#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

Kwani kanisa ni ilo tu, kama anadhani kuna mambo hayaendi sawa na jeopardize maisha yake si ahame kanisa?
 
Kwa

Kwa hiyo kwa kifupi wakristo mnahujumiana wenyewe kwa wenyewe. Nimekuelewa
Ila naomba uwe mwangalifu kwenye maswala haya ya hujuma. Unaweza ukaiona hujuma imefanyika kwa jirani yako, kumbe ukija kuchimba kwa undani zaidi, imekuumiza zaidi wewe kuliko hata huyo jirani yako. Kwa mfano, unaweza ukakuta mtu analalamika anafanyiwa hujuma kumbe hujuma hizo zinatokana na yeye kuhakikisha, Billion 28 za kila mwezi zinazopelekwa kwa ajili elimu bure haziibiwi. Sasa unaweza ukakuta wewe watoto wako wanne wako shule, yeye hana mtoto hata mmoja anayesoma shule. Hawa watu wawili kati ya mlalamikaji na wewe, nani anaweza kuwa amehujumiwa zaidi, assuming hizo pesa zingeweza kuibiwa zisifike kule zilikokuwa zimeelekezwa? Ukiona mtu analalamika, angalia kule, usiangalia kwenye ncha za vidole vyako hapo uliposimama
 
nitasoma vizuri nikitulia. ila nimependa mdau anavyotenga muda wa kumtumikia Mungu. Mungu nisaidie na mimi hii kitu
Mimi huwa kila mara namuuliza ni nini kinamfanya awe na juhudi kiasi kile kwa ajili ya Mungu; na jibu lake ambalo huwa ananipa hili:

"KWA YALE AMBAYO MUNGU AMESHANIFUNULIA MPAKA MUDA HUU, IKITOKEA KWA BAHATI NA WEWE AKAKUFUNULIA KWA JINSI HIYO, NINA WASIWASI WEWE UNAWEZA UKAHAMISHIA KABISA GODORO NA KITANDA CHAKO PALE PALE KANISANI.

Jibu lake huwa ni hilo siku zote
 
Ni mao ya kiroho zadi. Zingatia kipengele hiki hapa:
SABA: Huyu bwana anadai kuwa kipindi kabla ya Corona, wakati watu walikuwa wako huru kushikana mikono, kuna watu wachache ambao alikuwa ameshawaainisha, ambao walikuwa wana tabia ya kuhakikisha kuwa wame-shake hands naye kabla Ibada haijaanza, na kwa nia ambayo yeye anadai kuwa haikuwa njema. Hawa watu walikuwa wamejipanga randomly kiasi kwamba usipokuwa makini, huwezi kuwatofautisha na wengine ambao walikuwa wanakwenda ku-shake hands naye kwa nia iliyo njema. Inaonyesha KAMA hawa shaker hands, wameanza kutumia sanitizer kwake, kama substitute yao baada ya Corona kuingia, maana haiwezekani tena ku-shake hands kwa sasa.
Mungu anisaidie hiki kichwa changu hakielewi kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mhusika kwa sasa bado hajanipa ruhusa ya kutaja sehemu, ila amesema kuwa given time, kuna uwezekano mkubwa akaja akatoa ruhusa hiyo muda siyo mrefu kwa sababu alichoruhusu kiruke hapa, ni kama asilimia 0.01% tu ya kile alichowahi kushuhudia tangu aanze kuabudu kwenye nyumba hiyo ya Ibada. Amekuwa kimya tangu mwaka 2011, takribani miaka 9 sasa! Anataka kwanza awe na uhakika kuwa haya matukio yana maanisha kitu na si coincidences tu, kwa sababau wakati mwingine zinaweza kuwa ni coincidences tu za bahati mbaya ambazo hazina maana yoyote!
Mkuu si umesema kanisa ni jipya ameanza kuabudu ndani ya miaka miwili au sijakuelewa
 
Yeye ana nini mpaka afanyiwe vitu vyote hivyo?
Hata yeye kichwani kwake ana swali kama hilo hilo unalouliza wewe hapa. Tuseme kwa mfano, watu WOTE wanaokuchukia wewe unawajua? Na kama tuseme unawajua, je sababu za wao kukuchukia nazo unazijua pia? Hili swali ulitakiwa uwaulize mahasimu wake, assuming ungekuwa unawajua
 
