Mjue Sheikh Ponda Issa Ponda na Kundecha

Sokomoko

JF-Expert Member
Mar 29, 2008
1,915
127
Asalam alaikum,

Habari za masiku ndugu zanguni.

Naanza kwa jina la Mwenyezimungu muumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake! mwenye kujua ya dhahiri na ya siri (yaliyo mioyoni mwetu) na rehma zimfikie kipenzi chetu Muhammad SAW.

Je Ponda ni nani?

Mimi awali nilikuwa najua Ponda na Kundecha kuwa ni wanaharakati wenye kupigania haki za waislamu lakini imeniuma sana kujua undani wa hawa watu! Mimi ni mwislamu na siku zote nilikuwa naona jamaa wanafanya kazi kwa maslahi ya umma wa kiislamu lakini kumbe kuna mambo nyuma ya pazia.

Manji Vs Ponda & Co

Kuna uwanja ambao ulikuwa mali ya East African Muslim Welfare Society na kurithishwa kwa bakwata sehemu ya eneo lile ambalo lipo maeneo ya chang'ombe bakwatwa ililiuza/gawa kwa jumuia ya shia ismailia ambao na wao walikuwa wana hisa kwenye East African Muslim Welfare Society na Ismailia wakamuuzia Manji.

Mkiangalia hapo juu hakuna mgogoro wowote wa kati ya Manji na Waislamu ila kina Ponda inavyoonyesha walikodiwa ili kuweka mazingira ya kumfrastrate manji apauze kwa bei poa.

Leo tumuulize Ponda alilipwa kiasi gani kuhakikisha Manji hapamiliki pale? na kwanini walinyamaza baada ya manji kukitema kiwanja kile? Kwa akili ndogo ya kuzaliwa utajua kuwa Ponda & Co walitumika kufanya umafia ili kiwanja kipatikane kirahisi.

Kukamatwa kwa Ponda.

Kuna eneo ambalo limebakia kwenye kiwanja cha East African Muslim Welfare Society ambacho kinasemekana kuuzwa miaka minne au mitano iliyopita Ponda na group lake walivamia siku ya Ijumaa na kujenga msikiti wa muda na kuweka mabaunsa na baadhi ya waumini kwa madai kuwa kiwanja ni cha waislamu! yale yale yaliyomkuta Manji! na habari za chini ya kapeti ni kuwa Ponda na watu wake wamelipwa 15 Mil kumobilize uvamizi ule!

Huyu jamaa anatumiwa kwa kuwa anaushawishi kwenye jamii yetu ya waislam lakini leo hii kama Mungu atadhihirisha kuwa anayoyafanya hayafanyi kwa ajili ya waislamu ila kwa maslahi ya mabwana zake basi nadhani shingo yake itakuwa halali ya Waislamu. Kwani wale waliokamatwa jana usiku pale Chang'ombe wengi wao hakupata mgao wa tajiri anaepataka pale zaidi ya chai ya asubuhi chakula cha mchana na maji ya chupa!

Najua kuna wanahabari humu jamvini mkimuhoji jaribuni kumhoji issue ya manji iliishaje? je walilipwa nini baada ya kufanikisha zoezi lile?


Narudia waislamu ifike muda tuchukue muda wa kufikiria tusikubali kuburuzwa na viongozi wanaoangalia matumbo yao na kusababisha matatizo kwa waislamu wasiojua set up ya matukio husika.

Ahsanteni sana na ni matumaini yangu mmepata kitu juu ya mada hii.

[h=3]Quality Group linked to land grabbing[/h] Quality Group linked to land grabbing

AN internal report from the National Muslims Council of Tanzania (BAKWATA) says Quality Group Limited run by businessman Yusuf Manji tried to grab a prime piece of land from the Council in Dar es Salaam by allegedly perpetrating systematic fraud, conspiracy and corruption. This occurred as a result of deliberate misconduct of a few BAKWATA officials who conspired with Quality Group to illegally transfer ownership of the Council’s plot at suburban Chang’ombe in the city, says the report. BAKWATA had earmarked the land for the construction of a university, but ownership was mysteriously transferred to Quality Group, which had other ideas for the property. The 27-page report written by BAKWATA’s permanent probe committee implicates Mr Manji, who is the CEO of Quality Group, in the alleged conspiracy, saying its property on Plot Number 311/1 Block T at Chang’ombe was fraudulently transferred to Quality Group using forged documents purportedly from Trustees of the Muslim University College. The offices of the Administrator-General in Dar es Salaam roundly dismissed the authenticity of the documents. According to our investigations, the Administrator-General, Ms Christabella Kaisi, declared that the trustees of the Muslim College were not registered with her office and remained unregistered until March, this year. Ms Kaisi had made the declaration after being requested to give expert opinion on the rightful ownership of the plot after Mr Manji’s company claimed ownership. ?Some trustees alleged to have signed the document? but never put pen to paper ... some of the signatures also appeared to have been forged,’’ she attested in a letter to the Commissioner for Land. She added: ’’When I asked the said trustees to come to my office and sign the document in my presence, they never turned up to date.? The report’s annexure shows that Mr Manji had on December 4, 2002, signed a suspect contract with ?the Registered Trustee of Muslim University College? as Director of Quality Group (1999) Limited before the company changed its name to Quality Group Limited and signed an addendum on February 10, 2004. ?The (BAKWATA) committee unearthed the contradictions, conspiracy and fraud and all means of maneuvering on the whole process of transferring the plot ownership to the so called investor -- Quality Group (1999) Limited,’’ says the report. It adds: ’’The plot was intended to build the first Islamic University with the name Millennium University of Tanzania.? Records show that the late Chief Sheikh of BAKWATA, Mufti Hemed Bin Jumaa Bin Hemed, appointed the Board of Trustees of the planned university under the chairmanship of former Planning Minister, Nasoro Malocho, who is now deceased. There are 10 other prominent Muslims, including the current Minister for Foreign Affairs and International Corporation, Dr Asha-Rose Migiro, who were also named on the Board of Trustees. Mr Alnoor Kassum, the late Mr Abdalah Ngororo, Ms Amina Salum Ally, Dr Athumani Mfutakamba, Mr Aunal Mnyuziwala, Prof Hassan Mfaume Mlawa, Mr Musadiq Mohamed Ally, Mr Kassim Jeizan and Mr Salum Abadalah Zagar, were the other trustees. Sources close to the probe committee formed by the current Chief Sheikh, Mufti Issa Shaaban Simba, which compiled the report say Quality Group (1999) Limited had planned to build a school and hospital building on the property. ?The committee was shocked to find out that Quality Group (1999) was assisted by some BAKWATA officials to get the title deed for the plot,? asserts part of the report. The report maintains that the agreement signed by Mr Manji and Mr Ankeet Asar, representing Quality Group (1999) Limited and Alhaj Sefu Moma and Rajabu Mndewa on behalf of BAKWATA Trustees was illegal. ?The agreement is illegal since Mr Mndewa is not a bona fide BAKWATA Trustee. On the other hand the fact that Alhaj Momba agreed to co-sign the document with Mr Mndewa knowing the latter was not a Trustee, is clear evidence of conspiracy and fraud in the matter,’’ says the report. Documents obtained by THISDAY show that Mr Manji personally pushed for a speedy transfer of the ownership of the property and its development under Quality Group. It is only after the new Chief Sheikh, Mufti Simba, moved in to form a probe team to investigate the scandal over BAKWATA’s property at Chang’ombe that the alleged fraud, conspiracy and corruption involving Quality Group was unearthed.

