kwenu kadri habari hizi zitakavyokuwa zinawajia. Karibia mara zote wamekuwa katika mipango yao, wakishirikiana na staff mate wake ambaye naye huwa anaabudu mahali pale. Huyu mtu siku hiyo ghafla alionekana amekaa pembeni ya mhusika ila wakati wa Ibada hakuwa amemuona. Mhusika anadai ataleta angalau tukio moja kuthibitisha hatari iliyoko mahali pale

Hata hivyo, mhusika siku hiyo aliamua kuondoka kikaoni hapo baada ya kuona kinaelekea kule ambako yeye hakuwa ametarajia, akarudi nyumbani



MWANDISHI WENU ATARUDI TENA
Endelea mkuu..
 
Nitarudi kusoma vizuri naona kuna jambo hapa.

Asante mleta mada

Sent using Jamii Forums mobile app
UPDATE 18/05/2020



MATUKIO YASIYOKUWA YA KAWAIDA AMBAYO MHUSIKA AMEKUMBANA NAYO KUTOKEA KANISANI NA AMBAYO YANAONEKANA KAMA YANA UHUSIANO NA STAFF MATE/ OFFICE MATE WAKE, (TUMWITE MR. X ) AMBAYE WANAABUDU WOTE KANISANI HAPO


  • Staff mate huyu (Mr. X) ni mtu ambaye wanafanya naye kazi idara moja, jengo moja ila ofisi tofauti, kwa takriban miaka 20 sasa
  • Pia wanaabudu wote kwenye nyumba moja ya Ibada tangu mwaka 2011. Ni kwamba mhusika wa taarifa hizi alimkuta mwenzake akiwa tayari aliashaanza kuabdudu kwenye nyumba hiyo ya Ibada tangu mwaka huo, ila hakuwa amekaribishwa na Mr. X, wala mhusika hakuwahi awali kujua kuwa Mr. X alikuwa anaabudu kwenye nyumba hiyo ya Ibada
  • Mhusika anapenda kuwaletea matukio ambayo anayaona KAMA huyu mwenzake alihusika, na ambayo kwake yeye anayaona kuwa si ya kawaida na baadhi yake yanaweza kuwa / yaliikuwa ya hatari kwa usalama wake
  • Mhusika anapenda kuwaletea matukio haya (ni baadhi yake tu na machache sana, na si yote) kuanzia na la hivi karibuni kabisa na kurudi nyuma


1: MASHAMBULIO MATANO YA KIAFYA

A: SHAMBULIO LA KWANZA

  • Mhusika alipata kwa mara nyingine tena, shambulio la koo siku ya kikao cha dharura cha wanaume Kanisani, kilichoitishwa J2 ya tarehe 26/04/2020
  • Shambulio hilo liliendelea hadi wiki iliyofuata, akatumia tiba stahiki na hatimaye kupona
  • Haikuwa mara yake ya kwanza kupata shambulio la aina hiyo (kutokea Kanisani), ni mara nyingi tu amekuwa akipata shambulio la aina hii
  • Kawaida huwa linaanza J2 akiwa Kanisani au baada ya kuwa ametoka kanisani J2 husika, na huendelea mpaka pale tiba stahiki inapokuwa imefanya kazi yake
  • Hata hivyo, mengi kati ya matukio ya shambulio hili, inaonyesha KAMA: matano (5) kati yake yanamhusisha moja kwa moja Mr. X, na kama siyo basi tunaweza kusema kuwa ni hali ambayo ni “just a rare coincidence”
  • Siku ya tukio, mhusika anadai kuwa alikuja akastukia ghafla Mr. X amekaa jirani naye kwenye kiti kilichokuwa kulia kwa mhusika
  • Anadai kuwa alimuona ghafla kwa sababu hakuwa amemuona Kanisani siku hiyo, kabla ya hapo. HILI SASA TULIITE SHAMBULIO LA KWANZA kufuatana na mlolongo uliopo kwenye maelezo haya
Kwa hiyo kwenye matukio yote matano ya sahambulio la aina hii na ambayo yanaonekana KAMA kumhusisha Mr. X pekee, mhusika anadai kuwa MARA ZOTE huwa yanatokea pale tu Mr X anapotokea kuwa / kukaa karibu na mhusika kwenye Ibada Kanisani

B: SHAMBULIO LA PILI

  • Kwa kuanzia; kawaida Mr X huwa hana kawaida ya kuhudhuria kipindi cha Morning Glory kanisani, (ambacho sasa hivi kimesitishwa sababu ya ugonjwa wa Corona), na safari ya mwisho ambayo mhusika walikuwa wote kwenye kipindi hicho na kukaribiana karibu kabisa na Mr X, (Mr X alikuwa akimfuata fuata mhusika kila alikokuwa akielekea, na hatimaye walisalimiana kwa kushikana mikono) ilikuwa ni kwenye kipindi cha Morning Glory, zaidi ya mwaka mmoja au miwili iliyopita.
  • Siku hiyo nayo pia mhusika alipata shambulio la koo (halikuwa s la kwanza) , sawa na hili alilopata mwezi jana. HILI TULIITE SHAMBULIO LA PILI, kufuatana na mlolongo uliopo kwenye maelezo haya
Tangu pale mhusika hakuwahi tena kumuona Mr X kwenye kipindi cha morning glory, na kama aliwahi kuhudhuria tena kwenye Ibada ya aina hiyo, basi itakuwa ni katika siku ambazo mhusika naye hakuwa amehudhuria na hivyo wawili hawa watakuwa walipishana

C: SHAMBULIO LA TATU

  • Vilevile mwaka jana mwezi May siku ya sikukuu ya wanaume, mhusika alipata tena shambulio la koo isipokuwa hakumbuki vizuri kama walikaa karibu na Mr X, au pengine labda walikaribiana na kusalimiana kwa kushikana mikono tu
  • Anachokumbuka siku hiyo ni kwamba alibahatika kuwa karibu na watoto wadogo wawili ambao ni rafiki zake, baada ya kuwa amepishana nao kwa wiki kadhaa bila kuonana nao Kanisani hapo
  • Marafiki hawa wa mhusika pia ni watoto wake na Mr. X
  • Aliwaona baada ya kipindi cha Morning Glory Kanisani hapo wakiwa wawili wamekaa peke yao, akawafuata na kuwachukua na kwenda kukaa nao pale alipokuwa amekaa yeye
  • Namna alivyoachana nao marafiki hawa ndiyo kitendo ambacho hana kumbukumbu nacho vizuri, ila anadhani KAMA hatimaye Mr X alikuja kuwachukua, na possibly wali-shake hands wakati wa tukio hilo
  • Na kama Mr X hakuja kuwachukua bali mtu mwingine, au pengine waliondoka wao wenyewe, chances ni kwamba kuna namna ambayo mhusika na Mr. X walibahatika kuwa karibu siku ya J2 hiyo
  • Kwa hiyo siku hiyo nayo pia mhusika alipata shambulio la koo. HILI TULIITE SHAMBULIO LA TATU, kufuatana na mlolongo uliopo kwenye maelezo haya
D: SHAMBULIO LA NNE

Tukio la nne lilitokea J2 moja ambayo mhusika alibahatika tena kukaa karibu na Mr. X

  • Wawili hawa walikaa karibu kwenye kipindi cha somo la uanafunzi na maandiko, mara baada ya Ibada ya kwanza kuisha
  • Kama ilivyo kawaida, Kiongozi Mkuu alianza kwa kuwapanga waumini, namna walivyotakiwa kukaa kwenye Ibada hiyo, na baada ya kuhakikisha kuwa wamekaa katika mfumo aliouhitaji, aliondoka kwenda kunywa chai
  • Wakati huo huo mhusika alifanikiwa kukaa kwenye kiti kilichokuwa pembezoni mwa korido ya katikati ya Kanisa
  • Mhusika akiwa amekaa (safu ya nyuma), hatimaye Mr. X naye alikuja na kukaa kwenye safu ya viti vilivyokuwa mbele ya safu ya mhusika, ila kwenye mstari uleule ambao mhusika alikuwa amekaa
  • Kwa ufafanuzi mwingine ni kwamba hawa watu walikaa jirani kwenye safu mbili tofauti za viti na zilizokuwa jirani, ila kwenye viti ambavyo vilikuwa kwenye mstari mmoja kwenye safu hizo, assuming mtu anatembea kutoka safu moja moja kwenda nyingine
  • siku hiyo nayo pia mhusika alipata tena shambulio la koo. HILI TULIITE SHAMBULIO LA NNE, kufuatana na mlolongo uliopo kwenye maelezo haya
E: SHAMBULIO LA TANO

Tukio la TANO na la mwisho (katika yale tu yanayoonekana kuhusiana na Mr. X), lilitokea siku ya uchaguzi wa viongozi Kanisani, wanaoitwa mashemasi, takribani mwaka mmoja uliopita.