UPDATE 04/05/2020

SABABU ZILIZO NYUMA YA PAZIA ZINAZOPELEKEA KANISA JIPYA LILILOJENGWA ALMAARUFU KAMA “JENGO JIPYA” KUTOKUTUMIKA MPAKA MUDA HUU


  • Kanisa jipya ambalo liko kwenye stage ambayo lingekuwa limeshaanza kutumika, halitumiki na uongozi mzima ulishalibatiza jina JENGO JIPYA.
  • Inaonyesha KAMA ni marufuku kuliita “KANISA JIPYA” na huwezi ukamsikia kiongozi YEYOTE pale Kanisani analitaja kuwa ni KANISA JIPYA, bali JENGO JIPYA
  • Haya majina yana implications zake kubwa sana kwenye ulimwengu war oho, kwa maana kuwa PEPO anaweza akakaa kirahisi tu ndani ya JENGO lolote lile, lakini ni vigumu sana kwake kukaa kwenye KANISA na ndiyo maana haliitwi KANISA JIPYA bali JENGO JIPYA, ili kutoa mwanya wa mapepo kuweza kupata hifadhi humo
  • Si kwamba hawezi kabisa kukaa kwenye kanisa, kama kuna jitihada za kumuwezesha afanye hivyo, ila ni vigumu kwake kukaa ndani ya kanisa na hasa kufanya makao permanent
  • Tofauti na ilivyo sehemu zingine, kwenye jengo la kawaida pepo anaweza akafanya makao permanent kirahisi tu, unless zimefanyika jitihada za kumwondoa
Sababu za kutokutumika Kanisa hilo jipya, yeye anaziona kama ifuatavvyo:

  • MADHABAHU YA KANISA LA ZAMANI (ambalo ni banda na huwa liko vulnerable sana na manyunyu ya mvua hata iwe ni ndogo tu) iko karibu na vyoo, na huko vyooni ndiko kuna hifadhi ya washiriki wa ziada (mapepo) wa Ibada zinazofanyika Kanisani hapo na hivyo kuna BAADHI ya wahudumu ambao huwa wanaanzia huko kwanza halafu wakitoka huko wanapanda moja kwa moja madhabadhuni na kuanza kuhudumu
  • Kawaida huwa wanapanda madhabahuni kupitia ubavuni mwa madhabahu wakiwa wanatokea vyooni, na si kwenye ngazi zilizoko upande wa mbele wa madhabahu
  • Washiriki hawa wa ziada (mapepo) huwa ni lazima wakae chooni, huko ndiko wanakopata hifadhi, hawawezi kukaa permanently Kanisani, sehemu ambapo Ibada huwa zinafanyika
  • Washiriki hawa huwa wanapatikana wakati wa maombezi ambayo huwa yanafanyika kila siku za wiki kuanzia Jumanne hadi Ijumaa
  • Kuna watu huwa wanakuja kutoka nje, wanatolewa mapepo, halafu mapepo hayo baadaye yanafanyiwa utaratibu wa kuhifadhiwa vyooni
  • Kazi ya kuyahifadhi vyooni huwa inafanyika na kikundi maalumu ambacho huwa kinajichanganya na waumini waaminifu, katika siku za maombi ya kuanzua saa 12.00 mpaka saa 2.00 usiku, pamoja na zile za maombi ya mkesha, ambazo ni Ijumaa usiku kuanzia saa 3.00 usiku na kuendelea Ndiyo maana ratiba ya maombi kwa nyumba hii ya Ibada huwa ni lazima kuanzia saa 12.00 jioni tu, na hakuna siku ambayo maombi yake huwa yanaanza kabla ya muda huo.
  • Isipokuwa tu kwa kipindi hiki cha Corona, ndiyo kumekuwepo na session nyingine mpya kabisa ya maombi yanayoanza saa 10:30 mpaka saa 12:00
Washiriki hawa ambao makazi yao maalumu (permanent) ni vyooni, huwa wanachukuliwa, na kuletwa kwenye Ibada kwa kutumia njia mbili:

  • MOSI: huchukuliwa kitaalamu kwa makusudi na wahusika wanaojua kuwa wamehifadhiwa humo na kuletwa kwenye Ibada
  • PILI: Wanaweza pia kuambatana na mtu mwingine yeyote anayeweza kuingia humo kwa shida yoyote ile, na kwa namna ile pasipo mhusika kuwa anajua, huweza kuambatana naye mpaka kwenye Ibada
Kazi yao kubwa kwenye Ibada ni kuhakikisha kuwa Ibada haifanyiki kama ambavyo waumini wa kweli na walio wengi, wangependa ifanyike.

