Mkapa anashitakika - Dk. Slaa

Mkapa anashitakika - Dk. Slaa

duh hivi kuna watu wanaamini kwamba kelele za dr. slaa ndizo zilizowapeleka kina mramba kisutu??

Kwa nini usijiulize kama hayo majina yalikuwemo kwenye ile orodha ya mafisadi iliyoanikwa Mwembe Yanga na Dr. Slaa!! Ukishapata jibu ujiulize tena wenye mamlaka walisema nini kuhusu orodha hiyo tukianzia Serikalini hadi Chamani ( chama cha mafisadi wenyewe). Ukishapata jibu jiulize tena mafisadi wenyewe walisema nini baada ya majina yao kuanikwa hadharani.
 
"Our real problem is not our strength today, it is rather the vital necessity of action today to ensure our strength tomorrow."

This statement is too sweat, but it is difficult to be understood by common mwanachi. You can write a book about it. I wish it could be explained or be expounded more then just leaving it hanging like that. May you do that sr?
Thanks.
Amani Nyoni.

Thanks Amani. Ni kweli kuwa statement hii ni pana na inaweza kuandikiwa kitabu. Ila nadhani inaeleweka pamoja na ufupi wake. Labda niiifungulie thread yake pekee ili kuielezea zaidi.

Shukrani Mkuu
 
In this post, I am going to be a little incoherent, naombeni mnisamehe!

Mkuu Plotinus, huna haja ya kutanguliza samahani. Mawazo yako ni ya haki kabisa. Ninavyoijua JF, hapa ndipo mahali pake kabisa.

Unajua kuna watu wanaboa sana, wanakaa kwenye computer zao halafu kazi ni kutoa ushauri na saa nyingine kubwatuka tu -

Kama ulivyoomba usamehewe, nawe usamehe wote wenye mawazo tofauti na wewe. Matumizi ya computer zao wenyewe nayo ni haki yao binafsi. Sioni kwa jinsi gani suala hilo linavyokukera. Unachoweza kufanya ni kuwaelewesha unachokiamini, wakikubaliana na wewe mtakuwa pamoja. Hoja kujengwa kwa hoja. Mkuu, ukumbi huu ni wa kuelimishana, na wengi hapa hawajali mtu anaeamua kuboreka kwa kauli zao.

Yaani Dr. Slaa ajitoe mhanga peke yake tu! Wewe unayesema unashauri afungue kesi, toka Dr. Slaa ameanza vita na mafisadi, umeshafanya nini? Umemuunga mkona kiasi gani? Umechanga shillingi ngapi za kusaidia hizo harakati; Uta-support vipi financing ya hizo kesi unazotaka afungue kwa nguvu zake? Kuna maswali milioni kidogo yanajitokeza. Huko kujitoa anakofanya mpaka sasa, hata hamuoni anachofanya...always asking someone else to go a step further! WEWE JE? WHY DONT YOU?

Mkuu mimi sio Dr. Slaa. Yeye ameamua kuishi maisha ya kisiasa, mimi sijaamua kufanya hivyo. Yeye ni Mbunge, mimi sio Mbunge. Yeye ameweza kupata ushahidi kuhusu mafisadi, mimi sijaweza kuupata. Yeye anajua anachokitaka katika ulingo wa siasa, mimi ninajua ninachokitaka katika ulingo ninaoutumikia. Kupambana na ufisadi ni jukumu la kila mtu. Jinsi ya kupambana nao inatofautiana na matokeo tunayoyataka. Yeye amekerwa sana na mambo aliyofanya Mkapa (kwa sababu zake), mimi sijakerwa kiasi hicho. Yeye anaumia koo akilia majukwaani, mimi sipandi jukwaani na koo haliniumi. Ndio maana namshauri, badala ya kuendelea kuumiza koo lake bila matokeo yoyote, ni vyema akatumia nguvu hizo kufanya yanayoweza kumpa matokeo ya haraka na ambayo anayategemea. Mimi sitaki kumshitaki Mkapa, yeye anataka Mkapa ashitakiwe (sioni tija yake). Ni dhahiri kuwa matarajio yake katika maisha sio sawa na yangu.