Siku hiyo nayo pia Mr. X na mhusika walikaa karibu na kwa pamoja kwenye kundi dogo maalumu la waumini waliokuwa wamejitenga kwa ajili ya shughuli hiyo ya uchaguzi. Kwa hiyo siku hiyo nayo pia mhusika alipata shambulio la koo. HILI SASA TULIITE SHAMBULIO LA TANO NA LA MWISHO, kufuatana na mlolongo uliopo kwenye maelezo haya

Hata hivyo, matukio haya yamekuwa yakitokea katika nyakati ambazo zina umbali mrefu kiasi (miezi kadhaa) kutoka tukio moja hadi jingine.

Nia kubwa hasa ya mhusika kuleta kwenu matukio haya ni ili yaweze kupata public opinions na watu waweze kuona kama pengine yanaangukia kwenye “rare coincidence” cases ama la

Baada ya shambulio la hivi karibuni lililotokea mwezi uliopota, J3 iliyofuata mhusika alihudhuria kwenye Kituo cha Afya kwenda kumuona Daktari kwa ajili ya matibabu. Baada ya kueleza tatizo lake, Daktari alimuuliza mhusika kama aidha yeye ni mhubiri au ni mwimbaji kanisani, kitu ambacho alikanusha. Kwa hiyo inaonyesha KAMA ingetokea kwa bahati nzuri akapata nafasi ya kuongea kwenye kikao cha wanaume (kama asingeamua kuondoka) kuna uwezekano sauti yake ingesikika mara ya mwisho siku hiyo, isingesikika tena baada ya pale, koo lingekwama



F: KUHUSIANA NA SHAMBULIIO LA HIVI KARIBUNI LA J2 YA TAREHE 26/04/2020: MHUSIKA ANACHODHANI KUWA NI ADDITIONAL MOTIVE BEHIND MR X’,s ACTION, ASSUMING NI KWELI ALIHUSIKA KWENYE SHAMBULIO HILO

  • Nia ya mhusika hapa ni kutaka kuonyesha uhusiano uliopo baina ya kitendo cha anayeweza kuwa ni mshambuliaji wake kwa tukio tajwa hapo juu, yaani Mr. X, na namna kinavyoweza kuwa kinahusiana na matendo ya hivi karibuni ya Mr. X ambayo amekuwa akiyafanya kwa mhusika
  • Yaani kitendo cha Mr. X cha J2 hiyo, kinavyoweza kuwa kinahusiana na matendo yake ya kabla, na ambayo ni ya hivi karibuni
  • Matukio mengine manne aliyoyayaelezea hapo juu. nayo pia yalikuwa na motives zake na anazijua, lakini si nia ya mhusika kuziongelea motives hizo
  • Kwa hiyo anataka kuongelea motive ya shambulio hili la hivi karibuni, na kwa kuanzia mbali kidogo


MHUSIKA ABAHATIKA KUWEPO KWENYE VIKAO VIWILI VILIVYOFANYIKA KWA NYAKATI TOFAUTI, VILIVYOMHAKIKISHIA KUWA MASLAHI YAKE AMBAYO HAJALIPWA NA ANAYODAI TANGIA JUNE 2014, YATALIPWA

Awali ya yote kabla hajaenda kwenye details za vikao, mhusika angependa kuweka wazi mambo kadhaa yafuatayo

  • Ni kwamba mhusika ana madai halali ofisini ambayo hayajaweza kulipwa mpaka leo
  • Si nia ya mhusika kuleta jukwaani humu swala la maslahi yake ya ofisini isipokuwa analazimika kutoa taarifa hizi kwa sababu matukio ambayo inabidi ayaelezzee, yanalazimisha agusie swala la maslahi hayo; vinginevyo haiwezekani namna ambavyo anaweza akatoa ufafanuzi na mtu yeyote aliye na akili timamu akapata kuelewa
  • Kwa hiyo kwa takribani miaka mitano iliyopita, mhusika amekuwa akifuatilia ili alipwe maslahi hayo lakini haikuwezekana, na zaidi akaendelea kuona kuwa kulikuwa na mitego mingi tu iliyokuwa inawekwa katika jitihada zake hizo, ambayo ni ya hatari kwake, kwa hiyo kufikia MWAKA JANA MWANZONI aliamua kusitisha kwanza ufuatiliaji wa maslahi hayo.
  • Kwa taarifa fupi tu ni kwamba mara ya mwisho alipanda daraja mwaka 2012, na kufikia June 2014, mshahara wake ulikatwa T. Shs 700,000/= , makato yasiyostahili na pasipo ridhaa yake
  • Pia tangu mwaka 2011/2012 anakatwa 25,000/=kila mwezi kwa ajili ya maji, nayo pasipo idhini yake wala pasipo kuwa na official notification juu ya makato hayo. Hata hivyo maji hayo kwa sasa yalishakatwa na huwa anachota maji kupandisha ghorofa ya kwanza. Yalikatwa tangu mwezi Novemba 2018, ila makato ya 25,000/= yenyewe bado yapo yanaendelea kila mwezi
  • Desemba 2014 alianza tena kukatwa asilimia 3% (na zinaendelea kukatwa hadi leo) kwa ajili ya uanachama wa mfuko ambao si mwanachama wake hadi leo nazo pia pasipo ridhaa yake;
  • Asilimia nyingine 7% ilianza kukatwa tena tangu Februari 2018 hadi leo, nayo pia ikiwa ni makato ambayo hastahili kukatwa na pasipo ridhaa yake
Yeye anaona kuwa makato haya mapya yaliyoanza Februari 2018, ni kama yalianzishwa kwa makusudi ya kumfanya aongeze zaidi jitihada zaidi za kufuatilia maslahi yake kwenye ofisi husika

  • Kwa ujumla, mpaka muda huu, mshahara wa mhusika unakatwa kiasi KISICHOPUNGUA T. Shs 1,100,000/= na kwa makato ambayo si halali, ilhali mshahara huo uliongezeka kwa mara ya mwisho Julai 2012
Kwa hiyo kabla ya vikao atakavyovielezea maudhui yake hapa chini, taarifa za awali zilizokuwepo ni kwamba mhusika alikuwa ameamua kuuacha kwanza mchakato wa kudai maslahi hayo kwa sababu ulionekana kuwa unakuwa ni wa hatari kwa usalama wake. Zaidi ni kuwa amekuwa akidai maslahi hayo kwa mfululizo kwa kipindi kisichopungua miaka minne lakini, pasipo mafanikio yoyote



KIKAO CHA KWANZA

  • Hiki hakikuwa kikao rasmi, na wala hakuwa amekaribishwa isipokuwa alikifumania tu kwa bahati nzuri na yeye akawa amejiunga katika maongezi yake, kwa kusikiliza zaidi kuliko kuongea
  • Yalikuwa ni maongezi ya kawaida tu ambayo watu wawili au watatu huwa wanafanya wakiwa ofisini, na ambayo hayakuwa na hadhi ya kuitwa kikao
  • Ilikuwa ni MWANZONI MWA MWAKA HUU, yaani JANUARI 2020
  • Maongezi yalikuwa ni ya watu wawili (mmoja tumwite Mr.T ,wakati yule wa pili alikuwa ni Mkuu wa Idara ambaye mhusika wa tukio hili, yuko chini ya mkuu huyo)
  • Mr.T alikuwa anasifu utendaji wa Serikali ya Awamu ya tano, kwa utendaji wake mzuri wa kazi kiasi kwamba imefanikiwa kulipa malimbikizo ya wafanyakazi kwa kuwaingizia fedha nyingi kwa mkupuo kwenye akaunti zao Benki
  • Mr.T alidai kuwa amekuta malimbikizo ya zaidi ya T.Shs million 50 zikiwa zimeingizwa kwenye account yake Benki
Hata hivyo, mhusika wa taarifa hizi alitilia shaka kidogo maongezi hayo, japo hakusema lolote juu ya malipo hayo kwa sababu Mr. T:



  • Alishastaafu miaka kadhaa nyuma (zaidi ya miaka miwili iliyopita)
  • Alishalipwa maslahi yake yote na kwa wakati huu anafanya kazi kwa mkataba, kitendo ambacho kinamfanya asiwe na madai ya malimbikizo yoyote yenye uwingi huo wa fedha
  • Alikuwa anaongea mbele ya Mkuu wa Idara, ambaye naye alionyesjha dalili za wazi kabisa kuwa taarifa hizo anazijua na ni sahihi


Tukirudi nyuma kidogo KWA UFUPI SANA, juu ya mahusiano yaliyopo kati ya Mr. T na mhusika wa taarifa hizi;

