Mjikumbushe Mzumbe High School

Kweli mdau umetukumbusha mbali....mi nilikuwepo pale miaka ya 1995. Nakumbuka wengi wa hao waalimu...enzi zetu Headmaster alikuwa Mr Msuka...as a matter of fact..hiyo ilikuwa statement yake ya kufungulia speech parade.
Kuna mwalimu mmoja tulikuwa tunamwita Chuck Norris.....nimesahau jina lake aisee.

Msamiati wa Uchi wa Shangazi mnaukumbuka? Morris dereva alikuwa anajiita form six-combination PCO..hahahaaaaa!!!

Mzumbe imewatoa wengi sana aisee....siku hizi hamna special anymore....nakumbuka si tulikuwa special wa mwanzo mwanzo..tehetehetehe.....!!!

Msamiati wa Mongwe ulikuwa una maanisha kuwa umechacha...huna hela.
 
Duh!Wadau mmenifanya nimecheka sana kwa ofisi maana mmenikumbusha misamiati iliyokuwa imeshanitoka kabisaa
 
Kwa wale mliyosoma miaka ya 2000's mnakumbuka kuosha macho mida ya jioni baada ya kula msuli?
 
kujikumbusha siyo mbaya ni nzuri pia inajenga mahusiano makubwa miongoni mwa watu hivyo wala msiwapinge hata mimi ambaye sijasoma huko na furahi sana kusoma hizi past kwani zina nikumbusha mbali sana
 
Mi namkumbuka emily patrick t.o 2003, sebastian maganga t.o2004 na wengineo jamaa walikuwa vichwa mbaya
 
Duh, ama kweli nimekumbuka mbali sana. Inaonekana brother mimindiokile ulikuwa unakaa KIJIJI cha MIRAMBO BWENI No 3, kwa sababu Church man, Kijana wa Mzinga Jeshini, Shukuru, Karadoga wote hawa walikuwa bweni hilo. Nami naomba niwakumbushe wana Mzumbe vita ya kugombea wachezaji wa football.....Phinias Phares amepangiwa Mirambo, itakuaje achezee SHAABAN ROBERT nk... Namkumbuka brother mmoja tulimwita ZINJATHROPOUS kutokana na kujaaliwa vinyweleo vingi mwilini. Ingekuwa vema kama kupitia JF tutatambuana uwepo wa kila mwanaMzumbe na kuunganisha mawazo yenye kujenga. ALUMNI ni wazo jema kabisa. Naukumbuka wimbo wa shule......... "Malezi ya Mzumbe, elimu yake ni kamilifu ya kitanzania daima mbele nyuma mwiko" kupitia wimbo ule tulitoa ahadi "vijijini pia na mijini matunda yake yaonekana" yaah those good old days. Nawakumbuka brother MKUMBO Mitula, John Mongela alikuwa Katibu wa KIJIJI cha Mirambo, James Bwana Sports Chairman na bonge la Midfield wa Mirambo. Brother PITA BILA M/Kiti wa kiji Mirambo. Mnaukumbuka wimbo wa BAGENDA ADUMU? Tumlinde na tumuenzi katika Mzumbe? Duh ni mengi ya kukumbuka.
 
Duh! Kweli nimezeeka. Nimejaribu kufuatilia thread hii labda nitakuta majina ya jamaa niliokuwa nao A level 1979/81 pale Mzumbe "Shule ya Wanaume' sijayaona. Kuna mmoja kamtaja Judge Makaramba. Huyo tulikuwa naye pamoja na akina SAIDI SAIDI BAHROON (marehemu) alikuwa akipiga soka wacha mchezo! Pia kulikuwa na wanasoka wengine mahiri kama akina FINTAN DUMA 'Super Six', MAULIDI, JUMA CHEGENI (Kipa). Kulikuwa pia na timu kali sana ya basketball ikiundwa na akina ALFRED BINADAMU, MWANJAPAHI, ABDUL TEKELO, NYANDUGA, RUGARABAMU, MWITUMBA, na wengineo nimewasahau kwa majina. Ni miaka mingi mno imepita! Ilikuwa ni enzi za Headmaster COSMAS GANDAWEGA. Nitafurahi sana kujua waliko baadhi ya washikaji wa enzi hizo. Namkumbuka pia CHARLES KENYELA (sasa RPC Kiinondoni) wakati huo akiwa Form Five. Halafu kulikuwa na vijana watundu sana 'O' Level akina ANTHONY NAKATI, MOHAMED KIGANJA, RABDI MARIJANI, OMARI KIJAZI, TIBANYENDERA, HUSSEIN MACHOZI, (sio huyu mwanamuziki) na wengine wengi.
 