This is why siku zote Tanzania haikomboleki, because at all times its about someone else doing something for the country, never mimi nafanya, hapana, NEVER! Kazi kulalamika na kubwatuka behind anonymity ya fake names in the forum! Mkimaliza mnaenda kufanya kazi za kujinufaisha nyinyi na familia zenu, peaceful! Kuna watu, Mikutano hawaendi (wanasubiri news because wananchi wa kawaida ndio wakukaa kusubiri hotuba za wanasiasa-wenyewe hapana, kura hawapigi (kwasababu CCM itashinda anyway, so why bother), activism hawafanyi (wako busy na professions nk. but pia hawana guts wala patriotism ya ku-sacrifice), contribution ya ku-support movements hatoi -(kisa, watanzania wote wezi tu, hela zitaliwa, buy and large ni ubinafsi tu) in all these things, anasubiri mwingine afanye!

Mkuu Plotinus, Tanzania haitakomboleka kwa kum-support au kutom-support mtu mmoja, au kundi fulani la watu tu. Tanzania itakomboleka kwa kutenda yanayotendeka kwa minajili ya kuiokomboa nchi yetu. Kila mtu anaowajibu wake katika ukombozi wa nchi yetu. Masuala ya ukombozi si ya kisiasa tu. Ukombozi ni wa-kiuchumi, kiulinzi na usalama, kijamii n.k.

Ndugu yangu, kubwatuka ni kazi ya mdomo. Kama inakukera pole sana. Maana hata wewe umebwatuka sana katika quote hiyo hapo juu. Ila hilo halikeri, kwakuwa kuna kubwatuka kunakokera zaidi (TUMIA HOJA, HAKUNA ANAELALAMIKA). Kuinufaisha familia yangu ni wajibu wangu binafsi. Maana nimeapa kufanya hivyo. Kimsingi nadhani unataka watu wote wamuunge mkono Dr. Slaa na CHADEMA yake. Hilo linajadilika. Ila halijadiliki kwa kulazimisha. Hakuna mtoto mdogo. Kila mtu ana matarajio yake na mapenzi yake katika itikadi anazoziamini. Ushindi wa kisiasa haufanywi hivyo. Ndio maana MAfisadi hao hao wanawashinda kila siku.

Mtikila amefungua ma-kesi mengi tu dhidi ya serikali, mlikuwa wapi, mbona hamkisaidia?!

Mtikila angeomba msaada angeweza kusaidiwa na wale wanaoona kesi za ni za msingi. Usipoomba hutapewa.

Hebu tuwe fair na tuwe tunafanya tathmini kama watu wenye hekima! Huo uwezo tu wakusoma katiba na kuzunguka nchi nzima-ku-counter statement za viongozi wa serikali mnadhani ni kitu kidogo...mnataka afanye zaidi!

Kuzunguka nchi nzima ni mapenzi yake na ni kazi yake. Mtu yeyote anaetaka kueneza itikadi yake kwa watu ni lazima afanye hivyo. Sasa unataka nilazimike kuunga jitihada za kila mtu kuzunguka nchi nzima kwasababu tu amefanya hivyo? C'mon do not be naive. Kama amechagua kuwa mwanasiasa ni lazima afanye siasa. sio lazima wote tuache kila kitu tuandamane nae. Yeye anajua faida ya kuwa mwanasiasa.

Saa nyingine ndio maana watu wakiingia madarakani wanawasahau wananchi, they just give so much, sacrifice so much, ili wewe u-relax akufanyie kila kitu!
Change inahitaji kufanyiwa kazi, inahitaji commitment inahitaji watu-tena wengi but it starts with an individual ku-participate!

