Pole mkuu. Zamani nilikuwa napenda kuangalia Isindingo. Kuna siku Georgie Zamdela alipata binti, akawa amepiga viagra. Wakati George anajiandaa kisaikolojia yule mtoto akapigiwa simu ya msiba, nadhani baba yake au mama yake alifariki. Yule mtoto akaanza kulia na akasema anaondoka. Ahh George alizunguka chumba kizima haamini wakati huku chini mambo tayari.
Ila mkuu wanaume hapo ndipo huwa tunakosea. Kwanza pombe na viagra haviendani. Kaka mwisho wake ni mauti.
Pili hiyo hela ingeenda hata kwa account ya mtoto. au katika maendeleo.
Ukifikisha miaka 40 hutaona jipya kwa wanawake, nakuambia ukweli. Akili hubadilika tu, unakuwa unawaza cementi na matofali.
Usije ukawa unahadithia wanao, ''hii sehemu zamani ilikuwa pori tu sasa hivi pamejengeka'' wakati hapo hata kiwanja huna.