Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Arusha ajiunga CHADEMA

Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Arusha ajiunga CHADEMA

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Chama cha Mapinduzi Arusha leo kimepata pigo kubwa baada ya Francis Ole Okayo kujitoa ndani ya chama hicho na kujiunga na Chadema.

Katika mkutano wa ndani unaoendelea muda huu jimboni Longido Okayo amekabidhi rasmi kadi yake kwa Katibu wa Kanda ya Kaskazini Amani Golugwa.

Mjumbe huyo wa Halmashauri kuu mkoa wa Arusha kati ya 2007-2012 ambaye ana nguvu kubwa jimboni Longido amesema CCM imeshakufa na kinachosubiriwa ni mazishi yake tu Oktoba mwaka huu.

Baadaye jioni mjumbe wa Kamati Kuu na Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema anatarajiwa kuwasili kwa chopa mjini Longido kuongoza mkutano mkubwa wa hadhara wa kumpokea rasmi Francis Ole Okayo CHADEMA.
 
Safi sana naona ukombozi sasa umeingia rasmi na kutambulika Longido.

Big up sana CHADEMA mkombozi wa wanyonge.
 
Kiki sasa si kifo cha kawaida, kinataka kuwa cha mende!!
 
ccm wakobusy kuisapot familia ya JK kumpiga vita Lowassa, uku ukawa wakizidi kuimarika.
 
Safi sana kamanda, umechagua njia sahihi, ni sawa na kwetu wakristo bila yesu mbingu hautoiona karibu kundini.
 
Kimsingi CCM ilishakufa, inasubiri kuzikwa. Tatizo nani wa kuizika? Hapo ndipo wananchi wanapochanganyikiwa hawaoni mbadala wanalazimika kuendelea na ccm. Nashauri vyama vya siasa vitulie vijiangalie vina mapungufu wapi vijirekebishe visahihishe makosa.Chonde chonde vyama vya siasa msiwachukie watu wanaowasema vibaya hao ndio watu wazuri kwenu kwani wanawaonyesha mnapokosea msipowasikiliza mnapotea. Sio vizuri kumsikiliza sana yule anayekusifia kwa muda mwingi huyu anakudanganya kwani wewe siyo malaika hata usifanye makosa !!!
 
ok.PNG
 
Hakika ccm hawana lao hapa tunakoelekea,Fua gamba Vaa Gwanda


Hongera sana Kamanda Fransis Ole Okayo.
 
Back
Top Bottom