Nadhani hueleweki ama hujui unachokisema. Mtu akiingia madarakani kwa kuchaguliwa, anakuwa amefanya jitihada kubwa kuchagulika. Hutumia njia mbalimbali kushawishi watu wamchague. Asipotekeleza mahitaji ya waliomchagua, basi ni dhahiri kuwa watamchagua mwingine mwenye kufaa zaidi. Hakuna favour kwenye siasa. Hakuna kiongozi ambae yuko madarakani eti kwasababu asipokuwepo pale wananchi watateseka. Aache basi aone kama wengine hawatafanya.

Ningeonelea bora ukosoe content ya alichokisema Dr. Slaa, technically or otherwise, but sio kusema afungue, kesi anangoja nini? ooh, chini ya CCM hayafiki popote! Impact ya kelele zake imefanya hata watu wazito wapande makarandinga, which was unthinkable-unprecedented kwa Tanzania, and its a start...pressure, participation, increasing political consiousness and participation in various ways and by all of us, ndio itafanya hata hizo kesi ziendelee na nyingine zifunguliwa na walioko maofisini waanze kuwa makini nk nk nk!

Katika thread hii, hakuna aliekosoa content ya Dr. Slaa kutaka Mkapa ashitakiwe. Ila umetolewa ushauri wa Dr. Slaa kufanya hivyo haraka kama anaweza. Kama hawezi kushitaki, anategemea wengine wafungue mashitaka hata kama hawataki kufanya hivyo? Wewe wa wapi?

Watanzania - Do something-toka kwenye comfort zone yako---acha ku-expect wengine tu ndio wafanye!

Kila mtu atimize wajibu wake. Nchi inahitaji kwenda mbele. Tuache porojo.
 
In this post, I am going to be a little incoherent, naombeni mnisamehe!

Unajua kuna watu wanaboa sana, wanakaa kwenye computer zao halafu kazi ni kutoa ushauri na saa nyingine kubwatuka tu -

Yaani Dr. Slaa ajitoe mhanga peke yake tu! Wewe unayesema unashauri afungue kesi, toka Dr. Slaa ameanza vita na mafisadi, umeshafanya nini? Umemuunga mkona kiasi gani? Umechanga shillingi ngapi za kusaidia hizo harakati; Uta-support vipi financing ya hizo kesi unazotaka afungue kwa nguvu zake? Kuna maswali milioni kidogo yanajitokeza. Huko kujitoa anakofanya mpaka sasa, hata hamuoni anachofanya...always asking someone else to go a step further! WEWE JE? WHY DONT YOU?

This is why siku zote Tanzania haikomboleki, because at all times its about someone else doing something for the country, never mimi nafanya, hapana, NEVER! Kazi kulalamika na kubwatuka behind anonymity ya fake names in the forum! Mkimaliza mnaenda kufanya kazi za kujinufaisha nyinyi na familia zenu, peaceful! Kuna watu, Mikutano hawaendi (wanasubiri news because wananchi wa kawaida ndio wakukaa kusubiri hotuba za wanasiasa-wenyewe hapana, kura hawapigi (kwasababu CCM itashinda anyway, so why bother), activism hawafanyi (wako busy na professions nk. but pia hawana guts wala patriotism ya ku-sacrifice), contribution ya ku-support movements hatoi -(kisa, watanzania wote wezi tu, hela zitaliwa, buy and large ni ubinafsi tu) in all these things, anasubiri mwingine afanye!

Mtikila amefungua ma-kesi mengi tu dhidi ya serikali, mlikuwa wapi, mbona hamkisaidia?!

Hebu tuwe fair na tuwe tunafanya tathmini kama watu wenye hekima! Huo uwezo tu wakusoma katiba na kuzunguka nchi nzima-ku-counter statement za viongozi wa serikali mnadhani ni kitu kidogo...mnataka afanye zaidi!

Saa nyingine ndio maana watu wakiingia madarakani wanawasahau wananchi, they just give so much, sacrifice so much, ili wewe u-relax akufanyie kila kitu!
Change inahitaji kufanyiwa kazi, inahitaji commitment inahitaji watu-tena wengi but it starts with an individual ku-participate!

