Mkapa, Vincent na Madaraka: What Else?


Ni kwamba Vicent kapewa jina la ukoo la nyerere, jina la nyerere halikuanzia kwa Julius Kambarage, Julius pia si nyerere kjina lake ni kambarage la nyerere ni la baba yake.Kwa maana nyingine jina la nyerere wamepewa watu mbali mbali ndani ya ukoo ule. mfano Masanja anapewa jina la masanja kwa kuitwa jina la babu lakini kina masanja ndani ya ukoo ule wako wengi.Hii ni kawaida huko lake zone.ndiyo zetu hizo
 


''Vijana wa ccm'' wamesusia uchaguzi huu maana mgombea waliyemtaka amechakachuliwa! Walikuwa wanamtaka Sarakikya lakini nguvu wa ukweni ikampitisha Sioi! kwahiyo wapo pembeni wanasubiri matokeo! nadhani tutasherehekea pamoja kwenye ofisi ya cdm mgombea wetu akitangazwa mshindi!
 
Mkandara mimi najadili kilichoandikwa kwenye bango na si vinginevyo. FMES yeye kaandika "familia" na si 'ukoo" kwa kuwa siku zote nasimamia ukweli ni kwamba Vincent si mwanafamilia ya Mwalimu ila ni ukoo mmoja na mwalimu. Vincent anaitwa "Vincent Josephat(Yaani kazaliwa na Josephat) Nyerere" wakati Madaraka anaitwa "Madaraka Julius (Yaani kazaliwa na Julius) Nyerere. Madaraka na Vincent undugu wao unakuja kwenye ukoo na wala si kwenye familia zao!!
 
Tafadhali ndugu Benjamin Mkapa usituulie na mama Maria Nyerere! You have been warned.......
 
Machinga na Mzanaki wapi na wapi ukoo/familia moja?
 

wengine hawana mvuto,sasa angeenda nani mwingine sasa na huyo mkaa hapa wanamwamin wao kama jembe kumbe ni kinyume chake! Mmmmh!
 
Duh ama kweli wewe mgumu sana kuelewa. Sizungumzii alichoandika FMES isipokuwa ulichoandika wewe dhidi ya maneno ya Mkapa.. Mkapa alisema hivi:-"Nimefanya kazi na Mwalimu kwa miaka 25, nikiwa mwandishi wake, Waziri na katika muda huo, nimemzika yeye, kaka yake na mama yake mzazi, sijawahi kusikia jina la mtu kama huyo katika familia hiyo".

Ndipo VN na Madaraka wakaingilia kati na kuweka habari hii sawa. Kwa kauli ya Mkapa alikuwa na maana Ukoo (katumia familia hiyo)maana kamhusisha hadi kaka na mama yake mwalimu ndio maana Madaraka na VN wakamwaga mboga.
 

kweli mkapa bomu!!! Yaani anawaongopea watanzania (wana arumeru) kuwa vicent nyerere mbunge wa musoma kuwa si ndugu wa nyerere??? Wakati ni ndugu kabisaa baba mkubwa na mdogo!! Ndio maana madaraka kathibitisha kuwa vicent ni ndugu yao!!!
 
Mkapa alikuwa anajua kuwa akisema hivyo,itaongeza idadi ya kura kumbe imemharibia,ameongea vitu kwa kuropoka tuu ,thankx madaraka nyerere kwa kutuwekea kumbukumbu nzuri kwenye hansard!!!!!!!,mzee alijua arumeru ni kisiwa watu wanajua kila kitu mh.b.mkapa unawajua watoto wote wa basil p.mramba........
 


Field Marshall ES,

Kwanini watu huwa mnapenda ku-post thread zenye utata na kufanya wasomaji waanze kuuliza maswali?
Tangu lini Benn William Mkapa alikuwa familia ya Nyerere? Vincent Nyerere na Madaraka Nyerere ndo
familia moja na si vinginevyo.

Mkapa aliposema kuwa hamjui Vincent Nyerere kama ni familia ya Nyerere kwa vile yeye Mkapa(akiwa Presida)hakuwahi kutambulishwa kwa Vincent kuwa ni familia ya Nyerere. That's all.

Tatizo la Mkapa ni kwamba amerukia jambo ambalo hakupaswa kabisa kulizungumzia kwenye kampeni za Chama chake cha Mafisadi. Mkapa amedhihirisha kuwa siyo mtu makini kwa kuanza kuzungumzia mtu badala ya maswala(issues) ambazo ni kero kwa Wana-Arumeru! Wazungu wana msemo unaosema: SHALLOW MINDS DISCUSS PEOPLE BUT INTELLIGENT MIND DISCUSS ISSUES!

Hivyo kitendo cha Mkapa kurukia swala la kifamilia la Vincent Nyerere ni kuonyesha kuwa Mkapa ni very shallow minded na sijui hata ilikuwaje Marehemu Mwalimu alimpigia debe kama Mr. Clean mpaka akaukwaa Urahisi kiurahisi kabisa. Hii yote inaonyesha kuwa CCM wote ni shallow minded maana kama wangelikuwa makini bila shaka walipaswa kumweleza Rais wao mstaafu nini cha kwenda kuzungumzia huko Arumeru Mash. na siyo kuzungumzia ukoo wa Vincent Nyerere!

Mkapa amechokoza moto ngoja umchome atie akili. Pambaf kabisa!
 

