Mitandao ya simu ya Tanzania ni ya hovyo sana

Mangungu

JF-Expert Member
Apr 22, 2012
2,392
3,017
Salamu kutoka kusini! Kusini Kuchele

Naanza na malalamiko yangu kwa hii mitandao ya simu ya Tanzania!

Moja. Hivi kuna ulazima gani, pindi mtu anaacha kutumia line ya mtandao flani au anafariki dunia,halafu hiyo line ya simu anapewa mtu mwingine baada ya miezi kadhaa?

Hivi inakuaje aliyekua anatumia hiyo line ya simu, kaifanyia mambo ya utapeli, kauwa watu, kaiba, kakaba watu hadi kufa, kabaka na matukio mengine ya kuogofya, hamuoni kwamba huyo mtu anakua kwenye kesi ambazo hazimuhusu?

Mbili! Nimechukua line ya mtandao flani hivi,kila siku napigiwa simu na Bank x,wanahitaji marejesho ya mkopo wao,ambao nilichukua, sasa mbona Mimi sijawahi chukua mkopo kwenye hiyo bank?

Kumbe aliyekua anatumia line ya hii simu ndo anayetafutwa! Mara nitumiwe sms za mapenzi! Mpenzi wangu siku hizi hata hunijali, hata pesa za matumizi hunitumii kabisa! Kuna siku kidogo nife, nilisoma, sms inayosema salio la kiasi flani, limetolewa kwenye account yako! Haaa nikatahamaki, kumbe ni hii line ya ajabu!

Tatu! Mnavunja ndoa za watu, hivi kweli nani ataelewa kwamba, hii sms sio ya kwangu,ni yatu mwingine?

Nne! Hivi mtu alifariki, na kwenye line zake kuna pesa,hua zinaenda wapi hizi pesa? Jamani tunapigwa mchana kweupe! Natamani kujua hii kitu!
 
Me kuna line ya voda imenibidi niachane nayo, yani kila siku napigiwa namba ngeni na watu nisio wajua.
 
Mawakala Hawa wanaposajili hukuta masalio kibao na kuyachukua kabla ya kumkabidhi mteja.
 
Mbili! Nimechukua line ya mtandao flani hivi,kila siku napigiwa simu na Bank x,wanahitaji marejesho ya mkopo wao,ambao nilichukua, sasa mbona Mimi sijawahi chukua mkopo kwenye hiyo bank?
Hiyo bank wana akili kama huyu mdudu hapa, wanampa mtu mkopo kwa dhamana ya line ya simu!!!
1624289050409.png
 
Yaan kuna kitu kimenishangaza sana eti watu wanaokufa line zao kama zina pesa serikali na mtandao husika ndio wafanye utaratibu hela ihamie serikalini... kweli kweli

Kwanini msifanye juhudi za lazima mkapata wafiwa wakapewa hiyo pesa ikawasaidia waliobaki... yaan ukisikia ile wanasema shamba lenye bangi ni mali yako lkn ardhi yenye madini ni mali ya serikali ndio hii sasa.
 
Salamu kutoka kusini! Kusini Kuchele

Naanza na malalamiko yangu kwa hii mitandao ya simu ya Tanzania!

Moja. Hivi kuna ulazima gani, pindi mtu anaacha kutumia line ya mtandao flani au anafariki dunia,halafu hiyo line ya simu anapewa mtu mwingine baada ya miezi kadhaa?

Hivi inakuaje aliyekua anatumia hiyo line ya simu, kaifanyia mambo ya utapeli, kauwa watu, kaiba, kakaba watu hadi kufa, kabaka na matukio mengine ya kuogofya, hamuoni kwamba huyo mtu anakua kwenye kesi ambazo hazimuhusu?

Mbili! Nimechukua line ya mtandao flani hivi,kila siku napigiwa simu na Bank x,wanahitaji marejesho ya mkopo wao,ambao nilichukua, sasa mbona Mimi sijawahi chukua mkopo kwenye hiyo bank?

Kumbe aliyekua anatumia line ya hii simu ndo anayetafutwa! Mara nitumiwe sms za mapenzi! Mpenzi wangu siku hizi hata hunijali, hata pesa za matumizi hunitumii kabisa! Kuna siku kidogo nife, nilisoma, sms inayosema salio la kiasi flani, limetolewa kwenye account yako! Haaa nikatahamaki, kumbe ni hii line ya ajabu!

Tatu! Mnavunja ndoa za watu, hivi kweli nani ataelewa kwamba, hii sms sio ya kwangu,ni yatu mwingine?

Nne! Hivi mtu alifariki, na kwenye line zake kuna pesa,hua zinaenda wapi hizi pesa? Jamani tunapigwa mchana kweupe! Natamani kujua hii kitu!
Mkuu na mimi ni hivyo hivyo nasumbuliwa na bank
 
Ili kuepuka kuendelea kusumbuliwa nenda kwenye mtandao husika waambie waifunge hiyo namba ya simu. Omba wakupatie namba nyingine ambayo haijawahi kutumiwa na mtu mwingine.
 
As Always lawama tunazitupa pale ambapo sipo....

Moja kila line ikiingia sokoni inalipiwa (serikali inachukua chao) kuendelea kutengeneza line ambazo hazifanyi kazi na sio kuzi-recycle ni ongezeko la uendeshaji wa Biashara ya mtandao husika...

Ukifa ni jukumu la ndugu zako / wasimamizi wa mirathi kufuatilia mali zako zote hio ni kwenye mitandao au benki husika, andika barua wewe kama msimamizi wa mirathi utapewa stahiki zako....

Ni hapo baada ya siku chache tu tutaendelea kulalamika gharama za mitandao kutuma na kupokea pesa kwamba ni wezi (kumbe behind the scenes serikali ndio inavuta mlungula)
 
Back
Top Bottom