Nimekumbuka mbali sana,miaka ile ya 91-93 ,yule mpishi shangazi,mr KABARE mwl wa BIOS ,mr NDALU CHEM,MAMA MWIYENGE na usmart wake,Marehem Mkomboti na Mr ABOOD bus.Graduation wakaja DAKAWA ikawa issue kwa KILEI,wale F.6 WA 93 mnakumbuka ugali na mahomeboys(DAGAA KAUZU),Vipi ule mchakamchaka c ulikuwa poa kiafya. Kweli mzumbe vimepita vichwa ,wakowapi RAMADHAN ZONGO,BENO CHELELE, na wengine wengi, NAUNGA MKONO WAZO LA KUWA MZUMBE EX BLOG
 
Ni furaha kubwa sana kurudi tena kwa mara ya pili ndani ya Jamii Forums, nilipolala i felt Memory ikianza kupata moto nami pia nimekumbuka baadhi ya majina ya Waalimu na Wanafunzi - Ignatus Nangawe, Wabu Matipuka, James Lugembe "Shoka", Francis Mataula, David Magwila, Erasmus Dennis Buberwa, David Athuman "Mchanifu", Kassim Msami, Rodrick Mpogolo, Emmanuel Mahimbo, Geofrey Mhando, Nuru Ndile, William George, Andrew Wawa, Faustine Mduda, Kigobanya, Obed Kayawaya, Peter Billa, Ekwabi Mijungu, Edson Makallo, Joseph Mathias, Paul Kitaly, Mdenye, Mdede, Lemuel Kilallo, Cretus Peter Mnyanga, Lucas, Christopher Shemahonge, Crystogonius Masusu, Wanini Athuman, Kashenge Kimario, Collins Lutenge, Francis Mbenjile, Mussa Sadock, Zhao Ngesile, Baraka, Zephania "Church Man", Abdallah "Mtoto wa Mzinga - Jeshini", Chalesi "Kinara", Shilinde Nzweke, Enock Ndezi "Bob Ndezi", Simon Pasua, Kigume, Ralph Meela, Nolasco Paul Mbepera, Dotto Andrew, Richard Mshyota, Shukuru Basana, Augustine Karadoga, Lupindilwa Luchagula Mulula, Mjusi, Kumalija Mbingu, Mchome, Gilman Nyamubi, Watson Nsaji Mwakyusa, Hanzen Sanga, Phineas, Kinara Maswaga, James Msalika, Nehemia Kamalango'mbe. Majina mengine yanakuja halafu yanapotea kwani ni miaka mingi sana toka mwaka 1991 ni takribani miaka 19 sasa!.

Waalimu - Mwl. Mgonde, Mwl. Chimile (RIP), Mwl. Mikapagalo, Mwalimu Ndiva, Kulikuwa pia na Mwalimu asiyeona jina limenitoka, Head Master

Bagenda, Headmaster Kihawa na Mkewe alikuwa Nesi pale Dispensary.[Headmaster huyu katika zunguka yangu kutafuta mlo alikuwa Wiza Schools - Mbeya ofcourse kama Headmaster, Mwl. Mlelwa mara ya mwisho nilimuona huko Handeni kama Headmaster wa Handeni Secondary
School. Jamani kuna Mwalimu pia jina limenitoka tuliambiwa alikuwa msanifu wa Wimbo wa Shule - "Shule Yetu Mzumbe yasifika sana........,
Malezi ya Mzumbe ni Kimilifu ya Kitanzania........, Elimu ya Mzumbe........ nakuendelea, Mwl. Minangi.