Source:THISDAY 21 JUNE 2006
Source LIJUE BARAZA LAKO-BAKWATA

[h=2]Friday, October 5, 2007[/h] [h=3]WAISLAMU WAMELOGWA NA NANI?[/h]

Waislamu wamelogwa na nani?

Na Saed Kubenea
“VICHWA visivyosikia nitavipiga marungu.” Hiyo ni kauli ya Shekh Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa bin Shaban bin Simba.
Aliitoa mwaka 2002 mara baada ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo. Uchaguzi wa Mufti ulifanyika kutokana na kifo cha Marehemu Hemed Bin Juma bin Hemed.
Kwa hakika, kinyang’anyiro cha uchaguzi ule kilikuwa na ushindani mkali kati ya Shekh Mkuu wa sasa, Mutfi Simba na Shekh Sulemani Gorogosi.
Uchaguzi ulifanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Biashara (CBE) mjini Dodoma. Bila shaka, si wengi waliomuelewa na wala si wengi walioelewa kauli halisi ya Mufti Simba.
Wengi walikuwa gizani. Lakini sasa ikiwa ni takribani miaka mitano tangu Shekh Simba achaguliwe kushika nafasi hiyo, wengi wameanza kumuelewa.
Kwamba kauli yake ya “Vichwa visivyosikia nitavipiga marungu,” iliwalenga “wanaolivuruga” Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).
Wakati huo, machoni mwa wengi, BAKWATA ilionekana kama chombo kilichopotea njia. Asilimia kubwa ya waislamu walikuwa hawaikubali.
Wengi waliona baraza hilo kama chombo cha serikali na chama tawala-CCM.
Baadhi yao walikuwa wanasema waziwazi kwamba BAKWATA imeingiliwa na serikali. Kipaumbele chake hakikujulikani machoni mwa waislamu wengi.
Maswali kama, BAKWATA inakwenda wapi au Baraza litafika kweli, yalikuwa yakisikika kila kona.
Mapambano kadhaa yalianzishwa kuipinga BAKWATA na viongozi wake. Kilikuwa ni kipindi cha harakati na hatua za kuikataa BAKWATA zilifika mbali.
Wanaharakati kadhaa walihubiri ubaya wa Baraza na kile lilichokiita “ndoa yake na serikali.” Hicho ndicho chanzo au kichocheo cha “mauaji ya Mwembechai.”
Kulikuwa na hata madai kwamba baadhi ya waislamu walipanga mapinduzi dhidi ya uongozi wa Baraza.
Mihadhara na makongamano vilifanyika usiku na mchana. Kila pembe ya nchi waislamu walisimama kulaani Baraza na kuituhumu serikali kwamba inawalinda viongozi wake.
Misikiti kadhaa ilianzisha harakati kwa madai kwamba BAKWATA imeshindwa kuutetea uislamu na waislamu kwa ujumla.
Wanaharakati mbalimbali walichipuka; wengine wakiwa na dhamira ya kweli na wengine wakiwa waganga njaa.
Baadhi yao wanafahamika hata kwa majina na matendo yao. Wote hawa walikuwa na madai yanayofanana kwamba BAKWATA imemezwa na serikali na imeshindwa kuutetea Uislamu.
Hata hivyo, watu makini waliyadharau madai hayo baada ya kuwapima watoa madai na matendo yao.
Wengi walijua tangu awali kwamba BAKWATA haikuingiliwa na serikali wala waumini wa dini nyingine; imeingiliwa na waislamu wenyewe.
Ni wale waliokuwa wanaitumia BAKWATA kujinufaisha. Baadhi yao wangalipo hadi sasa, lakini wengi wameondolewa.
Hakuna aliyejua au hata kufikiri kwamba Mufti Simba angeweza kuwang’oa ndani ya BAKWATA; baadhi ya viongozi walionekana kuwa kikwanzo kwa maendeleo ya uislamu.
Watu kama Ali Mubaraka, aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya BAKWATA, Mussa Hemed, Naibu Katibu Mkuu Dini, Abas Kihemba na wengineo tayari walikuwa wameweka mizizi yao ndani ya baraza hilo.
Wapo waliondoka wenyewe baada ya kuona mambo yanakwenda kombo, lakini wapo wengi pia ambao wameondoka kwa kung’olewa na kimbuga cha Mufti Simba.
Kwa hakika, Shekh Simba amekuwa simba kweli. Amejitahidi kurudisha hadhi na heshima ya baraza hilo mbele ya jamii. Amefanikiwa japo si kwa kiasi kikubwa kurudisha umoja na mshikamano miongoni mwa waislamu.
Tayari sasa baadhi ya waislamu wanalikubali baraza lao. Wengi sasa wanajua kwamba adui yao mkubwa si serikali, wala madhehebu mengine, bali waislamu wenzao.
Na hili linathibitika sasa wakati mgogoro unaofukuta kati ya mfanyabiashara Yusuf Manji anayemiliki kampuni ya Quality Group na baadhi ya waislamu wakiongozwa na mwanaharakati mahiri, Shekh Khalifa Khamisi.
Kiwanja kinachogombewa ni Na. 311/1 kilichopo Kitalu T Chang’ombe, Dar es Salaam.
Taarifa zinasema kiwanja hicho kilimilikishwa kwa kampuni ya Quality Group na baadhi ya waliokuwa wafanyakazi wa BAKWATA, ambao tayari Mufti amewashughulikia.
Hadi sasa, haijulikani ni kiasi gani wale “wasaliti” walilipwa kwa kazi hiyo.
Linalofahamika ni kwamba watendaji hao, wakiongozwa na Katibu Mkuu wa BAKWATA, Abass Kihemba, walifukuzwa kazi kwa madai ya kukiuka maadili ya kazi yao.
Hicho ndicho chanzo au kichocheo cha harakati na malalamiko ya sasa yanayoongozwa na Shekh Khalifa Khamisi.
Lakini kwamba aliyemilikishwa na waliomilikisha, wote ni waislamu, ni jambo linalodhihirisha kuwa BAKWATA na uislamu havivurugwi na serikali, bali na waislamu wenyewe.
BAKWATA ni moja ya taasisi ya kidini nchini iliyopata bahati ya kumiliki mali na vitegauchumi vikubwa.
Mwaka 1968 ilimilikishwa na serikali mali za iliyokuwa Taasisi ya Waislamu ya Afrika Mashariki (East Afrika Muslim).
BAKWATA ilirithi majumba, pamoja na vitegauchumi mbalimbali kwa dhamira kuendeleza uislamu.
Bahati mbaya hayo hayakufanyika. Kila mmoja anafahamu kwamba kama BAKWATA ingetumia mali na rasilimali zake vizuri, leo ingekuwa mbali kimaendeleo.
Kama raslimali zake zingetumika vizuri, waislamu wangekuwa juu. Wangepata elimu bila kutegemea msaada mkubwa kutoka kwa serikali. Na hata malalamiko yanayoenezwa sasa kwamba serikali imewasahau waislamu yasingesikika.
Lakini bahati mbaya ni kwamba waliopewa dhamana ya kusimamia mali na rasilimali za waislamu ndiyo haohao waliogeuka na kuzitafuna.
Wakati madhehebu mengine yako katika mbio kali za maendeleo, bado BAKWATA inatambaa.
Angalia madhehebu mengine yanamiliki Hospitari za rufaa (Bugando-Mwanza na KCMC-Moshi), BAKWATA imeishia kumiliki zahanati.
Wakati madhehebu mengine yanamiliki vyuo vikuu, kwa mfano Chuo Kikuu cha Tumaini mkoani Iringa na Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine – Nyegezi, Mwanza, BAKWATA imeishia kumiliki sekondari.