  • Ni kwamba mwaka 2008 (August/ Septemba), mhusika alikuwa anaishi peke yake kwenye nyumba ambayo ni ghororfa, na kuna wakazi wengine pia aliokuwa anaishi nao mahali pale, ila yeye nyumbani kwake alikuwa anaishi peke yake
  • Miezi hiyo ya August/ Septemba mhusika aliamua kuchukua likizo na wakati huo wageni wawili ndugu zake wa karibu, walimtembelea kutoka kijijini kwao, japo mmoja alikuwa pia na mahitaji ya tiba
  • Zaidi ni kuwa Mr. T na mhusika wanayo mahusaiano ya karibu tangu kipindi kirefu nyuma, kiasi kwamba Mr. T alikuwa na taarifa zote kwamba mhusika yuko likizo
  • Na katika kujaribu kusaidiana, Mr. T aliamua kumsaidia mhusika kwa kumtafutia kazi ya kuingiza kipato cha ziada wakati huo akiwa yuko likizo, bila mhusika kujua
  • Baada ya kazi hiyo kuwa imepatikana, Mr. T alimuita ofisini mhusika na kumwambia kuwa kuna kazi ya kufanya kama anaweza basi aende akaifanye, na mhusika alikubali
  • Baada ya mhusika kukubaliana na ofa hiyo nzuri, Mr. T. alimuunganisha na mhusika wa kazi hiyo, na baada ya mawasiliano kati yao, walikubaliana kukutana ofisini kwa mwenye kazi, ofisi zilizokuwa pale Namanga karibu na Ubalozi wa Marekani
  • Baada ya mhusika kukutana na mwenye kazi, waliongea na wakaachana kwa makubaliano kuwa watawasiliana tena ndani ya siku chache sana, kwa sababu siku ya kuondoka kuelekea kazini ilikuwa ndani ya wiki hiyo
  • Safari kuelekea kazini ilikuwa ni kwa usafriri wa ndege, na kazi ilikuwa ifanyike mkoani nje ya Dare s Salaam
  • Baada ya maongezo kuisha, wakati mhusika anatoka ofisini hapo, na akiwa pia ametambulishwa kwa baadhi ya watu kwenye timu atakayokwenda nayo, baadhi ya watu wa timu hiyo walianza kusisitiza kuwa afanye hima kwa sababu hata ticket yake ya ndege walikuwa tayari wameshabook
  • Mhusika alipotoka ofisi hiyo alirudi moja kwa moja ofisini na kuonana na Mr. T, akampa feedback za kule alikoenda na zaidi akamsisitiza Mr. T kuwa ajaribu kumkumbusha mwenye kazi atume haraka barua ya mkataba wa kazi, ili mhusika aitumie kuomba ruhusa kazini na waweze kuondoka kuelekea kazini kwa sababu ofisi husika kwa ajili ya kazi hiyo ilikuwa inaonyesha kuwa iko kwenye rush hour
Baada ya hapo, kukawa kimya kila mahali, wenye kazi wakawa kimya, vilevile Mr. T. Kwa hiyo mhusika hakufanikiwa kwenda kufanya kazi hiyo, mchakato wake ukawa umeishia hapo

Hat hivyo, baada ya miaka kdhaa kupita (nadhani ilikuwa mwaka 2014) tangu ofa hiyo ya kazi kutolewa, na matukio mengine kadhaa kuwa yamejitokeza, hatimaye mhusika alikuja kubaini mtego katika mpango mzima wa kazi hiyo ambayo ililetwa kwake na Mr. T.

Mhusika aligudua mambo kadhaa, baadhi yake ikiwa ni:

  • Wote Mr. T pamoja na mwenye kazi, walitarajia kuwa mhusika angeenda kufanya kazi hiyo pasipo kuomba ruhusa kazini kwake, kwa sababu alikuwa yuko likizo
  • Mhusika angeondoka kwenda kufanya kazi hiyo bila kuomba ruhusa kwa mwajiri wake, pamoja na kwamba alikuwa likizo, just in case of anything unexpected, mwajiri wake angemchukulia kuwa alikuwa ni mtoro kazini kwa sababu kisheria alitakiwa aombe ruhusa ya kwenda kufanya kazi hiyo, na mkataba wake auweke wazi kwa mwajiri wake. Zaidi ni kuwa alikuwa likizo lakini akiwa bado anaishi kwenye mazingira ya mwajiri wake, na kwenye nyumba ya Serikali
  • Na kwa sababu nyumbani alikuwa anaishi pake yake, mahali alipokuwa anaishi watu walikuwa na mazoea ya kujua kuwa yupo nyumbani kwa kuangalia gari lake kama lipo kwenye parking; kama ni mchana, na kwa kuangalia taa za nyumbani kwake kama zinawaka, ikiwa ni usiku
  • Na kwa sababu katika kipindi chicho alicholetewa kazi hiyo, kuna wageni walikuwa wameshakuja nyumbani kwake, utaratibu huu wa watu kujua kuwa yupo kwa kuangalia gari au taa za nyumbani kwake usiku, usingeweza kufanya kazi tena kwa sababu kama angeondoka, alikua haondoki na gari lake
  • Kwa hiyo watu wangeendelea kuona gari lipo kwenye parking, na wale walioozoea kuona taa za nyumbani zinawaka usiku, wangeendelea kuziona zinawaka, lakini yeye wakati huo angekuwa hayupo, ameenda kufanya kazi mbali
Kwa hiyo by 2014, mhusika alikuja kubaini kuwa aliachwa asiende kufanya kazi hiyo kwa sababu alitaka kuiweka kiofisi zaidi, kitu ambacho kilikuwa hakiatkiwi Kilichokuwa kinatakiwa ni kwamba alitakiwa asafiri, pasipo watu kujua kuwa amesafiri



MWANDISHI WENU ATARUDI
 
UPDATE 19 MAY 2020

Mwendelezo kuhusiana na kazi ambayo mhusika aliletewa na Mr. T


Zaidi ni kuwa safari hiyo ilikuwa na ughafla wa aina fulani uliokuwa unaashiria KAMA mhusika alitakiwa aondoke pasipo watu wengi kujua. Akakumbuka pia mwaka 1999 aliwahi kukumbana na hali ya namna hiyo wakati akiwa anasaka ajira ya kudumu.

Kumbuka kuwa maelezo haya ameyaleta kwa ajili ya kugusia kidogo tu uhusiano uliopo mpaka sasa, kati yake na Mr. T, ambaye alimthibitisha kuwa tayari yeye ameshapokea malipo zaidi ya million 50 kama malimbikizo.

Msomaji inabidi akumbuke pia kuwa hapa mhusika yeye alikuwa tayari ameshasimama kudai maslahi yake miezi kadhaa nyuma, baada ya kuona kuwa mchakato huo unakuwa wa hatari kwake.

Hata hivyo, pamoja na taarifa hizi za Mr. T, mhusika:

  • Yeye bado hajalipwa malimbikizo hayo mpaka leo
  • Kwa hiyo inaonyesha KAMA wote Mr T pamoja na Mkuu wa Idara walikuwa na nia ya kum-trigger aanze tena kufuatilia maslahi hayo, na ndiyo maana hajaweza kulipwa mpaka leo
  • Na kama ni kweli kwamba walikuwa na nia ya kumuanzisha ili aanzishe tena mchakato wa kudai masslahi hayo, basi obviously kulikuwa na set-up ya mitego mingine mipya kwenye mchakato wa kudai maslahi hayo
Hata hivyo, mhusika pamoja na kupata taarifa hizo nzuri kutoka kwa Mr T, bado hakuweza kuwa tempted kubadilisha msimamo wake, aliendelea na msimamo wa kuendelea kuusitisha kwa muda mchakato huo



KIKAO (CHA PILI) CHA DHARURA NA AMBACHO KILICHOITISHWA NA MR X

  • Tofauti na kile cha mwanzo ambacho kilimhusisha Mr T, hiki cha pili kilikuwa ni rasmi
  • Kilikuwa ni cha dharura, na kilifanyika mwezi wa pili mwishoni au wa tatau mwanzoni
  • MR X alimfuata mhusika ofisini kwake na kumkaribisha mhusika kwenye kikao hicho kikiwa na agenda ya moja tu ya kumthibitishia kuwa atarekebishiwa maslahi na mshahara wake March 2020 na hatimaye malimbikizo ya mshahara huo mwezi unaofuata; maslahi ambayo amekuwa akiyadai kwa takribani miaka mitano (5) sasa
  • Kikao hicho kilihudhuriwa na watu takribani 6 wenyeji pale ofisini, na mtu mwingine mmoja mgeni kutoka nje ya ofisi, na ambaye ni mstaafu wa pale, ila alikuwa akifanyia idara nyingine
  • Kwa hiyo, Mr X alimfuata mhusika ofisini kwake siku hiyo na kumuomba ahudhurie kikao hicho cha dharura akimweleza kuwa yeye ndiye alikuwa ni mdau mkubwa wa kikao hicho
  • Mhusika alikubali na alihudhuria kikao hicho na ambacho kiliweka wazi kuwa mwezi huo huo, ambao ulikuwa ni March 2020, angelipwa mshahara uliorekebishwa na kwamba malimbikizo ya mshahara huo uliorekebishwa, yangefuata mwezi unaofuata, yaani baada ya ule wa malipo ya mshahara mpya
  • Mkuu wa Idara hakuwepo kwenye mkutano huo ila ilionyesha wazi kabisa kuwa waliokuwa waki-coordinate mkutano huo walikuwa na mandate yake, yaani alikuwa amewa-authorise kuendesha kikao hicho
  • Hata hivyo hadi leo, hali haijatokea sawasawa na minutes za kikao hicho
Pamoja na kwamba hali haijatokea hivyo mpaka leo (May 2020) kwa maana kuwa hakuna malipo yoyote ambayo yameshafanywa kwa mhusika kulingana na minutes za kikao hicho, bado mhusika hana sababu yoyote ya kutilia shaka kilichojadiliwa kwenye kikao hicho