Mganga wa Shule - Jina lake lilikuwa Maganga? Sikumbuki vizuri.

Tulikuwa na Gazeti la Wanafunzi wakora kule ****** - shule ambapo Waandishi na Wachoraji Mahiri walikuwa wanatoa habari nyeti na motomoto kuhusiana na matukio mbalimbali yaliokuwa yakitokea pale shuleni. Katika safari ya maisha kuna wengi ambao tayari wametangulia mbele ya Haki:
1. Raphael Mwatwinza.
2. Conrad Dustan Mnywambele "Sauti ya Kamachumu".
3. Nijimbele Gideon.
4. George Sindani.
5. Lusimba Midaba.
Naambiwa list ni ndefu sana hivyo kwa yeyote mwenye jipya atumuvuzishie - Zuri au Baya.

Msamiati: Mavuzi - Mboga ya Kabichi, Hunde - akina dada wale wanaofanana na baba zao, walikuwa wanagombaniwa sana pale ka mpira wa
kona, Mchanifu - Msanii, Anasa - Maandazi ya mke wa Mwl. Omari [alikuwa Kocha pia] nimewahi kumuona huko Pangani, Mharibifu - msamiati huu ulikuja baada ya mfanyakazi mmoja wa pale shule kuoa mdada ambaye alikuwa hawalingani kiumri hivyo watundu wakaja na usemi huu kuwa ni mharibifu, Killer Kala - Rangi inayoua [Msamiati huu uliletwa na watu wenye msimamo mkali kuhusiana na dada zenu hao kutupeleka kasi hata tuliwahi kama sikukumbuki vizuri tulicheza Bull Dance once na baadae tulifanya partneship na wanafunzi wa Kwilo],
Mbu Jazz Band - Nadhani mwakumbuka wale Mbu pale na Cerebral Malaria [Joining Instructions ilikuwa na phrase tata - Net ni muhimu lakini sio lazima au Net ni lazima lakini sio muhimu, sikumbuki vizuri. Dikodiko - Siku za Jumamosi vijana walikuwa wanakarabati vyakula kwa majiko ya umeme mabwenini, kwa kuchanga na kununua kuku IDM almradi Chakula siku ile kilikuwa kinaleta raha esp. Mirambo Village.

Nisiyoyasahau:
1. Dispensary haikuwa na dawa na mganga naye alikuwa na mambo mengi, kama kawaida wanafunzi tulikuwa na tabia ya kuunga Azimio la Arusha kwenda Mzinga Hospital tena kwa kutoroka siku ya Jumamosi bahati mbaya kufika Hospitali badala ya kupata huduma na kurudi shule Daktari aligoma kabisa kuniruhusu kwakuwa hali haikuwa nzuri, Kimbembe kilikuwa kwa mwenzangu ambaye ndie alinisindikiza atawaambia vipi utawala wa shule, kuna mwanafunzi amelazwa?!.

2. Baada ya pitapita ya Promosheni ya Waalimu pale shule, nadhani baada ya Bagenda kuondoka. Mwl. Chimile (RIP) alipata U-Second Master, sasa wakati ule tayari tulikuwa tunakaribia sana kufanya mithihani, kila mtu alikuwa na excuse zake kutokwenda Assembly mie nikiwa mmoja wao, Si mwakumbuka net zilikuwa lazima zitundikwe juu. Kuna jamaa ule mtego wa Mbu ulishapoteza dira, ilikuwa nyeupe lakini hakuwa akiitendea haki ilibadilika ikawa ndio chaka la wakwepa Assembly ukiireremsha hakuna aliekuwa akikuona basi hilo ndilo lilikuwa chaka langu mpaka muda wa kuingia darasani. Nadhani Mwl. Chimile (RIP) alikuwa anafuatilia kwa karibu sana kwani siku ile nilikamatwa kama Saddam pale pangoni. Nilikuwa bize naendelea kupata shule nadhani alikaa kama dk. 5 mimi nilikuwa simuoni. Alifunua Net akasema nenda Assembly nikapiga Magoti mpaka muda wa Assembly umeisha, Nikaingia Darasani that was it hakuwahi kuniuliza wala kupata Adhabu zaidi ya ile ambayo ilikuwa hardly 10 Minutes.

3. Mnakumbuka enzi za Disco kule Kilei na hata Mzumbe kulikuwa na Madaraja ukumbini from First Class mpaka Third Class huko watu ni muziki kwa kwenda mbele yaani washika mchuma [un-mademu] na mademu kutudanganya majina wengine walikuwa wanapewa majina ya mabasi. Walahi ufisadi ulianza zamani, na visiting day watu wanapeleka mikate na siku hiyo unapiga mswaki sana, nywele unapiga cut iliyokwenda shule si mnawakumbuka vinyozi maarufu. Pale Morogoro kulikuwa na jamaa alikuwa anawatia watu joto kuhusu watoto wa killer Colour - Alex Mikate, Mnamkumbuka.

4. Je, Siku za kazi shambani na Club's day na Prep ya mchana baada ya mlo, Si waalimu wakali walikuwa wanapita kuangalia wanaopiga stori na kulala mchana. Hivyo solution ilikuwa kupanda na kujificha juu ya dari. Kuna jamaa aliteremka nalo, jina silikumbuki vizuri ndio ukawa mchezo huo umepungua.

5. Kuiba machungwa ya shule na kuficha kwenye Ma-locker au viazi na kuchemsha kwa Heater Mwitu [Spring za Vitanda]

6. Uzamiaji wa msosi Mzumbe, Unaoga na kuvaa koti pamoja na kijiko. Kwanini Koti?, Lilikuwa linajenga personality. Ole wako ushtukiwe na
walinzi watakufukuza kama mwizi na kijiko chako mkononi. Tabia hii ilipungua watu wakawa wanakula kwa Ma-poti wao [Home boy] mabwenini pale chuoni.

7. Vita vya kujikomboa kutoka kuvaa Kaptura za kaki hadi kuvaa Suruali nyeusi.

8. Mgomo baridi wa chakula ambacho hakikuwa kizuri especially madondo lakini jamaa zetu wengine wakatusaliti walizidiwa na njaa ikabidi wale tu, nadhani mnawakumbuka.

9. Michezo na vijana wa mazimbu - wapigania uhuru.

10. Siku ambayo vijana walikula doria usiku mzima baada ya kutembelewa na Kina dada wa Msalato Girls. Mnaikumbuka hiyo?. Walilala Mirambo Village Dorm. #4 or #3. Ikaleta manungu'niko kwa dada zetu wa Kilakala.

11. Siku ya Nyali na Nyama au siku ya ugali na kabichi - {Siku ya kabichi ilikuwa siku ngumu sana na haswa kama huna jinsi ya kukarakachua miundo mbinu ili upate mbadala]

12. Siku ya Jumamosi ilikuwa ni kama siku ambayo unajikomboa, kwani baada ya shughuli ya usafi na ukaguzi na matangazo ya hapa na pale,
unakuwa huru ukisubiri misosi ya mitaani au unaenda kubadilisha mkaango mjini au pale mwanzo wa lami ya kupaka kuja chuoni IDM ukila miwa. Jioni unawahi Roll Call halafu wasubiria wali tena ukivuta hisia ya Kideo cha Mwl. Myenge. Wengine watafuata Uzo "gongo" Changalawe. Watu wa dini watakuwa wakisali na kuimba. Almradi Jmosi ilikuwa inasaidia sana kutoa msongo.

