Mitandao ya Kijasusi

Mchango Wa CIA Katika Ujasusi

Likiwa shirika huru la ujasusi linalowajibika chini ya ofisi ya Rais, limekuwa liendesha shughuli zake kupitia kamati na taasisi za usalama wa taifa zilizo chini ya baraza la Congress. Lengo la CIA ni pamoja na kumsaidia Rais, baraza la usalama taifa na watendaji wote wanaoandaa na kuzitekeleza sera za usalama wa taifa. Kwa ajili hiyo hufanya yafuatayo:

Kutafuta, kukusanya, kutafiti, kuchambua, kutathmini na kutoa habari sahihi, bayana na zilizo ndani ya wakati kuhusiana na masuala ya usalama. Kudhibiti mashirika mengine ya ujasusi duniani (counter intelligence activities), kufanya shughuli maalumu za kijasusi na nyinginezo zinazohusiana na ujasusi nje na ndani ya Marekani kama inavyoagizwa na Rais.


Lengo La CIA:
Kuwa chanzo muhimu cha taarifa za kijasusi nchini Marekani, zitakazoelekeza na kuathiri maamuzi ya Taifa juu ya masuala mbali mbali duniani, kadhalika kujijengea hadhi kwa ubora wa kazi zake, na umakini wa watendaji wake.
Kwa ajili hiyo, CIA linasimamia:

1. Ujasusi ambao huongeza thamani ya muelekeano katika usimamizi wa upeo wa migogoro, mwenendo wa vita na maendeleo ya sera.
2. Kutazama pande mbili za kiini cha msingi, uimara, uthabiti, ukubwa, ukweli, na uhalisia wa ujasusi, ikizama katika uwajibikaji kwa walengwa kwa kuzingatia muundo wake na wakati uliopo.

Kwa hiyo CIA linafanya shughuli zake kupitia:
1. Taasisi na watu waaminifu wakiwemo wanataaluma wateule waliosoma kwao na vyuo vikuu vilivyo mikononi mwao duniani kote.
2. Kufanyakazi kwa pamoja na kushirikiana na mashirika na Jumuiya ya kijasusi.
3. Kuwajibika kikamilifu ili kuifanya kwa ufanisi shughuli ya ujasusi.
4. Kuvumbua mambo mapya na kupambana na madhara yoyote yatakayotokea ili kazi husika zifanyike kwa ufanisi.
5. Kurekebisha mabadiliko ya mazingira ya Ulimwengu ili kukidhi hitajio la wateja wake.
6. Kuwajibika na kujitathmini kwa vitendo vyake.
7. Uendelevu wa kiutendaji.
 
Muhtasari Wa Sheria Ya Usalama Wa Taifa Ya Mwaka 1947

Kanuni ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1947 (The National Security Act of 1947), iliidhinisha kuundwa upya sera za nje na kuasisi taasisi za kijeshi za serikali ya Marekani. Sheria hiyo, ikaunda Taasisi nyingi ambazo Rais aliona ni muhimu katika kuandaa na kutekeleza sera za nje, ikiwemo baraza la Usalama la Taifa (National Security Council - NSC). Baraza hilo lilimjumuisha Rais wa nchi, makamu wake, waziri wa mambo ya nje (Secretary of State), Waziri wa Ulinzi (Secretary of Defense) na wanachama wengine kama vile Mkurugenzi wa CIA (Director of the Central Intelligence Agency), ambao hukutana Ikulu ya White House kujadili matatizo ya muda mrefu na kutokuelewana kunakoweza kuhatarisha usalama wa taifa. Watendaji wachache wa NSC hukodiwa kuratibu yanayotakiwa kuwemo katika sera za nje, toka mashirika mengine kwa ajili ya ofisi ya Rais.

Kuanzia mwaka 1953 msaidizi wa rais wa masuala ya usalama wa taifa, amekuwa akiongoza watendaji hawa. Kila Rais wa Marekani, hutoa miongozo muhimu kwa NSC na hutoa uhuru fulani wa kujitawala watendaji wa NSC na hata ushawishi juu ya mashirika mengine ya ulinzi na usalama wa nchi hiyo, ikiwemo idara ya mambo ya nje na ile ya ulinzi. Rais Dwight D. Eisenhower, kwa mfano, alitumia mikutano ya NSC kupitisha maamuzi mazito na muhimu ya sera za nje ilhali Rais John F. Kennedy na Lyndon B. Johnson, walipendelea kuendesha shughuli zao isivyo rasmi kupitia taasisi walizoziamini.

