Mkakati wa Lowassa kuiangamiza CCM

Mkakati wa Lowassa kuiangamiza CCM

Abdull Kazi

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2012
Posts
344
Reaction score
306
Muda mfupi baada ya vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi Ukawa kumkaribisha rasmi, waziri mkuu aliyejiuzulu,Edward Lowasa, mkakati kabambe wa kuimaliza CCM umebainika

Watu walio karibu na Lowasa wanaeleza kuwa njia ya kwanza ni kwa wagombea 80 wa CCM wanaomuunga mkono kuhakikisha wanapitishwa katika majimbo kuwa wagombea wa Chama hicho.

Watu hao wakishajihakikishia kuwa wateule wa CCM hatua inayofuata ni kuchukua fomu za Tume ya uchaguzi na kuzijaza kupitia CCM kisha fomu hizo watakaa nazo mpaka saa moja kabla ya muda wa Mwisho wa kurudisha kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi

Wakati muda ukiwa unayoyoma wagombea hao kwa pamoja watatangaza kujitoa katika kinyang'anyiro hicho kupitia CCM na kutangaza kujiunga na vyama vinavyounda UKAWA wakati huo watakuwa tayari wameshachukuliwa fomu za kuwania majimbo hayo hayo kwa tiketi ya vyama walivyojiunga navyo

Hatua hiyo itahitimishwa kwa wagombea wa vyama vilivyo katika UKAWA kwa sasa kuwaachia nafasi wale waliotoka CCM hasa katika maeneo ambayo upinzani hauna nguvu

Katika hatua ya Kwanza CCM itakuwa haina wagombea katika majimbo 80 na hili litakuwa ni pigo lao la kwanza kwani wagombea wanaounda ukawa watapita bila kizuizi kikubwa

Nitaendelea kuwaletea mkakati huo kadiri utakavyokuwa unapatikana.
 
Mnazidi kumpakazia…mbona mlidai mmezuia mafuriko kwa kiganja cha mkono?? mbona mlidai hana wafuasi?? ndio maan mmeanza kumpakazia kesi ya Richmond??? Mnaruka ruka wakati sindano hazijawagusa???…Subirini kesho muone moto wake
 
Oyoooooo oyyooooooooooooo.....

Lowassa is the KING of Politics wa bongo..anajua hii michezo jamaniiiiii......


Oyoooooooooo...daaaah hili wazooo kaliiiiii kama chenga za messsssiiiiiii


Oyooooooo....oyoooooo Ukawaaaa, Chademaaaaa....Lowassaaaaaa....👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏
 
Mnazidi kumpakazia…mbona mlidai mmezuia mafuriko kwa kiganja cha mkono?? mbona mlidai hana wafuasi?? ndio maan mmeanza kumpakazia kesi ya Richmond??? Mnaruka ruka wakati sindano hazijawagusa???…Subirini kesho muone moto wake

duuhh sasa hivi anapakaziwa?
 
Na bado mtaishi kwa assumption sana na mbaya zaidi kwa sababu hamtakuwa na mamna nyingine ya kuokoa jahazi
#zUiAgOlIlaMkOnO campaign
jiandikishe, tunza card ya kupiga Kura aka "kichinjio"
 
Khaa!! Hizo pesa za kununua uongozi kazipata wapi?? Atazirudishaje? Watanzania si wajinga kiasi hiki. Taratibu rangi zinaanza kuonekana
 
Kuua chama dola si kazi rahisi hasa kwa chama kilichopitia mifumo ya kijamaa.Ni rahisi kusambaratisha chama kilichopitia mfumo wa kibepari.Cha kijamaa kama CCM ni shughuli pevu TENA PEVU HASA.Chama cha kijamaa kina wenyewe na mara nyingi hao wenyewe hata huwa hawawi kwenye medani za siasa za msitari wa mbele.Huwa wako kimya tu kwenye maabara za kisiasa.Si rahisi kama unavyodhani lakini shukrani kwa taarifa.
 
Watu hao wakishajihakikishia kuwa wateule wa CCM hatua inayofuata ni kuchukua fomu za Tume ya uchaguzi na kuzijaza kupitia CCM kisha fomu hizo watakaa nazo mpaka saa moja kabla ya muda wa Mwisho wa kurudisha kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi

Wakati muda ukiwa unayoyoma wagombea hao kwa pamoja watatangaza kujitoa katika kinyang'anyiro hicho kupitia CCM na kutangaza kujiunga na vyama vinavyounda UKAWA wakati huo watakuwa tayari wameshachukuliwa fomu za kuwania majimbo hayo hayo kwa tiketi ya vyama walivyojiunga navyo
[/QUOTE]

Hii ni cooked story halaf kumbuka Tume ni ccm ikibaki sa moja kurudisha fom wanaweza wakaongeza ata wiki ili wachaguliwe wengne kuwakilisha ccm Stor yako haina mashiko
 
Abdull Kazi

Unaposema watachukua fomu za ubunge za tume halafu wakae nazo na wajitoe saa moja kabla muda wa kuzirudisha basi ujue kwa muda huo uliobaki haiwezekani mtu mwingine achukue form upya kwa kuwa muda hautaruhusu. Ila wakijitoa itakua faida kwa wale au yule aliebakia.
 
Last edited by a moderator:
Abdull Kazi


Hata upeo mdogo wa kufikiri huna!unaijua mikakati wewe!!! unaenda kuchukua form kwa tiketi ya ccm,then watu wengne wanakuchukulia form hapohapo kwa tiket ya chama kingne kwa majina gani labda!!
huwa sipendi kuita watu kama wewe wapumbavu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom