ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Enzi zile ambazo hata mawasiliano ya simu au barua hayakuwa rahisi, ilikuwa haipiti mwezi bila kupokea mgeni kutoka kijijini kwetu na mara nyingi ni ndugu wa mbali na karibu ambao wengi wakija wanasema wanapita kwenda sehemu na wameelekezwa tu nyumbani (kijijini) wafikie kwetu au pengine kama ni ndugu wanasema "wamekuja kupumzika tu, kilimo kigumu huko kijijini".
Wakati ule ilitulazimu sisi watoto kutoka vyumbani na tulale chini sebuleni au barazani ili kupisha mgeni . Hali pia hata ya chakula ilikuwa ngumu kwani kipato cha mzee hakikuwa njema sana hivyo hata kama ilikuwa ratiba ya nyama na "mpunga", ilibidi tuhamishiwe kwenye "ugali wa dona" na maharagwe au "dagaa wa Mwanza" ili kujibana kwa ukubwa ule wa familia(ni zile enzi za sera za uhujumu uchumi).
Mara zote utakuta hata wakiwa wanaondoka ilimlazimu mzee wape nauli kwani siku hizo walidai hata nauli ya kujia walikopa huko kijiji. Hali nilidhani itabadilika baada ya Mzee kustaafu na kurejea kijijini, ambapo hata hivyo alikuwa akiishi kwa kuchekwa na wanakijji kuwa amechezea maisha akiwa kazini mpaka imembidi arudi shoka mbaya huko kijijini utadhani hakufanya kazi.
Wajibu wa kuhudumia ndugu ni kama uliahmia "automatic" toka kwa wazazi na kuja kwetu watoto baada ya wao kuzeeka. Nikiwa bado sijaoa, mjomba alizoe kuja toka kijiji akiwa na biashara ya kule "koroboi" kwenye soko kubwa ambapo aliuza kwa jumla kupitia madalali. Kwa kuwa nilikuwa na vyumba viwili vya kulala alikuwa akilala katika moja ya hicho chumba.
Hata baada ya kuoa, Mjomba aliendelea kuja tu....sasa Mungu katujalia na Mke wangu tuna watoto wawili. Hivi karibuni Mjomba alikuja na cha kusikitisha alikuja na mwanamke ambaye anadai ni "shangazi mdogo" (mimi sikuwahi kumwona wala kusikia).
Kwa kuwa chumba alichozoea kufikia Mjomba walikuwa wakilala watoto na isitoshe hakina "ceiling board", baada ya kujadiliana sana mke wangu tulikubalina kuwa kwa heshima, labda nimuulize kama mjomba atakubali ulala sebulani na huyo "shangazi" alale na watoto chumbani au vipi tuwatafutie nyumba ya kulala wageni (gesti)
Baada ya kumweleza Mjomba , alikuja juu kama mbogo akidai kuwa yeye hawezi kutenganishwa na mkewe na kuwa uamuzi wa kumtafutia gesti ni kumdhalilisha sana kwani yeye hajawahi kulala gesti hata siku moja na mkewe katika maisha yake wakati yupo karibu na ndugu. Ailidai kuwa kama ni kutafuta gesti basi angefanya mwenyewe na sio sisi watoto tumtafutie yeye akalale na mkewe huko...
Akiwa na hasira kali , jioni hiyo hiyo alikusanya mizigo yake na huyo "shangazi", na pasipo hata kuaga akatimka zake na siku iliyofuata tukatapa taarifa kuwa alitafuta ndugu wa kwetu alikuwa akimfahamu akaenda kulala kwake na kusimulia kisa kuwa sisi tulimfukuza na kuapa kuwa kamwe hatakanyaga tena kwetu kwa dharau zile tulizomwonyesha mbele ya mkewe....
Wakati ule ilitulazimu sisi watoto kutoka vyumbani na tulale chini sebuleni au barazani ili kupisha mgeni . Hali pia hata ya chakula ilikuwa ngumu kwani kipato cha mzee hakikuwa njema sana hivyo hata kama ilikuwa ratiba ya nyama na "mpunga", ilibidi tuhamishiwe kwenye "ugali wa dona" na maharagwe au "dagaa wa Mwanza" ili kujibana kwa ukubwa ule wa familia(ni zile enzi za sera za uhujumu uchumi).
Mara zote utakuta hata wakiwa wanaondoka ilimlazimu mzee wape nauli kwani siku hizo walidai hata nauli ya kujia walikopa huko kijiji. Hali nilidhani itabadilika baada ya Mzee kustaafu na kurejea kijijini, ambapo hata hivyo alikuwa akiishi kwa kuchekwa na wanakijji kuwa amechezea maisha akiwa kazini mpaka imembidi arudi shoka mbaya huko kijijini utadhani hakufanya kazi.
Wajibu wa kuhudumia ndugu ni kama uliahmia "automatic" toka kwa wazazi na kuja kwetu watoto baada ya wao kuzeeka. Nikiwa bado sijaoa, mjomba alizoe kuja toka kijiji akiwa na biashara ya kule "koroboi" kwenye soko kubwa ambapo aliuza kwa jumla kupitia madalali. Kwa kuwa nilikuwa na vyumba viwili vya kulala alikuwa akilala katika moja ya hicho chumba.
Hata baada ya kuoa, Mjomba aliendelea kuja tu....sasa Mungu katujalia na Mke wangu tuna watoto wawili. Hivi karibuni Mjomba alikuja na cha kusikitisha alikuja na mwanamke ambaye anadai ni "shangazi mdogo" (mimi sikuwahi kumwona wala kusikia).
Kwa kuwa chumba alichozoea kufikia Mjomba walikuwa wakilala watoto na isitoshe hakina "ceiling board", baada ya kujadiliana sana mke wangu tulikubalina kuwa kwa heshima, labda nimuulize kama mjomba atakubali ulala sebulani na huyo "shangazi" alale na watoto chumbani au vipi tuwatafutie nyumba ya kulala wageni (gesti)
Baada ya kumweleza Mjomba , alikuja juu kama mbogo akidai kuwa yeye hawezi kutenganishwa na mkewe na kuwa uamuzi wa kumtafutia gesti ni kumdhalilisha sana kwani yeye hajawahi kulala gesti hata siku moja na mkewe katika maisha yake wakati yupo karibu na ndugu. Ailidai kuwa kama ni kutafuta gesti basi angefanya mwenyewe na sio sisi watoto tumtafutie yeye akalale na mkewe huko...
Akiwa na hasira kali , jioni hiyo hiyo alikusanya mizigo yake na huyo "shangazi", na pasipo hata kuaga akatimka zake na siku iliyofuata tukatapa taarifa kuwa alitafuta ndugu wa kwetu alikuwa akimfahamu akaenda kulala kwake na kusimulia kisa kuwa sisi tulimfukuza na kuapa kuwa kamwe hatakanyaga tena kwetu kwa dharau zile tulizomwonyesha mbele ya mkewe....