Source: MKATAMBUGA: WAISLAMU WAMELOGWA NA NANI?

Waislamu wataka jengo lao toka Quality Group
Na Muhibu Said

KAMATI ya Maimamu ya Kuokoa Mali za Waislamu nchini, imeipa siku 20 kampuni ya Quality Group (1999) Limited, kurejesha kiwanja cha Waislamu kilichopo katika eneo la Chang'ombe, Wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam na kumuomba Rais Jakaya Kikwete kuifutia kampuni hiyo umiliki wa kiwanja hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Msikiti wa Mtoro, jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa Kamati hiyo, Sheikh Khalifa Khamisi, alisema wamefikia hatua hiyo kwa kuwa kiwanja hicho ni mali halali ya Waislamu waliyopewa na Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere kwa ajili ya kujenga Chuo Kikuu na Mwalimu mwenyewe aliomba msaada kwa Rais (wa zamani) wa Misri, Gamal Abdel Nasser ili kufanikisha azma hiyo.

Sheikh Khalifa alisema kiwanja hicho chenye ukubwa wa ekari 9.5 kinachomilikiwa kwa hati namba ID/195976, baada ya kukabidhiwa Waislamu, kilisajiliwa kwa jina la taasisi ya Muslim University of Tanzania iliyo chini ya Baraza Kuu la Waislamu nchini (Bakwata).

Hata hivyo, Sheikh Khalifa alisema baadaye, wadhamini wawili wa Bakwata walisaini mkataba na Quality Group (1999) Limited wa uendelezaji wa kiwanja hicho.

Alisema, katika mkataba huo uliotiwa saini Oktoba 4, mwaka 2002, Quality Group (1999) Limited ilikubaliana na Bakwata kwamba, ingejenga katika kiwanja hicho hospitali na shule ya msingi ambazo zingekuwa mali ya Bakwata na ujenzi wa vyumba vya madarasa ungekuwa umekamilika ndani ya miezi sita.

Alisema pia walikubaliana kwamba Bakwata ingekabidhi sehemu ya kiwanja kuwa miliki halali ya kampuni hiyo na kwamba, mara mradi wa ujenzi wa shule ungekamilika, kila upande ungebaki na miliki yake halali na uhusiano wa kibiashara kati yao ungekuwa umekoma.

Sheikh Khalifa alisema baada ya makubaliano hayo kufikiwa, kampuni hiyo ilipata hati ya kumiliki kiwanja hicho Desemba 8, mwaka 2003, lakini hadi sasa hakuna mahali popote katika kiwanja hicho palipojengwa hospitali wala shule ya msingi, kinyume na makubaliano yaliyofikiwa baina yao.

