Mjadala: Kwanini vichaa hawaugui ovyo?

Mjadala: Kwanini vichaa hawaugui ovyo?

mtu anaweza akapimwa akagundulika ana magonjwa mengi at the same time nazungumzia ugonjwa anaoweza kupata baada ya ukichaa wake mfano tumbo, kipindupindu,tyfod etc
anaweza kuyapata hayo magonjwa uliyoyataja,lakini ni kwamba hawezi kukuambia au kwenda hospitali,
unaweza kumuona amejiharishia au kujinyea na nzi wengi wanamfuata ukadhani sio ugonjwa wa tumbo bali ni kwasababu ni kichaa ndio amejinyea.
 
inawezekana mtu yoyote hata (yule mzima) asipokuwa na hofu hawezi kuumwa? (nipo kwenye utafiti kwa hili)

Kuna kiwango cha maambukizi ambacho kama huna hofu kinasaidia mwili kutengeneza kinga. Kuna kiwango ambacho hata kama huna hofu utaugua. Kutokuwa na hofu sio mwarobaini bali ni msaada dose ndogo haiwezi kukuathiri, labda swali kubwa litabaki ni namna ya kuondokana na hofu ili tuwe tunaugua pale dose inapokuwa kubwa hapo tuombe msaada kwa watu wa saikolojia.
 
:msela:timu ya mpira wa miguu bila kufanya mazoezi ya kutosha na kupata usumbufu hapa na pale, ikishiriki ligi inakuwa msindikizaji. hivyo na miili yetu inavyokuwa.:msela::msela::msela:
 
Habarini ndugu wadau wa JF. Amani iwe kwenu,

Nimejaribu kufanya kautafiti kangu kadogo nikagundua kwamba ni mara chache sana kumkuta kichaa au muokota makopo anaumwa ama kalazwa kwa tatizo la majonjwa mfano Kipindupindu. Malaria. Kuhara. Malaria. Kwashakoo. Kaswendwe. Kisonono. Kichwa ama matatizo yanayoendana na hayo.

Kuna kipindi unamuona kichaa anaokota makopo na kula vitu vichafu chafu huko majalalani lakini huwezi muona anaumwa magonjwa ya mlipuko akalazwa hospitali seriously kama watu wengine.

Nini mbinu yao hawa wenzetu?
 
Habarini ndugu wadau wa JF.Amani iwe kwenu!

Nimejaribu kufanya kautafiti kangu kadogo nikagundua kwamba ni mara chache sana kumkuta kichaa au muokota makopo anaumwa ama kalazwa kwa tatizo la majonjwa mfano Kipindupindu. Malaria. Kuhara. Malaria. Kwashiako. Kaswendwe. Kisonono. Kichwa ama matatizo yanayoendana na hayo!

Kuna kipindi unamuona kichaa anaokota makopo na kula vitu vichafu chafu huko majalalani lakini huwezi muona anaumwa magonjwa ya mlipuko akalazwa hospitali seriously kama watu wengine!

Nini mbinu yao hawa wenzetu?
Huo utafiti uliufanyia wapi??
Kama ni mtaani its obvious kwamba utakaemkuta mtaani basi atakuwa mzima...
Lakini jaribu kwenda hosiptali ukaulize..

Au ukitaka research yako iwe complete chukua idadi yote ya vichaa uone ni wangapi wanaumwa magonjwa yote..

Halafu uchukue idadi yoote ya watu wasio vichaa uone ni wangapi wanaumwa magonjwa ya kawaida kama kuharisha na malaria
 
Sio kweli
Huwa wanaugua sana na wengine mpaka umauti unawakuta.
Utafiti wako usiwe wa kuangalia tu ila jaribu kuwasaidia pia kama kuwanyoa nywele au kuwaogesha ingawa inataka nguvu ya ziada pia kuwa nao karibu utakamilisha utafiti wako.
Utafiti sio kazi ndogo kama unavyoiona inataka dedication
 
Habarini ndugu wadau wa JF. Amani iwe kwenu,

Nimejaribu kufanya kautafiti kangu kadogo nikagundua kwamba ni mara chache sana kumkuta kichaa au muokota makopo anaumwa ama kalazwa kwa tatizo la majonjwa mfano Kipindupindu. Malaria. Kuhara. Malaria. Kwashakoo. Kaswendwe. Kisonono. Kichwa ama matatizo yanayoendana na hayo.

Kuna kipindi unamuona kichaa anaokota makopo na kula vitu vichafu chafu huko majalalani lakini huwezi muona anaumwa magonjwa ya mlipuko akalazwa hospitali seriously kama watu wengine.

Nini mbinu yao hawa wenzetu?
Unaposema ni aghalabu una maanisha ni mara nyingi au mara kwa mara. Aghalabu haibebi UCHACHE wa jambo inawakilisha WINGI.

Hivyo kichwa cha habari kipo tofauti na maelezo uliyoyatoa.
 
