Mitandao ya simu, hawa watu wanatoa wapi namba zetu?

Mitandao ya simu, hawa watu wanatoa wapi namba zetu?

Naomba kuuliza mitandao ya simu hawa watu wanatoa wapi namba zetu? Mana imekuwa mtindo wao kujitangaza kwa mtindo huu kujifanya wamekosea kutuma ujumbe, Mtakuwa mna 10% zenu kwenye haya matangazo inaonekana View attachment 695416View attachment 695417
wakuu naomba niwajibu hizi namba huwa zinapatikana vipi ,hawa watu huwa wananunua line zilizotumika kwa sh 500 mpaka 1000 za kitanzania kwa line moja na wanaowauzia hizi line ni mateja, wezi wa simu, au wanunuzi wa simu za wizi. Yaani kama mimi nina namba yako kwenye phonebook then napoteza simu au naibiwa basi line yangu peke yake ni dili sababu contacts zangu zote zipo hivyo ikifika kwenye mkono wa teja yeye anaenda kuuza hiyo line kwa hawa matapeli hivyo wanatumia hiyo line kutuma hizo spam msg wakimaliza phonebook nzima hapo line inavunjwa.Nakaribisha maswali .
 
Sidhani kama wananunua namba kwenye vitabu maana kuna siku nilinunua line mpya kwa ajili ya beki tatu wangu home tukaisajili ofisi za mtandao kabisa tukiwa njiani tunarudi home messeji ya aina hiyo ikaingia. Akanionyesha nikashangaa sana maana mimi nilishazizoea. Nadhani wana kamtambo kakudaka mambo ya simu. Watu wana utaalam mwingi sana mitaani huko.
 
wakuu naomba niwajibu hizi namba huwa zinapatikana vipi ,hawa watu huwa wananunua line zilizotumika kwa sh 500 mpaka 1000 za kitanzania kwa line moja na wanaowauzia hizi line ni mateja, wezi wa simu, au wanunuzi wa simu za wizi. Yaani kama mimi nina namba yako kwenye phonebook then napoteza simu au naibiwa basi line yangu peke yake ni dili sababu contacts zangu zote zipo hivyo ikifika kwenye mkono wa teja yeye anaenda kuuza hiyo line kwa hawa matapeli hivyo wanatumia hiyo line kutuma hizo spam msg wakimaliza phonebook nzima hapo line inavunjwa.Nakaribisha maswali .
1. Ukiibiwa laini huwa unaripot mtandao Husika Kuifunga Hata Kama siyo On The spot Lakini baada Ya Muda Uta Swap Na inakuwa Vigumu Kwa mwizi Kuweza Kupata Contact Via stolen Sim Card.

2. simu Nyingi Huwa Ziko Locked Wakati Zinaibiwa na Kwa Vyovyote Huwez Itumia Simu Hadi uFlash mean while Ukiflash unafuta na Contact Za Phone book.

3. Mara Nyingi Wanaotumia Namba Baada Ya Kuiba Huwa ni Matapeli Wa Tuma Pesa Nipo Hospital Na Siyo Hawa Witch Drs.

Hawa Watu Huwa Wanabuni Namba Za Watu Na Kuwa Tumia Sms. Na Kwa Hali ilivyo Sasa Kila Namba Utayobuni ipo Active.
 
Naomba kuuliza mitandao ya simu hawa watu wanatoa wapi namba zetu? Mana imekuwa mtindo wao kujitangaza kwa mtindo huu kujifanya wamekosea kutuma ujumbe, Mtakuwa mna 10% zenu kwenye haya matangazo inaonekana View attachment 695416View attachment 695417

We umejiunga na magroup ya whatsapp zaidi ya kumi na huko namba yako inaonekana kila group, na kila link unataka kujiunga
 
Yani hawa Washirikina siwapendi mpaka busi Mara kwa Mara wananitumia SMS sizijibu lakini hawakati tamaa
 
ed47674df44537835579b6a02cbe4ba4.jpg
 
Mimi tokea wanitumie mara moja na nikawaandikia Mkeka wa Matusi / Shombo wenye Urefu wa Tegeta Nyuki hadi Mbagala Kizuiani hadi leo sijaona tena meseji nyingi ikitumwa Kwangu na nahisi labda huwa wanakuwa na hamu ya Kunitumia ila wakifanya tu review na matusi niliyowapa wanaufyata / wananywea.
 
