falcon mombasa
JF-Expert Member
- Mar 5, 2015
- 9,189
- 9,298
wakuu habari
leo ningependezwa kama tungemjadili mfanyabiashara maarufu toka viunga vya magharibi mwa kingston Jamaica
si mwingine bali ni christopher dudus coke mzaliwa wa Jamaica huku akiwa amezaliwa katika familia ya watoto wanne, yeye dudus na kaka zake wawili na dada yake ambao nao waliuwahi kuwawa kutokana na visa vya serikali
Baba yake ambaye alikuwa anaitwa Lester au maarufu kama Jim brown alikuwa anatafutwa kipindi kirefu cha maisha yake na serikali kutokana madai ya kumiliki genge la mihadarati(drug cartel) lililoitwa shower posses ambapo jina hilo lilitokana na madai ya kuwamiminia risasi watu zaidi elfu moja miaka 1980.lakin alifariki mwaka 1992 kwa moto baada sero aliyokuwa amehifadhiwa kusubiri kupelekwa US kujibu mashtaka ya kuuza madawa ya kulevya kuungua
Kwa mujibu wa serikali ya marekani dudus alirithi biashara aliyokuwa anafanya baba yake iki ni pamoja na biashara ya kampuni za ujenzi na burudani
mara kadhaa mwanasheria wake Tom Tavares Finson alinukuliwa akisema mteja wake ni mfanyabiashara na wala hajihusishi na biashara za mihadarati
Dudus alifanikiwa kujiingiza kwenye siasa za jamaica kwa kupata ushawishi ndani ya chama tawala cha Jamaica Labour Party chini ya waziri mkuu wake Bruce Gordin
Dudus "YESU" wa jiji la kingston kwenye viunga vya Tivoli garden vilivyopo magharibi mwa jiji hilo alikuwa ni mtu mwenye ushawishi uliopindukia kwa jamii inayomzunguka.huku akiwa mstari wa mbele kusomesha maelfu ya wajamaica kwa kutumia pesa zake, ni dudus pekee ambaye alikuwa bingwa wa kuchangia pesa nyingi kwenye shughuli zote za kijamii zilizofanyika Tivoli Gardens huku akiwa mstari wa mbele kuhakikisha watu wa Tivoli wanaishi kwa raha mustarehe kwa gharama zake.
Serikali ya marekani ikaanzisha msako wa kumsaka dudus kwa gharama zozote zile
kwa kile kilichoaminika ni muuzaji mkubwa wa dawa za kulevya katika ukanda wa latin America caribean america hadi uk. ndipo kwa kushirikiana na vyombo vya usalama vya jamaica wakaanzisha msako uliodumu wiki nzima kumsaka dudus ndani ya Tivoli huku vikosi vya serikali vikipata upinzani mkubwa toka kwa wananchi walijidhatiti kufa kwa ajili ya kumuokoa dudus wao. ambapo vijana wa jiji la kingston walishikamana kuhakikisha wanapambana na majeshi lakin sio dudu akamatwe kwani nao walijidhatiti na silaha za kivita kwa ajili ya kumlinda YESU wa Tivoli Gardens.
Hadi muda huu "Coke" yuko gerezani anatumikia kifungo chake cha miaka 23 ambapo alihukumiwa mwaka 2010 huku akiwa ameacha mali zinazokadiriwa kufikia dollar za jamaica milion 300.
asanteni
imeandaliwa na
falcon mombasa
leo ningependezwa kama tungemjadili mfanyabiashara maarufu toka viunga vya magharibi mwa kingston Jamaica
si mwingine bali ni christopher dudus coke mzaliwa wa Jamaica huku akiwa amezaliwa katika familia ya watoto wanne, yeye dudus na kaka zake wawili na dada yake ambao nao waliuwahi kuwawa kutokana na visa vya serikali
Baba yake ambaye alikuwa anaitwa Lester au maarufu kama Jim brown alikuwa anatafutwa kipindi kirefu cha maisha yake na serikali kutokana madai ya kumiliki genge la mihadarati(drug cartel) lililoitwa shower posses ambapo jina hilo lilitokana na madai ya kuwamiminia risasi watu zaidi elfu moja miaka 1980.lakin alifariki mwaka 1992 kwa moto baada sero aliyokuwa amehifadhiwa kusubiri kupelekwa US kujibu mashtaka ya kuuza madawa ya kulevya kuungua
Kwa mujibu wa serikali ya marekani dudus alirithi biashara aliyokuwa anafanya baba yake iki ni pamoja na biashara ya kampuni za ujenzi na burudani
mara kadhaa mwanasheria wake Tom Tavares Finson alinukuliwa akisema mteja wake ni mfanyabiashara na wala hajihusishi na biashara za mihadarati
Dudus alifanikiwa kujiingiza kwenye siasa za jamaica kwa kupata ushawishi ndani ya chama tawala cha Jamaica Labour Party chini ya waziri mkuu wake Bruce Gordin
Dudus "YESU" wa jiji la kingston kwenye viunga vya Tivoli garden vilivyopo magharibi mwa jiji hilo alikuwa ni mtu mwenye ushawishi uliopindukia kwa jamii inayomzunguka.huku akiwa mstari wa mbele kusomesha maelfu ya wajamaica kwa kutumia pesa zake, ni dudus pekee ambaye alikuwa bingwa wa kuchangia pesa nyingi kwenye shughuli zote za kijamii zilizofanyika Tivoli Gardens huku akiwa mstari wa mbele kuhakikisha watu wa Tivoli wanaishi kwa raha mustarehe kwa gharama zake.
Serikali ya marekani ikaanzisha msako wa kumsaka dudus kwa gharama zozote zile
kwa kile kilichoaminika ni muuzaji mkubwa wa dawa za kulevya katika ukanda wa latin America caribean america hadi uk. ndipo kwa kushirikiana na vyombo vya usalama vya jamaica wakaanzisha msako uliodumu wiki nzima kumsaka dudus ndani ya Tivoli huku vikosi vya serikali vikipata upinzani mkubwa toka kwa wananchi walijidhatiti kufa kwa ajili ya kumuokoa dudus wao. ambapo vijana wa jiji la kingston walishikamana kuhakikisha wanapambana na majeshi lakin sio dudu akamatwe kwani nao walijidhatiti na silaha za kivita kwa ajili ya kumlinda YESU wa Tivoli Gardens.
Hadi muda huu "Coke" yuko gerezani anatumikia kifungo chake cha miaka 23 ambapo alihukumiwa mwaka 2010 huku akiwa ameacha mali zinazokadiriwa kufikia dollar za jamaica milion 300.
asanteni
imeandaliwa na
falcon mombasa