Mkandara Mkandara Mkandara! Pole pole aka taratibu!
Anamaanisha kama kuna kitu kimejificha waje watu wenye upeo mzuri na hcho kitu waki-expose ili kiwe bayana na watu wengi wakielewe, na si kwamba wakachimbue kaburi la Mwalimu!

 

Kosa si langu ni lako Mkandara!! Mimi sikuwa najua kama Mkapa kajumlisha na hao wengine akadai ni "familia" hilo ni kosa lake na si langu. Na mimi sikuwa narekebisha maneno ya Mkapa bali nilikuwa naweka sawa kwa wale waliotafsiri kwamba Mkapa alikana kwamba Vincent si mtoto wa Mwalimu jambo ambalo ndilo nalisema kwamba ni kweli kwamba Vincent si mtoto wa Mwalimu bali ni ukoo mmoja ni Mwalimu. Hilo ndilo tatizo la kutokujua kiswahili vizuri!!
 
Mkandara Mkandara Mkandara! Pole pole aka taratibu!
Anamaanisha kama kuna kitu kimejificha waje watu wenye upeo mzuri na hcho kitu waki-expose ili kiwe bayana na watu wengi wakielewe, na si kwamba wakachimbue kaburi la Mwalimu!

Ili iweje?..mkuu wangu hivi unaijua Bongo na wewe mbona bado mnayaendeleza. Yaani nani aseme nini na kiaminike ili hali VN kasema tu Mkapa anahusika tayari watu mmeisha anza kum doubt! ila Mkapa ndio mkweli.. si bora wachimbue kaburi tupate uhakika kuwepo kwa homicide..
 
Kwa hiyo mimi ndio mwenye makosa sio" hata kama umeyaandika haya
 

Hebu watu msitake kumtetea Mkapa kuwa hajui Kiswahili. Yeye tayari kesha jinadi kuwa alikuwa Mwandishi wa Mwalimu kwa hiyo anaijua vizuri familia ya Nyerere. Sasa ni mwandishi gani asiyejua hata maana ya MAJINA YA UKOO(SURNAMES). Yeye kwao Mkapa kuna kina Mkapa wangapi? Au hilo jina la Mkapa ni la kwake tu na si la ukoo? Majina ya ukoo huwa yanaendelea kutumika kwa koo zote za familia husika toka Babu wa Babu,Baba,Wajukuu,Vitukuu,Vining'ina mpaka Vilembwe.

Kwa hiyo hoja ya Mkapa kuhusu ubini wa Vincent Nyerere haina mashiko haijalishi yeye allikuwa amekariri majina yote ya ukoo wa Mwalimu. Tunachongoja sasa ni Mkapa kujibu TUHUMA ZA MAUAJI YA MWALIMU ILI WATANZANIA WAAMUE NINI CHA KUMFANYA MKAPA,CCM NA SERIKALI YAKE YA MAFISADI!
 

Mkuu Hapa Issue sio Kushinda bali Kuelewa na kuelewana, Mkandara amejitahidi sana kukufafanulia mpaka amekuletea maneno yote yaliyosemwa na wahusika, Sasa hapa kuna kitu gani kigumu?? Katika Familia za Kiafrika Familia haiishii kwa Baba, Mama na Watoto bali inaenda zaidi ya Hapo, au wewe si Mwafrika? Kama ni Mwafrika hilo Halina Ubishi.

Suala la Familia(Ukoo) wa Nyerere kumu -asili mkapa kama mwana Familia huenda lilikuwa na utashi wa Kisiasa na kimaslahi zaidi Kwao! Inawezekana hawakuwa na uhakika sana juu ya Hatima yao baada ya Kifo cha JKN na ukizingatia kuwa wengi walizoea kuishi kwa Jina la Mwalimu.

Hivyo kitendo cha Kuondokewa na Jembe lao waliona kuwa BWM ndio mhimili mwingine kwao, Ndio maana wakampa uhawana Familia kwa maslahi yao, na mtakumbuka kuwa katika kipindi chote Mkapa aliwabeba sana.
 
Na jibu la yote haya lipo ktk Signature yako mkuu wangu inasema hivi:- Usually when people are sad, they don't do anything. They just cry over their condition. But when they get angry, they bring about a change
 

Mkuu salute na habari za siku.

Back to your qn, nadhani watu wengi hawajagundua kwa nini unamtaja Mkapa kama sehemu ya familia ya Mwl. Ni kweli wanafamilia walitamka kwamba Mkapa ni mtoto na sehemu yako, nadhani miaka kama 5 au 7 hivi nyuma. Pili kwa CCM kumtuma Mkapa katika kampeni hizi kunaonesha dhahiri kabisa kwamba CCM imko taabani, na bahati mbaya zaidi huyo aliyedhaniwa kuwa na ushawishi pekee ndani ya CCM ndiyo keshajipoteza mwenyewe.

Wakati mwingine inabidi kuukubali tu ukweli kwamba nothing lasts forever. Ilianguka Roman Empire sembuse CCM? Hizi ni naked symptoms za CCM kupotea kabisa.
 
Kifupi Mkapa kachemsha na watu wengi sana walikuwa hawamjui Mkapa anapozungumza bila kutayarishiwa hotuba. Hawajui kama ni jeuri, mropokaji na msema ovyo sasa kakutana na vishoka. Kafanya makosa sana kufanya haya kwenye mhadhara wa watu na mwenyewe kakubali na kutubu yamekwisha, lakini tayari kisha jiwekea doa kubwa zaidi kufumua donda la wanandugu..

Sasa hapa ndipo FMES anatupeleka kutafuta kilichojificha zaidi nyuma ya pazia hili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…