Wakati wa rais Richard M. Nixon, watendaji wa NSC wakati huo wakiongozwa na Henry A. Kissinger, wakafanyiwa marekebisho ya kiutendaji toka bodi ya kuratibu na kuwa taasisi imara iliyojihusisha pia na viongozi wa mataifa ya kigeni na kutekeleza maamuzi ya Rais. Vikao vya baraza la Usalama wa Taifa, vyenyewe hata hivyo ,viliweza kupitisha maamuzi kinyume kulingana na taarifa zilizokusanywa. Kanuni ya usalama wa taifa ndiyo ilifanikisha kuanzishwa kwa CIA mara baada ya vita kuu ya pili ambayo iliandamana na uanzishaji wa taasisi ndogo za ujasusi. Awali CIA ndiyo iliyokuwa taasisi kuu na ya kuaminika katika ukusanyaji wa taarifa za kijasusi serikalini. Baadae, idara ya usalama jeshini iliyoongozwa na wizara ya ulinzi ikafanywa ndiyo Bodi kuu ya masuala yote ya ujasusi na usalama wa taifa.
Neno ‘intelligence’ kwa mujibu wa kanuni ya usalama wa Taifa ya Marekani linajumuisha usalama wa taifa wenyewe, ujasusi na ukachero ndani, nje na udhibiti wa ujasusi dhidi ya mashirika mengine ya kijasusi(counterintelligence).

Neno ujasusi wa nje (foreign intelligence) linajumuisha ukusanyaji wa taarifa na habari zote zinazohusiana na uwezo, madhumuni au matendo ya serikali nyingine au taasisi na mashirika mengine, mtu wa kigeni au matendo yoyote yenye sura ya kimapambano dhidi ya Marekani. Neno udhibiti wa mashirika mengine ya ujasusi (counterintelligence) lina maana ya habari au taarifa zote zinazokusanywa, au uendeshaji wa shughuli zote za kijasusi zenye shabaha ya kulilinda taifa dhidi ya ujasusi. Ujasusi huo ni ule unaofanywa na mashirika, taasisi za kigeni, raia, nchi nyingine, jumuiya yoyote au shughuli zote za kijasusi za mataifa mengine, hujuma (sabotage) mauaji ya kisiasa(assasinations) yanayoendeshwa na serikali au kwa niaba ya serikali au taasisi fulani ya kigeni.

Kwa mujibu wa kifungu 105(3) cha kanuni ya usalama wa taifa nchini Marekani, jumuiya ya ujasusi inakusanya ofisi ya mkurugenzi wa CIA, ambayo inamjumuisha pia naibu wake mkurugenzi na Mwenyekiti wa baraza la ujasusi la Taifa(National Intelligence Council). Idara nyingine ni pamoja na idara ya usalama wa Taifa (The National Security Agency); idara ya ujasusi jeshini (The Defense Intelligence Agency) na idara ya upelelezi(The National Reconnaissance Office).
 
GRU: Majasusi Waliotawala Dunia 1920-1948

Umadhubuti na kutoeleweka vyema kwa mfumo wa ulinzi, usalama, ukachero na ujasusi wa Umoja wa kisovieti kuliifanya nchi hiyo itawale uwanja huo zama za vita baridi na nyuma kidogo. Pamoja na kukabiliwa na upinzani wa mashirika ya CIA na FBI ya Marekani kwa upande mmoja na MI5 na MI6 ya Uingereza kwa upande mwingine yote yakiwa chini ya udhibiti wa Mossad na ShinBeth ya Israil, mashirika ya kijasusi ya Urusi na vitengo vyake ndiyo yaliyotawala medani ya ujasusi nje ya Soviet Union. GRU (Glavnoye Razvedyvatelnoye Uprvleniye) ilikuwa moja ya Kurugenzi Kuu za mfumo wa ujasusi wa Soviet Union.

GRU ilihusika na uendeshaji wa operesheni zote za kijasusi jeshini na uraiani kuanzia mwaka 1920 hadi mwishoni mwa miaka ya 1960. GRU ilitambulika kama divisheni iliyokusanya shughuli zote za ujasusi nchini Urusi ikiwa pia kitengo maalum cha ushushushu jeshini (Military Intelligence).