  • Na kwa sababu waumini walio wengi hawako kwenye mpango huo na wala hawaujui, Ibada zinapokuwa zinaendelea wakati mwingine mapepo huzidiwa nguvu kutokana na upako wa watu wanaofanya Ibada, hivyo hulazimika kukimbia kwa muda
  • Inapotokea kuwa yamekimbia, kundi linalohusika hufanya tena jitihada ya kuyarudisha, kwa wiki inayofuata, Mbinu zinazotumika ni kwa kutumia aidha maombezi, maombi ya usiku au maombi ya mkesha. Kundi linalofanya haya ni dogo ila linashirikiana na uongozi, kiongozi mkuu wa kanisa akiwa mmoja wao, na washiriki walio wengi inaonyesha KAMA hawana taarifa ya kinachoendelea, na walio wengi huwa wanashiriki vizuri tu Ibada hizo ila pasipo kuwa na taarifa ya uwepo wa vitu vingine ambavyo huwa viko tofauti na Ibda.
  • Kwa hiyo cycle ya kuwa-restore washiriki hawa, yaani mapepo, huwa inafanyika kwa mtindo huo, na ndiyo maana maombi ni mengi zaidi kuliko mafundisho, ni kwa sababu kwenye maombi huwa kuna kazi ya ziada inayofanyika kisirisiri na ambayo wengi hawaijui
  • Tuchukulie kwa mfano kwa mwaka huu tangu uanze, kwa mara ya kwanza mafundisho yamefanyika J5 ya tarehe 15 April 2020, na kuanzia pale yameanza kufululiza kila j5 kwa sababu ya Corona. Kabla ya tarehe hiyo, tangu mwaka huu uanze, hapakuwahi kuwepo j5 ya mafundisho, isipokuwa maombi au kitu kingine ila si mafundisho
  • Sehemu nyingine inayotumika kuwahifadhi hawa washiriki ni kwenye “JENGO JIPYA” na ndiyo maana haliitwi KANISA JIPYA kwa sababu ukishaliita KANISA, kiroho unakuwa automatically umemu-deny pepo uhalali wa kupata hifadhi humo, japo si lazima kuwa ndiyo hawezi kabisa kukaa humo. Jitihada inayopaswa ikifanyika, bado anaweza kukaa humo pia
  • Na kwa mtindo uleule, kwenye JENGO JIPYA, namo pia pepo hawa huwa wanafikia hatua ya kutaharuki siku za Ibada halafu wanakimbia, na kazi ya kuwarudisha inafanyika tena wiki inayofuata kwa kutumia mkakati na mbinu zile zile kama nilizozieleza hapo juu
  • MHUSIKA ANADAI KUWA KUNA UWEZEKANO ZIPO PIA SEHEMU ZINGINE ZINAZOHIFADHI HAWA VIUMBE, NDANI YA NYUMBA HIYO YA IBADA. Kwa mfano, utafiti wake mpaka muda huu ameshajiridhisha kabisa kuwa kinyesi kilichokuwa kinatirrirka kutoka kwenye chemba za maji machafu, ilikuwa ni mojawapo ya hifadhi ya hawa viumbe. Walikuwa wanakaa kwenye harufu, na kwenye maji yaliyokuwa yamechanganyikana na kinyesi hicho, na ndiyo maana kinyesi hicho kilikuwa kinaachwa kitiririke makusudi!


