Mkapa: Najuta

Sijawahi na sito waamini watawala
 
Kama watanzania kweli si wanafiki, hakuna mtu tunayetakiwa kumshutumu au kumpeleka jela Kama huyu BWM, alidiriki kusign mikataba ya mpaka miaka 100 kwenye ardhi zetu zenye rutuba na madini.. huyu ndiye source ya matatizo yote leo hii hakuna mchawi mwingine kuanzia miaka ya 1990 mpaka leo 2016. Kwa unafiki wetu tunamtetea sana ila leo nafsi inamsuta maana miaka kumi yake hakuna alichotuachia zaidi ya Uwanja wa taifa na daraja Mkapa pale lindi vingine ni unafiki tu wawatanzania.
Tukiwa wakweli na kuacha unafiki tutajenga hii nchi.
 
Na kama kulikuwa na rais mbishi mbabe na asiyeambilika yeye aliongoza.... and now I can see the reincarnation of him at this phase
Reincarnation haiwezi kutokea wakati roho yake bado imo mwilini mwake. Reincarnation is the soul rebirth.
Huyu Mzee alikuwa mbishi kweli kweli. Nilianza kukubali usemi usemao watu wafupi ni wabishi kweli. Huyu ali prove usemi huo.
 
Kuna mchangiaji hapo juu anaendeleza uleule unafiki kwa kusema " eti BWM hilo ni fumbo anataka JK naye aombe msamaha" tuache unafiki watanzania matatizo yakiutendaji aliyoyaacha BWM yamesababisha makovu kwa kizazi mpaka kizazi karne mpaka karne, " ubinafsishaji bila usimamizi,uzalendo na uwajibikaji" matokeo yake ni failure ya miaka Mingi mno maana hatuna chetu leo ukivunja mkataba tumeliwa. Makosa ya JK ni yapi hebu yasemwe, maana kubwa linaloonekana ni hilo la ufisadi na wizi ambao nalo ni kaa la moto alilolikuta kama matokeo ya kufail kwa ubinafsishaji.

Tuache unafiki tuwe wakweli.
 
Huyu anatusanifu sisi tuliovijenga viwanda vya umma na kuchangia miradi mingine ya maendeleo pamoja na viwanja vya michezo na majengo ambayo ccm wamejichukulia bila kulipa chochote hazina. Awaambie ccm irudishe miradi ile ya kabla ya 1993 serikalini. Arudishe na nyumba za umma na kisha aje kivyake atuombe msamaha.
 
Na kama kulikuwa na rais mbishi mbabe na asiyeambilika yeye aliongoza.... and now I can see the reincarnation of him at this phase
Then anashauri wengine wasikilize wakati Yeye hakusikiliza pamoja na watu kupiga kelele. Latina vitu atajibu Huyu mheshimiwa ni kumsingizia baba wa Taifa Kuwa alikuwa happy na huo uwejezaji wake ikiwemo bank ya Taifa na wish angekuwepo amjibu. Hivi Kama kosa analotubu tu ni ubinafsishwaji hivi Bado hajaguswa na uuzwaji wa nyumba za serikali?? Ama nao ni ubinafsishwaji basi Kama Bado atakuwa na Ngozi Ngumu sana
 
Ifikie muda sasa viongozi wetu waache tabia za kuwadharau wananchi wake kwa kutokuwasikiliza wanataka nini. Hili suala la kutowasikiliza wananchi inatokana na sheria mbaya ambazo zinawalinda viongozi wetu ambazo hupelekea kujiona wapo juu ya sheria kuliko wengine inamaana hata wakifanya makosa hakuna kushitakiwa.

Hivyo basi yatubidi tuige nchi za wenzetu wanavyofanya mfano Brazil, south Africa..
 
Nakumbuka alikuwa mbishi ka nini eti Leo ndo anaomba msamaha basi tutarajie na jk kuomba msamaha baada ya miaka kadhaa mbele.

