Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
Watanzania wenzangu, binafsi naona upo umuhimu wa Idara ya haki za binadamu ya Chadema na wakereketwa wengine kuifungulia mashtaka polisi mahakamani, kwani tukio la Iringa lina ushahidi tosha ambao ndio pa kusimamia kujenga hoja, na katika hili naona vyombo vya habari vimeguswa kwa kuondokewa na mmoja wapo katika tasnia yao.
Bila hatua hiyo, kwa vile utawala umepanga hayo yatokee, basi mchezo utaendelea na hatimaye mabomu hayo ipo siku yatatua na kusambaratisha viongozi wa siasa wa upinzani na wanaharakati wengine. Ni maoni ya ndoto yangu, lazima tuamue na hatua ichukuliwe.
Tundu Lisu alivyosema kuhusu yaliyotokea Morogoro,
leo yametokea tena Iringa kukiwa na ushahidi usiopingika,
- sababu tunazo,
- uwezo tunao,
- haki tunayo,
Nawasilisha.