Unaposema ni aghalabu una maanisha ni mara nyingi au mara kwa mara. Aghalabu haibebi UCHACHE wa jambo inawakilisha WINGI.

Hivyo kichwa cha habari kipo tofauti na maelezo uliyoyatoa.
neno, "Aghalabu" maana yake ni: mara kwa mara, mara nyingi au kwa kawaida. Kwa English ni: always, often or usually.
Nafikiri ungesema, "Ni nadra sana...
 
Kiimani.

Kama tungekuwa na imani katika mambo yetu kama waaminivyo vichaa, dunia ingempendeza Mungu siku zote.

Hebu fikiria uchafu, muozo na harufu mbaya ya vyakula vya jalalani inavyokuwa, lakini bado kichaa kwake huamini ile ndiyo pilau/ pizzas kwake.

Naamini imani yao huwakinga na majanga hayo na Mungu huwatetea kwa hali hiyo.
 
Habarini ndugu wadau wa JF. Amani iwe kwenu,

Nimejaribu kufanya kautafiti kangu kadogo nikagundua kwamba ni mara chache sana kumkuta kichaa au muokota makopo anaumwa ama kalazwa kwa tatizo la majonjwa mfano Kipindupindu. Malaria. Kuhara. Malaria. Kwashakoo. Kaswendwe. Kisonono. Kichwa ama matatizo yanayoendana na hayo.

Kuna kipindi unamuona kichaa anaokota makopo na kula vitu vichafu chafu huko majalalani lakini huwezi muona anaumwa magonjwa ya mlipuko akalazwa hospitali seriously kama watu wengine.

Nini mbinu yao hawa wenzetu?
Aghalabu...au ulitaka kumaanisha "nadra"??
 
Miili yao ime-adapt, wale vichaa ambao hawakuadapt wameshakufa na ndio maana huwaoni
 
Mimi hua naamini chanzo cha baadhi ya magonjwa yanatokana na fikra tu za mtu mwenyewe!na mengine yanatokana na tabia fulani fulani ktk maisha yetu ya kila siku mf.uvutaji wa sigara,ngono n.k!sasa kichaa anafanya mambo pasipo kujali,kufikiri au kuwaza chochote!!endapo ugonjwa wowote umetokea kukupata unaweza ukajiponya kwa kutumia fikra tu au kujiaminisha ktk lolote na ukapona!!
NB:unaweza kula chakula kichafu sana,ukiwa na fikra za kuumwa,UTAUMWA!!lakini ukila pasipo kufikiria kuumwa,HUTOUMWA!!
 
Hawaumwi mwili(body) kirahisi kwa sababu hakuna command inayotoka akilini (mind) mwao kwenda kwenye body. Mfano, wewe uliye mzima (yaani mwenye degree chache sana za ukichaa-kumbuka kila mtu ana degree zake za akili kichaa na akili nzima) ukila chakula kichafu jalalani command itatoka kwenye mind itaenda kwenye body kisha body itatafsiri kwamba niumwe kipindupindu au kuendesha. Hawa wenzetu hawana hiyo command. Ili uelewe dhana hii, rejea somo kuhusu: roho (soul), akili (mind) na mwili (body).
 
... Naogopa ku-comment chochote... Neno "aghalabu" nadhani watu wengi hawalielewi kabisa.... Ukilitamka linaleta utamu wa kama vile, mara chache au adimu. Lakini tafsiri sahihi ni, mara nyingi..
 
Hawaumwi mwili(body) kirahisi kwa sababu hakuna command inayotoka akilini (mind) mwao kwenda kwenye body. Mfano, wewe uliye mzima (yaani mwenye degree chache sana za ukichaa-kumbuka kila mtu ana degree zake za akili kichaa na akili nzima) ukila chakula kichafu jalalani command itatoka kwenye mind itaenda kwenye body kisha body itatafsiri kwamba niumwe kipindupindu au kuendesha. Hawa wenzetu hawana hiyo command. Ili uelewe dhana hii, rejea somo kuhusu: roho (soul), akili (mind) na mwili (body).
Law of attraction
 
G4N na wengine mliotoa michango ya kufanana wote nami nawaunga mkono.

Wazungu wanapotoka ulaya kuja Afrika hutoka huko wameshameza kabisa dawa za kutibu malaria kwakuwa wanafahamu hawajawahi kuumwa na mbu wa malaria toka kuzaliwa kwao hivyo wakiumwa tu na huyo mbu kabla ya kumeza dawa ya kinga kifo kipo njenje, tuliwahi mpoteza mzungu mmoja huko pwani kwa malaria licha ya kuwahi hospitalini akiwa hajazidiwa.

Hizi chanjo za magonjwa mbalimbali mnazozisikia zinatolewa kutulinda hufanya kazi sawa na hayo maisha ya wehu na watoto wa mitaani kwani katika chanjo mtu huwekewa mwilini wadudu wa ugojwa husika waliodhohofishwa au sumu yake sasa siku wakija wale wenyewe mwili huwatambua haraka sana na kuwaangamiza.
 
Back
Top Bottom