Hao ni matapeli, mimi huwa nazifutaga tu hizo jumbe. Inawezekana hakuna anae wapa hizo namba bali wanazibuni.
 
Mimi tokea wanitumie mara moja na nikawaandikia Mkeka wa Matusi / Shombo wenye Urefu wa Tegeta Nyuki hadi Mbagala Kizuiani hadi leo sijaona tena meseji nyingi ikitumwa Kwangu na nahisi labda huwa wanakuwa na hamu ya Kunitumia ila wakifanya tu review na matusi niliyowapa wanaufyata / wananywea.
Nilitumiwa ujumbe mara mbili, ikanikera nikawapigia lakini hawakupokea. Nilitaka kuwapa maneno ya ajabu yangewashangaza wao na familia zao.

Yamkini waling'amua kuwa wameingia ndani ya 18. Mpaka leo sijaona huo upuuzi.
 
Nilitumiwa ujumbe mara mbili, ikanikera nikawapigia lakini hawakupokea. Nilitaka kuwapa maneno ya ajabu yangewashangaza wao na familia zao.

Yamkini waling'amua kuwa wameingia ndani ya 18. Mpaka leo sijaona huo upuuzi.

Wala walihisi kuwa na Wewe ulikuwa unajipanga kuwatolea Matusi / Shombo ambayo pengine yangewafanya hata waachane kabisa na huo Uganga wao wa Kipopoma / Kingumbaru / Kijinga. Yaani Mimi nahisi kwamba ule Mkeka wangu wa niliowatumia kila siku huwa wanaupitia na wanatetemeka mno kwani nilitema Cheche za Kufa Mtu na siku hiyo ndiyo ilikuwa mwanzo na mwisho Wao kunitumia mameseji yao hayo. Nawashangaa mno wanaosema kwamba kila siku huwa wanatumiwa tu hizo hizo meseji.
 
Wala walihisi kuwa na Wewe ulikuwa unajipanga kuwatolea Matusi / Shombo ambayo pengine yangewafanya hata waachane kabisa na huo Uganga wao wa Kipopoma / Kingumbaru / Kijinga. Yaani Mimi nahisi kwamba ule Mkeka wangu wa niliowatumia kila siku huwa wanaupitia na wanatetemeka mno kwani nilitema Cheche za Kufa Mtu na siku hiyo ndiyo ilikuwa mwanzo na mwisho Wao kunitumia mameseji yao hayo. Nawashangaa mno wanaosema kwamba kila siku huwa wanatumiwa tu hizo hizo meseji.
Safi sana. Na hakika hawatakaa waje wakusahau kwa jinsi unavyoelezea huo mkeka urefu wa hizo kilometers mpaka Mbagala, nadhani hata TCRA wale waganga wakituma tu wana unaublock usije wako
 
Sidhani kama wananunua namba kwenye vitabu maana kuna siku nilinunua line mpya kwa ajili ya beki tatu wangu home tukaisajili ofisi za mtandao kabisa tukiwa njiani tunarudi home messeji ya aina hiyo ikaingia. Akanionyesha nikashangaa sana maana mimi nilishazizoea. Nadhani wana kamtambo kakudaka mambo ya simu. Watu wana utaalam mwingi sana mitaani huko.
Usimuite msaidizi wako wa nyumbani "beki tatu", hilo ni neno la kudhalilisha kwa mtu anayekusaidia malezi ya watoto na familia yako.

Ni neno linaleta ukakasi sana. If you think of it utaacha kumuita msaidizi wako "beki tatu".
 
Back
Top Bottom