HATA HIVYO: Mhusika anaona KAMA Mr X alimpeleka mhusika kwenye kikao ambacho pengine

  • HAKIKUWA SHAHIHI na wala taarifa zake hazikuwa sahihi, nia ikiwa ni kum-trigger mhusika aanze kupita pita tena kwenye ofisi ambazo huko mwanzo alikuwa ameamua kuacha kupitapita kwa sababu alikuwa tayari ameshaona hatari katika mchakato huo
  • KILIKUWA SAHIHI isipokuwa taarifa zake kwamba malipo yake yangeweza kufanyika mwezi huo hazikuwa sahihi, nia yake ikiwa ni ile ile ya kum-trigger mhusika aanze kupita pita tena kwenye ofisi ambazo huko mwanzo alikuwa ameamua kuacha kwa sababu alikuwa tayari ameshaona kuna hatari katika pita pita hizo
  • Alifanya hivyo baada ya trigger ya Mr. T (aliyedai kulipwa zaidi ya million 50) kuwa imeshindwa kufanya kazi
Hii inatkna na ukweli kwamba vikao vyote viwili vinaonekana kuwa na taarifa ambazo haziko sahihi sana, na hivyo kumfanya mhusika kuwa na notion kwamba wote Mr X na Mr T walikuwa na nia ya kum-trigger ili aanze tena kupita pita kwenye maofisi ya watu ambao tayari ameshayaogopa.

Zaidi ni kuwa mahusiano yaliyopo kati ya mhusika na watoa taarifa hizi njema, na kama alivyoyaainisha kwa kifupi sana hapo juu, hayako sawia sana kiasi cha kumfanya mhusika asiwe katika hali ya kiwango ambacho angeweza kuendelea kuwaamini tena, kama ambavyo anaweza kuwaamini binadamu wengine wa kawaida. Ni kwa sababu muda wote wako tricky na kwa ndani siyo watu ambao anaweza akasema kuwa ni marafiki kwake

Kwa hali hiyo basi, assuming sasa mhusika angepata shauku ya kutaka kujua ni nini kinaendelea kuhusiana na maslahi yake, halafu akaamua kuyafuatilia kwenye ofisi husika, na kwa bahati mbaya katika kupita pita kwenye maofisi ya watu, kukatokea chochote kile ambacho ni cha madhara kwake, picha ya haraka haraka ambayo ingejitokeza ni kuwa mhusika angekuwa responsible kwa madhara yale ambayo yangempata, kwa sababu lazima watu wangehoji, kama huyu mtu alikuwa ameamua kusitissha mchakato wa kufuatilia maslahi hayo, na akatangaza hivyo hadharani , je kilichomfanya auanzishe tena ni nini? Wengine wangeweza hata kufikia conclusion kuwa kwa vile alikuwa anadai maslahi, possibly ameshafrustrate na hivyo alikuwa katika mchakato wa kuwadhuru wengine, isipokuwa kwa bahati mbaya madhara yakamrudia yeye mwenyewe



MWANDISHI WENU ATARUDI KWA MATUKIO ZAIDI YASIYO YA KAWAIDA, YANAYOMHUSISHA MR X NA WASHIRIKA WAKE
 
Big earthquakes might make sea level rise worse. Here's how.

The Samoan islands are sinking faster than expected due to warming alone, and a pair of huge quakes is likely to blame.











Source: Big earthquakes might make sea level rise worse. Here's how.

Big earthquakes might make sea level rise worse. Here's how.

The Samoan islands are sinking faster than expected due to warming alone, and a pair of huge quakes is likely to blame.


PUBLISHED June 17, 2019

A geologic one-two punch rocked the South Pacific in September 2009, as a magnitude 8.1 earthquake struck off the coast of the island nation of Samoa, followed mere moments later by a similarly intense temblor. A towering tsunami soon crashed onto the shores of islands nearby, leaving more than 180 dead and communities in ruins in Samoa, the neighboring U.S. territory of American Samoa, and surrounding islands.

But a new study, published in the Journal of Geophysical Research: Solid Earth, reveals that the quakes also sparked a slow-burning danger for the more than 55,000 residents of American Samoa: sea level rise that is five times as fast as the global average.
Earthquakes 101 Earthquakes can leave behind incredible devastation, while also creating some of the planet's most magnificent formations.


Like other island and coastal regions around the world, Samoa and American Samoa are facing encroaching waters as our warming world sends sea levels soaring at accelerating rates. In the wake of the mega-quakes, though, the researchers discovered that these Pacific islands are also sinking. The situation is particularly concerning for American Samoa, where the team estimates that, over the next 50 to a hundred years, local sea levels could rise by roughly a foot in addition to the anticipated effects of climate change.

While the contributions of big earthquakes won’t be the same everywhere, the discovery emphasizes the sometimes overlooked effects that geology can have on the increasing number of people around the world who call coastlines home. (Also find out how powerful quakes are priming the region around Mount Everest for a huge disaster.)

“Everybody is talking about climate change issues ... but they overlooked the impact of the earthquake and associated land subsidence,” says study leader Shin-Chan Han of the University of Newcastle, Australia, referring to documents from regional governments on sea level rise.

“This is a really important thing to point out,” says geophysicist Laura Wallace of the geoscience consultancy firm GNS Science, Te Pū Ao, in New Zealand, who was not involved in the study. “It obviously has a big impact on the relative sea level changes people are going to see in places like [the Samoan islands].”



Plate tectonics is constantly reshaping the surface of our planet—a role particularly evident during an earthquake. Generally speaking, these events occur where tectonic plates are colliding or sliding against each other, building up geologic stress. When that pent-up energy is released suddenly, it can send blocks of the planet’s crust careening out of place. (Find out how smaller “hidden” earthquakes are affecting California.)

But not all the change from a big earthquake is immediate. Unlike the rigid crust, the rocks of the mantle below flow like cold molasses and gradually adjust to the sudden surface jolt, Wallace says. This can cause either sinking or uplift of the land that can continue for decades after a temblor strikes.

This prolonged landscape deformation is what intrigues Han. For years, he’s scoured data from the Gravity Recovery and Climate Experiment, or GRACE, satellites to hunt for the rise and fall of land after a quake. This satellite duo orbited Earth in a line from 2002 to 2017 and precisely tracked the gap between the spacecraft. As they passed over zones with slightly more mass, and thus stronger gravity, the leading craft would feel the tug just before the trailing one. This tweaked the space in between and registered as a wobble in the planet’s gravitational field that can reveal changes in the landmass below.

In the case of the 2009 earthquake, such changes were minute on a day-to-day basis. But eventually, the effects were large enough that Han saw something strange happening in the Samoan islands while poring over the GRACE data.
A rare coincidence

The 2009 event was a particularly unusual earthquake that initially baffled scientists, since the pair of powerful temblors ripped through the Earth nearly at the same time. One broke along a so-called normal fault, created due to the flex of the oceanic crust as it plunges under another tectonic plate in what’s known as a subduction zone. Another quake broke within the subduction zone due to the compressive forces of the colliding plates.

The researchers investigated the lingering impacts of these quakes using a combination of GRACE data and local GPS and tide gauge records. They then built a computer model to tease apart the complex interplay between the temblors and what is happening at the surface.

This data showed slow sinking of the landscape, driven primarily by the normal-fault quake. This particular earthquake causes one side of the landscape to fall in relation to the other, which sent the nearby islands sinking downward.

The team found that nearly a decade after the event, the island of Samoa has sunk by roughly 0.4 inches a year. The situation is particularly acute for American Samoa, which has seen more than 0.6 inches of subsidence each year, and it doesn’t look like it’s stopping anytime soon.

The pace outstrips the estimated rate of global sea level rise, which is creeping upward at some 0.13 inches a year. Flooding and seawater intrusion in freshwater aquifers are already grave concerns for residents of American Samoa, Han says, and the latest find only adds to the worry.
Bathtub oceans

It’s possible similar effects could happen on other islands near where plates collide, but a lot of factors influence what ensues post-quake. The overall importance of the new work is highlighting that the causes of sea level change in any given locale are a lot more complicated than melting ice and warming seas.