Na zile trip za Tangeni zilisaidia sana kuamsha ari ya kufanya kazi kwa bidii, usafi bila viboko.

Ya kukumbuka ni mengi sana i hope wengine watasaidia kuleta raha ya zamani.

Natarajia kusikia mengi kutoka pembe mbalimbazi za dunia hii.

Naomba kuwasilisha.

NB: HuXiang umenena itakuwa ni kitu cha maana kuwa na wavuti dedicated kwa Wazumbe [Alumni].


Brother Mimindiokile umenikumbusha sana Kijiji cha MIRAMBO hasa bweni namba 3. Church man, Karadoga, Shukuru, Clemence Mwashambwa na wengi uliowataja nilikuwa nakaa nao katika bweni hilo. Huenda nikawa nafit ktk utambulisho wako wa Mtoto wa Mzinga Jeshini...............Kuna muungwana amemtaja brother Ndezi, Bob Ndezi, nasikitika kusema kuwa nilimkuta home kwao Igunga, anaonekana kutatizika na matatizo ya ufahamu kwa sasa, nilimsababhi na kumkumbusha kuhusu Mzumbe lakini hatukua ktk frequence moja. Jamaa wa pembeni wakasema anasumbuka na matatizo ya akili. Mungu amsaidie apone. Yako mengi ya kukumbuka kuhusu MZUMBE. Wazo la kuwa na Alumni ni zuri sana, litatuunganisha na kutoa mchango wa kuisaidia shule kwa namna moja ama nyingine.
Mungu ibariki Mzumbe
 
Well well man wangu.......ma TO nawaona ovyoo sana kazi hawajui material hamna kichwani i could say that walikuwa wanakariri as Wibonele(nimem miss Wibo) alivyowalikishia pepa......Nani asiyejua mzumbe wanapewa pepa(maswali) kabla ya mtihani.Kuna To mmoja nilienda nae sehemu fulani alikimbia akarudi Bongo kwenye elimu ya kukariri.

Kwenye red and his wife are no more in this world!!!!!!!!!
 
mmenikumbusha mbali sana mimimnilikuwa mzumbe kwa miaka sita 1995-2000 nilikuwa mkwawa namba nne namkumbuka mwalimu minja alitutandika darasa zima form one A kisa kumkumbushia muda wa kipindi chake cha english ulikuwa bado; tunawakumbuka enzi hizo mwalimu mkumbo ,bitwale, T.D.K. MSUKAhead master,mwasha marehemu wibonele, kabale(mganda) wazumbe wengi ni madaktari,mainjinia na wahasibu,tuache chuki binafsi kama ulishindwa kuachieve ulipokuwa mzumbe usitake kuwaaminisha watu kama wazumbe walikuwa wanpewa paper,katika darasa letu la PCB tulikuwa 25 ishirini wote tulikwenda muhimbili,2 walikwenda abrod na wawili walikwenda mlimani kuchukua bicom
 
Minja bado yupo.
Sapila,Mtawajibu,Malale,Mtesigwa wamepata Kuwa Head Master kwenye shule za Kata.
Matekele yuko Mzumbe University anapigisha vijana elimu.

Sapila du nimemmiss. Minja anawakumbuka almost wanafunzi wote aliowafundisha. Those days. Those days!!
 
jamani mimi nawakumbuka GREYSON NYANTAMBA,LUSEKELO KIBONA,BENJAMIN AMOS,ASAJILE JOHN,JOSIAH NOMBO,DANIEL NGONDYA,KWAME etc
 
Bila shaka Wana Mzumbe mpo hapa JF, nimetumwa kuwakumbuka wafuatao John Mongela, James Bwana, Michael Thomas Sebastian Sarota, Hassan Rajab Hassan, Patrick Maleva, Anderson Segereti, David Black, Obed Mwakitalika, Clement Mwashambwa, Kwela Mgaya, Theophil Alexander, Njaule Mdendu, Johnson Jasson, Sollomon Shati, Obed Msenga, Charles Nakembetwa, Gideon Mandesi, Isaac Kassanga, Dereck Kassanga, Deus Changala, Timilai Sheshangali, Shemaghembe Ntulwe, Sainet Katulunga, na wengine wengi sana. Waliosoma pale mmeombwa kuongezea majina ya wale mnaowakumbuka.

