X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
- Thread starter
- #21
Mchango Wa CIA Katika Ujasusi
Likiwa shirika huru la ujasusi linalowajibika chini ya ofisi ya Rais, limekuwa liendesha shughuli zake kupitia kamati na taasisi za usalama wa taifa zilizo chini ya baraza la Congress. Lengo la CIA ni pamoja na kumsaidia Rais, baraza la usalama taifa na watendaji wote wanaoandaa na kuzitekeleza sera za usalama wa taifa. Kwa ajili hiyo hufanya yafuatayo:
Kutafuta, kukusanya, kutafiti, kuchambua, kutathmini na kutoa habari sahihi, bayana na zilizo ndani ya wakati kuhusiana na masuala ya usalama. Kudhibiti mashirika mengine ya ujasusi duniani (counter intelligence activities), kufanya shughuli maalumu za kijasusi na nyinginezo zinazohusiana na ujasusi nje na ndani ya Marekani kama inavyoagizwa na Rais.
Lengo La CIA:
Kuwa chanzo muhimu cha taarifa za kijasusi nchini Marekani, zitakazoelekeza na kuathiri maamuzi ya Taifa juu ya masuala mbali mbali duniani, kadhalika kujijengea hadhi kwa ubora wa kazi zake, na umakini wa watendaji wake.
Kwa ajili hiyo, CIA linasimamia:
1. Ujasusi ambao huongeza thamani ya muelekeano katika usimamizi wa upeo wa migogoro, mwenendo wa vita na maendeleo ya sera.
2. Kutazama pande mbili za kiini cha msingi, uimara, uthabiti, ukubwa, ukweli, na uhalisia wa ujasusi, ikizama katika uwajibikaji kwa walengwa kwa kuzingatia muundo wake na wakati uliopo.
Kwa hiyo CIA linafanya shughuli zake kupitia:
1. Taasisi na watu waaminifu wakiwemo wanataaluma wateule waliosoma kwao na vyuo vikuu vilivyo mikononi mwao duniani kote.
2. Kufanyakazi kwa pamoja na kushirikiana na mashirika na Jumuiya ya kijasusi.
3. Kuwajibika kikamilifu ili kuifanya kwa ufanisi shughuli ya ujasusi.
4. Kuvumbua mambo mapya na kupambana na madhara yoyote yatakayotokea ili kazi husika zifanyike kwa ufanisi.
5. Kurekebisha mabadiliko ya mazingira ya Ulimwengu ili kukidhi hitajio la wateja wake.
6. Kuwajibika na kujitathmini kwa vitendo vyake.
7. Uendelevu wa kiutendaji.
Likiwa shirika huru la ujasusi linalowajibika chini ya ofisi ya Rais, limekuwa liendesha shughuli zake kupitia kamati na taasisi za usalama wa taifa zilizo chini ya baraza la Congress. Lengo la CIA ni pamoja na kumsaidia Rais, baraza la usalama taifa na watendaji wote wanaoandaa na kuzitekeleza sera za usalama wa taifa. Kwa ajili hiyo hufanya yafuatayo:
Kutafuta, kukusanya, kutafiti, kuchambua, kutathmini na kutoa habari sahihi, bayana na zilizo ndani ya wakati kuhusiana na masuala ya usalama. Kudhibiti mashirika mengine ya ujasusi duniani (counter intelligence activities), kufanya shughuli maalumu za kijasusi na nyinginezo zinazohusiana na ujasusi nje na ndani ya Marekani kama inavyoagizwa na Rais.
Lengo La CIA:
Kuwa chanzo muhimu cha taarifa za kijasusi nchini Marekani, zitakazoelekeza na kuathiri maamuzi ya Taifa juu ya masuala mbali mbali duniani, kadhalika kujijengea hadhi kwa ubora wa kazi zake, na umakini wa watendaji wake.
Kwa ajili hiyo, CIA linasimamia:
1. Ujasusi ambao huongeza thamani ya muelekeano katika usimamizi wa upeo wa migogoro, mwenendo wa vita na maendeleo ya sera.
2. Kutazama pande mbili za kiini cha msingi, uimara, uthabiti, ukubwa, ukweli, na uhalisia wa ujasusi, ikizama katika uwajibikaji kwa walengwa kwa kuzingatia muundo wake na wakati uliopo.
Kwa hiyo CIA linafanya shughuli zake kupitia:
1. Taasisi na watu waaminifu wakiwemo wanataaluma wateule waliosoma kwao na vyuo vikuu vilivyo mikononi mwao duniani kote.
2. Kufanyakazi kwa pamoja na kushirikiana na mashirika na Jumuiya ya kijasusi.
3. Kuwajibika kikamilifu ili kuifanya kwa ufanisi shughuli ya ujasusi.
4. Kuvumbua mambo mapya na kupambana na madhara yoyote yatakayotokea ili kazi husika zifanyike kwa ufanisi.
5. Kurekebisha mabadiliko ya mazingira ya Ulimwengu ili kukidhi hitajio la wateja wake.
6. Kuwajibika na kujitathmini kwa vitendo vyake.
7. Uendelevu wa kiutendaji.