Ningeonelea bora ukosoe content ya alichokisema Dr. Slaa, technically or otherwise, but sio kusema afungue, kesi anangoja nini? ooh, chini ya CCM hayafiki popote! Impact ya kelele zake imefanya hata watu wazito wapande makarandinga, which was unthinkable-unprecedented kwa Tanzania, and its a start...pressure, participation, increasing political consiousness and participation in various ways and by all of us, ndio itafanya hata hizo kesi ziendelee na nyingine zifunguliwa na walioko maofisini waanze kuwa makini nk nk nk!

Watanzania - Do something-toka kwenye comfort zone yako---acha ku-expect wengine tu ndio wafanye!

NAUNGA MKONO HOJA HII; ingawa kidogo ulikuwa mkali nimeelewa ni hasira watu wanakera; tena mie nauita WATZ kama hawa ni wagonjwa wakubwa wa taifa; kusubiri Dr Slaa akufanyie wewe ukiwa hoi; do something; join him if u feel he is right or do yours the other way; hakuna chochote mineno mitupu; Dr Slaa ni shujaa wa miaka karibu mitatu sasa; hayupo kama yeye TZ hii mwenye ujasiri; hana simile; viongozi wanaanza kumuogopa sasa ( umeona hata Masha recently). Unataka afanye nini kweli; jamani naungana mkonona mtoa hoja hii hapo juu
 
Hili ni tatizo la jamii ya akina Slaa kuogopa kuitwika lawama Serikali ya CCM inayoongozwa na Kikwete ,Dr Willbroad Sla ni mwoga anaogopa kuitonesha serikali iliyopo madarakani ,Slaa hakupaswa kumuandama Mkapa ,kwani Mkapa hivi sasa yupo Uraiani ,aliyeko madarakani ni Kikwete ,Kikwete ameshawahi kusema Mkapa aachwe kama alivyo ,sasa kurudia rudia kuhusu kinga au hana kinga ,wananchi wanalielewa na wameshaeleweshwa kitambo ,ninachomshauri Dr Slaa ni kuikalia kooni Serikali ni kuiponda serikali ni kuidharau serikali CCM chini ya Kikwete kuwa inashindwa imeshindwa haijiamini.Hivyo haifai kuwepo madarakani.

Kama nilivyosema katika topiki fulani kuwa jamii ya akina Slaa inabana mtu mmoja mmoja na inakuwa rahisi kwa serikali kufanya au kutimiza yale yanayodaiwa na Slaa na mifano ipo ,na kumfanya mwananchi wa kawaida aone serikali imefanya ,lakini kwa ukweli ni kuisema serikali na hawa akina Mkapa kuwa kama dondoo ili kutilia nguvu hoja ya kuiponda serikali.Ili kushinda ni lazima wananchi waikane serikali kuwa sio makini na haifai na sio kumuona Mkapa ni fisadi hafai kuachiwa kuzurura.Haya ni mambo mawili tofauti na inafaa yaeleweke upinzani ni kuipinga serikali na sio kumuingia mtu mmoja mmoja na kumuandama ,haya kesho Kikwete akiamua Mkapa afikishwe mahakamani kutakuwepo na jingine la kusema ,maana serikali kuyatimiza haya ni kuwakwamisha akina Slaa ,lakini ukishaiponda serikali mbele ya macho ya wananchi ni vigumu wananchi kuikubali serikali hata ikiwakamata mafisadi wote ,ni vigumu sana kwani mwananchi atakuwa ameshajenga msimamo kuwa serikali na Chama chake haifai hivyo waondoke.