Mkweree aombe msamaha wa kuwaachia wezi wa EPA;kupitisha makontena ya swahiba zake bila kulipa kodi bandarini, kuwalinda wauza madawa ya kulevya au kuwauzia waarabu Twiga?? Mtangoja sana kwa mkweree kutoka Msoga aje kuwaomba radhi!!
 
Kama kuna kitu mwalimu alipinga kwa nguvu zote ni hili la kubinafsishwa kwa NBC Benki iliyokuwa ina mtandao mkubwa zaidi nchini (upo ushahidi kwenye hili)na mzimu wake unamuandama mpaka sasa
Waafrica bado tunahaki ya kutawaliwa hatujaweza kabisa kujitawala zaid ya viongozi kuwa wababe katika madaraka na mijizi ikimaza muda huomba msamaha Africa yote zaid ya Gaddafi hakuna kiongozi
 
Yes
Yes na Kama jk asingekuta magangwe ya ufisadi yaneshaota mizizi nadhani mpaka Leo angekuwa one of the best leaders. Jk amefanya mambo mengi sana ya kizalendo kaacha vitu vingi vya kizalendo Kabisa tofauti na cartel za kiunyonyaji zilizoshamiri before him. Ubinafsishwaji ulikosa uzalendo Kabisa Wala si issue ya sera .kwani mzarendo ingemuuma aka rectify hata kabla ya kuaga
 
Shetani akizeeka anakuwa malaika .... kumbuka kauli hii toka mmoja wa wale alokuwa nao kwenye uongozi
"Ndege ya rais lazima inunuliwe hata kama wananchi watakula nyasi"
Hahahaha shetani ni shetani tu hawi malaika mijizi ikisha iba ndio huomba msamaha tuikatae msamaha wao Leo Hosp hata panadol hamna halafu linakuja kuomba msamaha inakera kweli
 
Kuomba msmaha si issue kubwa kama kila ajaye ataendekeza makosa na baadae kirahisi tu anakuja kuomba radhi.

Maamuzi makubwa yatoke kwa wananchi wote kupitia uwakilishi wao ili mtu mmoja asijebebeshwa mzigo. Mfano hata sasa tunamwachia mtu mmoja aamue mustakali wa taifa letu tuna ignore uwakilishi wa kidemkrasia. Tunasubiri yaharibike halafu aje aombe radhi. Kuna maana gani tunaposema tumuunge mkono mheshimiwa au tumpe nafasi au tusimhukumu.

Kwa nntunapohoji kila hatua tunapigwa stop. Kwa nini mfano kundi moja linamsapoti mtu lingine linampinga na hatujihoji?

Ikiwa tutaamua wote basi tunakujajilaumu wenyewe.

Kwa hivi tujiulize ni nani aliamua ubinafsihaji na ni kwa nini awe yeye na sio sisi na kama ni sisi ni kwa nini aombe radhi?
 

Huo ndio ukweli mkuu maana JK anasemwa kwa Mengi utafikiri aliikuta nchi iko kama china au USA vile yeye akairudisha kuwa tanzania.

Ubinafsishaji kama mfumo ulioachwa unaleta shida mpaka leo hii kwa JPM maana kodi leo tunategemea kwa walevi na wavuta sigara kwingineko watu wako kwenye probabation bado wakiona inakaribia kuisha wanabadilisha majina.

Watanzania leo hii wanasahau tuna MW za umeme za kutosha kilichobaki ni kulekebisha miundo mbinu.

Plant nyingi za umeme leo hii ni mali ya tanzania na hii ni juhudi ya utawala wa Jk maana BWM alituachia IPTL,SONGAS, na Aggreko ambazo zinatutafuna mpaka wa kesho.

Leo hii watu wanasahau chanzo cha ufisadi wa leo ni sera za kijinga za 1995 - 2005.
Watanzania tuwe wakweli na tuache unafiki taifa lisonge mbele.
 
