mchillo
JF-Expert Member
- Oct 13, 2010
- 500
- 224
Mafundisho ya kiislamu yako wazi, hilo suala ni haramu. Suala la mahakama kutokutoa maamuzi magumu, sijajua unaongelea kesi gani hapa. Maana ni sawa na mwizi auawe mtaani na wananchi wanaoitwa wana hasira halafu wewe uulize ni kwa nini mahakama ya hakimu mkazi kisutu haitoi maamuzi magumu.
Kitu kingine acha kuchanyanganya mambo, hakuna mtu anayeweza kumtetea Mungu. watu wako tayari kupambana kusimamia kile wanachokiamini na hili ni jambo la kawaida kwa watu wenye akili na wanaojitambua. Kwa mfano hata Marekani iko tayari kupambana kutetea demokrasia kwa kuwa ndio kitu inachokiamini na kusimamia, hata Urusi kuna kipindi walikuwa tayari kupambana kutetea ukomunisti. Kwa muktadha huo huo, hata waislamu nao wako tayari kutetea kile wanachokiamini, acha kupotosha kuwa wanamtetea Mungu. Mungu haitaji kutetewa na yeyote. Wewe kama unaamini kitu halafu huwezi kukisimamia utakuwa na matatizo sana katika kile unachokiamini.
Kusimamia unachokiamini ni pamoja na kuwateka nyara vigori, kwenda kuwabaka na wengine kuwagawa kwa "wanaohitaji" huduma, kujilipua ukiuwa watu wa kila aina, waislamu kwa wasio waislamu, ikiwa ni pamoja na watoto, kina mama waja wazito tena kwa jina la mungu mnayemtambulisha kwa jina la Allah?