GRU kimsingi ilihusika na ubunifu, ukusanyaji na upangaji wa mikakati, mbinu na mambo ya kiufundi kama kitengo cha ujasusi cha jeshi la uliokuwa Umoja wa kisovieti. Ingawa GRU ilihusika na ukachero katika vita vya msituni dhidi ya maadui, kiutendaji haikuwa chini ya shirika la kijasusi la KGB. Ilikuwa na vyuo, shule na nafasi maalumu katika balozi za Urusi sehemu mbali mbali duniani. Ilikuwa ikiendesha operesheni zake bila ya kusubiri au kuhitaji maelekezo au ushauri wa KGB. GRU ilikuwa na utaratibu na njia zake maalum za uwasilishaji taarifa mjini Moscow. Karibu waambata wote wa kijeshi waliokuwa katika balozi za Urusi duniani walikuwa maafisa wa GRU kama ilivyokuwa kwa wanadiplomasia wote Warusi waliofanya kazi katika ofisi na mashirika mbali mbali nje ya nchi.

Shughuli za kijasusi za GRU zilipewa umuhimu mkubwa zaidi nchini Urusi na kutokana na ustadi wake zilikuwa tishio kwa mataifa yote ya dunia. Hata hivyo kwa maoni ya baadhi ya wachambuzi wa mambo ya kijasusi, utendaji wa GRU ulifunikwa na shirika la KGB ambazo ziliitazama GRU kama kitengo chenye shughuli maalum za ujasusi tofauti na zile za KGB zilizohusisha maeneo yote ya kijamii.

GRU ilianzishwa mwaka 1920 baada ya Jeshi la Poland kuvuka mpaka na kuingia Urusi na kusonga mbele hadi jimbo la Ukraine kabla halijarejeshwa nyuma kisha kufukuzwa na Jeshi la Umoja wa kisovieti. Kutokana na kupotoshwa na taarifa za kijasusi kuwa Wapoli walikuwa tayari kupindua serikali yao, Vladimir Lenin aliamuru Jeshi la Urusi (Red Army) liishambulie Poland kama ulipizaji wa kisasi. Kinyume na matarajio, Wapoli waliliunga mkono jeshi lao kukabili uvamizi wa Warusi na walifanikiwa kuwaondoa wavamizi.

Kama ni matokeo ya kupigwa huko, Dzerzhinsky aliyekuwa Mkurugenzi wa Usalama, alimuagiza naibu wake makini, Yan Karlovic Berzin kuongoza Idara ya Masjala ya Cheka ambaye baadaye akawa ndiye muhusika mkuu wa ukusanyaji wa taarifa zote za ujasusi jeshini. Muda mfupi baadaye kurugenzi maalumu huru ya ujasusi ikaundwa chini ya ukurugenzi wa Berzin kuchukua shughuli za CRD (Cheka Registry Department). Na kadri muda ulivyokwenda, kidogokidogo ikafanywa kuwa kurugenzi kuu, GRU, ikiwa mdogo wa kurugenzi mama wa shughuli zote za ujasusi nchini Urusi.

Wakati wa Starlin, pakahimizwa ushindani wa kiutendaji kati ya GRU na idara ya polisi wa uraiani ambapo katika ushindani huo, GRU ilifanikiwa kuizidi idara ya polisi kiutendaji katika kila nyanja nje ya yale zile wajibati zake za ujasusi wa kijeshi.

Mnamo mwaka 1920 na mwanzoni mwa miaka ya 1930 mataifa mengi yalisitisha kuzitambua shughuli za kidiplomasia za Urusi kwa kuzishuku zilikuwa za kijasusi zaidi kuliko kidiplomasia, kwa ajili hiyo yakailazimisha Urusi isitishe mpango wake wa kujaza makachero katika balozi zake. Hatua hiyo ikailazimisha GRU kubadili mbinu kwa kufanya kazi zile zile za kijasusi kinyume na kanuni lakini kwa usiri na umakini mkubwa kuliko hata ilivyokuwa nyuma. Usiri chini ya uchunguzi mkubwa wa mataifa yote ukailazimisha GRU kuendesha shughuli zake za kijasusi kwa mbinu za hali ya juu na ustadi mkubwa hivyo kuifanya ilipofika miaka ya 1936 hadi 1938 ikawa mashuhuri na yenye utaalamu mkubwa kulinganisha na idara ya polisi hasa katika kitengo cha operesheni za nje.