Binafsi khali hii ya viongozi wetu kufanya makosa yanayo gharimu maisha ya watu na kuchukulia is simple thing and normal DAIMA SITOKUBALIANA NA KAULI HIZI NA SITAKI KUWA MMOJA WATAKAO PATA HUKUMU HII.
Ni hivi Watz. wote haijalishi Itikadi, Dini,Ukanda n.k.n.k kwanza tuachane na vyote hivyo, alafu tusimamia hoja zenye ukweli kuwa LAZIMA KATIBA IBADILISHWE VIONGOZI WOTE YAANI MARAIS, MAWAZIRI N.K WOTE wafanyiwe tathimini ktk vipindi vyao walivyo tuongoza na kutufikisha hapa tulipo ambapo kula tu ni shida.

Baada ya hapo kwa wale wote walio hujumu nchi hii au kutoa mawazo yaliyo ligharimu Taifa au kwa kutonufaisha katiba mpya ya Wananchi ipatikane na itoe tamko nini cha kufanya na hukumu zao baada ya kuthibitika kisheria.
Kwa mfano kama Rais au Waziri au DC au RC n.k. amelisababishia Taifa Majanga ambayo hadi sasa Watz. tunateseka kwa kukosa huduma za msingi alafu leo mtu anasema ninaomba radhi wakati yeye na Familia yake wakiishi kama peponi na alifanya kwa kukurupuka yafuatayo yanyike:
1. Afilisiwe mali zake zote na Familia yake.
2. Ahukumiwe kifungo cha jela na viboko juu kutwa mara 3.
3. Au Adhabu zote Na 1. na Na 2 kwa pamoja zitumike kwa usahihi na ufasha.
3. Au anyongwe hadi kufa na hii ndiyo ruler itakayo wanyoosha viongozi wote na kuheshimu wananchi na maisha yao na kujua kuwa hakuna aliye juu ya sheria na kuachana na mwendo kasi ideas,zaidi ya ku base on Logic/reliality/productivity.
Vinginevyo Watz. WOTE mjue ya kwamba kuna maisha zaidi ya haya ambapo tukiendelea hivi HAKIKA MAKABURI YETU HUENDA YAKAJA KUCHAPWA NA VIZAZI VIJAVYO KUWA TULIKUWA BEYOND USELESS ON EARTH KTK UHAI WETU kwani tunapoelekea huenda hata Tembo wakaja kumsoma ktk histori kuwa kulikuwepo na mnyama mkubwa duniani anaitwa tembo...wakati hawapo tena kisa TU wachache.
No regret any more than payment, let change my Dear Tz... keep on knowing we'll be paid after our work at end of every one life,so let paid others soon before be paid by God.NA HAPA NDIYO TUTAHESHIMIANA NA KUACHANA NA UNAFIKI..SHERIA IFUATE MKONDO WAKE...
Na siyo kusikia eti Muuza Mirungi au Mla mirungu kahukumiwa Maisha wakati Viongozi waliolitea Taifa Ulemavu na Majnga ya Maisha keeping survival and say sorry what???????
Na siyo zile adhabu za kufagia ma hospitali.....NO..NO...for sure this world is not fair but it can be Fair if a man can decide to create Fairness himself/herself.
 
Hii ni moja ya speech ya ki.pu.mba.vu na kilo.fa zaidi toka kwa kiongozi kuliko upu.mbavu na ulo.fa aliouna kwa watu waliompa heshima ya kuwa kiongozi wa nchi.Ubinafsishaji anaojaribu kuujutia hapa ndiyo uliompa fursa ya kufanya biashara akiwa ikulu.

Kupitia Sera ya ubinafsishaji aliyoisimamia mwenyewe,aliweza kufungua kampuni ya ANBEN na kujimilikisha kinyume na sheria za nchi mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira.Leo hii anapojaribu kutoa kilio cha machozi ya mamba,anapaswa alisemee hili,akiri hadharani kuwa aliitumia ofisi ya Umma kujinufaisha binafsi.

Ni katika uongozi wake rais wa sasa alisimamia uuzwaji wa nyumba za serikali kwa bei ya kutupwa huku baadhi ya nyumba hizo zikitolewa kwa "vidosho" wa wanene.

Pamoja na kukiri kushindwa kwake,uongozi wake uliacha majeraha mengi ambayo hayatasahaulika milele.Ni katika uongozi wake Taifa lilishuhudia mauwaji ya wapemba waliouliwa kikatili na majeshi yetu yaliyoapa kuilinda mipaka ya nchi yetu,lakini kwa mara ya kwanza badala ya kuilinda mipaka yetu,yaliwageukia Watanzania na kuwafyeka mithiri ya kuku alaye mayai yake.Kwa Mara ya kwanza nchi yetu ilizalisha wakimbizi baada ya kukimbilia nchi jirani ya Kenya kuukimbia mkono wa chuma na vifaru vya majeshi yetu vilivyokuwa vikiwaswaga kwa amri ya Mkuu wa nchi.

Huu waweza kuwa uchochezi kwa Tafsiri ya Policcm,lakini haya ninayoyaandika si uchochezi bali ni ukweli mchungu ambao viongozi wetu wanatamani waufute katika kumbukumbu za vichwa vyetu lakini hawawezi kwa sababu hawana mamlaka ya kutawala na kuzitiisha akili na dhamiri zetu,wataishia kutawala viwiliwili vyetu tu lakini si ufahamu wetu.

Viwiliwili wanaweza kuvitawala hata kwa taarifa za intelejensia feki ya policcm inayowapa kibali cha kuswaga watu kwa mabomu na Maji ya kuwasha.Unafiki wa watawala wetu na wapambe wao ukijaribu kuuweka katika viwango vya kidunia,waweza kuwa ni unafiki wa kiwango cha PhD.

Mtu anakurupuka bungeni mithiri ya msukule na kuiomba serikali ijenge uwanja wa kumbukumbu ya push-ups na bado waziri mwenye dhamana badala ya kukemea upuuzi huo,anamuunga mkono kwa kuahidi kufikiri namna ya kujenga kumbukumbu hiyo.Kati ya push-ups na mauwaji ya Wazanzibar yaliyosimamiwa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ni kipi kilipaswa kujengewa kumbukumbu?

Wazanzibar waliouliwa makumi kwa makumi mwaka 2001,maadhimisho yake hadi leo hupigwa marufuku na jeshi la police kana kwamba waliouliwa Zanzibar walikuwa ni magaidi,lakini kutokana na mparaganyiko wa maono ya kiutawala,watu wanaomba kumbukumbu za push-ups na serikali inaridhia,je hoja za aina hii haziwezi kuwa kigezo cha kulifanya Taifa letu kuandikwa kwenye Vitabu vya maajabu ya Dunia kama Taifa la watu wa.pumba.vu zaidi Duniani?

Hii ni nchi ya ajabu sana ambayo ukijipa muda wa kuitafakari unaweza kuishia korokoroni kwa kuitwa mchochezi kwa kuwa tu unajaribu kusema ukweli ambao viongozi wetu hawapendi kuusikia.Mungu tusaidie kupata viongozi wenye hofu ya kweli kuliko hawa wa kumbukumbu za push-ups.Amen.
 

Hata mimi naona hivyo hivyo, lakini sasa hao anaowatumia salamu naona kama angesema tu moja kwa moja tena kwa kuwataja majina ili wajue kuwa anawatumia salamu wao kwasababu, mh! sidhani kama hayo maono wanayo
 
Hata mimi naona hivyo hivyo, lakini sasa hao anaowatumia salamu naona kama angesema tu moja kwa moja tena kwa kuwataja majina ili wajue kuwa anawatumia salamu wao kwasababu, mh! sidhani kama hayo maono wanayo
Hapana hawezi kwenda hivyo kwakuwa yeye ni ndani yao sio mpinzani na anatumia lugha ya diplomasia
 
Hapana hawezi kwenda hivyo kwakuwa yeye ni ndani yao sio mpinzani na anatumia lugha ya diplomasia

Wenyewe hiyo lugha Sina hakika kama wanaielewa wala sidhani kama wasaidizi wao hata kama watang'amua ukweli huo kama wanaweza kudhubutu kuwaambia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…