Mjumbe wa Bodi ya wadhamini ya CHADEMA ajiuzulu nafasi yake

Mjumbe wa Bodi ya wadhamini ya CHADEMA ajiuzulu nafasi yake

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Mjumbe wa Bodi ya wadhamini ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Mary Florian Joachim ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ujumbe wa Chadema, nafasi ambayo ameitumikia kwa takribani miaka kumi na tano sasa.

Katika barua yake ya leo Juni 02, 2025 aliyoituma kwa Katibu wa Bodi ya wadhamini wa Chadema, Bi Mary ametanabaisha kuwa sababu ya kujiuzulu kwake ni za binafsi, akiamini kwamba kwasasa atashindwa kuitumikia nafasi yake vyema ndani ya Chama hicho Kikuu cha Upinzani nchini Tanzania.

Chanzo: Jambo TV
 
Namba za wafuatiliaji wa hii KESI online kupitia Youtube ZINATISHA.

MAHAKAMA: 15K viewers

Mwanzo TV : 1.4K viewers

Mwananchi Digital: 1K viewers

millard Ayo : 17K viewers

Jambo TV : 670 viewers

Zamaradi TV: 630 viewers

#FreeTunduLissuNow
 
Mjumbe wa Bodi ya wadhamini ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Mary Florian Joachim ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ujumbe wa Chadema, nafasi ambayo ameitumikia kwa takribani miaka kumi na tano sasa.

Katika barua yake ya leo Juni 02, 2025 aliyoituma kwa Katibu wa Bodi ya wadhamini wa Chadema, Bi Mary ametanabaisha kuwa sababu ya kujiuzulu kwake ni za binafsi, akiamini kwamba kwasasa atashindwa kuitumikia nafasi yake vyema ndani ya Chama hicho Kikuu cha Upinzani nchini Tanzania.

Chanzo: Jambo TV
Tunamtakia uzima tele,
halitabakia jiwe juu ya jiwe mpaka chadema ibaki nyeupe pee na huo ndo utakuwa ukombozi kwa taifa.
Kulikuwepo mchanganyiko wa chuma na udongo,tunataka tubaki na chuma tupu.
 
Kwa hiyo miaka yote hiyo mlikuwa mnalea fisadi
Mbwa mwitu aliyevaa vazi la kondoo huwezi kumjua,mpaka pale atakapoanza kuonyesha dalili za kukimbiza panya na nguchiro.ndo unagundua kwamba anatakiwa kutengwa kwenye zizi,maana akibaki atakula kondoo wenzake.
 
Fisadi yeyote na mchumia tumbo hawezi kukaa Chadema
Hili la kutoheshimu maamuzi ya mtu na kuanza kuwatukana linawaharibia sana nyie chadema chakavu. Unajua anayopitia au unatukana tu wakati mtu amesema ana sababu zake binafsi? Mbona mnakuwa wajinga namna hiyo nyie?!!!
 
CHAMA HAKINA MVUTO TENA WATU WAMESHASHTUKA
Chopa imepata kibali? Chama cha mvuto CHAUMMA kinaweza kupaki helikopta kule kule angani,wao washushe spika kwa kamba waanze kusema tutasikia tu halafu watuletee fomu ya malipo.
 
Back
Top Bottom