Shughuli za GRU zikaja kuwa muhimu zaidi wakati wa Vita Kuu ya Pili hasa kutokana na maafisa wake wengi kuishi katika nchi za Ujerumani, Japan, Uingereza na Amerika ya kaskazini. Kigogo mmoja wa GRU kwa jina Richard Sorge aliyekuwa nchini Japan atabakia kutajwa kuwa ndiye aliyekuwa muhimu zaidi katika ulimwengu wa ukachero wakati wa Vita Kuu ya Pili ya dunia. Taarifa za kijasusi zilizoandikwa na kuwasilishwa na maafisa wa GRU waliopandikizwa nchini Ujerumani nazo zilikuwa muhimu vile vile ingawa nyingi ya hizo nyaraka husika zinafahamisha kuwa hazikuwahi kutumika. Hata hivyo, GRU ilianza kuyumba kiutendaji kufuatia vifo vya kawaida vya baadhi ya maafisa wake, wengine kunaswa hali iliyosababisha ilipofikia miaka ya 1947 na 1948 kwa kiasi fulani kuashiria kusambaratika kwa taasisi hilo la ukachero lililotamba duniani. Baadaye kutokana na kuongezeka kwa vitendo vyenye kutishia usalama wa nchi, kupinduliwa kwa serikali na taarifa za upotoshaji, majasusi mashuhuri na baadhi ya wanasiasa waandamizi waliokuwa pia majasusi wa GRU wakaajiriwa ili kupanua shughuli za kijasusi nje ya nchi kupitia zaidi mtandao wa KGB kuliko ule wa kijeshi (Military Intelligence).

Kuporomoka kwa GRU kulianza mwaka 1958 pale KGB ilipogundua kuwa Luteni Kanali wa GRU, Yuri Popov alikuwa jasusi wa CIA. Kufuatia taarifa hiyo, Khrushchev alimuamuru Mwenyekiti wa KGB, veterani wa idara maalum ya taaluma ya ujasusi, Ivan Serov kuendesha operesheni maalum dhidi ya watendaji wa GRU ili kuisafisha. Katika operesheni hiyo, mwaka 1962 KGB tena ikafanikiwa kumnasa afisa mwingine mwandamizi wa GRU Kanali Uleg Penkovsky ambaye taarifa za kijasusi zilionesha alikuwa akitumiwa na shirika la ujasusi wa nje la Uingereza, MI6 wakati huo huo akiwa wakala wa CIA (Central Itelligence Agency). Hata hivyo, Serov kwa huzuni kubwa alilazimika kuiacha nafasi ambayo ilishikwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa KGB Luteni Jenerali Petr Ivanovich Ivashutin ambaye ndiye aliyekuwa mkuu wa majeshi ya Vita nchini Urusi. Luteni Jenerali Petr Ivanovich, jitu nene lililokuwa na sura ya uchangamfu hata hivyo halikuwa likipendeza katika taasisi za ulinzi kwa tabia yake ya ukali, ukatili, majivuno na mwenye dharau kwa watendaji wa ngazi za chini.

Ili kuushika vyema wadhifa aliokabidhiwa, Luteni Jenerali Petr Ivanovich aliwateuwa maafisa wengine waandamizi watano wa KGB ambao aliwaweka katika nafasi za juu kiutawala katika GRU. Huo ndio uliokuwa mwanzo wa mfumo wa ujasusi jeshini nchini Urusi kushikwa na maafisa wataalamu waandamizi wa KGB. Baadaye ikawa sharti kwa GRU kutomuajiri yeyote awe afisa au wakala wake bila ya kwanza kupata kibali cha KGB, wakati huo huo KGB yenyewe ikitumia fursa hiyo kuchukua maafisa kadhaa wa GRU kuwa watendaji wake ndani ya GRU na katika maeneo mengine ya kijamii. Hongo na hadaa zinataarifawa kutumiwa na KGB katika kuwarubuni watendaji wa iliyokuwa GRU kuwa wapasha habari wake. Ilifanywa hivyo kwa mazingatio kwamba GRU ndiyo iliyokuwa makini zaidi kiutendaji katika mfumo mzima wa ukachero nchini Urusi. Hata hivyo mbinu za ukachero zilizotumiwa na GRU hazikuwa zikitofautiana sana na zile za KGB. Hata hivyo pamoja na usiri mkubwa uliokuwepo huku kila moja ikitoa taarifa za kijasusi kwa taratibu zake, kiutendaji GRU na KGB zilikuwa zikifanya kazi pamoja chini ya Komandi kuu ya mjini Moscow. Hata hivyo, kimaamuzi KGB ilikuwa juu kuizidi GRU.