Alisema pamoja na hali hiyo, Mei 25, 2004 kampuni hiyo ilipewa kibali cha kuzungusha uzio katika kiwanja hicho na Februari 18, mwaka jana kibali hicho kikaidhinishwa na Manispaa ya Temeke. "Wakati huo Bakwata haikuwa imepokea hata shilingi moja kutoka kampuni hiyo," alisema Sheikh Khalifa.

Alisema kutokana na hali hiyo, Kamati ya Maimamu ilimwandikia barua Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Magufuli kumuomba ahakikishe kiwanja hicho kinarudi kwa Waislamu na Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu, Issa bin Shaban Simba akiongozana na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Bakwata Taifa, walitoa msimamo wa baraza mbele ya waziri huyo wakitaka serikali kukirejesha kiwanja hicho mikononi mwake.

"Msimamo huo ulitolewa baada ya Waziri kuitaka Halmashauri Kuu ya Bakwata kutoa msimamo wake juu ya umiliki wa kiwanja hicho.

Baada ya kimya cha muda mrefu serikali imekataa kuifuta hati aliyopewa Quality Group (1999) Limited na badala yake Bakwata imepokea fedha kidogo kutoka kampuni hiyo. Tarehe 31/5/2007 Bakwata iliingiza katika akaunti yake hundi yenye thamani ya Sh86,740,000 kutoka kampuni hiyo kama kifuta jasho, baada ya serikali kukataa maombi ya Waislamu wa nchi nzima," alisema Sheikh Khalifa.

Alipoulizwa jana na Mwananchi, Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu Taifa ya Bakwata, Sheikh Khamis Mataka, alikiri Bakwata kuingiziwa fedha hizo katika akaunti yake.

Kutokana na hali hiyo, Sheikh Khalifa aliitaka kampuni hiyo kwenda kuchukua fedha ilizoipa Bakwata, akisema kuwa mkataba uliosainiwa na baadhi ya viongozi wa Bakwata na kampuni hiyo kuhusu mauzo ya kiwanja hicho, haukuzingatia maslahi ya umma wala shabaha ya serikali kutoa kiwanja hicho.

"Ni jambo la kushangaza na kusikitisha kuona kwamba serikali iliyochaguliwa na umma kwa manufaa ya umma licha ya kuahidi kupitia Waziri Magufuli kutekeleza maombi ya umma wa Waislamu wa Tanzania nzima, imeyapuuza maombi yao ili kulinda maslahi binafsi ya mfanyabiashara mmoja," alisema Sheikh Khalifa.

Juhudi za kumpata mmiliki wa Quality Group, Yusuf Manji ziligonga mwamba baada ya msaidizi wake kudai kuwa yuko nje ya nchi.https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/4041-waislamu-wataka-jengo-lao-toka-quality-group.html

