Mjue Donald Trump

Urais ulikuwa wake

Ila ishu ya kujenga ukuta kule mpaka wa meksiko
Pmj na maneno ya kuudhi anaropoka vimemkosesha point

Sio kwamba mama clinton ni mgombea mzuri, ila kwa sababu wanapambana na mtu ambaye tayari ashashindwa kisaikolojia

Mgombea jeb bush ambaye alipigwa chini kwenye kura za maoni angekuwa Rais bora zaid baada ya obama
 
Mgombea bora hadi sasa ni trump hao wengine ni politians they all talk but no action
 
Hizi ni hisia za kipuuzi. Unachotakiwa kujiuliza:
1) Hivi ndani ya Republican hakuna watu wenye uwezo wa kisiasa kuwazidi hawa wa kwetu?
2) Mpaka pale alipofikia hatua ya kuwa mteule wa Chama alijifikisha mwenyewe au watu walimchagua?
3) Kuna wakati mpaka kwenye kura za maoni Trump amekuwa akimzidi Hilary Clinton, ina maana hizo kura za maoni anajipa mwenyewe?
4) Hivi wanaomjua mtu atakayeiongoza Marekani vizuri ni Watanzania au Wamarekani?

Mimi ninaamini kuwa kwa Marekani, mpaka alipofikia huyu Trump ni lazima ana uwezo katika maeneo mengi ambayo Wamarekani wengi hawana. Trump anaweza kushinda uchaguzi wa Marekani kama alivyoshinda Obama (wengi walisema Obama asingeshinda). Na hata akishindwa, mpishano wa kura hautakuwa mkubwa. Hiyo inaonesha kuwa Wamarekani wengi, kwa ulinganisho, wanaona wagombea hawa wawili wanakaribiana sana.

Kwenye ubaguzi sina uhakika kama Trump ni mbaguzi. Marekani ni ya Wamarekani, siyo Wanigeria au Wasaudia au Watanzania. Nchi ya Marekani ambayo watu wake wamewahi kuuwa na magaidi mara kadhaa, magaidi wote wakiwa ni wageni, hata ningekuwa mimi, kwa usalama wa watu wangu ningependekeza hatua kali za udhibiti wa wageni kwaajili ya usalama wa watu wengi.

Trump ameongelea zaidi udhibiti wa wageni, na bahati mbaya wageni hao ni Waarabu, Waafrika na Walatino. Huku hawa wote wakiwa na rekodi mbaya ya matukio ya uhalifu nchini Marekani.

Tujenge nchi zetu ili ziwe ni mahali pazuri pa kuishi kuliko kukimbilia nchi za wengine, tukiamini tunaweza kudictate sera na sheria za ugenini.
 
Kwa historia hii ina maana Trump ni Mmarekani hasa, kama wazazi wake walihamia miaka ya 1800, basi ni Mmarekani asilia maana wengi wa Wamarekani wazazi wao walihamia USA miaka ya 1600 - 1800, ukiwaacha Red Indians.
 
Wamarekani wanaomuunga mkono Trump wanasema kuwa Trump wanamwona ni mkweli wa nafsi yake. Anatamka kilichopo moyoni na akilini mwake, na wanaamini atatenda kama anavyonena.

Wanasema Clinton anatamka kile anachohisi Wamarekani wangependa kusikia hata kama yeye mwenyewe hakiamini. Wamarekani wanataka mtu mkweli kwa nafsi, kauli na vitendo.
 
Mheshimiwa sana Msambichaka Mkinga nilikuwa nakutafuta sana please naomba nisaidie nakupata vipi ndugu yangu samahani kwa kuingilia mada
 
Sipendi kweli hii tabia ya familia flani ndio zinatakiwa zitawale walianza kina Bush now Clinton ni kama hapa kwetu baba alikuwa kiongozi then anajenga mazingira na watoto wake anawaacha kwenye system
 
anabagua waislamu, wamexico weusi, huyu hafai
 
Kujisifu kote kumbe alirithishwa kampuni. Marekani hawana rais kwa staili hii
Hata kama alirithishwa kampuni!! Na ndio imemfanya aje kuwa MTU mkubwa hivo bado n MTU makini kwan wangap wanarithishwa vitu Mali na wazee wao wanakua wa kwanza kufirisika nafkiri mifano hai! Hapa hapa nyumbani!!
 
Nadhani Wamarekani wamelichoka jina la Bush White House.
 
Fikra zako zinasadifu za kwangu,yaani mule mule, nukta kwa nukta neno kwa neno.
Kuna mtu hapo juu anasema wenye mtazamo kama huu ni akili za Lumumba. Yeye anataka jukwa lote wakubaliene na mtazamo wake ndo afurahi
 
ingekua bongo tungesema hana sifa ya kugombea kwani ikulu ni patakatifu hawaingii wanamieleka
Hahahaah
Trump ashafanya mengi sana ambayo angefanya mtu mwingine hata asinge kuwa mgombea, wana nchi wakichoka huwa wana fanya lolote.
Pia mieleka ni bussiness kama nyingine ndio maana kina McMahon wenyewe wanapiga siasa vizuri tuu, so kama ikulu walikaa alikaa Bill Clinton na JFK wachepukaji wazuri tuu kwa nini Trump asifae kisa mieleka!
 
Kwa historia hii ina maana Trump ni Mmarekani hasa, kama wazazi wake walihamia miaka ya 1800, basi ni Mmarekani asilia maana wengi wa Wamarekani wazazi wao walihamia USA miaka ya 1600 - 1800, ukiwaacha Red Indians.
Nakubaliana na wewe kwa sababu kuzaliwa tu Marekani kunakufanya uwe raia hata kama wazazi wako siyo raia. Ila issue hapa ni kwamba kuna Weusi wamekuja miaka mingi, wengine wamezaliwa uko na wazazi ni raia, kuna Wamexico in the same category lakini anawaita bado ni immigrants. Sasa yeye tumuiteje na mke wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…