Wengine ni Yohana Punguja, Mathew Maziku, Fikiri Charles, Batandika Mtaganya, Nkuba, Paul Daud.
 
mmenikumbusha mbali sana mimimnilikuwa mzumbe kwa miaka sita 1995-2000 nilikuwa mkwawa namba nne namkumbuka mwalimu minja alitutandika darasa zima form one A kisa kumkumbushia muda wa kipindi chake cha english ulikuwa bado; tunawakumbuka enzi hizo mwalimu mkumbo ,bitwale, T.D.K. MSUKAhead master,mwasha marehemu wibonele, kabale(mganda) wazumbe wengi ni madaktari,mainjinia na wahasibu,tuache chuki binafsi kama ulishindwa kuachieve ulipokuwa mzumbe usitake kuwaaminisha watu kama wazumbe walikuwa wanpewa paper,katika darasa letu la PCB tulikuwa 25 ishirini wote tulikwenda muhimbili,2 walikwenda abrod na wawili walikwenda mlimani kuchukua bicom

Hahahah......Sasa mtwambie Jamii ya waTanzania mnaisaidiaje baada ya kupata elimu iliyotukuka? Maana wengi wa hawa watu ndo wamekuja kuwa zao na kizazi cha mafisadi Tanzania yetu ya leo.
 
Daaah! My Goosebumps Have Erected Mlipotaja IDM, Mongwe, Salo
Kilakala, Kilima Hewa, Nk
By The Way Nilikuwa Member Wa Mkwawa 4 Mpaka Namaliza A-level
Mvua Ikinyesha Ilo Tope Ni Kero
Indeed Mzumbe Was Unforgettable
Place To Every Person Who Ever Lived There.
Viva Mzumbe Secondary
School Song- Shule Yetu Mzumbe
 
Intake Yetu Tulikuwa Na Hawa Giants Of Ages
Hudson Walter Kitambawazi,Ntuli Kelvin Mwamukonda, Lucas Ferran Kweka, Hussein Hamza Hussein, Patrick Henry Mtui, Misana Masami Manyege, Godfrey Jordan Mahai, Lameck Liheta, Ibrahim Ramadhan, Ibrahim Mdalingwa, Aidan Alexander Kitaly, Gilbert William Shechambo, Samuel Safari Mbughi, Francis Mlelwa, Dastan Mbunda , Kelvin Peter Mruma, Innocen Ngonyani Kasuti, Jordan Seimu, Prosper Mkongwa, Hatibu Diwani, Daud Ndunguru, Sadam Mpacha, Mathias Raphael, Everest Madata, Israel Kihanga, Maige Joseph Maige, Stanslaus Frolence, Francis Ndiwayi, Kasian Kayombo.
 
Msabila Right Now Ni Lecturer Wa Mzumbe University Pia Mwenyekiti Wa Bodi Ya Mzumbe Sekondari.
 
Bubu Msemaovyo ...You have made my day! Leo ujasema ovyo! By the way, jina lako na unayoyasema hayaendani! Good memories are good things to cherish, najua HuXiang yapo yaliyokupata hata hataki kusikia majina kama bonge la mwanasoka wa enzi hizo na mwanasheria mzuri wa leo 'James Mbwana' au mzamiaji wa kilakala (mtoto wa mama, na rafiki yangu) na mkuu wa mkoa wa leo Mr John Mongela just to name a few! Wengine tunakumbuka mengi na sio kwa sifa wala sio kwa yaliyokupata HuXiang!
 
Back
Top Bottom