SABABU ZINGINE ZINAZOPELEKEA KANISA LA ZAMANI KUENDELEA KUTUMIKA MPAKA MUDA HUU

  • Uchunguzi wa mhusika wa taarifa hizi unadai kuwa kuna kipindi washiriki hawa (mapepo) walionekana wamepotea kabisa, kanisani hapo, hasa kwenye Kanisa la zamani
  • Hali hiyo ilipelekea kiongozi mkuu kutengeneza utaratibu wa kufanya test ya kuhamia kwenye JENGO JIPYA, kwenda kuona kama kwenyewe labda kutakuwa kuna ahueni
  • Kwa hiyo Ibada za J2 mbili mfululizo zliifanyika kwenye JENGO JIPYA, lakini ikaonekana kwenyewe ndiyo hali ilikuwa mbaya zaidi, hawakwuwepo kabisa, Ibada zikawa almost haziendesheki
  • Baada ya kuona hivyo, ukatengenezwa utaratibu kupitia mafundi mitambo wa vyombo vya sauti na muziki, ikafanywa trick kiongozi mkuu akiwa amesimama madhabahuni anaongea, baadhi ya washiriki wakawa hawamsikii
  • Baadaye zikatolewa sababu kuwa kuna mwangwi kwenye jeingo jipya, na hivyo inabidi lisitumike kwanza.
  • Mbinu hii ndiyo ikasababisha kurudi tena kwenye kanisa la zamani, lakini ukweli ni kwamba hakuna mwangwi unaoweza kuwashibda mafundi mitambo kuurekebisha, tena kwenye kanisa ambalo hata kuta bado hazijawekwa.
Ni mchezo ulifanyika hapa na sababu zilizopelekea kufanyika mchezo huu ni kama ifuatavyo:

  • KANISA JIPYA, kama ambavyo yeye huwa analiita, kutokana na jinsi lilivyo, wakati wa Ibada za majaribio zilizofanyika kwa J2 mbili mfululizo, wakati wa Ibada, lilianza kutoa sauti zinazoimba (melody), ya hali ya juu sana; melody ambayo hata kichaa akiisikia, anajua kuwa kuna watu wa MUNGU wako kwenye Ibada. Melody hii ilichangia kwa kiwango kikubwa kusababisha mapepo yakimbie mbali zaidi, kitu ambacho hakikuwa kimetarajiwa
  • Pia BAADHI ya wahudumu wa Ibada (Praise and Worship) zinazohusiana na uimbaji, walikosa option ile ya kuanzia chooni halafu ndiyo mtu anapanda moja kwa moja madhabahuni, na kama ilivyo hadi sasa kwa madhabahu ya kanisa la zamani. Ni kwa sababu madhababu ya Kanisa jipya iko mbali na vyoo, na hata wale ambao wangetamani kufanya hivyo, with time wangeweza kuja kujulikana, kwa sababu ingebidi waonyeshe pattern fulani ambayo hata mtu ambaye hakuwa makini nao, angeweza kuiona; madhbahu ya Kanisa jipya iko mbali na vyoo, na wale ambao wangekuwa na tabia ya kuanzia chooni kwanza halafu ndiyo waelekee madhbabahuni, ingebidi waonekane na kila mtu


SABABU NYINGINE INAYOPIGILIA MSUMARI KU-SUPPORT KWAMBA KANISA JIPYA LIMETELEKEZWA KWA SABABU LINATOA MELODY NZURI SANA WAKATI WA IBADA, AMBAYO HAITAKIWII NA MAPEPO YANAYOHIFADHIWA HUMO