KGB kwa upande mwingine ilikuwa na fursa ya kujua kila kilichokuwa kinaendelea ndani ya GRU kupitia majasusi iliyowapandikiza ndani ya GRU na kupitia taarifa zilizokuwa zikiwasilishwa makao makuu mjini Moscow. Kwa fursa hiyo iliweza kuingilia na kuelekeza utekelezaji wa operesheni zote za GRU kulingana na matakwa na maslahi yake. GRU ilisifiwa kwa miongo isiyopungua minne kuanzia mwaka 1920 kwa ustadi kupenyeza maafisa na maajenti wake (penetrations) katika mashirika mengine ya kijasusi, idara, jumuiya na taasisi za kijamii na kiulinzi. Wakati huo huo, GRU ilikuwa hodari wa kurubuni na kuhonga watendaji wa ngazi mbali mbali katika jumuiya, taasisi na nchi mbali mbali ili kupata taarifa muhimu za kijasusi kwa maslahi ya Urusi (infiltrations). Hata hivyo, katika operesheni zake GRU haikukosa kufikwa na mikasa mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukamatwa kwa baadhi ya maafisa wake sehemu mbali mbali duniani.

Mwaka 1963, Kanali Stig Eric Wennerstrom alikamatwa nchini Sweden na Luteni Kanali William Henry Whalen alinaswa nchini Marekani mwaka 1966. Mpaka kufikia mwaka 1967 zaidi ya makachero 29 wa GRU waliopenyezwa katika nchi saba duniani walinaswa kufuatia tukio la kutekwa nyara kwa Giorgio Rinaldi wa Italia. GRU kwa utendaji na malengo yake, inabaki kuwa taasisi kongwe, mashuhuri, na iliyotawala duru za kijasusi duniani ambayo hata hivyo inabaki kuwa kitengo kisaidizi cha Dubwana la kutisha la KGB la uliokuwa Umoja wa kisovieti wa Kikomunisti. Maelezo yaliyotolewa humu yanapatikana katika marejeleo kadhaa ya duru za kijasusi kikiwemo kitabu maarufu kijulikanacho kama kazi ya siri ya mawakala wa siri wa kisovieti (“The Secret Work of Soviet Secret Agents”).
 
Shirika La KGB

Shirika la ujasusi lisilo mfano wake katika historia huko nyuma na hata sasa ni KGB. Shirika hilo lilivuma sana karne ya 20. Ni vigumu kuweza kuujua undani wa KGB kwa kulinganisha na jumuia au taasisi nyingine zenye kujihusisha na ujasusi. Wala haliwezi kufahamika kwa maelezo tu ya kiistilahi kuwa ni taasisi la ujasusi kama linavyolezwa na Ulimwengu wa Magharibi. Lakini ukubwa na unyeti wake waweza kuonekana pale tu liliposambaratisha iliyokuwa USSR.

KGB iliweza kudhibiti kila kitu katika jamii ya Warusi zikiwemo dini, sanaa, sayansi, elimu, fikra, hotuba, vyombo vya habari, polisi, jeshi, idara za usalama, mila na tabia za wanajamii. KGB iliweza kuzichunguza shughuli zote za kijamii zikiwemo za makundi madogo na makubwa ya kijamii, safari za Warusi, kuwachunguza watu mmoja mmoja, kuwafuatilia watu walioonesha kupinga hali iliyokuwepo, waliotaka mageuzi, wenye ushawishi katika jamii kupitia mazungumzo kwenye magenge na mikusanyiko na katika maandiko. Watendaji wote katika balozi za nchi hiyo walikuwa maafisa wa KGB na walikuwa wakichunguzana wenyewe bila kujuana.

