Watu wana maajabu.
duh hivi kuna watu wanaamini kwamba kelele za dr. slaa ndizo zilizowapeleka kina mramba kisutu??
"Our real problem is not our strength today, it is rather the vital necessity of action today to ensure our strength tomorrow."
This statement is too sweat, but it is difficult to be understood by common mwanachi. You can write a book about it. I wish it could be explained or be expounded more then just leaving it hanging like that. May you do that sr?
Thanks.
Amani Nyoni.
In this post, I am going to be a little incoherent, naombeni mnisamehe!
Unajua kuna watu wanaboa sana, wanakaa kwenye computer zao halafu kazi ni kutoa ushauri na saa nyingine kubwatuka tu -
Yaani Dr. Slaa ajitoe mhanga peke yake tu! Wewe unayesema unashauri afungue kesi, toka Dr. Slaa ameanza vita na mafisadi, umeshafanya nini? Umemuunga mkona kiasi gani? Umechanga shillingi ngapi za kusaidia hizo harakati; Uta-support vipi financing ya hizo kesi unazotaka afungue kwa nguvu zake? Kuna maswali milioni kidogo yanajitokeza. Huko kujitoa anakofanya mpaka sasa, hata hamuoni anachofanya...always asking someone else to go a step further! WEWE JE? WHY DONT YOU?
This is why siku zote Tanzania haikomboleki, because at all times its about someone else doing something for the country, never mimi nafanya, hapana, NEVER! Kazi kulalamika na kubwatuka behind anonymity ya fake names in the forum! Mkimaliza mnaenda kufanya kazi za kujinufaisha nyinyi na familia zenu, peaceful! Kuna watu, Mikutano hawaendi (wanasubiri news because wananchi wa kawaida ndio wakukaa kusubiri hotuba za wanasiasa-wenyewe hapana, kura hawapigi (kwasababu CCM itashinda anyway, so why bother), activism hawafanyi (wako busy na professions nk. but pia hawana guts wala patriotism ya ku-sacrifice), contribution ya ku-support movements hatoi -(kisa, watanzania wote wezi tu, hela zitaliwa, buy and large ni ubinafsi tu) in all these things, anasubiri mwingine afanye!
Mtikila amefungua ma-kesi mengi tu dhidi ya serikali, mlikuwa wapi, mbona hamkisaidia?!
Hebu tuwe fair na tuwe tunafanya tathmini kama watu wenye hekima! Huo uwezo tu wakusoma katiba na kuzunguka nchi nzima-ku-counter statement za viongozi wa serikali mnadhani ni kitu kidogo...mnataka afanye zaidi!
Saa nyingine ndio maana watu wakiingia madarakani wanawasahau wananchi, they just give so much, sacrifice so much, ili wewe u-relax akufanyie kila kitu!
Change inahitaji kufanyiwa kazi, inahitaji commitment inahitaji watu-tena wengi but it starts with an individual ku-participate!
Ningeonelea bora ukosoe content ya alichokisema Dr. Slaa, technically or otherwise, but sio kusema afungue, kesi anangoja nini? ooh, chini ya CCM hayafiki popote! Impact ya kelele zake imefanya hata watu wazito wapande makarandinga, which was unthinkable-unprecedented kwa Tanzania, and its a start...pressure, participation, increasing political consiousness and participation in various ways and by all of us, ndio itafanya hata hizo kesi ziendelee na nyingine zifunguliwa na walioko maofisini waanze kuwa makini nk nk nk!
Watanzania - Do something-toka kwenye comfort zone yako---acha ku-expect wengine tu ndio wafanye!
In this post, I am going to be a little incoherent, naombeni mnisamehe!