  • Kutokana na tahadhari ya ugonjwa wa corona, siku ya Ibada ya Ijumaa kuu tarehe 10/04/2020 ndiyo siku ya kwanza ambayo viti vilianza kupangwa umbali wa mita moja kutoka mtu mmoja hadi mwingine, na hivyo ilibidi visambae hadi sehemu karibia yote ya kanisa jipya pia
  • Kutokana na hali hiyo, ilibidi spika za muziki na sauti zisambazwe hadi kwenye eneo hilo la Kanisa jipya
  • MELODY ya Ibada ya siku ya Ijumaa kuu ilikuwa nzuri muno, watu walikuwa wakiimba unasikika mziki mtamu utadhani unatokea mbinguni
  • Baada ya siku hiyo, Jumapili ya Pasaka ghafla zikaongezwa ngoma pamoja na sahani kwenye kikundi cha waimbaji wa Praise and Worship, vyombo ambavyo mhusika hakuwa amewahi kuviona vikitumika pale tangu aanze kuabudu pale mwaka 2011
  • Drums hizi zilizoongezeka zina tabia ya kusababisha kelele na kuchuja utamu wa mziki, na ndiyo maana zimeongezwa ili kuchuja ile melody ya mziki inayotokana na sauti ya waumini pamoja na vyombo vya muziki vinavyokuwemo ndani ya Kanisa jipya
  • Drums na sahani zimeongezeka kwa sababu JENGO JIPYA inabidi liendelee kutumika lote kwa ujumla wake mpaka pale Corona itakapoisha. Kabla ya hapo, lilikuwa linatumika sehemu tu, ambayo ilikuwa haihitaji sana mafundi mitambo kusambaza vyombo vya sauti na muziki ndani ya jengo hilo
  • Zaidi ni kuwa mpigaji drum ni mgeni, inaonyesha amehamishwa kutoka sehemu moja kuhamia pale kwa ajli ya kazi hiyo tu, hata hivyo cha kushangaza zaidi ni kuwa HAJAONEKANA AKIWEKEWA MIKONO MBELE YA MADHABAHU NA MBELE YA WASHIRIKI, KWA SABABU WAHUDUMU WOTE WANAOHUDUMU KWENYE KIKUNDI HICHO NI LAZIMA WAWE WAMEWEKEWA MIKONO. Huyu mgeni aliyekuja hajaonekena akipitia hatua hiyo, kwa sababu ameibuka ghafla siku ya J2 ya pasaka, na kabla ya hapo hakuwahi kuwepo Kanisani hapo
  • Kwa kumbukumbu zake za mbali sana mhusika wa taarifa hiii, yeye anadai kuwa kipindi cha nyuma kwenye miaka kati ya 2011-2013, aliwahi kuona drum hizo zimenunuliwa ila hakuwahi kuziona zimetumika. Zililetwa madhabahuni na kuonyeshwa na mhusika wa manunuzi mbele ya kanisa zima, lakini hakuwahi kuziona zimetumika tangu pale
  • Mbali na haya yote, Kanisa hili lilitakiwa kuwa limeshaanza kutumika mwaka jana, possibly muda kama huu, kama sikosei. Hela kwa ajili ya ujenzi wa madhabahu zilishachangwa nadhani zaidi ya mil 300. Baada ya hela kuchangwa ilifanyika kaziya kujenga kwanza ngazi za madhabahu kwa kutumia tofali tu na baada ya hapo pilika pilika zote zikasita hadi leo. Na kama madhabahu ilitakiwa kuagizwa kutoka China, bado kulikuwa na muda wa kutosha, kwamba madhabahu hiyo ingekuwa imeshawasili Dar es salaam hata kabla ya kuanza kwa gonjwa hili la Corona.
  • Mhusika wa taarifa hii anadhani kuwa pengine sasa hivi mtu akiuuliza uongozi kwa nini madhabahu bado haijakamilika, anaweza akaambiwa kuwa ni sababu ya Corona
Kwa hiyo KANISA JIPYA, almaarufu kama JENGO JIPYA, halitakiwi kutumika kwa sababu kuu mbili, noja ikiwa ni melody nzuri inayotokana na Kanisa hilo, kiasi kwamba imesababisha hadi drums za muziki ziongezeke kwenye timu ya waimbaji na pili ni kwa sababu linatumika kama hifadhi ya washiriki wengine wa kisirisiri ndani ya nyumba hiyo ya Ibada

Mhusika anatoa wito kuwa kama kweli kuna mwangwi umesababisha kanisa jipya lisitumike, anashauri iletwe timu huru ya wataaalmu wa vyombo vya muziki, ije iverify kama kweli kutna tatizo hilo. Nyumba ambayo haina hata kuta bado haiwezi kuwa na mwangwi ambao ni complicated kiasi cha kuwashinda wataalamu kuudhibiti. Nyumba zingine zina kuta na mwangwi hazina. Anadai kuwa ni rahisi zaidi kupata mwangwi kwenye nyumba iliyo na kuta, kuliko ile ambayo haina. Waletwe wataalamu waje wathibistishe hilo, kama upo uwezekano huo



KANISA JIPYA, ALMAARUFU KAMA JENGO JIPYA NA UHUSIANO AMBAO UMEKUWEPO KATI YAKE NA KIPINDI CHA KILA J2 CHA SOMO LA UANAFUNZI NA MAANDIKO