Sasa Mwiba, ndiyo maana kuna haja ya kuwaunga mkono kina Slaa katika mapambano haya. Sisi Raia pia tunalo jukumu la kufanya katika kuonyesha kuwa serikali haitutimizii matakwa yetu. Nani ambaye ana wajibu wa kuibana serikali kama siyo mpiga kura? Maisha bora hakuahidiwa Slaa na wapiganaji wenzake, bali kwa kila Mtanzania kwa sababu rasilimali ambazo zimepangwa kutumika katika kuhakikisha maisha bora yanapatikana ni zo umma wa watanzania wote. Tujenge ujasiri wa kuwasimamisha viongozi wanapozurura mikoani na Mashangingi na kuwahoji hayo maisha bora yako wapi? wakitupa majibu ya rejareja, tujenge tabia ya kutumia kura zetu kuwawajibisha.
 
Hapa naona wachangiaji kuna jambo wanashindwa kulielewa kwa kina , ngoja nitoe ufafanuzi kidogo kwa jinsi ninavyoelewa ishu za Mkapa.

Itakumbukwa kuwa Mkapa alilazimisha kubinafsishwa kwa iliyokuwa benki ya taifa ya Biashara NBC LTD, Na mara baada ya Benki hiyo kuvunjwa na kuzaa NMB basi kipande kilichobakia kikauzwa kwa ABSA ya Afrika ya Kusini.

Baada ya dili hilo Mkapa aloilipwa na ABSA shilingi milioni mia tano (500,000,000) jiulize zilikuwa za kazi gani? Rais wa Nchi alipewa zawadi ama ilikuwa ni deni alikuwa anawadai hao jamaa?

Pili, kuhusu kuuzwa kwa Kiwira kwa asilimia 85, ambalo ni shirika aliloliunda mwalimu Nyerere kwa ajili ya watanzania ila yeye Mkapa , Mkewe Anna , mwanaye Nicolaus, Mkwewe Mbuna na aliyekuwa waziri wa Nishati na madini Daniel Yona walijiuzia Kiwira kwa bei ya kutupwa na hata hivyo hawajalipa mpaka leo deni lao .

Kibaya zaidi ni kuwa waliingia mkataba na TANESCO ambao ni mkataba usiokuwa na kikomo yaani hauna mwisho kuwa utaisha lini na kila siku itokayo kwa Mungu wanalipwa kiasi cha shilingi milioni mia tatu (300,000,000) kama Capacity charge hii ni kuwa wawe wamezalisha ama hawajazalisha umeme wanatakiwa kulipwa na TANESCO.

Na mkataba huo unaonyesha kuwa watakapoanza kuzalisha umeme wao utatakiwa kulipiwa service charge yaani gharama za huduma hiyo huu ni wizi .

Sasa nawashangaa wanaosema eti asishitakiwe wakati yeye mkataba wake ni mbaya kuliko ule wa RICHMOND ambao tulikuwa tunapoteza kiasi cha shilingi milioni 152 kwa siku huu ni mara mbili yake.

Anapaswa kushitakiwa kama wakina Mramba na wenzake ,ili kuwa fundisho kwa wengine laa sivyo nchi inateketea, watanzania tunakosa umeme kwa sababu TANESCO hawawezi kusambaza nyaya kutokana na kukosa fedha ambazo wanawalipa jamaa hawa kila kukicha.
 
Baada ya dili hilo Mkapa aloilipwa na ABSA shilingi milioni mia tano (500,000,000) jiulize zilikuwa za kazi gani? Rais wa Nchi alipewa zawadi ama ilikuwa ni deni alikuwa anawadai hao jamaa?