Unajua kuna watu wanaboa sana, wanakaa kwenye computer zao halafu kazi ni kutoa ushauri na saa nyingine kubwatuka tu -
Yaani Dr. Slaa ajitoe mhanga peke yake tu! Wewe unayesema unashauri afungue kesi, toka Dr. Slaa ameanza vita na mafisadi, umeshafanya nini? Umemuunga mkona kiasi gani? Umechanga shillingi ngapi za kusaidia hizo harakati; Uta-support vipi financing ya hizo kesi unazotaka afungue kwa nguvu zake? Kuna maswali milioni kidogo yanajitokeza. Huko kujitoa anakofanya mpaka sasa, hata hamuoni anachofanya...always asking someone else to go a step further! WEWE JE? WHY DONT YOU?
This is why siku zote Tanzania haikomboleki, because at all times its about someone else doing something for the country, never mimi nafanya, hapana, NEVER! Kazi kulalamika na kubwatuka behind anonymity ya fake names in the forum! Mkimaliza mnaenda kufanya kazi za kujinufaisha nyinyi na familia zenu, peaceful! Kuna watu, Mikutano hawaendi (wanasubiri news because wananchi wa kawaida ndio wakukaa kusubiri hotuba za wanasiasa-wenyewe hapana, kura hawapigi (kwasababu CCM itashinda anyway, so why bother), activism hawafanyi (wako busy na professions nk. but pia hawana guts wala patriotism ya ku-sacrifice), contribution ya ku-support movements hatoi -(kisa, watanzania wote wezi tu, hela zitaliwa, buy and large ni ubinafsi tu) in all these things, anasubiri mwingine afanye!
Mtikila amefungua ma-kesi mengi tu dhidi ya serikali, mlikuwa wapi, mbona hamkisaidia?!
Hebu tuwe fair na tuwe tunafanya tathmini kama watu wenye hekima! Huo uwezo tu wakusoma katiba na kuzunguka nchi nzima-ku-counter statement za viongozi wa serikali mnadhani ni kitu kidogo...mnataka afanye zaidi!
Saa nyingine ndio maana watu wakiingia madarakani wanawasahau wananchi, they just give so much, sacrifice so much, ili wewe u-relax akufanyie kila kitu!
Change inahitaji kufanyiwa kazi, inahitaji commitment inahitaji watu-tena wengi but it starts with an individual ku-participate!
Ningeonelea bora ukosoe content ya alichokisema Dr. Slaa, technically or otherwise, but sio kusema afungue, kesi anangoja nini? ooh, chini ya CCM hayafiki popote! Impact ya kelele zake imefanya hata watu wazito wapande makarandinga, which was unthinkable-unprecedented kwa Tanzania, and its a start...pressure, participation, increasing political consiousness and participation in various ways and by all of us, ndio itafanya hata hizo kesi ziendelee na nyingine zifunguliwa na walioko maofisini waanze kuwa makini nk nk nk!
Watanzania - Do something-toka kwenye comfort zone yako---acha ku-expect wengine tu ndio wafanye!
Hili ni tatizo la jamii ya akina Slaa kuogopa kuitwika lawama Serikali ya CCM inayoongozwa na Kikwete ,Dr Willbroad Sla ni mwoga anaogopa kuitonesha serikali iliyopo madarakani ,Slaa hakupaswa kumuandama Mkapa ,kwani Mkapa hivi sasa yupo Uraiani ,aliyeko madarakani ni Kikwete ,Kikwete ameshawahi kusema Mkapa aachwe kama alivyo ,sasa kurudia rudia kuhusu kinga au hana kinga ,wananchi wanalielewa na wameshaeleweshwa kitambo ,ninachomshauri Dr Slaa ni kuikalia kooni Serikali ni kuiponda serikali ni kuidharau serikali CCM chini ya Kikwete kuwa inashindwa imeshindwa haijiamini.Hivyo haifai kuwepo madarakani.
