VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Kwakuwa sitaki mabishano nitakwenda na nadharia mbili. Kwanza, nitachulia, sitaki tubishane hapa kwakuwa hakuna yeyote kati yetu aliyethibitisha wala wao kukanusha, kuwa waliotajwa Mwembeyanga mwaka 2007 kama Mafisadi wa nchi hii ni mafisadi kweli. Mafisadi 11.
Waliotajwa ni Rostam, Chenge, Lowassa, Rutabanzibwa, Yona, Mramba, Kikwete, Mkapa, Balali, Karamagi na Mkono. Kati ya hao, mmoja ni Marehemu-Balali. Wawili wamefungwa jela-Mramba na Yona. Wawili ni Marais wastaafu-Mkapa na Kikwete. Mmoja aligombea Urais kupitia CHADEMA-Lowassa. Mmoja ni Mbunge-Mkono.
Kivyama, hadi naandika hapa, 10 ni wa CCM na mmoja ni wa CHADEMA. Ni 10 kwa 1. Nasema bila kutafakari mara mbilimbili kuwa hao 11 ndiyo, hadi leo, wanamiliki na kuziendesha siasa za nchi hii na hata nchi yenyewe. Ndiyo hasa 'wenye nchi'. hadi hapo, kama ni mizani ya ufisadi, CCM ina uzito zaidi. CCM ni chafu zaidi ya CHADEMA yenye mmoja tu-Lowassa.
Nadharia ya pili,katika kashfa mpya ya Stanbic Bank, wanatajwa watu mbalimbali kuhusika. Wanatajwa waliokuwa Mawaziri kwenye Serikali iliyopita, Maafisa wa TRA na hata mtoto wa Waziri wa Serikali iliyotangulia. Pia, wapo maafisa wa benki na kampuni inayohusishwa na kashfa hiyo. WanaCCM wanaopenda mambo rahisirahisi na kufichaficha ukweli, wanamng'ang'ania Awale na kuwaacha wengine. Ni kwakuwa wengine ni wa CCM?
Nasema kuwa mizani ya ufisadi bado ina uzito mkubwa kwa CCM. Kama chama tawala, hatupaswi kushangilia kuushinda ufisadi. Bado tuna safari ndefu. Tumuunge mkono Rais Magufuli katika mapambano yake dhidi ya ufisadi lakini tukumbuke wajibu wetu kichama kupambana na ufisadi chamani. Hatuna muda wa kupindisha ukweli na kuvunga kuwa hatuna makandokando na uvundo wa ufisadi.
Tuache chongo kuliita kengeza!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Waliotajwa ni Rostam, Chenge, Lowassa, Rutabanzibwa, Yona, Mramba, Kikwete, Mkapa, Balali, Karamagi na Mkono. Kati ya hao, mmoja ni Marehemu-Balali. Wawili wamefungwa jela-Mramba na Yona. Wawili ni Marais wastaafu-Mkapa na Kikwete. Mmoja aligombea Urais kupitia CHADEMA-Lowassa. Mmoja ni Mbunge-Mkono.
Kivyama, hadi naandika hapa, 10 ni wa CCM na mmoja ni wa CHADEMA. Ni 10 kwa 1. Nasema bila kutafakari mara mbilimbili kuwa hao 11 ndiyo, hadi leo, wanamiliki na kuziendesha siasa za nchi hii na hata nchi yenyewe. Ndiyo hasa 'wenye nchi'. hadi hapo, kama ni mizani ya ufisadi, CCM ina uzito zaidi. CCM ni chafu zaidi ya CHADEMA yenye mmoja tu-Lowassa.
Nadharia ya pili,katika kashfa mpya ya Stanbic Bank, wanatajwa watu mbalimbali kuhusika. Wanatajwa waliokuwa Mawaziri kwenye Serikali iliyopita, Maafisa wa TRA na hata mtoto wa Waziri wa Serikali iliyotangulia. Pia, wapo maafisa wa benki na kampuni inayohusishwa na kashfa hiyo. WanaCCM wanaopenda mambo rahisirahisi na kufichaficha ukweli, wanamng'ang'ania Awale na kuwaacha wengine. Ni kwakuwa wengine ni wa CCM?
Nasema kuwa mizani ya ufisadi bado ina uzito mkubwa kwa CCM. Kama chama tawala, hatupaswi kushangilia kuushinda ufisadi. Bado tuna safari ndefu. Tumuunge mkono Rais Magufuli katika mapambano yake dhidi ya ufisadi lakini tukumbuke wajibu wetu kichama kupambana na ufisadi chamani. Hatuna muda wa kupindisha ukweli na kuvunga kuwa hatuna makandokando na uvundo wa ufisadi.
Tuache chongo kuliita kengeza!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam