MKAPA: "Dunia itatikisika CCM ikianguka"

MKAPA: "Dunia itatikisika CCM ikianguka"

DATAZ

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2012
Posts
4,712
Reaction score
11,981
Hayo ni maneno ya Rais Mstaafu Bwana mkapa alipokuwa Tanga kwenye kampeni za chama tawala.

Lakini kauli hii bado inazua maswali mengi, kwamba hiyo dunia itatikisika vipi kwa kuanguka kwa CCM?.
Kuna harufu fulani hapa.
 
Hayo ni maneno ya Raisi Mstaafu Bwana mkapa alipokuwa Tanga kwenye kampeni za chama tawala.

Lakini kauli hii bado inazua maswali mengi, kwamba hiyo dunia itatikisika vipi kwa kuanguka kwa CCM?.
Kuna harufu fulani hapa.
Ni yeye atatikisika... atawekwa jela kwa ufisadi wa kujiuzia mgodi wa makaa!
 
Kweli lazima itikisike maana mikataba mibovu yote lazima tuitoe....
Wachina wenye maduka Kariakooo lazima warudi China mapema
 
Yaani upuuzi sana dunia itikisike sababu ccm..ccm nani kwa mungu
 
Kwanini wanaogopa kuachia madaraka? Nini kipo nyuma ya pazia?
Alidondoka Gadafi dunia hakutikisika sembuse ccm?

Itatikisika kwa maana hii: Tanzania itakuwa inakwenda kufanya mabadiliko makubwa. Maliasili zitakuwa mwisho kwenda nje bure, tutatumia uranium yetu kuzalisha umeme halo lazima dunia itikisike. Tutafuta mikataba ya hovyo ya china, India nk. Marais waliopita watajibu tuhuma zao. Pesa zilizofichwa nje zitawekwa wazi. No lazima dunia itikisike
 
Tutawashinda na dunia itaendelea kama hakuna kilichotokea
 
Wacheni nyie ccm ndio inakamata uchumi wa dunia kila kitu hapa bureee
 
Hayo ni maneno ya Raisi Mstaafu Bwana mkapa alipokuwa Tanga kwenye kampeni za chama tawala.

Lakini kauli hii bado inazua maswali mengi, kwamba hiyo dunia itatikisika vipi kwa kuanguka kwa CCM?.
Kuna harufu fulani hapa.

Yaani CCM ya Nape na Mwigulu itikise dunia? au dunia ni MKapa mwenyewe.
 
Apeleke ujinga huko tunaenda kuitoa sasa tuone kama dunia itatikisika
 

Magufuli ukiingia ikulu funga viwanda vyote vya viroba fake vijana Wasiangamie. Uhuru Kenyatta alivisambaratisha kule kwake. Kiwanda cha Konyagi ambacho kina viwango kiafya kinatosha.
 
Wanaume mnaotaka Mabadiliko anzeni kwanza mabadiliko kwa kubeba Mimba- Mkapa
 
itasikitika kwa sababu wataumbuka ,, na hawataweza kuja kutuletea mikataba mfu na fake .. kiukweli wajiandae kulia tu huko duniani
 
Back
Top Bottom