Kaka hapa ndo napapata kwa mara ya kwanza..... Mungu wangu nimjuae mimi
 
The kitu kibaya ni kuwa TANPOWER RESOURCES LTD inamilikiwa na watu wafuatao,

1.Daniel Yona - alikuwa waziri wa Nishati na madini 2004 wakati wanaichukua kiwira.
2. Advocate Mbuna - huyu ni mkwe wa Mkapa kwani mwanaye Mkapa kamuoa binti wa Mbuna.
3. Anna Mkapa - alikuwa nasema alikuwa kwani sina ushahidi kama bado ni mke wa Rais mstaafu Mkapa, alipitia ANBEM.
4. Nicholaus Mkapa - huyu ni mwanaye Mkapa sijui anajishughulisha na shughuli gani kwa sasa na hata wakati huo alikuwa nani.
5. Mapundi - huyu hajaulikani ni nani na anafanya nini ama alikuwa akifanya nini.
6.Benjamini Mkapa - alikuwa Rais 2004 wakati mkataba unaingiwa na alipitia kampuni la ANBEM.

Familia imeamua kuchukua rasilimali za Taifa bila huruma na kuna watu wanasema eti asishitakiwe kwa lipi?

Ajitokeze na aombe radhi na arudishe mali zetu hapo anaweza kusamehewa ila sio kumuacha aendelee kulinyonga Taifa hili.
 
Dr.tumekuelewa lakini si wote tuna mheshimu rais aliyeko madarakani.mbona DR. anampinga rais ambaye alisha sema mwacheni mzee wa watu apumzike.
 
Hapa naona wachangiaji kuna jambo wanashindwa kulielewa kwa kina , ngoja nitoe ufafanuzi kidogo kwa jinsi ninavyoelewa ishu za Mkapa.

Itakumbukwa kuwa Mkapa alilazimisha kubinafsishwa kwa iliyokuwa benki ya taifa ya Biashara NBC LTD, Na mara baada ya Benki hiyo kuvunjwa na kuzaa NMB basi kipande kilichobakia kikauzwa kwa ABSA ya Afrika ya Kusini.

Baada ya dili hilo Mkapa aloilipwa na ABSA shilingi milioni mia tano (500,000,000) jiulize zilikuwa za kazi gani? Rais wa Nchi alipewa zawadi ama ilikuwa ni deni alikuwa anawadai hao jamaa?

Pili, kuhusu kuuzwa kwa Kiwira kwa asilimia 85, ambalo ni shirika aliloliunda mwalimu Nyerere kwa ajili ya watanzania ila yeye Mkapa , Mkewe Anna , mwanaye Nicolaus, Mkwewe Mbuna na aliyekuwa waziri wa Nishati na madini Daniel Yona walijiuzia Kiwira kwa bei ya kutupwa na hata hivyo hawajalipa mpaka leo deni lao .

Kibaya zaidi ni kuwa waliingia mkataba na TANESCO ambao ni mkataba usiokuwa na kikomo yaani hauna mwisho kuwa utaisha lini na kila siku itokayo kwa Mungu wanalipwa kiasi cha shilingi milioni mia tatu (300,000,000) kama Capacity charge hii ni kuwa wawe wamezalisha ama hawajazalisha umeme wanatakiwa kulipwa na TANESCO.

Na mkataba huo unaonyesha kuwa watakapoanza kuzalisha umeme wao utatakiwa kulipiwa service charge yaani gharama za huduma hiyo huu ni wizi .

Sasa nawashangaa wanaosema eti asishitakiwe wakati yeye mkataba wake ni mbaya kuliko ule wa RICHMOND ambao tulikuwa tunapoteza kiasi cha shilingi milioni 152 kwa siku huu ni mara mbili yake.

Anapaswa kushitakiwa kama wakina Mramba na wenzake ,ili kuwa fundisho kwa wengine laa sivyo nchi inateketea, watanzania tunakosa umeme kwa sababu TANESCO hawawezi kusambaza nyaya kutokana na kukosa fedha ambazo wanawalipa jamaa hawa kila kukicha.
Alafu leo anasisima jukwaani tunamuangalia tu! Alitakiwa aendelee kukaa kimya kama alivyosusa kuwaomba radhi Watanzania!
 
ashitakiwe huu ndio utawala wa sheria.kwani imeelekeza watu wa kushitakiwa walio tenda makosa?wengine mnasema aombe radhi mbana watu wengine au akina mramba hawakuambiwa waombe radhi?
 