na Ratifa Baranyikwa na Prisca Nsemwa


POLISI Kanda Maalum ya Dar es Salaam, imeyapiga marufuku maandamano yaliyopangwa kufanywa na waumini wa dini ya Kiislamu kesho, kushinikiza kurejeshwa kwa kiwanja wanachodai kimeuzwa kinyume cha taratibu kwa kampuni moja jijini Dar es Salaam. Maandamano hayo yamepigwa marufuku wakati Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) likitoa taarifa kusisitiza kuwa, kiwanja hicho kimeuzwa kihalali kwa kampuni moja ya jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Alfred Tibaigana, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, maandamano hayo yamepigwa marufuku baada ya polisi kubaini kuwa kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kutokea uvunjifu wa amani na kumwagika kwa damu iwapo yangeruhusiwa.
“Hali hiyo inatokana na mvutano uliokuwepo baina ya pande mbili zinazopingana kuhusu suala hilo,” Tibaigana alisema na kubainisha kuwa aliishuhudia hali hiyo alipojadiliana na wawakilishi wa pande hizo ofisini kwake.
Tibaigana alisema kuwa wakati bado anatafakari baada ya kupokea barua toka kwa Sheikh Khalifa Khamis ya kuomba kuandamana siku ya Ijumaa, alipokea barua nyingine toka kwa Kamati ya Maimamu ya kuokoa mali ya waislamu, iliyosainiwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Ustadh Said Mwaipopo na Mkurugenzi wa Habari, Chief Hussen Msopa, wakimuomba asitishe maandamano hayo, huku wakitoa sababu saba.
Alisema kuwa barua hiyo inatokana na kikao cha maimamu wapatao 15 wa misikiti ya Tegeta, Buguruni, Tandika, Magomeni, Mwananyamala, Vingunguti, Keko, Kurasini, Tabata, Ubungo, Kimara, Mbezi Beach, Mabibo na Mwenge.
Tibaigana alisema kuwa kati ya sababu walizozitoa, ilikuwepo iliyoeleza kuwa zimepangwa njama na kundi moja, kuingia katika maandamano hayo kwa nia ya kuwadhuru baadhi ya watu, na kudai kuwa kuna vijana wengine walikuwa wamepangwa na Sheikh Khalifa ili kwenda kuvamia na kuiba mabati katika kiwanja hicho kilichopo Chang’ombe.
Aidha, Tibaigana alisema kuwa alitahadharishwa kuwa kuna kundi kubwa la vijana ambao walipanga kuswali katika misikiti ya Manyema, Idrisa, Lindi na Chipata na baada ya swala watajipanga kuzuia maandamano hayo.
Tibaigana alisema kuwa, uamuzi wa kusitisha maandamo hayo unakuja baada ya kufanya majadiliano ofisini kwake na makundi yote mawili.
“Nilijadiliana nao kwa saa tatu, nilitumia busara nyingi ku-control (kudhibiti) kikao hicho, wote walikuwa na chuki kubwa,” alisema Tibaigana.
Hata hivyo, alisema kuwa vitisho vilivyo katika barua ya kundi la Mwaipopo na Msopa, viliendelea kujionyesha waziwazi katika kikao hicho, hadi akafikia hatua ya kuagiza kufunguliwa kwa jalada la uchunguzi.
Alisema kuwa, uchunguzi huo ulioanza jana, utamuwezesha kujua kama kweli vitisho vya kudhuriana na kumwaga damu ni vya kweli, ili kama ni vya kweli, wanaohusika waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
Wakati huo huo, Sheikh Khalifa Khamis alisema kuwa Waislamu wameridhia kauli iliyotolewa na Jeshi la Polisi la kusitisha maandamano hayo, hadi uchunguzi utakapokamilika.
Sheikh Khalifa alieleza kuwa, Kamanda Tibaigana aliwaahidi kuwa uchunguzi utakamilika katika kipindi cha siku 14 na mara utakapokamilika, maandamano yataendelea kama kawaida.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Msikiti wa Mtoro uliopo Kariakoo, alieleza kuwa Waislamu watambue kuwa maandamano hayo yataendelea mara baada ya uchunguzi wa polisi kukamilika.
Aidha aliwataka Waislamu kuacha njaa ya fedha katika vitu vya Mungu, hususani kiwanja hicho, ambacho alidai ni wakfu wa Waislamu kwa sababu njia zilizotumika kumilikishwa kiwanja hicho ni za kitapeli.
Alionyesha kudharau vitisho vilivyotolewa na maimamu, kwamba watavuruga maandamano hayo na kusema kuwa harakati za Waislamu hazitakatishwa na vitisho vya mtu yeyote.
Sakata hilo linatokana na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kudaiwa kuuza kiwanja hicho, kinachoelezwa kuwa ni wakfu wa Waislamu, kwa Kampuni ya Quality Group Ltd, inayomilikiwa na Yusuf Manji.
Kwa maana hiyo, Sheikh Khalifa anaongoza harakati za kutaka kiwanja hicho kirejeshwa na pia kumtaka Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Magufuli, ajiuzulu kwa kushindwa kukirejesha kiwanja hicho kwa Waislamu.
Hata hivyo, inaelezwa kuwa uamuzi wa kumilikisha kiwanja kwa Quality Group Limited uliofanywa na vyombo vya juu kabisa vya BAKWATA, ni wa mwisho na hauwezi kubatilishwa.
Habari kutoka ndani ya BAKWATA zilisema kwamba, kikao cha Halmashauri Kuu, Maulamaa na Baraza la Wadhamini kilichofanyika Julai mwaka huu, kiliafiki na kuridhia kiwanja hicho chenye namba 311/1 kilichopo Chang’ombe, wilayani Temeke, Dar es Salaam kuwa ni mali halali ya Quality Group kwa mujibu wa sheria.
Mkutano wa Halmashauri Kuu ulifanyika chini ya mwenyekiti wake, Sheikh Hamisi Mataka na Baraza la Maulamaa lilikutana chini ya uenyekiti wa Sheikh Mkuu, Mufti Issa bin Shaaban Simba.
Taarifa ya BAKWATA ilisema kwamba, si sahihi kwa Waislamu kuchochewa kuacha kushughulikia mambo ya msingi badala ya kuingia katika mitego ya ‘wachache wenye njaa’ wanaotaka kuwatumia.
Viongozi hao wa BAKWATA wamesema kwamba, haistahili hata kidogo Waislamu kuburuzwa na kikundi kinachodai kwamba kinatetea maslahi na haki za Waislamu.
BAKWATA imesema kwamba, Quality Group Limited iliuziwa kiwanja hicho na ikafanya malipo yote kwa mujibu wa mikataba na haiwezekani kuanza tena kurudi nyuma na kuanza kutaka kubatilisha mkataba huo.
“Mtu akishapewa hati ya kumiliki ardhi, hakuna mamlaka yoyote inayoweza kufuta au kubatilisha hati hiyo, isipokuwa rais tu, ambaye naye hufanya hivyo kwa manufaa ya umma au sababu nyinginezo baada ya kuridhika kwamba kuna umuhimu huo,” ilisema taarifa hiyo.
Hata hivyo, BAKWATA ilisema kwamba katika suala hili la kiwanja kilichouzwa kwa Quality Group Limited, hakuna kurudi nyuma, kwani kufanya hivyo itakuwa ni dhuluma tupu.
“BAKWATA haina madai wala lawama zozote kwa Quality Group Limited wala mmiliki wake kijana Yusuf Manji, kwani kila kitu kilifanyika kwa mujibu wa makubaliano na sheria ilifuatwa kikamilifu,” alisema kiongozi mmoja wa BAKWATA ambaye alikuwa miongoni mwa waliofikia uamuzi wa Julai 21, mwaka huu. Polisi yazuia Waislamu

[h=1]Waislamu wataka jengo lao toka Quality Group[/h] Posted on July 26, 2007 by admin

KAMATI ya Maimamu ya Kuokoa Mali za Waislamu nchini, imeipa siku 20 kampuni ya Quality Group (1999) Limited, kurejesha kiwanja cha Waislamu kilichopo katika eneo la Chang’ombe, Wilaya ya Temeke


Na Muhibu Said

KAMATI ya Maimamu ya Kuokoa Mali za Waislamu nchini, imeipa siku 20 kampuni ya Quality Group (1999) Limited, kurejesha kiwanja cha Waislamu kilichopo katika eneo la Chang’ombe, Wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam na kumuomba Rais Jakaya Kikwete kuifutia kampuni hiyo umiliki wa kiwanja hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Msikiti wa Mtoro, jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa Kamati hiyo, Sheikh Khalifa Khamisi, alisema wamefikia hatua hiyo kwa kuwa kiwanja hicho ni mali halali ya Waislamu waliyopewa na Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere kwa ajili ya kujenga Chuo Kikuu na Mwalimu mwenyewe aliomba msaada kwa Rais (wa zamani) wa Misri, Gamal Abdel Nasser ili kufanikisha azma hiyo.

