Nilishawahi kusikiliza hayo mahojiano yake. Michuzi ni mtupu, mwandishi mdosho.
Kwanza, hajui nini cha kusema au kutosema hadharani. Niko dedicated kwenye Blog yangu kuliko kazi yangu Daily News. Kwa kauli hii, angekuwa nchi zenye uwajibikaji, bosi wake angemfukuza kazi. Huyu ni Mhariri Mkuu wa Daily News anasema hivi!
Pili, hajui Kiswahili hata kidogo. Bahati mbaya ama nzuri nilikuwa na Mwalimu mmoja alinifundisha kupiga picha. Sasa, kwa nini bahati mbaya? Alipoulizwa aliingiaje kwenye ku-blog: Namsifu au namlaumu ndugu Ndesanjo kwa kunitia moyo, kunisaidia kuingia kwenye ku-blog. Sasa kwa nini umlaumu? Pia, kasema Daily News ina autononomy, sijui nisemeje Kiswahili. Kumbuka, huyu ni mwandishi wa habari, tena aliyeishi Magomeni, hawezi kujifanya anashindwa kutafsiri au kuelezea neno mamlaka au kujitegemea.
Mwisho lakini sio mwisho kabisa, haelewi nini kinaendelea kisiasa. Alipoulizwa kuhusu ubora wa Kikwete, akaanza kummiminia sifa kama: Kikwete ana mvuto, ni handsome boy. Lakini, Kikwete alisifika kwa ujana, sio uzuri wa sura. Na pia, mtu mzima hawezi kuwa handsome boy kwa sababu sio boy. Labda angesema ana baby face. Angekuwa hajajifanya hajui kujieleza kwa Kiswahili nisingemkosoa kwa sababu sio lugha yake. Akizidi kumsifu Handsome boy Kikwete, kasema huwezi kumshinda kwa wanawake. Tatizo la huyu Handsome boy ni kwamba anadhani matatizo ya nchi ni Mungu kapanga.
Mwisho kabisa, hata kwenye fani yake hiyo hiyo ya upiga picha anachemsha. Blog yake ina picha ambazo zinaorodhesha majina ya walioko kwenye picha bila kusema ni mtu ni wa kushoto au kulia.
Michuzi na Kikwete wote mdosho.