The kitu kibaya ni kuwa TANPOWER RESOURCES LTD inamilikiwa na watu wafuatao,

1.Daniel Yona - alikuwa waziri wa Nishati na madini 2004 wakati wanaichukua kiwira.
2. Advocate Mbuna - huyu ni mkwe wa Mkapa kwani mwanaye Mkapa kamuoa binti wa Mbuna.
3. Anna Mkapa - alikuwa nasema alikuwa kwani sina ushahidi kama bado ni mke wa Rais mstaafu Mkapa, alipitia ANBEM.
4. Nicholaus Mkapa - huyu ni mwanaye Mkapa sijui anajishughulisha na shughuli gani kwa sasa na hata wakati huo alikuwa nani.
5. Mapundi - huyu hajaulikani ni nani na anafanya nini ama alikuwa akifanya nini.
6.Benjamini Mkapa - alikuwa Rais 2004 wakati mkataba unaingiwa na alipitia kampuni la ANBEM.

Familia imeamua kuchukua rasilimali za Taifa bila huruma na kuna watu wanasema eti asishitakiwe kwa lipi?

Ajitokeze na aombe radhi na arudishe mali zetu hapo anaweza kusamehewa ila sio kumuacha aendelee kulinyonga Taifa hili.
Kwa madudu haya alafu huyu mtu anakuja kusimama jukwaani kufanya siasa alafu tunamkenulia meno! Ajibu tuhuma zake!
 
Kazi kwenu wana Arumeru,msikubali kutumika na watu kama hawa!
 
Dr slaa is just a leader...people need to take action when they are ready!
 
Mkapa anashitakika - Dk. Slaa

na Edward Kinabo
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeendelea kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete kumchukulia hatua za kisheria Rais wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, kwa kutumia vibaya madaraka yake wakati wa kipindi chake cha uongozi.

Chama hicho kimewataka Watanzania kutokubali kuendelea kupotoshwa na baadhi ya watu wanaokuwa wanadai kuwa Mkapa hawezi kushitakiwa hadi Bunge limwondolee kinga.

CHADEMA imesisitiza kuwa Rais Mkapa, sawa na rais yeyote mstaafu, hana kinga kikatiba inayozuia asishitakiwe dhidi ya makosa aliyoyafanya akiwa madarakani kama mtu binafsi.


Hayo yalisemwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa, katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Sokoni, Kawe, Dar es Salaam, juzi, ikiwa ni mfululizo wa mikutano ya kuimarisha chama hicho iliyopewa jina la Operesheni Sangara.

Alisema katiba ya sasa pamoja na kuwa na upungufu, haijatamka kuwa rais mstaafu hawezi kushitakiwa kwa makosa aliyofanya akiwa madarakani kama aliyoyafanya Rais Mkapa wakati wa kipindi chake cha uongozi.

“Watanzania mpende kusoma. Mmekuwa mkipotoshwa kwamba Mkapa hawezi kushitakiwa kwa sababu ana kinga ya kikatiba. Tunasema kwa katiba yetu hii hii pamoja na upungufu wake, bado anaweza kushitakiwa kwa makosa aliyofanya akiwa madarakani…

“Ibara ya 46 ya katiba yetu inafafanua wazi kuwa iwapo kutakuwa na haja ya rais mstaafu kufunguliwa mashitaka kwa makosa aliyofanya, ataandikiwa notisi ya siku 60 kuhusu kusudio la kumfungulia mashitaka kabla ya shauri hilo kupelekwa mahakamani.

“Watu wanapotosha kuwa hawezi kushitakiwa hadi aondolewe kinga bungeni. Kinga gani? Katiba yetu haizungumzii chochote kuhusu kinga dhidi ya mtu aliyetenda mambo binafsi wakati akiwa madarakani,” alisema Dk. Slaa.