“People think of global mean sea level rise as the bathtub just filling and emptying,” says University of South Florida’s Don Chambers, who is an expert in the use of satellite gravity data to study sea level. But a host of other factors perturb our vast oceanic tubs. Some of these are human caused, like groundwater extraction or sediments being compacted by expanding cities, which makes the land sink. This effect is a culprit along the Louisiana coast, where waters are rising by an inch every two years in some sections.

Tectonic mischief, like that seen in the Samoan islands, is also a common factor, but the effects depend on the geometry of the faults, says Jeffrey Freymueller, a geophysicist at Michigan State University who was not involved in the new work. In many places, tectonic jostling causes uplift rather than subsidence. For example, Han has tracked post-earthquake changes in Japan and New Zealand, both of which have instead been moving upward for years.

But around Samoa and elsewhere, subsidence due to earthquakes is a real worry for sea level rise. Freymueller points to a recent study in Marine Geology that documented considerable sea level rise for Thailand’s Phuket Island following the magnitude 9.2 Sumatra-Andaman earthquake in 2004. Local waters have risen nearly five inches as of 2019—a combined effect of climate change and post-earthquake sinking.

This latest study emphasizes the need for greater awareness and continued monitoring to mitigate the potential effects of mega-quakes, Wallace says. However, predicting such sea level effects before an earthquake strikes is not feasible, since earthquake prediction itself remains elusive.

“This might be a problem that suddenly causes you heartburn next week,” Freymueller says, “or it might not cause any problem for the next century
 


UPDATE 20/05/2020

TUKIO LA PILI: TUKIO LILILOPANGWA NA MR X KWA KUSHIRIKIANA NA KIONGOZI MKUU, SIKU YA (J5) IBADA YA JIONI KANISANI


MAELEZO YA UTANGULIZI KUHUSIANA NA TUKIO LENYEWE

  • Tukio hili lilipangwa na Mr X (possibly pamoja na mke wake Mr X pia) akishirikiana na Kiongozi Mkuu wa Kanisa ambalo mhusika ni muumini wa pale mpaka muda huu (tuliite Kanisa A kwa sasa)
  • Plan ilikuwa ni kwamba mhusika atengenezewe mazingira ya kum-trigger ili aweze kuomba appointment ya kuongea na Kiongozi Mkuu, ofisini kwa kiongozi huyo
  • Kama angefanya hivyo, tukio hilo la hatari lingemtokea, na ambalo lingeonyesha kuwa Kiongozi Mkuu hakuhusika nalo
  • Tukio hilo lingeonyesha pia kuwa mhusika aliomba appointment ya kuongea na kiongozi mkuu akiwa hana nia njema naye, alitaka kumdhuru ila kwa bahati nzuri likampata mhusika na kumkosa mlengwa
  • Kulingana na Saikolojia ya mhusika, yeye anadai kuwa anaona kwamba tukio hilo (lililokuwa limepangwa kwa ajili yake), lingempata katika muda ambao angeachwa peke yake kwa muda mfupi ofisini kwa kiongozi huyo, na kwa wakati ambao maongezi yangekuwa bado hayajamalizika/ yanaendelea, baada ya mwenye ofisi kuwa amepata udhuru wa kutoka kidogo nje ya ofisi hiyo
  • Mhusika anadai pia kuwa MFUMO wa tukio hilo ambalo ni aina ya shambulio la hatari sana, ulibuniwa na KIKUNDI KIDOGO cha waumini wa Kanisa B, ambako aliwahi kukimbilia kipindi fulani nyuma, akiwa anatokea Kanisa A, ambako alidumu akiwa muumi kwa takribani muda wa miaka mitatu,
  • Baada ya miaka hiyo kupita akiwa huko, mhusika alikimbia tena kutoka Kanisa B na kurudi tena Kanisa A, ambako ndiko aliko mpaka muda huu
Mhusika anadai kuwa kwa uchambuzi wake kuhusiana na makanisa haya mawili, yaani Kanisa A na Kanisa B

  • Kikundi sumbufu cha Kanisa A (mhusika aliko mpaka sasa) KINA WATU WENGI ILA WAOGA KIASI, ukilinganisha na kile cha Kanisa B; kwa maana kuwa kikundi sumbufu cha Kanisa B (alikowahi kuhamia halafu nako akakimbia tena) KINA WATU WACHACHEI ILA MAJASIRI SANA, na ndiyo maana hata kiliweza kubuni mfumo wa shambulio hilo la hatari, na ambalo mtego wake bado unaendelea kutumika hadi leo, katika mazingira yote ambayo mhusika huwa anakuwepo, KAMA VILE OFISINI.
  • Kwa kifupi sana, maelezo kuhusiana na hama hama hii yako kama ifuatavyo hapa chini:
Mhusika aliamua kuhama kutoka Kanisa A, kwenda Kanisa B, baada ya kikundi kidogo cha watu fulani kuwa kimemubugudhi kikiwa kinashirikiana na viongozi karibia wote wa Kanisa A. Wakati anakimbia kutoka A na kwenda B, wengi wa waumini aliowaacha A waliamini kuwa yeye ndiyo ana matatizo, kwa sababu haiwezekani viongozi wote washiriki kukuhamisha halafu bado uwe wewe ndiyo msafi. Alipofika Kanisa B akitokea A, alipokelewa vizuri halafu baadaye na huko nako ukaundwa mtandao uliokusudiwa kumhamisha akimbie Kanisa B, akitarajiwa safari hii kuwa angekimbilia Kanisa jingine, possibly Kanisa C. Baada ya takriban miaka mitatu hivi akiwa huko Kanisa B, akachoshwa na hila hizo pamoja na ujinga aliokuwa akiendelea kutendewa, na hivyo akaamua kurudi tena Kanisa A, tofauti kabisa na matarajio ya mtandao uliokuwa ukimbugudhi.

Alifanya hivyo ili kuthibitisha kuwa alihama wakati yeye akiwa si mwenye bugudha, bali baada ya yeye kuwa amebugudhiwa

Akiwa yuko Kanisa B (baada ya kutoka A), mambo mengi sana yalimtokea, baadhi yake yakiwa ni haya yafuatayo

  • Baada ya takribani miezi sita hivi tangu kuhama kwake, Kiongozi Mkuu wa Kanisa A, (kule alikohana) alitembelea Kanisa B (kule alikokuwa amehania) kwa ajili ya kutoa huduma Kanisani pale
  • Kabla ya Kiongozi huyu kutembelea Kanisani hili B, nyuma yake watoto wake waliwahi kufika Kanisani hapo kwa ajili ya huduma ya Ibada na hivyo kufanikiwa kuonana na mhusika, japo hakuwapa salaam kumpelekea Kiongozi huyo
  • Kwa hiyo ni wazi kabisa kuwa Kiongozi Mkuu kutoka Kanisa A, alifika Kanisa B akiwa ana taarifa kuwa mhusika alikuwa anaabudu pale
  • J2 hiyo, kabla ya muda wa huduma kuanza, mhusika alibahatika kuonana na kiongozi huyu mgeni kwa ghafla nje mlangoni; mhusika akiwa anatoka nje ya Kanisa na Kiongozi mgeni naye akiwa anajaribu kutaka kuingia ndani
  • Ilikuwa ni mpishano wa ghafla tu na hivyo walisalimiana na hawakuweza kuongea, isipokuwa Kiongozi mgeni alibahatika kupata nafasi ya kumwambia mhusika kuwa hakujua kuwa alihamia kwenye nyumba hiyo ya Ibada, kwa sababu wakati anaondoka kanisani kwake hakumuaga
  • Kiongozi huyu mgeni, alimwambia mhusika maneno hayo mbele ya Kiongozi mwingine mwenyeji wa Kanisa B, ambaye walikuwa wameambatana naye wakiwa katika harakati za kutaka kuingia ndani ya nyumba ya Ibada
  • Kabla mhusika hajajibu chochote, KWA HARAKA SANA kiongozi mwenyeji alidakia kwa kusema “AAH KUMBE HUYU MTU ALIONDOKA KANISANI KWAKO BILA HAKUAGA”?
  • Wakati huo viongozi hao tayari walikuwa wameshaanza kukanyaga ngazi za mlango tayari kwa kuingia ndani
  • Mhusika hakupata nafasi ya kujibu chochote na maongezi yao yaliishia hapo, mhusika akaelekea kule alikokuwa anaelekea, na viongozi hao nao wakaingia ndani ya nyumba ya Ibada
  • Zaidi ni kuwa, hakuna mtu mwingine yeyote Kanisani hapo J2 hiyo, aliyeshuhudia mhusika na Kiongozi mgeni wakikutana na kusalimiana, isipokuwa Kiongozi mwenyeji ambaye alikuwa ameambatana na mgeni huyo wakati wa kupishana mlangoni
Baada ya huduma ya siku hiyo kuisha na ambayo iliongozwa na Kiongozi mgeni, waumini walitawanyika na wengi wao wakiwa na matarajio ya kumuona mhusika akienda kumpa mkono wa salamu, Kiongozi mgeni kwa sababu walikuwa awanajua kuwa mhusika alifika Kanisani hapo akiwa anatokea kule anakohudumu Kiongozi huyo mgeni.