Sheikh Khalifa alisema kiwanja hicho chenye ukubwa wa ekari 9.5 kinachomilikiwa kwa hati namba ID/195976, baada ya kukabidhiwa Waislamu, kilisajiliwa kwa jina la taasisi ya Muslim University of Tanzania iliyo chini ya Baraza Kuu la Waislamu nchini (Bakwata).

Hata hivyo, Sheikh Khalifa alisema baadaye, wadhamini wawili wa Bakwata walisaini mkataba na Quality Group (1999) Limited wa uendelezaji wa kiwanja hicho.

Alisema, katika mkataba huo uliotiwa saini Oktoba 4, mwaka 2002, Quality Group (1999) Limited ilikubaliana na Bakwata kwamba, ingejenga katika kiwanja hicho hospitali na shule ya msingi ambazo zingekuwa mali ya Bakwata na ujenzi wa vyumba vya madarasa ungekuwa umekamilika ndani ya miezi sita.

Alisema pia walikubaliana kwamba Bakwata ingekabidhi sehemu ya kiwanja kuwa miliki halali ya kampuni hiyo na kwamba, mara mradi wa ujenzi wa shule ungekamilika, kila upande ungebaki na miliki yake halali na uhusiano wa kibiashara kati yao ungekuwa umekoma.

Sheikh Khalifa alisema baada ya makubaliano hayo kufikiwa, kampuni hiyo ilipata hati ya kumiliki kiwanja hicho Desemba 8, mwaka 2003, lakini hadi sasa hakuna mahali popote katika kiwanja hicho palipojengwa hospitali wala shule ya msingi, kinyume na makubaliano yaliyofikiwa baina yao.

Alisema pamoja na hali hiyo, Mei 25, 2004 kampuni hiyo ilipewa kibali cha kuzungusha uzio katika kiwanja hicho na Februari 18, mwaka jana kibali hicho kikaidhinishwa na Manispaa ya Temeke. “Wakati huo Bakwata haikuwa imepokea hata shilingi moja kutoka kampuni hiyo,” alisema Sheikh Khalifa.

Alisema kutokana na hali hiyo, Kamati ya Maimamu ilimwandikia barua Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Magufuli kumuomba ahakikishe kiwanja hicho kinarudi kwa Waislamu na Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu, Issa bin Shaban Simba akiongozana na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Bakwata Taifa, walitoa msimamo wa baraza mbele ya waziri huyo wakitaka serikali kukirejesha kiwanja hicho mikononi mwake.

“Msimamo huo ulitolewa baada ya Waziri kuitaka Halmashauri Kuu ya Bakwata kutoa msimamo wake juu ya umiliki wa kiwanja hicho.

Baada ya kimya cha muda mrefu serikali imekataa kuifuta hati aliyopewa Quality Group (1999) Limited na badala yake Bakwata imepokea fedha kidogo kutoka kampuni hiyo. Tarehe 31/5/2007 Bakwata iliingiza katika akaunti yake hundi yenye thamani ya Sh86,740,000 kutoka kampuni hiyo kama kifuta jasho, baada ya serikali kukataa maombi ya Waislamu wa nchi nzima,” alisema Sheikh Khalifa.

Alipoulizwa jana na Mwananchi, Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu Taifa ya Bakwata, Sheikh Khamis Mataka, alikiri Bakwata kuingiziwa fedha hizo katika akaunti yake.

Kutokana na hali hiyo, Sheikh Khalifa aliitaka kampuni hiyo kwenda kuchukua fedha ilizoipa Bakwata, akisema kuwa mkataba uliosainiwa na baadhi ya viongozi wa Bakwata na kampuni hiyo kuhusu mauzo ya kiwanja hicho, haukuzingatia maslahi ya umma wala shabaha ya serikali kutoa kiwanja hicho.

“Ni jambo la kushangaza na kusikitisha kuona kwamba serikali iliyochaguliwa na umma kwa manufaa ya umma licha ya kuahidi kupitia Waziri Magufuli kutekeleza maombi ya umma wa Waislamu wa Tanzania nzima, imeyapuuza maombi yao ili kulinda maslahi binafsi ya mfanyabiashara mmoja,” alisema Sheikh Khalifa.

Juhudi za kumpata mmiliki wa Quality Group, Yusuf Manji ziligonga mwamba baada ya msaidizi wake kudai kuwa yuko nje ya nchi.

Source: Mwananchi http://www.bongo5.com/waislamu-wataka-jengo-lao-toka-quality-group-07-2007/
Waislamu kutoa Tamko kesho baada ya Quality Group kugoma kurudisha kiwanja

1696642.jpg

Thursday, April 09, 2009 11:20 AM
WAUMINI wa Kiislamu kesho wanatarajia kutoa tamko lao baada ya Mkurugenzi wa Quality Group kugoma kurudisha kiwanja hicho.
Tamko hilo linatarajiwa kutolewa na Baraza la Habari Tanzania [Bahakita]kufuatia muda waliotoa kwa aliyenunua kiwanja hicho kuka kimya muda wote ho bila majibu.

Akizungumza na vyombo vya habari Mkurugenzi wa Baraza hilo Oustadhi Said Mwaipopo amesema kuwa kutokana na hilo kesho wanatoa tamko rasmi.

Amesema kuwa awali walitoa muda ili Mkurugenzi wa Kampuni ya Quality Group kurudisha kiwanja alichonunua kutoka kwa Manji alichouziwa kinyemela akirudishe.

Hivyo kwakuwa hali imeonekana kuwa kugoma kurudisha kiwanja hicho ambaacho ni mali ya waislamu kesho itajulikana baada ya kutoa tamko kwa waislamu.

Kiwanja hicho kilichopo Chang'ombe Temeke jijini Dar es Salaam walipewa waumini wa dini ya Kiislamu ambapo walipewa na Hayati Baba a Taifa Mwl.Jk Nyerere kwa ajili ya kujengea chuo kikuuu cha Waislamu.

Amesema kutokana na uroho wa baadhi ya viongozi wa kiislamu kiwanja hicho waliweza kukiuza kinyemela na kumuuzia Bw Yusuph Manji kwa Mil. 80 na Manji na yeye ameweza kukiuza.