Kama nilivyosema katika topiki fulani kuwa jamii ya akina Slaa inabana mtu mmoja mmoja na inakuwa rahisi kwa serikali kufanya au kutimiza yale yanayodaiwa na Slaa na mifano ipo ,na kumfanya mwananchi wa kawaida aone serikali imefanya ,lakini kwa ukweli ni kuisema serikali na hawa akina Mkapa kuwa kama dondoo ili kutilia nguvu hoja ya kuiponda serikali.Ili kushinda ni lazima wananchi waikane serikali kuwa sio makini na haifai na sio kumuona Mkapa ni fisadi hafai kuachiwa kuzurura.Haya ni mambo mawili tofauti na inafaa yaeleweke upinzani ni kuipinga serikali na sio kumuingia mtu mmoja mmoja na kumuandama ,haya kesho Kikwete akiamua Mkapa afikishwe mahakamani kutakuwepo na jingine la kusema ,maana serikali kuyatimiza haya ni kuwakwamisha akina Slaa ,lakini ukishaiponda serikali mbele ya macho ya wananchi ni vigumu wananchi kuikubali serikali hata ikiwakamata mafisadi wote ,ni vigumu sana kwani mwananchi atakuwa ameshajenga msimamo kuwa serikali na Chama chake haifai hivyo waondoke.
Baada ya dili hilo Mkapa aloilipwa na ABSA shilingi milioni mia tano (500,000,000) jiulize zilikuwa za kazi gani? Rais wa Nchi alipewa zawadi ama ilikuwa ni deni alikuwa anawadai hao jamaa?
Alafu leo anasisima jukwaani tunamuangalia tu! Alitakiwa aendelee kukaa kimya kama alivyosusa kuwaomba radhi Watanzania!Hapa naona wachangiaji kuna jambo wanashindwa kulielewa kwa kina , ngoja nitoe ufafanuzi kidogo kwa jinsi ninavyoelewa ishu za Mkapa.
Itakumbukwa kuwa Mkapa alilazimisha kubinafsishwa kwa iliyokuwa benki ya taifa ya Biashara NBC LTD, Na mara baada ya Benki hiyo kuvunjwa na kuzaa NMB basi kipande kilichobakia kikauzwa kwa ABSA ya Afrika ya Kusini.
Baada ya dili hilo Mkapa aloilipwa na ABSA shilingi milioni mia tano (500,000,000) jiulize zilikuwa za kazi gani? Rais wa Nchi alipewa zawadi ama ilikuwa ni deni alikuwa anawadai hao jamaa?
Pili, kuhusu kuuzwa kwa Kiwira kwa asilimia 85, ambalo ni shirika aliloliunda mwalimu Nyerere kwa ajili ya watanzania ila yeye Mkapa , Mkewe Anna , mwanaye Nicolaus, Mkwewe Mbuna na aliyekuwa waziri wa Nishati na madini Daniel Yona walijiuzia Kiwira kwa bei ya kutupwa na hata hivyo hawajalipa mpaka leo deni lao .
Kibaya zaidi ni kuwa waliingia mkataba na TANESCO ambao ni mkataba usiokuwa na kikomo yaani hauna mwisho kuwa utaisha lini na kila siku itokayo kwa Mungu wanalipwa kiasi cha shilingi milioni mia tatu (300,000,000) kama Capacity charge hii ni kuwa wawe wamezalisha ama hawajazalisha umeme wanatakiwa kulipwa na TANESCO.
Na mkataba huo unaonyesha kuwa watakapoanza kuzalisha umeme wao utatakiwa kulipiwa service charge yaani gharama za huduma hiyo huu ni wizi .
Sasa nawashangaa wanaosema eti asishitakiwe wakati yeye mkataba wake ni mbaya kuliko ule wa RICHMOND ambao tulikuwa tunapoteza kiasi cha shilingi milioni 152 kwa siku huu ni mara mbili yake.
Anapaswa kushitakiwa kama wakina Mramba na wenzake ,ili kuwa fundisho kwa wengine laa sivyo nchi inateketea, watanzania tunakosa umeme kwa sababu TANESCO hawawezi kusambaza nyaya kutokana na kukosa fedha ambazo wanawalipa jamaa hawa kila kukicha.
