Mkakati wa Lowassa kuiangamiza CCM

Mkakati wa Lowassa kuiangamiza CCM

Watu hao wakishajihakikishia kuwa wateule wa CCM hatua inayofuata ni kuchukua fomu za Tume ya uchaguzi na kuzijaza kupitia CCM kisha fomu hizo watakaa nazo mpaka saa moja kabla ya muda wa Mwisho wa kurudisha kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi

Wakati muda ukiwa unayoyoma wagombea hao kwa pamoja watatangaza kujitoa katika kinyang'anyiro hicho kupitia CCM na kutangaza kujiunga na vyama vinavyounda UKAWA wakati huo watakuwa tayari wameshachukuliwa fomu za kuwania majimbo hayo hayo kwa tiketi ya vyama walivyojiunga navyo

Hii ni cooked story halaf kumbuka Tume ni ccm ikibaki sa moja kurudisha fom wanaweza wakaongeza ata wiki ili wachaguliwe wengne kuwakilisha ccm Stor yako haina mashiko[/QUOTE]

na huko si kuna kura za maoni au wanapitishwa moja kwa moja
 
Only if unajua kwamba CCM ndio yenye TUME na kila kitu within!! For that uchaguzi utaahirishwa, na watachukuliwa wagombea wengine, huelewi goli la mkono wewe!

Hili goal la mkono nina wasiwasi nalo kama litapatikana safari hii .......... kama kumbukumbu zangu ziko sawa, Mwenyekiti wa Tume ni Shemeji wa Lowasa!! CCM timing ilisha kuwa mbaya and it might backfire this time around!!

Hivi watu mnafikiri KANU, UNIP, MMD nk. walipenda kutoka!!?? Au huko hawajui magoli ya mkono!!??
 
Lowassa hana nia mbaya Na ccm alikipenda sana chama chake ila wakubwa hawakumpenda CHADEMA wamempenda ZAIDI Mungu mbariki LOWASSA Mungu wabariki WAPINZANI
 
Story ya kupika tu.ukawa imejipanga vizuri wala haotegemei hizo assumption
 
Kuua chama dola si kazi rahisi hasa kwa chama kilichopitia mifumo ya kijamaa.Ni rahisi kusambaratisha chama kilichopitia mfumo wa kibepari.Cha kijamaa kama CCM ni shughuli pevu TENA PEVU HASA.Chama cha kijamaa kina wenyewe na mara nyingi hao wenyewe hata huwa hawawi kwenye medani za siasa za msitari wa mbele.Huwa wako kimya tu kwenye maabara za kisiasa.Si rahisi kama unavyodhani lakini shukrani kwa taarifa.

Lowasa mwenyewe kama kweli ataenda chadema mission ni anakuja kuifuta ktk ramani chadema, Kingunge -> Lowasa -> Mwangonda = Wafanyakazi watiifu wa CCM na hata wakifanywa nn watalalamika lakini wataendelea kuitumikia. Naiona cdm ikifutika
 
We ndo utafutika na c chadema kamwe cdm kimeshajiimarisha cku nyingi kwa hyo acha kuandika ujinga mitandaon
 
Mtoa mada taja umri na elimu yako tafadhal!?
 
CCM ni rahis kudhibiti hilo.
Mgombea anatakiwa arudishe form kabla ya siku X. Ikifika siku X hajarudisha anakuwa automatically disqualified wanachukua mshindi wa pili.
 
hiyo plan haiwezmake.
mda wa kurudisha fomu utaongezwa ama hao watakaohama fomu zao nao zitachelewa.pia ujue kule ukawa pia kula za maoni zitakua zimepita kwahiyo hawatakubali kuwapisha wale wahamiaji
 
Watu zaidi 20 kujitoa dakika za mwisho ni sabotage ya wazi.
Hapo kweli mda wa kurudisha form lazima unawezwa ongezwa
 
Edward Ngoyayi Lowassa (amezaliwa 26 Agosti 1953) ni mwanasiasa nchini Tanzania. Alichaguliwa kuwa Waziri Mkuu wa kumi wa nchi hii tarehe 30 Desemba 2005 na kujiuzulu tarehe 7 Februari 2008 kwa kutajwa katika kamati ya bunge ya uchunguzi katika utoaji wa tenda kwa kampuni ya umeme ya Richmond kutokana na uzembe wa watendaji walio chini yake..
Lowassa ni mwenyeji na mbunge wa Monduli katika Mkoa wa Arusha. Alisoma shahada ya kwanza katika mada ya tamthilia kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, halafu shahada ya pili katika sayansi ya maendeleo ya jamii kwenye Chuo Kikuu cha Hull nchini (Uingereza).
 
Unawafanya CCM kama genge la wapiga debe. Kama huna la kusema usipotezee watu muda wao
 
Back
Top Bottom