Hivyo kwa kuwa Bahakita inataka kuondoa ufisadi ndani ya Bakwata lazima kiwanja hicho kirudishwe alisema MWaipopo.


Source Waislamu kutoa Tamko kesho baada ya Quality Group kugoma kurudisha kiwanja


Ikiwa Mufti alisema uuzwaji wa kiwanja namba 311 kwa kampuni ya Quality Group hautambiliki na Bakwata nadhani Ponda kama ana nia njema na waislamu basi angesaidia Bakwata kuweza kurejesha eneo hilo ambalo linakadiriwa kuwa na ukubwa wa hekari zaidi ya 6 ili kuweza kujenga chuo kikuu cha kiislamu. Lakini ikiwa Ponda anataka eneo la heka 3 ambalo limeuzwa kihalali kwa mujibu wa Mufti kwa kampuni ya Agritanza.

Kova pia alisema kuwa mnamo Oktoba 12,mwaka huu Ponda aliwaongoza wafuasi wake na kuvamia kiwanja namba 311/2/4 block T chang’ombe mali ya kampuni ya Agritanza kwa madai ya kulikomboa.



“Ponda akiwa na wafuasi wake walivamia kiwanja hicho cha agritanza na kudai kuwa wanakomboa mali za waislamu zilizouzwa na Bakwata,uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa kiwanja hicho kina hati miliki namba 93773 iliyotolewa na Wizara ya Ardhi pamoja na mikataba mbalimbali ya kuuziana”alisema


Aidha Kova alisema kuwa uongozi wa Bakwata ulipeleka mashahidi kuthibitisha uhalali wa kiwanja hicho na kusema kuwa watu waliovamia wanakabiliwa na shitaka la kuingia kwa jinai pamoja na uharibifu wa mali. MTANGAZAJI

Kuna gazeti lilimnukuu mnunuzi/mmiliki wa eneo lililovamiwa na Ponda na wenzake akisema Ponda alitoa wazo wa kumrudishia pesa walizolipa Bakwata na kuifanya iwe siri bila Bakwata kujua. Mmmiliki huyo alipouliza je heka zake 40 alizotoa kwa bakwata kama sehemu ya "deal" ile watamrudishia? Inasemekana Ponda hakuwa na jibu.

Inavyoonekana Ponda anatumiwa na "wakubwa" wanaomezea mate eneo hilo. Na kama hali ipo hivyo basi Ponda anawajibika moja kwa moja mbele ya Mungu kuwa anasababisha madhila kwa waislamu wanaomtetea wakijua kuwa anafanya kwa ajili ya dini ilihali anafanya kwa maslahi yake mwenyewe. Inasikitisha sana kuona kuwa Mungu amempa kipaji cha kuwashawishi waislamu lakini anakitumia kwa maslahi yake binafsi na sio kwa ajili ya kuwaendeleza waislamu kielimu na kiuchumi.

Nawakilisha.
 
nakuunga mkono japo naendelea na utafiti wangu kuhusu huyu mrundi,hiyo avatar yako inaonyesha unatekeka kirahisi na wageni,wale vilaza kutoka mombasa naona wameshakula kichwa kwako.
 
Hivi uislamu inaruhusu kujenga misikiti ktk ardhi ya dulma!? hivi hata huyo Mungu unayemuomba atakusikiliza kweli??? dahh! jamani sasa naona kila kukicha watu wanazua mitazamo yao ktk kubadirisha makusudio ya dini zetu.
 
Ponda ni wa kupuuzwa, nashukuru umeliona hilo mkuu. huyu jamaa ni tatizo. Msisahau huyo ndiye aliyekuwa anahamasisha Muslims wasishiriki sensa ya watu na makazi 2012. Huku akijua ni kosa kutokuhesabiwa, yeye na familia yake wakahesabiwa wenzake aliowadanganya wakalala selo. Huyu jamaa tatizo
 
Hivi uislamu inaruhusu kujenga misikiti ktk ardhi ya dulma!? hivi hata huyo Mungu unayemuomba atakusikiliza kweli??? dahh! jamani sasa naona kila kukicha watu wanazua mitazamo yao ktk kubadirisha makusudio ya dini zetu.

sijui dhulma gani unaongea. nadhani ukisema ujue unachosema. kile kiwanja cha waislam lkn BAKWATA Wakaamua kukipora na kama kawaida yao eti kuwakomoa waislam. lkn kwa bahati hakujua mnunuzi kwamba kauziwa Hewa. na msikiti ule utajulikana kama Masjid Sheikh Suleiaman takadiri. Mufti wa kwnza tz
 
Ponda ni wa kupuuzwa, nashukuru umeliona hilo mkuu. huyu jamaa ni tatizo. Msisahau huyo ndiye aliyekuwa anahamasisha Muslims wasishiriki sensa ya watu na makazi 2012. Huku akijua ni kosa kutokuhesabiwa, yeye na familia yake wakahesabiwa wenzake aliowadanganya wakalala selo. Huyu jamaa tatizo

lkn waislam wengi wasomi wanamkubali kwa kuwafumbua macho watz maambo yanayoendelea hapa tz. pengine namfananisha na dk slaa.
 
sijui dhulma gani unaongea. nadhani ukisema ujue unachosema. kile kiwanja cha waislam lkn BAKWATA Wakaamua kukipora na kama kawaida yao eti kuwakomoa waislam. lkn kwa bahati hakujua mnunuzi kwamba kauziwa Hewa. na msikiti ule utajulikana kama Masjid Sheikh Suleiaman takadiri. Mufti wa kwnza tz

kwani bakwata wao ni wakristo?
 