Kwa madudu haya alafu huyu mtu anakuja kusimama jukwaani kufanya siasa alafu tunamkenulia meno! Ajibu tuhuma zake!The kitu kibaya ni kuwa TANPOWER RESOURCES LTD inamilikiwa na watu wafuatao,
1.Daniel Yona - alikuwa waziri wa Nishati na madini 2004 wakati wanaichukua kiwira.
2. Advocate Mbuna - huyu ni mkwe wa Mkapa kwani mwanaye Mkapa kamuoa binti wa Mbuna.
3. Anna Mkapa - alikuwa nasema alikuwa kwani sina ushahidi kama bado ni mke wa Rais mstaafu Mkapa, alipitia ANBEM.
4. Nicholaus Mkapa - huyu ni mwanaye Mkapa sijui anajishughulisha na shughuli gani kwa sasa na hata wakati huo alikuwa nani.
5. Mapundi - huyu hajaulikani ni nani na anafanya nini ama alikuwa akifanya nini.
6.Benjamini Mkapa - alikuwa Rais 2004 wakati mkataba unaingiwa na alipitia kampuni la ANBEM.
Familia imeamua kuchukua rasilimali za Taifa bila huruma na kuna watu wanasema eti asishitakiwe kwa lipi?
Ajitokeze na aombe radhi na arudishe mali zetu hapo anaweza kusamehewa ila sio kumuacha aendelee kulinyonga Taifa hili.
to be honest mkapa hastahili kushtakiwa,unless chuki binafsidr. Slaa for presidency!
Mkapa anashitakika - Dk. Slaa
na Edward Kinabo
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeendelea kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete kumchukulia hatua za kisheria Rais wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, kwa kutumia vibaya madaraka yake wakati wa kipindi chake cha uongozi.
Chama hicho kimewataka Watanzania kutokubali kuendelea kupotoshwa na baadhi ya watu wanaokuwa wanadai kuwa Mkapa hawezi kushitakiwa hadi Bunge limwondolee kinga.
CHADEMA imesisitiza kuwa Rais Mkapa, sawa na rais yeyote mstaafu, hana kinga kikatiba inayozuia asishitakiwe dhidi ya makosa aliyoyafanya akiwa madarakani kama mtu binafsi.
Hayo yalisemwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa, katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Sokoni, Kawe, Dar es Salaam, juzi, ikiwa ni mfululizo wa mikutano ya kuimarisha chama hicho iliyopewa jina la Operesheni Sangara.
Alisema katiba ya sasa pamoja na kuwa na upungufu, haijatamka kuwa rais mstaafu hawezi kushitakiwa kwa makosa aliyofanya akiwa madarakani kama aliyoyafanya Rais Mkapa wakati wa kipindi chake cha uongozi.
Watanzania mpende kusoma. Mmekuwa mkipotoshwa kwamba Mkapa hawezi kushitakiwa kwa sababu ana kinga ya kikatiba. Tunasema kwa katiba yetu hii hii pamoja na upungufu wake, bado anaweza kushitakiwa kwa makosa aliyofanya akiwa madarakani
Ibara ya 46 ya katiba yetu inafafanua wazi kuwa iwapo kutakuwa na haja ya rais mstaafu kufunguliwa mashitaka kwa makosa aliyofanya, ataandikiwa notisi ya siku 60 kuhusu kusudio la kumfungulia mashitaka kabla ya shauri hilo kupelekwa mahakamani.
Watu wanapotosha kuwa hawezi kushitakiwa hadi aondolewe kinga bungeni. Kinga gani? Katiba yetu haizungumzii chochote kuhusu kinga dhidi ya mtu aliyetenda mambo binafsi wakati akiwa madarakani, alisema Dk. Slaa.