  • Inapotokea kuwa kuna somo la uanafunzi na maandiko, ambalo kawaida lilitakiwa kuwepo kila j2 ila huwa linakuwepo kwa mara chache sana, kiongozi mkuu huwa anasimama kidete kuwapanga watu kuhakiksha kuwa wamekaa kwa kusogeleana na kuenea ndani ya kanisa la zamani, wasije wakafikia hatua ya kusambaa hadi kwenye kanisa jipya, kiasi kwamba washiriki wa somo hilo inabidi wawe ni wale tu waliokaa na kuenea kwenye kanisa la zamani
  • Huwa anahakikisha anafanya hili kwa umakini mkubwa halafu baadaye anaondoka kwenda kunywa chai, yeye huwa siyo kawaida yake kushiriki somo hilo.
  • Pia huwa anahakikisha kuwa waumini walioko kwenye kanisa jipya ambao hawashiriki somo hilo, wamekaa mbali kiasi cha kutoweza kuwa wanasikia kinachofundishwa kwenye kanisa la zamani, ili isije kwa namna moja ama nyingine, mafundisho hayo yakawafikia halafu wakaambukiza upako kwenye JENGO JIPYA, na kusababisha washiriki wa akiba, kukimbia ndani ya jengo hilo


PEPO MAARUFU ANAYETAMBA KANISANI HAPO KWA SASA, ANAYETUMIA SAUTI ZA WATU NA ZA VYOMBO VYA MUZIKI, ALIYERUSHWA J5 YA TAREHE 15/04/2020 WAKATI WA IBADA YA JIONI YA MAFUNDISHO YA MAANDIKO MATAKATIFU