Hata hivyo walishangaa kumuona mhusika akiondoka Kanisani hapo pasipo kwenda kumpa mkono wa salamu kiongozi mgeni. Na kwa vile walikuwa wanajua kuwa kule alikotoka aliondoka katika mazingira yasiyo ya kawaida, waumini hawa wa Kanisa B wakawa na dhana kichwani kwamba mhusika amemkimbia Kiongozi wake wa kule alikotokea na hivyo ikaoenekana kuwa

  • Yeye ndiyo alikorofisha huko na kukimbia kwa sababu isingewezekana asiende kumpa mkono wa salamu Kiongozi wake wa zamani
  • Alikuwa anamkwepa Kiongozi huyu mgeni kwa sababu alijua kuwa ana hatia, akiogopa kuhojiwa maswali mbele ya Viongozi wake wapya wa Kanisa B
  • Kuanzia pale, Kiongozi mwenyeji aliyekuwa na mgeni wakati wanakutana na mhusika mlangoni , alianza sasa kutumika kama shahidi wa kuonyesha kuwa mhusika alitoroka Kanisani kwa Kiongozi mgeni, na Kiongozi mgeni alikuwa hata hajui kama alikuwa anaabudu hapo, sawasawa kabisa na maneno aliyoyatamka kiongozi mgeni akimlalamikia mhusika, walipokuwa wakipishana mlangoni J2 husika
  • Kwa hiyo tangia pale, ikajulikana kuwa mhusika ndiyo ana matatizo, alikorofisha kwa kiongozi mgeni halafu akaondoka na kukimbilia Kanisa B
Hata hivyo, mhusika baadaye alikuja kubaini kuwa huu ulikuwa ni mchoro uliokuwa umechorwa kwa ushirikiano wa Kiongozi mgeni na Kiongozi mwenyeji

  • Ni kwamba Kiongozi mwenyeji alikuwa ame-predict pattern ya movement za mhusika J2 hiyo na baada ya hapo akawa ameiwasilisha kwa Kiongozi mgeni
  • Kiongozi mgeni akiwa tayari amewasili Kanisa B, wawili hao wakaamua kukaa karibu kabisa na mlango wa kutokea nje, katika namna ambayo ilionyesha kama wanajadili kitu Fulani
  • Walikaa upande ule ambao mhusika huwa anapenda kuchoropokea akiwa anatoka nje ya Kanisa, wakiwa wame-predict kuwa lazima tu ndani ya mda Fulani mfupi, mhusika atatoka nje
  • Na kweli ilitokea hivyo, na wawili hao kwa haraka sana, wakamzonga mhusika pale mlangoni kwa maongezi mafupi na ya haraka sana ili watu wengine wasije wakaona wala kusikia
  • Viongozi hawa wawili walijua pia kuwa kama itatokea kama walivyokuwa wamepanga, baada ya Ibada kuisha, mhusika hataona tena haja ya kwenda kuongea na kiongozi ambaye tayari wameshasalimiana na ambaye anashikilia rekodi ya kumsababisha mhusika akimbie Kanisani kwake huku akiwa na kinyongo
  • Vilevile, viongozi hawa walijua pia kuwa picha itakaoyotokea kwa waumini wengine baada ya pale itaonyesha dhahiri kabisa kuwa mhusika aliogopa kukutana na Kiongozi mgeni, na hivyo kuamua kumkimbia pasipo hata kusalimiana naye na hivyo yeye ndiyo ana matatizo na si Kiongozi wake
Kwa hiyo baada ya matukio haya yote kutokea, Kiongozi mgeni baada ya kuwa ameondoka siku hiyo, akawa kuanzia pale tayari amewajenga waumini pamoja na viongozi wote wa Kanisa B kuwa mhusika aliondoka Kanisa A akiwa na hatia, na ushahidi ulionekana J2 hiyo kwamba alimkimbia Kiongozi wake wa Kanisa kule alikokuwa ametokea, mchana kweupe na waumini na viongozi wote wa kanisa B wakiwa wanashuhudia.

Zaidi ni kuwa Kiongozi huyu tayari alikuwa ameshapata refa Kanisani hapo wa kuendelea kumpigia filimbi; huyu si mwingine bali ni kiongozi mwenyeji wa kanisa hilo ambaye alikuwa ameshuhudia alicholalamikiwa mhusika na Kiongozi wake wa zamani, pindi walipokuwa wanapishana mlangoni

Hata hivyo, kila kitu hatimaye kilikuja kubadilika ghafla takribani miaka mitatu baadaye. Mhusika baada ya kuona bugudha zimezidi sana tena akiwa Kanisa B, aliamua kurudi tena Kanisa A, huku akitoa taarifa Kanisa B kuwa wakimubugudhi tena Kanisa A (ambacho ndicho wanachofanya tena sasa), atarudi tena Kanisa B, na hivyo kazi yake itakuwa ni ku-shuttle between churches A and B forever, mpaka pale bugudha zitakapokoma

Hatua hii ya kurudi Kanisa A iliwashangaza wengi kwa sababu:

  • Tayari waumini wa makanisa yote haya mawili walikuwa wamesha-stabilize kwenye ukweli kwamba mhusika ndiye alikuwa na matatizo
  • Waumini wa makanisa yote mawili walikuwa na taarifa za uhakika kuwa mhusika aliwahi kumkimbia Kiongozi wa kanisa A (ambako ndiko aliko sasa), pindi alipokuwa ametembelea Kanisa B (ambako ndiko alishahama tena, hayupo huko tena kwa sasa)
  • Wengi walitarajia kuwa mhusika atakapoamua kuhama tena kutoka Kanisa B, ataenda Kanisa jingine ambalo siyo Kanisa A (possibly ataenda Kanisa jingine C)
Baada ya haya yote kuwa yametokea na mhusika kuwa amerudi tena Kanisa A, jitihada sasa za kurekebisha uelewa wa waumini waliokuwa wameujenga mwanzo zikaanza kufanyika kwa jitihada kubwa, lengo ikiwa ni Kiongozi wa Kanisa A kujisafisha., Jitihada hizo zilihusisha mambo mengi, kubwa zaidi ikiwa ni mitego iliyokusudiwa kusababisha hatari kwa mhusika. Kwa hiyo mmojawapo ya mitego hiyo ndiyo mhusika anapenda kuuleta kwenu wasomaji. Ni mtego ambao uliundwa kwa ushirikiano wa MR X (possibly na mke wake MR X pia) na Kiongozi Mkuu wa Kanisa A.

Maelezo yake bado ni marefu kidogo na hivyo mhusika anazidi kuwaomba wasomaji waendelee kuwa wavumilivu kidogo

MWANDISHI WENU ATARUDI TENA
 

UPDATE 21/05/2020

TUKIO LA PILI: TUKIO LILILOPANGWA NA MR X KWA KUSHIRIKIANA NA KIONGOZI MKUU, SIKU YA (J5) IBADA YA JIONI KANISANI



……Inaendelea




MWANYA ULIOJITOKEZA NA KUSABABISHA MAANDALIZI YA TUKIO LENYEWE

Kabla ya kuendelea mbele mhusika anapenda kuleta kwenu kwa kifupi mlolongo wa tarehe za matukio haya muhimu:

  • Mr X alianza kuabudu kwenye nyumba ya Ibada Kanisa A mwaka 2005 na hajawahi kuhama
  • Mhusika alianza kuabudu kwenye nyumba ya Ibada Kanisa A tangu May 2011 na ameshawahi kuhama
  • Mhusika alihama kwa mara ya kwanza kutoka Kanisa A kwenda Kanisa B, tarehe 8 June 2014
  • Kiongozi mkuu kutoka Kanisa A alitembelea Kanisa B kwa ajili ya kutoa huduma kanisani hapo, J2 moja ambayo tarehe yake ilikuwa ni kati ya Septemba na Oktoba 2014
  • Mhusika alihama tena kwa mara nyingine kutoka Kanisa B (alikohamia mwanzo) na kurudi Kanisa A (alikohama mwanzo), tarehe 14 April 2017 na mpaka muda huu, bado anaabudu kwenye nyumba hiyo ya Ibada
Mhusika baada ya kuwa amerudi Kanisa A, alikuta utaratibu mpya wa kufanya usafi ambao wakati anaondoka hakuuacha. Kulikuwa na ratiba ya waumini wote kuhudhuria usafi Kanisani hapo kila wiki kwa siku za Jumamosi tu.