Akifafanua zaidi suala hilo, alisema matendo ambayo rais mstaafu hawezi kufunguliwa kesi hadi aondolewe kinga ni yale tu aliyoyafanya kama rais, katika madaraka yake kisheria kama kuwaachia huru wafungwa, kuidhinisha sheria na masuala mengine yaliyoainishwa kwenye katiba ya nchi.
Masuala kama ya Rais Mkapa kufanya biashara akiwa Ikulu hayahitaji kuondolewa kinga ili ashitakiwe, kwani aliyafanya nje ya mamlaka ya rais aliyopewa.
Rais Mkapa anapaswa kushitakiwa kama watu wengine kwa kutumia Ikulu kujimilikisha hisa katika mgodi wa makaa ya mawe, kupitia kampuni aliyoiunda ya Tan Power Resources Limited na kuiingiza nchi katika hasara.
Dk. Slaa alitoa msimamo huo kupinga kauli za baadhi ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) hususan kauli ya Mbunge wa Singida, Lazaro Nyalandu, ambaye hivi karibuni kupitia kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na kituo cha TBC1, alisema Mkapa aachwe ampumzike, kwani amelitendea taifa mambo mengi mazuri badala ya kuendelea kuandamwa na wanasiasa.
Akielezea kushangazwa kwake na kauli hiyo, alisema hakutarajia mtu kama mbunge huyo kutoa kauli kama hiyo.
Sikutarajia kumsikia mbunge akitoa kauli kama hiyo. Hivi mtu akifanya mambo mema mia moja lakini akafanya kosa moja, polisi haimkamati? alihoji Dk. Slaa.
Alisema kwa sababu ya Mkapa, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lililazimika kuilipa Tan Power Resources Limited sh milioni 300 kwa siku, kiasi alichosema ni kikubwa kuliko kile kilichokuwa kikilipwa kwa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond ya Marekani.
Mkataba wa TANESCO na Richmond kabla ya kuvunjwa ulikuwa ukililazimisha shirika hilo kuilipa Richmond na mrithi wake, Dowans, sh milioni 152 kila siku hata kama hazikuzalisha umeme.
Aliwaambia wananchi hao kuwa familia ya Mkapa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini katika serikali ya awamu ya tatu, Daniel Yona, walijimilikisha hisa za asilimia 85 za mgodi wa Kiwira.
Kutokana na Mkapa kuhusika kwa kiasi kikubwa na ufisadi, hatua zinazochukuliwa na serikali za kuwashitaki watuhumiwa wa ufisadi bado haziridhishi, hadi hapo Mkapa na watuhumiwa wengine walioachwa watakapokamatwa na kushitakiwa.
Kama serikali ingesimamia vizuri rasilimali za taifa, Tanzania isingehitaji hata senti moja kutoka nchi wahisani. Ameishutumu serikali ya Rais Kikwete kwa kushindwa kukusanya kodi.
Alisema kama serikali ingekusanya vizuri mapato yatokanayo na sekta ya mifugo na uvuvi, ingeweza kupata mapato ambayo ni karibu mara tatu ya mapato yatokanayo na dhahabu.
Dk. Slaa aliwataka wananchi hao kuiunga mkono CHADEMA na kukiimarisha chama hicho katika maeneo yao, ili kuipatia viongozi wa serikali za mitaa katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba mwaka huu.
Kwa muda mrefu sasa baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa Rais Mkapa hawezi kushitakiwa kwa makosa anayodaiwa kufanya akiwa madarakani, kwa sababu ana kinga ya kikatiba ya kutoshitakiwa kwa makosa aliyotenda akiwa rais.
Watu hao ambao baadhi yao ni wasomi, wamekuwa wakipendekeza kuwa ikiwa kuna haja ya rais huyo mstaafu kushitakiwa, basi kinachopaswa kufanywa ni Bunge kuondoa kinga hiyo.