Mjadala wa Mikoa Masikini Waligawa Bunge

Mjadala wa Mikoa Masikini Waligawa Bunge

tupate orginal source ya hizo data na details kidogo, maana huwezi kupinga kwa kusikia bila kuperuzi hizo orginal sensus data
 
Jamani Mwanza na kagera ni masikini na inahitaji msaada mkubwa wakiserikali
 
Tanzania yote ni masikini hakuna cha dodoma,mbeya,Dar es salam wala Arusha yenye unafuuu sehemu zote hizo vitu vingi ambavyo ni matumizi ya kawaida tuu inaonekana ni anasa...
Yote kwa kweli choka mbaya, basi tu kibongobongo tunajifariji, lakini kiuhalisia hamna kitu!
 
Ndo kusema Dodoma ninayoifahamu ina unafuu (utajiri ) kushinda Mwanza?
Nchi takwimu nyingi zitolewazo huwa ni za jikoni.
Katika uhalisia na hali yoyote Pwani, Shinyanga, Dodoma, Mara, Tabora na mikoa mingine mingi haiwezi izidi Mwanza kiuchumi kwa leo labda kesho.
Mtoa takwimu ni vyema akatuambia hizo data ni za mwaka huu au some decades back to 19kweusi.
 
Ndo kusema Dodoma ninayoifahamu ina unafuu (utajiri ) kushinda Mwanza?
Nchi takwimu nyingi zitolewazo huwa ni za jikoni.
Katika uhalisia na hali yoyote Pwani, Shinyanga, Dodoma, Mara, Tabora na mikoa mingine mingi haiwezi izidi Mwanza kiuchumi kwa leo labda kesho.
Mtoa takwimu ni vyema akatuambia hizo data ni za mwaka huu au some decades back to 19kweusi.
 
Takwimu za mwendokasi ili kuhalalisha upendeleo kwa mkoa flani uliofichwa ndani ya mikoa tajwa. Akili za kuambiwa........
 
1 mkoa maskini ni jiji na una mitandao ya barabara zinazopitika misimu yote hii haiwezekani jiji lkikawa maskini kuliko miji ya kawaida labda mimi nimefikiria kwa kichwa kidogo?

2 mkoa maskini unalipa kodi kuliko mikoa mingine nchini isipokuwa mmoja tu, maskini wanatoa wapi pesa ya kulipa kodi kama hata ya mlo mmoja ni shida? au hii kodi siku hizi inakusanywa kwa kupora?

3 mkoa maskini una ziwa kubwa na viwanda vya pamba na kuchakata samaki ni wapi penye miundo mbinu ya namna hii pakawa maskini?

4 mkoa maskini una mgodi mkubwa kabisa wa dhahabu na ardhi safi ya kilimo na ufugaji inawezekanaje au mimi siijui geita?

5 mkoa maskini kabisa tunashindwa kupeleka huduma za kuondoa umaskin huo badala yake tunapeleka uwanja wa ndege are we serious? nani apande hizo ndege kwenda mkoa maskini?

6 mkoa wenye tajiri miezi kadhaa iliyopita wananchi wake walilazimika kula viwavi kutokana na balaa la njaa hii nayo inatokea tanzania tu. maskini hana njaa tajiri analazimika kula viwavi. duh.😵

7 mkoa maskini kabisa una ziwa zuri sana kwa uvuvi ardhi safi ya kilimo na haujawahi kuripotiwa popote kukumbwa na ukame wala njaa mikoa iliyokuwa na ukame na hatua za dharura kuondoa njaa ni tajiri. duh hii sasa dharau.

8 mkoa ambao watu wanashinda kwenye corridors wakicheza bao uko poa sana maisha kama ahela 😵 usiniulize nimetoa wapi data hii ni kazi ya mpango.

9 eti na kule kwa kina nshomire nako kuna njaa ? hawajawahi kosa mvua, hawajawahi kosa maji, kina nshomire wapo kila ofisi kumbe kwao hamna msosi serious? hawajawahi lala njaa wao kwao kila siku matoke na senene tu hivi senene anapatikana kwenye njaa? waulize watu wa dodoma kama wanamjua hata huyo senene.

10 mkoa maskini unapakana na mkoa tajiri eeh hao maskini si wangefuata fursa jaman? eeh au hakuna hata barabara ya kwenda huko kwenye utajiri?😵

hivi huu umaskini umekuja lini? maana huko nyuma huko kulikuwa na ahueni kumbe inawezekana kuendelea kwa kupata umaskini et? advanced poverty.

nawaza tu ngoja niishie hapa nisije nikazingirwa.
 
Hivi kweli hizi takwimu hata ni za kweli au ndo chenga la macho!!!! mwanza inazidiwa na mikoa ya Mara, Pwani, Dodoma, Manyara na kigoma kweli????
 
Mi mwenyewe nimeshangaa hizi takwimu koko. Haiwezekani kabisa Manyara ilivyonkame namna ile ikaizidi Mwanza kwa kipato. No way. Kwamba Dodoma ni tajiri kuliko Kagera? Huu ni mkakati maalum wa kuiwezessha kanda ya ziwa kupora rasilimali za Jamhuri hii.
 
Naomba kuuliza hiyo mikoa minne iliyotajwa kama ina uafadhali kwenye kipato ndo haitapewa kipaumbele kwa miradi ya maendeleo!!?? na mkoa wa pwani una sifa gani kuwepo kwenye mikoa yenye umaskini mdogo hapo kuna siasa za kuigawa nchi si kweli mwanza na umaskini kushinda manyara kuna dalili za kuitenga mikoa iliyoikataa ccm kwenye uchaguzi mkuu kuigawia miradi ya maendeleo ni kitendo cha aibu na kukataliwa kutoa takwimu za kugandamiza watu fulani
 
hahaha! jamaa anataka apeleke kila kitu kwao kwa kisingizio!
Dhahabu, almas, bati, ziwa, samaki, mifugo, pamba,airport, Viwanda, reli, barabara kuu to Mara,kagera, kisumu mmh, hali ya hewa safi(equatorial climate) maskini tena!
 
Miaka nenda rudi tunasikia mikoa ya pwani, dodoma, lindi, mtwara, manyara ndio maskini wa kutupwa na ni kweli ukienda kwenye mikoa hiyo huatapinga takwimu hizo. Mikoa hii haitegemei kitu chocolate cha maana cha kiuchumi, kilimo hola, miundombinu hola, viwanda hola. Hii mikoa kila mwaka inapigwa na njaa na ukame. Makazi ya watu hovyo,. Halafu leo mnatwambia kanda ya ziwa ndo maskini wa kutupwa, mikoa tajiri miaka na miaka, haijawahi pigwa na ukame,hapana, kuna mpango maalumu mtu kwao. tena geita na mwanza ni tajiri kuliko kilimanjaro.
 
Back
Top Bottom