  • Alirushwa kwa kutumia “secret code” inayotumia neno “UZINZI”(Secret code hii ina maelezo yake ya kina na itafafanuliwa peke yake katika sehemu itakayofuata)
  • Ana uwezo wa kurushwa kwako kwa kutumia njia ya mtu kukusemesha, kukusalimia au kusemezana naye tu
  • Alirushwa na kiongozi yule yule aliyesemekana kuwa ni mhusika wa manunuzi ya Sanitizer, kwenye Ibada ya mafundisho ya maandiko matakatifu J5 ya wiki iliyofuata wiki ya pasaka
  • Kiongozi huyo alikaribishwa kuchangia kwa sababu somo liliendeshwa kwa mjadala, na kama kawaida yake, akataja neno UZINZI, ambalo tayari mhusika alishaling’amua kuwa huwa ni secret code ambayo huwa anaitumia kuita mapepo, na kipindi fulani nyuma amewahi kuitumia kwa karibia mwaka mzima
  • Wakati pepo huyo anarushwa, Ilikuwa j5 ya kwanza (kwa mwaka huu tangu uanze), kwa somo la maandiko matakatifu kufundishwa kanisani hapo. J5 zingine zote zilizopita tangu mwaka huu uanze, zilikuwa zinatumika kwa maombi kwa mara zilizo nyingi na au/semina/ibada za shukrani kwa mara chache sana
  • Kawaida siku zote, mafundisho ya j5 huwa yanaendeshwa na mtumishi mmoja wa Mungu kusimama mbele na kuanza kufundisha, wengine wakiwa wasikilizaji
  • Hata hivyo, KWA MARA YA KWANZA utaratibu siku hiyo ulibadilika, na ikabidi uwe wa majibizano, na kwa kutoa majibu ya maswali ambayo mchungaji mhusika alitoa maswali yake
  • Inaonyesha KAMA pepo huyu ana-operate vizuri zaidi katika mazingira ambayo sauti za watu wengi zinahusika, especially sauti moja kwa wakati na si kwa sauti ambazo ni za jumla kama vile za watu wanaoimba kwa pamoja au wanaofanya maombi kwa pamoja
  • Kuanzia pale sasa, hata vipindi vingine vilivyofuata vya mafundisho ya j5 imebidi sasa viwe kwa mtindo huo wa majadiliano. Maelezo yalitolewa kuwa utaratibu huo ni agizo kutoka ngazi za juu, kutokana na ratiba za J2 kuingiliwa na ugonjwa wa corona
  • Ukiangalia kuiuhalisia, agizo hili linapingana na tahadhari ya corona kwa sababu inabidi sasa mic moja ya kuongelea ishikwe na mikono isiyopungua kumi ndani ya lisaa limoja, na mouth piece itumike na midomo isiyopungua idadi hiyo hiyo na ndani ya muda huo huo. Sasa mtu hapa atajiuliza maswali, hii ngazi ya juu iliyotoa agizo hili, yenyewe haikuona hoja hii ya wazi juu ya tahadhari ya Corona, hoja iliyo wazi namna hii wala haijajificha?
  • Inaonyesha KAMA “test signal” ya J5 ya tarehe 15 siku ambayo somo la kwanza lilifundishwa kwa mwaka huu ilizaa matunda bora zaidi na yaliyokusudiwa na hivyo sasa kuanzia pale ikapendeza kuwa mafundisho yote ya siku za J5 yawe ya majibizano
  • Kuanzia pale sasa hata siku zingine zote za j5 mafundisho ni kwa njia ya majibizano mpaka pale corona itakapoisha
  • HATA HIVYO MHUSIKA ANAOMBA KUSHAURI KINYUME CHAKE. MAFUNDISHO HAYA YA J5 YAFUATE UTARATIBU KAMA ILIVYOKUWA ZAMANI KABLA YA CORONA, YAANI MTU MMOJA KUSIMAMA MBELE YA HADHIRA, NA KUFUNDISHA, NA PASIWE NA MAJIBIZANO MPAKA PALE CORONA ITAKAPOISHA
  • Pepo huyu anayejadiliwa hapa, ana uwezo wa kusambaa kutoka mtu mmoja hadi mwingine kupitia maongezi
  • Ana uwezo wa kushambulia kupitia sauti ya mtu unayemsikiliza akiongea redioni, anaweza kupitishiwa kwenye sauti ya redio kwenye mita band ulizotune radio yako
  • Ana uwezo wa kushambulia sauti ya chombo chocote pia. Nyumbani kwake mhusika wa habari hii, tayari ameshaharibu micro-wave oven kupitia alarm ile ya micro-wave ambayo huwa inapigwa muda wa kupasha/ kupika chakula ukishatimia. Alishambulia micro wave kupita alarm hiyo ambayo huwa inaita ili mtu akatoe chakula kwenye micro-wave kikishakuwa tayari kimeshapata joto
  • Pia ameshaunguza pasi ya kunyooshea nguo, alikuwa akisikiliza mahubiri redioni wakati akiwa ananyoosha nguo
  • Kwa hiyo anaweza pia kushambulia sauti za vyombo vya muziki vitumikavyo kanisani wakati wa Ibada, na hasa vile ambavyo vinakuwa havijawekwa wakfu, au vile ambavyo vinaweza kuwa viliwekwa wakfu kwa kuegesha, ili baadaye vitumike kwa kusudi jingine
  • Na hapa mhusika pia ana wasiwasi sana na drums zilizoongezeka kwenye vyombo vya Ibada kuanzia J2 ya pasaka
  • Ana uwezo pia wa kurushwa kwa kutumia sauti ya mtu aliyesimama madhabahuni akitoa neno au mahu
Mwisho kwa sehemu hii:

Mhusika wa tukio anadai kuwa yeye si mtaalamu sana wa mambo haya ya kiroho na hivyo kuna sehemu pengine anaweza kuwa ametoa maelezo ambayo hayako sawa, especially kuhuisana na sehemu ambazo mapepo wanahifadhiwa, lakini UHAKIKA NI KUWA HAWA MAPEPO WAPO KANISANI HAPO NA PIA WANAHIFADHIWA. Kama kuna sehemu atakuwa amekosea, basi itakuwa ni sehemu ambapo mapepo wanahifadhiwa, ila utakatishaji au urutubishaji wa mapepo hayo upo hilo hana shaka nalo!

NITARUDI

SEHEMU INAYOFUATA

POPULAR KEY WORDS AU POPULAR SECRET CODES ZINAZOTUMIKA KUWAITA MAPEPO NA /AU KU-ACKNOWLEDGE UWEPO WAO, WAKATI WA IBADA
 
Back
Top Bottom