Hata hivyo, baada ya wiki kadhaa kupita pasipo kuwa ameweza kuhudhuria huduma hiyo, akapata wazo ambalo aliamua kumshirikisha mmojawapo wa mashemasi kanisani hapo. Wazo lenyewe ni kwamba alipendekeza kama kuna uwezekano, (kwa wale waliokuwa watoro kwenye huduma hiyo), kufidia shughuli hiyo ya usafi kwa kutoa sadaka, yaani kuwe na sadaka maalumu ya usafi kwa yule atakayejisikia kutoa kwa ridhaa yake, kama fidia ya kutoweza kufika kila Jumamosi Kanisani hapo kwa ajili ya usafi huo.

Baada ya maongezi hayo kufanyika

  • Shemasi alipokea ombi hilo na kuahidi kuwa atalifikisha kwenye ngazi husika na atarudisha majibu kwa mhusika
  • Baada ya siku kadhaa, kweli shemasi alirudisha majibu kuwa ombi la mhusika lilikubaliwa, na kwamba alitakiwa afanye kibinafsi tu kama yeye, kwa kuwa utaratibu wa kiujumla wa kufanya hivyo usingekuwepo
  • Mhusika alipokea majibu na hakuona kasoro yoyote kwenye majibu hayo.
Baada ya siku kadhaa kupita (kama wiki hivi na siku kadhaa) tokea siku mhusika apokee majibu ya ombi lake, ikatokea siku moja kwenye Ibada ya J5 jioni kwa ajli ya kujifunza maandiko matakatifu

  • Mwalimu wa somo (siku hiyo) alikuwa ni Kiongozi Mkuu
  • Akiwa anafundisha somo hilo, alifika sehemu akatoa mfano uliohusiana na kile alichokuwa anaendelea kufundisha
  • Mfano huu ulikuwa unaonya juu ya tabia ya waumini kujisikia wako juu kuliko watu wengine, na aliendelea mbele kwa kusema kuwa WAKATI MWINGINE MTU ANASHINDWA HATA KUJA KUFANYA SHUGHULI ZA USAFI WA JUMAMOSI KANISANI, KWA SABABU YEYE ANAJIONA YUKO JUU KULIKO WENGINE’
  • Kipindi somo hili linafundishwa, mhusika alikuwa hajamaliza hata nusu mwaka tangu arudi kutoka Kanisa B alikokuwa amekimbila
  • Zaidi ni kuwa alikuwa hajapata hata nafasi ya kuongea na Kiongozi Mkuu, na hakuwa na mpango wa kufanya hivyo isipokuwa tu pale ambapo pengine angeombwa na Kiongozi huyo, kufanya hivyo
  • Siku hiyo mhusika alikuwa amekaa kwenye safu ya mbele kabisa wa viti ambayo hufuatia ile ya viongozi, kiti cha kwanza jirani na korido ya katikati ya Kanisa
  • Nyuma yake mhusika (kama safu moja au mbili kutoka kwa ile ya mhusika), upande ule ule aliokuwa amekaa mhusika, walikaa Mr X na mke wake, nao kwenye viti vilivyokuwa jirani kabisa na korido hiyo ya kanisa
Labda tu kwa angalizo kidogo hapa kuhusu Mr X ni kwamba mhusika anadai kuwa muumini huyu huwa hana kawaida ya kuhudhuria Ibada za katikati ya wiki, au zile za asubuhi sana J2 (morning glory) na mara nyingi (japo si mara zote) anapokuwa ameonekana kwenye Ibada hizo, lazima awe ana jukumu maalumu kichwani kwake ambalo liko nje kabisa na mambo ya Ibada

  • Kwa hiyo, mhusika alikaa jirani sana na viti walivyokuwa wamekaa viongozi na mara baada ya Ibada kuisha, alisogea mbele kwenye safu ya viti vyao na kuanza kuwasalimia mmoja baada ya mwingine, akiwemo Kiongozi Mkuu
  • Baada ya hapo alianza kurudi akipita kwenye korido, ambapo umbali si mrefu alisimama tena kusalimiana na Mr X na mke wake
  • Kabla mhusika hajaendelea mbele, ghafla Kiongozi Mkuu naye akawa amewasili mahali pale na kupelekea mahali pale kuwepo na kundi dogo la watu wanne
  • Mhusika hakuongea tena na Kiongozi Mkuu kwa sababu walikuwa tayari wameshasalimiana, na aliondoka hapo akawaacha wenzake wakiendelea na maongezi na Kiongozi Mkuu
Muda mfupi baadaye, mhusika katika kujaribu kuchambua kilicotokea kwenye Ibada siku hiyo, akaja akakutana na mambo kadhaa ambayo hakuyaona kuwa ya kawaida sana. Mambo hayo ni kama yafuatayo

  • Huko nyuma kabla, hakuwahi hata siku moja kumuona Kiongozi Mkuu amemuongeela mtu yeyote kimafumbo fumbo akiwa amesimama mbele ya madhabahu, lakini siku hiyo alifanya hivyo.
  • Kutokana na hali hiyo, mhusika aliamua kuweka akiba rohoni KWAMBA, KAMA ITATOKEA HIVI KARIBUNI KIONGOZI HUYO AKAMUHITAJI KWA AJILI YA MAONGEZI, BASI ATAJUA KWA UHAKIKA KABISA KUWA KILA ALICHOKUWA ANAFANYA (KIONGOZI HUYO) SIKU HIYO YA IBADA, ALIKUWA AMEKIPANGA KWA MAKUSUDI NA HAKIKUTKEA KWA BAHATI MBAYA TU
Hata hivyo, kitu ambacho mhusika alikuwa ameshawahi kumuona kiongozi huyo akifanya pindi anapokuwa amekumbana na kero fulani, ni kuitisha mkutano wa dharura wa Kanisa zima na kutaja kero yake mbele ya Kanisa zima, na alishawahi kumuona akifanya hivyo kwa takribani mara mbili, kipindi kirefu nyuma kabla hajahamia kanisa B

Baada ya kuwaza na kuwazua jambo hili, mhusika pia alibaini mambo mengine kadhaa yafuatayo

  • Baada ya Ibada, Kiongozi Mkuu alipita njia ya korido la katikati ya Kanisa, njia ambayo mara zote huwa hapiti. Kawaida, awe anaingia au anatoka kwenye huduma ya Ibada, njia hiyo huwa hapiti, hadi leo
  • Kwa kuzingatia ukweli huo hapo juu, kiongozi huyu alionekana kuwa siku hiyo alipanga kupita njia hiyo
Vile vile, mafumbo ya malalamiko aliyoyatoa kiongozi huyu kuhusiana na usafi wa Jumamosi, na ambayo yalimlenga moja kwa moja mhusika: yalikusudiwa kum-dissappoint mhusika na kumfanya aone kuwa kumbe kulikuwa na unafiki ulikuwa unaendelea juu ya ombi alilopeleka kwa kiongozi huyo

Disappointment hiyo nayo ililenga tena aidha

  • Kum-prompt mhusika aondoke bila kuwasalimia viongozi waliokuwa wamekaa karibu kabisa mbele yake AU
  • Kum-prompt mhusika kwenda kusalimiana na viongozi hao na hatimaye kumuomba appointment ya maongezi Kiongoozi Mkuu, viongozi wenzake wakiwa wanashuhudia ombi lake hilo
Kwa ujumla Kiongozi huyu alikuwa anatengeneza mazingira ya kumlazimisha mhusika (pasipo yeye kujua), aombe appointment ya kuongea na kiongozi huyo na MBELE YA MASHAHIDI waliokusudiwa kuja kuwahakikishia wengine kuwa ni mhusika aliyeomba appointment kwa Kiongozi Mkuu na si kwamba Kiongozi Mkuu alimuomba mhusika wakutane na kuongea, ukizingatia pia kuwa mhusika aliondoka Kanisani hapo kwa kukimbia, na sasa amerudi tena na katika kipindi ambacho siyo kirefu, bugudha zimeanza tena. Kwa hiyo ilitarajiwa kuwa kwa namna yoyote ile yeye angekuwa wa kwanza kuanzisha mazungumzo na kuomba appointment ya kukutana na kiongozi huyo, na si Kiongozi Mkuu mwenyewe

Kinyume chake, baada ya mhusika kusalimiana na viongozi hao na akaondoka pasipo kuongea chochote, ikabidi sasa PLAN B itumike. Kiongozi Mkuu akaamua kumuwahi sasa akiwa bado anasalimiana na akina Mr X na mke wake, akitarajia kuwa pengine mhusika angeweza kupata wazo hilo la kuomba appointment, Mr X na mke wake wakiwa ni mashuhuda wa ombi lake hilo



