Mizinga ni Janga la Mapenzi!

Mizinga ni Janga la Mapenzi!

Muuza simu used

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2017
Posts
4,393
Reaction score
7,101
Ni hv nimeamka zangu mapema nikasema Leo Nina buku 6 acha nikanunue nyama nipike nile gheto nipumzike kula ugali na Mayai!basi wakati nimefika tu sokoni nakutana na koloni langu(Japo nilishampa Uhuru kitambo)nikampa hai kwa mbali na kumpotezea kimtindo! Kumbe ananifuatilia kwa nyuma bila ya Mimi kujua kabla ya kuanza kununua nyama nikaona ninunue nyanya kwanza ili nikampige sound muuza nyama apunguze bei sasa wakati naanza kuchukua nyanya akafika yule koloni akaanza na yeye kuchukua nyanya,vitunguu,karoti na vitu vingine vingine vidogo na kumwambia muuzaji kwamba nitalipa mimi!nikataka kumwambia mimi sina hela akaniambia wakati ule wakati nadate naye sikuwahi kumpa hata shilingi!mzee mzima nikabaki nimeduwaa tu mara demu huyo akaondoka zake!kupiga mahesabu amechukua vitu vya buku tatu!ndio hapo nikahairisha mpango wa kununua nyama nikaamua tu nilipe deni la watu sasa hv nipo gheto nakula ugali na kachumbari! Wanawake mnavyofanya sio fair
 
Ulibaki na buku ngapi...sababu Buku moja mia tano ungepata kongoro la kutosha mkuu ungepiga kitu cha rosti ....acha kula ugali bila mboga kila mara mkuu
 
Ni hv nimeamka zangu mapema nikasema Leo Nina buku 6 acha nikanunue nyama nipike nile gheto nipumzike kula ugali na Mayai!basi wakati nimefika tu sokoni nakutana na koloni langu(Japo nilishampa Uhuru kitambo)nikampa hai kwa mbali na kumpotezea kimtindo! Kumbe ananifuatilia kwa nyuma bila ya Mimi kujua kabla ya kuanza kununua nyama nikaona ninunue nyanya kwanza ili nikampige sound muuza nyama apunguze bei sasa wakati naanza kuchukua nyanya akafika yule koloni akaanza na yeye kuchukua nyanya,vitunguu,karoti na vitu vingine vingine vidogo na kumwambia muuzaji kwamba nitalipa mimi!nikataka kumwambia mimi sina hela akaniambia wakati ule wakati nadate naye sikuwahi kumpa hata shilingi!mzee mzima nikabaki nimeduwaa tu mara demu huyo akaondoka zake!kupiga mahesabu amechukua vitu vya buku tatu!ndio hapo nikahairisha mpango wa kununua nyama nikaamua tu nilipe deni la watu sasa hv nipo gheto nakula ugali na kachumbari! Wanawake mnavyofanya sio fair
Kweli hii itasogeza masaa..,siku iishe
 
Back
Top Bottom