Akifafanua zaidi suala hilo, alisema matendo ambayo rais mstaafu hawezi kufunguliwa kesi hadi aondolewe kinga ni yale tu aliyoyafanya kama rais, katika madaraka yake kisheria kama kuwaachia huru wafungwa, kuidhinisha sheria na masuala mengine yaliyoainishwa kwenye katiba ya nchi.

Masuala kama ya Rais Mkapa kufanya biashara akiwa Ikulu hayahitaji kuondolewa kinga ili ashitakiwe, kwani aliyafanya nje ya mamlaka ya rais aliyopewa.

Rais Mkapa anapaswa kushitakiwa kama watu wengine kwa kutumia Ikulu kujimilikisha hisa katika mgodi wa makaa ya mawe, kupitia kampuni aliyoiunda ya Tan Power Resources Limited na kuiingiza nchi katika hasara.

Dk. Slaa alitoa msimamo huo kupinga kauli za baadhi ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) hususan kauli ya Mbunge wa Singida, Lazaro Nyalandu, ambaye hivi karibuni kupitia kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na kituo cha TBC1, alisema Mkapa aachwe ampumzike, kwani amelitendea taifa mambo mengi mazuri badala ya kuendelea kuandamwa na wanasiasa.

Akielezea kushangazwa kwake na kauli hiyo, alisema hakutarajia mtu kama mbunge huyo kutoa kauli kama hiyo.

“Sikutarajia kumsikia mbunge akitoa kauli kama hiyo. Hivi mtu akifanya mambo mema mia moja lakini akafanya kosa moja, polisi haimkamati”? alihoji Dk. Slaa.

Alisema kwa sababu ya Mkapa, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lililazimika kuilipa Tan Power Resources Limited sh milioni 300 kwa siku, kiasi alichosema ni kikubwa kuliko kile kilichokuwa kikilipwa kwa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond ya Marekani.


Mkataba wa TANESCO na Richmond kabla ya kuvunjwa ulikuwa ukililazimisha shirika hilo kuilipa Richmond na mrithi wake, Dowans, sh milioni 152 kila siku hata kama hazikuzalisha umeme.

Aliwaambia wananchi hao kuwa familia ya Mkapa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini katika serikali ya awamu ya tatu, Daniel Yona, walijimilikisha hisa za asilimia 85 za mgodi wa Kiwira.

Kutokana na Mkapa kuhusika kwa kiasi kikubwa na ufisadi, hatua zinazochukuliwa na serikali za kuwashitaki watuhumiwa wa ufisadi bado haziridhishi, hadi hapo Mkapa na watuhumiwa wengine walioachwa watakapokamatwa na kushitakiwa.

Kama serikali ingesimamia vizuri rasilimali za taifa, Tanzania isingehitaji hata senti moja kutoka nchi wahisani. Ameishutumu serikali ya Rais Kikwete kwa kushindwa kukusanya kodi.


Alisema kama serikali ingekusanya vizuri mapato yatokanayo na sekta ya mifugo na uvuvi, ingeweza kupata mapato ambayo ni karibu mara tatu ya mapato yatokanayo na dhahabu.

Dk. Slaa aliwataka wananchi hao kuiunga mkono CHADEMA na kukiimarisha chama hicho katika maeneo yao, ili kuipatia viongozi wa serikali za mitaa katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba mwaka huu.

Kwa muda mrefu sasa baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa Rais Mkapa hawezi kushitakiwa kwa makosa anayodaiwa kufanya akiwa madarakani, kwa sababu ana kinga ya kikatiba ya kutoshitakiwa kwa makosa aliyotenda akiwa rais.

Watu hao ambao baadhi yao ni wasomi, wamekuwa wakipendekeza kuwa ikiwa kuna haja ya rais huyo mstaafu kushitakiwa, basi kinachopaswa kufanywa ni Bunge kuondoa kinga hiyo.

tuache majungu,Mkapa anastahili heshima yake kwa mchango wake...kuna MWINYI na NYERERE,je hawakufanya makosa?
 
Back
Top Bottom