ITAENDELEA
 
UPDATE 26/05/2020

TUKIO LA PILI: TUKIO LILILOPANGWA NA MR X KWA KUSHIRIKIANA NA KIONGOZI MKUU, SIKU YA (J5) IBADA YA JIONI KANISANI

……Inaendelea


MWANYA ULIOJITOKEZA NA KUSABABISHA MAANDALIZI YA TUKIO LENYEWE

Kwa hiyo mpaka muda huu, tunaona kuwa mwanya pekee uliojitokeza na kusababisha shambulio hili kwa mhusika ni kile kitendo cha mhusika kushauri utaratibu wa sadaka maalumu kwa wale ambao wanakuwa watoro kwenye usafi Kanisani siku ya Jumamosi asubuhi

Kumbuka maneno haya kwenye mwendelezo wa mada hii, yamendikwa mahali fulani kwenye sehemu iliyopita hapo juu

Kutokana na hali hiyo, mhusika aliamua kuweka akiba rohoni KWAMBA, KAMA ITATOKEA HIVI KARIBUNI KIONGOZI HUYO AKAMUHITAJI KWA AJILI YA MAONGEZI, BASI ATAJUA KWA UHAKIKA KABISA KUWA KILA ALICHOKUWA ANAFANYA (KIONGOZI HUYO) SIKU HIYO YA IBADA, ALIKUWA AMEKIPANGA KWA MAKUSUDI NA HAKIKUTKEA KWA BAHATI MBAYA TU

  • Mhusika aliondoka kwenye ibada hiyo ya jioni (J5), akiwaacha Mr X na mke wake pamoja na Kiongozi Mkuu, wakiendelea na maongezi
  • Mhusika pia hakudiriki kuomba appointment yoyote ya maongezi kutoka kwa kiongozi huyo
Hata hivyo, Jumapili ya wiki hiyo hiyo mara baada ya Ibada ya kwanza kuisha, Kiongozi Mkuu alimfuata mhusika na kumuomba kama ana nafasi ili waonane ofisini kwa ajili ya mongezi, na mhusika alikubali.

Baada ya Kiongozi Mkuu kuwa amefanya hivyo

  • Mhusika alihakikisha pasipo shaka kabisa kuwa kile alichokuwa ameki-predict kwenye Ibada ya J5 kilikuwa kiko sahihi
  • Siku ilipofika aliitikia wito na maongezi yakafanyika japo hayakumalizika, ilionekana kuwa kiongozi Mkuu alikuwa na appointment nyingine tena siku hiyo
  • Maongezi yalianza kwa sala, yakamalizika kwa kuachana ghafla bila sala kwa sababu kuna kiongozi mwingine alikuwa anakaa anachungulia chungulia mlangoni kuonyesha kumhitaji mwenzake aliyekuwa anafanya maongezi na mhusika
  • Wakati wa maongezi ya wawili hao, mhusika pia aliweka wazi kwa kiongozi huyo aina ya mashambulio ambayo kipindi fulani huko nyuma, yaliwahi kuelekezwa kwake kwa kutumia simu ya mkononi aina ya smartphone.
  • Wiki iliyofuata baada ya maongezi hayo, mhusika alitumiwa salio la T. Shs 1 kwenye aacount yake ya pesa za kwenye simu (siyo kwenye salio)
  • Ni akaunti ambayo mhusika alikuwa ameacha kuitumia kwa takribani zaidi ya miaka miwili, kwa sababu mara nyingi ilikuwa ainambatana na mashambulio
  • Ni akaunti ambayo wala haikuwa na salio lolote, ila ilikuwa ina-exist
  • Pesa hii ilisababisha SHAMBULIO JINGINE LA KOO, (hili sasa tuliite shambulio la sita, katika mlolongo wa mashambulio ya aina hii)
  • Ni shambulio sawa kabisa na yale matano ambayo mhusika ameshayaelezea hapo juu, na yanayomhusisha Mr. X
  • Kufikia siku ya J2 wakati anatoka kwenye Ibada, sahambulio likawa limekuwa severe, kiasi kwamba sauti yake ilikuwa karibia inakata ashindwe kabisa kuongea (Na hii ndiyo maana juzi ali-predict kuwa sahambulio la hivi karibuni lililofanyika J2 ambayo kikao cha wanaume kilifanyika, lilikuwa limeelnga kumfanya akate kauli na asiweze kuongea tena)
  • Hatimaye J2 hiyo aliamua kwenda Mlimani City na kuwaomba wahusika wafunge kabisa akaunti hiyo ya simu, kitu ambacho walifanya
  • Baada ya hapo koo lilipona, ila akaunti hiyo alishaifunga kimoja haifanyi kazi hadi leo
Kwenye shambulio hili, mhusika aliona mambo makubwa mawili ambayo mojawapo ni sahihi

Ni kwamba kuna taarifa muhimu za mashambulio alizomshirikisha Kiongozi Mkuu huyo siku hiyo ambazo yeye anadhani kuwa AIDHA:

  • Taarifa hizo baadaye zilitumika vibaya pengine baada ya Kiongozi huyo naye kuwa amezi-share na watu wengine ambao hakujua kuwa si wazuri, na ambao hatimaye waliamua ku-launch mashamabulizi kwa mhusika kwa kutumia taarifa hizo AU
  • Kiongozi Mkuu mwenyewe alihusika katika shambulizi hilo, na iwapo taarifa hizo alizishare na watu wengine, basi ilikuwa ni kwa makusudi hayo
Hii ni kutokana na uwiano au ukaribu wa muda ulijitokeza kati ya kutokea kwa sahambulio hilo na kutolewa kwa taarrifa za siri zinazohusiana na matukio ya nyuma, yaliyofanana na tukio hilo (providing confidential information to a confidant, who them turns on you by using them (such information) against you)

Kwa kifupi kwenye tukio hili tunanona kuwa

  • Mhusika alitakiwa aombe appointment, ila hakufanya hivyo
  • Kabla hajarudi tena Kanisa A, waumini wa makanisa yote mawili, Kanisa A na Kanisa B, walijua kuwa mhusika ndiyo chanzo cha matatizo
  • Baada ya Mhusika kurudi Kanisa A, ikabidi sasa Kiongozi Mkuu aanze kutafuta mbinu za kujinasua kutoka kwenye kile ambacho waumini wa makanisa yote haya mawili alikuwa amewapelekea wakiamini.
Na kama mhusika angefanya uamuzi usio sahihi wa kuhama tena kutoka Kanisa B na kwenda Kanisa Jingine tuseme C, (badala ya kurudi Kanisa A kama alivyofanya), picha pekee ya mhusika ambayo ingejitokeza kwa makanisa yote haya matatu(yaani Kanisa A, Kanisa B na Kanisa C) ingekuwa kwamba yeye ndiye ana matatizo kwa sababu:

  • Aliwahi kuhama kutoka Kanisa A na kwenda Kanisa B, pasipo kuwa ameuaga uongozi wa Kanisa A
  • Alihama kwa matatizo yake mwenyewe, hakuhamishwa na mtu yeyote
  • Aliwahi kumkwepa Kiongozi wa Kanisa A pindi alipokuwa ametembelea Kanisa B, Kanisa ambalo mhusika alihamia baada ya kutoka Kanisa A
  • Waumini wote pamoja na viongozi wote wa makanisa A na B wanajua kuwa mhusika ndiyo ana matatizo na si viongozi wake
  • Waumini wa Kanisa C nao pia sasa wangejumuika na uelewa wa waumini wenzao wa makanisa hayo mawili, kujua kuwa mhusika ndiyo ana matatizo na si viongozi wake
AMBACHO MHUSIKA HATIMAYE ANGEKUJA KUVUNA KAMA MATOKEO YAKE YA HAMA HAMA KUANZIA KANISA A MPAKA KANISA C

Kwa hiyo mwisho wake ingekuja kueleweka kuwa mhusika aamekuwa akihama hama makanisa kwa sababu anazozijua mwenyewe binafsi na pasipokuwa amebugudhiwa na mtu yeyote, ila akiwa na lengo la kuwachafua viongozi wa makanisa anakokuwa ametokea

  • Uelewa wa waumini wa makanisa yote haya matatu, ulikuwa na nguvu kubwa mno na kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwa ungechukuliwa kuwa ndiyo uelewa wa PUBLIC
  • uelewa wa PUBLIC, ni uelewa wa DOLA
  • DOLA sasa hapa lazima ingeingia kazini kutaka kujua kwa nini huyu mtu anafanya mambo kama anavyotaka yeye, na ambayo yanaashiria jinai ndani yake
Kumbuka pia kuwa, hapa kulikuwa na uwezekano wa DOLA kutojijishughulisha na kuhoji sana isipokuwa ingechukua uelewa wa PUBLIC tu na kuanza kuufanyia kazi



MWANDISHI WENU ATARUDI KWA AJLI YA MATUKO MENGINE MAWILI ZAIDI, LA TATU NA LA NNE
 
Back
Top Bottom