Ponda ni adui wa uislam na ukristo pia.He is the enemy of my religion and yours, tuungane pamoja tumshinde huyu shwetani.
 
sijui dhulma gani unaongea. nadhani ukisema ujue unachosema. kile kiwanja cha waislam lkn BAKWATA Wakaamua kukipora na kama kawaida yao eti kuwakomoa waislam. lkn kwa bahati hakujua mnunuzi kwamba kauziwa Hewa. na msikiti ule utajulikana kama Masjid Sheikh Suleiaman takadiri. Mufti wa kwnza tz

Mkuu elewa kuna tajiri anataka lile eneo kina ponda wametumiwa na zimetoka 15 mil ku mobilize kwa kuwa wanaushawishi mkubwa watu kama wewe ndio wale mnaokamatwa mkafunguliwa kesi halafu mkakosa wadhamini maana hata hujui what is behind the scene!

Ni hivi kina Ponda walitakiwa wadeal na viongozi wa bakwata na sio alienunua ili bakwata arjeshe pesa kwa mununuzi na ardhi irudi bakwata. Hayo ndio waliyoambiwa na mnunuzi lakini kina Ponda hawataki wanataka pesa irudishwe na waliowatuma ardhi iende kwa aliewatuma.

Kwa kifupi kina Ponda wanalipwa kwa ile kazi wewe kalaga bhaho eti utajengwa msikiti utaitwa jina la mufti wa kwanza. Mambo yataenda kimya kimya kama ilivyokuwa kwa manji watu watakula mshiko hakuta jengwa msikiti wala madrasa!
 
lkn waislam wengi wasomi wanamkubali kwa kuwafumbua macho watz maambo yanayoendelea hapa tz. pengine namfananisha na dk slaa.


Wasomi hao wamuulize ile vita kuhusu uwanja uliouzwa kwa manji ambao ni sehemu tu ya sehemu hiyo hiyo wanayoidai leo waliimalizaje? je walitumiwa na anaemiliki sasa na wakanyamazishwa kwa pesa? je wameikodisha na wanalipwa rent? au walilipwa kiasi gani kwa shughuli ile? maana inasemekana hii kazi mpya wameshapokea 15 Mil kwa mtu anaepataka pale.

Fungua macho hakuna issue ya uislamu hapa kuna vigogo wanapigana vikumbo kuchukua ile ardhi kina Ponda wanatumiwa kufanikisha mission refer to Manji vs Waislam saga.
 
sijui dhulma gani unaongea. nadhani ukisema ujue unachosema. kile kiwanja cha waislam lkn BAKWATA Wakaamua kukipora na kama kawaida yao eti kuwakomoa waislam. lkn kwa bahati hakujua mnunuzi kwamba kauziwa Hewa. na msikiti ule utajulikana kama Masjid Sheikh Suleiaman takadiri. Mufti wa kwnza tz


Nadhani wewe ndio hufahamu omba ujulishwe kiwanja kile kilitolewa na Nyerere kujengwe chuo kikuu cha kiislam wakati wa East African Muslim Welfare Society. Wakati huo Waislam walikuwa wanajumui moja tu! yaani madhehebu yote yalikuwa chini ya chombo kimoja nachi ni East African Muslim Welfare Society baada ya kuvunjwa ile ardhi ilihamishwa na kumilikiwa na chombo kipya nacho ni Bakwata wakati huo Ponda hajulikani hata! Baadae Bakwata ikakiwanya kiwanja kile kwa jumuia za kiislamu zilizokuwemo kwenye East African Muslim Welfare Society. Dhehebu la Ismailia lilipewa eneo waliloliuza kwa muumini wao Yusuf Manji kwa ridhaa yao wenyewe! Yusuf Manji hakulinunua eneo lile kutoka kwa Bakwata kina Ponda wanajua hili lakini wanawatumia watu wenye ubongo mdogo kama wewe kufanya fujo ili wao wafaidike!

Kipande kingine waligaiwa Madhehebu ya Ibadhi, Ibadhi nao wakauza kwa muumini wao na kipande kingine walipewa Sunni wamejenga shule ya DYCCC, kipande kingine kuna Markaz kilichobakia kikawa cha bakwata ambacho wameuza na kupewa kiwanja kingine che ukubwa wa hekari 100! ili lile lengo la kujenga chuo cha kiislamu litekelezwe kule kwenye zile heka mia moja. Kina Ponda wanajua hilo lakini hawataki wanataka aliewatuma ndio amilikishwe pale na wao walipe ujira wao!
 
Nadhani wewe ndio hufahamu omba ujulishwe kiwanja kile kilitolewa na Nyerere kujengwe chuo kikuu cha kiislam wakati wa East African Muslim Welfare Society. Wakati huo Waislam walikuwa wanajumui moja tu! yaani madhehebu yote yalikuwa chini ya chombo kimoja nachi ni East African Muslim Welfare Society baada ya kuvunjwa ile ardhi ilihamishwa na kumilikiwa na chombo kipya nacho ni Bakwata wakati huo Ponda hajulikani hata! Baadae Bakwata ikakiwanya kiwanja kile kwa jumuia za kiislamu zilizokuwemo kwenye East African Muslim Welfare Society. Dhehebu la Ismailia lilipewa eneo waliloliuza kwa muumini wao Yusuf Manji kwa ridhaa yao wenyewe! Yusuf Manji hakulinunua eneo lile kutoka kwa Bakwata kina Ponda wanajua hili lakini wanawatumia watu wenye ubongo mdogo kama wewe kufanya fujo ili wao wafaidike!

Kipande kingine waligaiwa Madhehebu ya Ibadhi, Ibadhi nao wakauza kwa muumini wao na kipande kingine walipewa Sunni wamejenga shule ya DYCCC, kipande kingine kuna Markaz kilichobakia kikawa cha bakwata ambacho wameuza na kupewa kiwanja kingine che ukubwa wa hekari 100! ili lile lengo la kujenga chuo cha kiislamu litekelezwe kule kwenye zile heka mia moja. Kina Ponda wanajua hilo lakini hawataki wanataka aliewatuma ndio amilikishwe pale na wao walipe ujira wao!

Asante mkuu kwa elimu hii kwetu sisi ambao tulikua hatujui kinachoendelea!
 
Back
Top Bottom