Mkaa VS Gesi

Nahisi ifikapo mwezi wa sita niwe nautizama tu mkaaa kwa majirani nataka pata pleasure cooker pia
 
Kwa unafuu wa uchumi mkaa unatosha ukitumia jiko bunifu gunia la elfu 80 utadumu nalo miezi 6 kama una familia kama hauna ni mwaka 1 na unapika haina yoyote ya chakula bila kujari ugumu wa chakula hicho kuiva
Mkuu kafanye research kwanza then uje na clarification hizi, hakika utagundua guni hilo la elfu 80 ni mitungi miwili hiyo ya gas na inatoboa hata miezi saba...
 
Mkuu kafanye research kwanza then uje na clarification hizi, hakika utagundua guni hilo la elfu 80 ni mitungi miwili hiyo ya gas na inatoboa hata miezi saba...
Ninalo liongea nina uhakika nalo gas bado hipo juu halafu kuna majiko sanifu mpaka ya kuni...Kuni mbili unapika msosi wa watu 10...Sema jiko sanifu la mkaa lina bei mengi yana anzia laki 1....na ukitumia mkaa mbadala wa kilo moja una uzwa 3500 una kaa wiki nzima..
 
Kunde ekeke au wewe ndio yule mtengenezaji wa ule mkaa niliposikia ukielezea kule mawingu radio
 
Gesi kwangu ni nafuu + uharaka

Mkaa mpaka ukoleze na bado ufanisi wake ni wa taratibu mno.
Swali la kichokozi,mkuu kama una watoto siku ikilipuka,au housegirl akitumia visivyo hatari yake...wengi wanaiogopa gesi kwa sababu ya madhara yake
 
Yani mimi wali uliopikwa na gesi siupendi kabisa kabisa.
 
Kila kimoja kina faida na hasara
Gesi iko haraka zaidi ila kwa mboga km maharage lazima uingie hasara

Mkaa uko taratibu,Ni mzuri kupikia chakula km wali
 
Maswala ya kulipuka mkuu ilikuwa zamani
Swali la kichokozi,mkuu kama una watoto siku ikilipuka,au housegirl akitumia visivyo hatari yake...wengi wanaiogopa gesi kwa sababu ya madhara yake
 
Mjadala huu ungefaa ukawapa watoto wanaosoma kidato cha pili ntaani kwenu kisha uturejeshee majibu maana obvious swali lako umeshajibu halafu swali hili kwa mtanzania anaehitaji maendeleo sio swali
 
Kuna majiko bunifu yana save sana mkaa gunia la mkaa la elfu 80 unatumia miezi 6
duh wewe umeliona wapi hilo jiko la mkaa linalotumia mkaagunia kwa miezi 6 hata km single na huchemshi maharage haiwezekani
tutumie kapicha usikute ni yale ya kuni na mkaa
halafu mtu umepanga ghorofani kuuwasha mkaa mpaka pumba na makaratasi kwanini usitumie gesi na umeme?
 
Hakuna apingaye unafuu wa gesi over mkaa; hakuna asiye fahamu hilo. TATIZO ni upatikanaji wa gesi na nishati nyingine MBADALA kama umeme to the majority of our people. Hiyo kwa kweli ndiyo HOJA, ukiachilia mbali gharama kubwa wa majiko ya gesi na umeme! Kwani huwezi kuwa na mtungi wa gesi tu - wa kampuni yoyote ile - nakuanza mapishi. Unhitaji hayo majiko, na bei zake, upatikanaji wake na hata ubora bado ni mtihani mkubwa kwa Watanzania wengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…