Makao makuu ya KGB yalikuwa katika jengo moja kubwa lililogawanywa shemu mbili; jengo kuu Derzhinsky Square. Ni jengo lililojengwa kwa mawe ambalo kabla ya mapinduzi ya kijamaa lilikuwa mali ya Kampuni ya Bima (All Russian Insuarance Company). Baadaye wafungwa wa kisiasa na askari wa Ujerumani waliokamatwa katika Vita Kuu ya Pili walitumika kama vibarua na mafundi katika ujenzi wa ghorofa ya tisa ya jengo hilo. Idara ya Utumishi ya KGB iliajiri wafanyakazi wasiopungua 400,000 waliokuwa makarani, walinzi wa jengo, walinzi wa mipakani, na waliokuwa katika kikosi maalum. Idadi ya makachero na majasusi wa KGB walikuwa ni mamia kwa maelfu. Hata hivyo idadi kamili ya maafisa wa KGB haikujulikana. Wafanyakazi waliohusika na shughuli za usalama tu walipaswa kuwa nje ya lango kuu la ofisi mnamo saa mbili asubuhi licha ya shughuli za kiofisi kuanza saa tatu. Derzhinsky Square ndilo jengo lililokuwa na ofisi za wakuu wa vitengo vyote vya KGB. Hata hivyo ofisi za operesheni zilikuwa katika majengo mbali mbali jijini Moscow. Baadhi ya wakuu wa KGB walikuwa mameneja, wakurugenzi, wakuu wa idara, viwanda, taasisi za kiraia na za kijeshi, jumuiya na makampuni mbali mbali nchini Urusi.

KGB iliundwa na kurugenzi kuu nne, kurugenzi saba zilizokuwa huru kiutendaji, na idara sita huru ambazo nazo ziligawanyika katika idara ndogo ndogo kadhaa. Shughuli zote za KGB zilifanyika chini ya vitengo, idara, kurugenzi na komandi. Kurugenzi Kuu (Chief Directorate) ndiyo iliyohusika na uendeshaji wa operesheni za nje ya Urusi. Kurugenzi Kuu ya pili (the Second Chief Directorate) ilihusika na usimamizi wa operesheni mbali mbali zilizokuwa dhidi ya maslahi ya taifa na wageni ndani ya Urusi. Kurugenzi Kuu ya ulinzi wa mipakani ambayo ilihusika na doria katika mipaka yote hasa ule uliokuwa upande wa China. KGB haikuwa na kurugenzi ya tatu na ya nne bali ilikuwa na kurugenzi ya tano iliyohusika na kazi maalumu ya usalama na udhibiti wa Warusi wenyewe ndani na nje ya Urusi. Kurugenzi huru ya saba ilihusika na ujasusi katika vyombo vya dola yakiwemo majeshi ya vita na yale ya usalama, operesheni za kiufundi, utawala, utumishi, uchunguzi (surveillance), mawasiliano na ulinzi. Idara huru sita zilihusika na upelelezi maalumu, fedha, uchambuzi na tathimini za operesheni, mawasiliano ya nchi, mfumo kamili wa ushushushu wa KGB (physical security of the KGB), masuala ya masijala na kuhifadhi kumbukumbu za operesheni mbali mbali. Kurugenzi Kuu ya kwanza, kurugenzi kuu ya pili na kurugenzi kuu ya tano kwa pamoja zikishirikiana na kurugenzi ya majeshi, zote kwa pamoja ndizo zilizoujenga na kuuendesha mfumo wa ujasusi wa KGB (Komitet Gosudarstvenoy Besopasnost) yaani kamati ya usalama wa dola (Committee for state security).
 
Umetafsiri kutoka kwenye kitabu gani?
naona jamaa ana-kopi toka kwenye hiki kitabu

MITANDAO YA UJASUSI DUNIANI
Ujasusi Wa Kizayuni Kutamalaki Dunia

Imeandikwa na: ‘Aabidiyn H. Kifea
Na Kupitiwa na: Muhammad Baawazir

Huda Publishers
Dar es Salaam

Chapisho La Kwanza 2006
Mitandao Ya Kijasusi
Ujasusi Wa Kizayuni Kutamalaki Dunia

Isbn 9987-441-10-6

Mtandao Wa Ujasusi Duniani - Harakati Za Kizayuni: 013 - Mifumo Mingine Ya Ujasusi Duniani: CIA, RGU, KGB | Alhidaaya.com
 
George Tenet is not only not a jew as reported (he is of Greek descent and Greek Orthodox religion) there are actually reports that he has anti semitic tendencies.

So the Jews take the blame for having had their man at the CIA, and their supposedly man rant some anti-semitic words after some Scotch at Prince Bandar's pool party.

Just one example of how flawed this whole propaganda is.

"The Protocols of The Elders of Zion" has been long debunked as a forgery see [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/The_Protocols_of_the_Elders_of_Zion"] here [/ame]

The Jews are overrated, and in this ovverating of the Jews, the gentiles are creating a self fulfilling prophecy.
 
Last edited:
naona jamaa ana-kopi toka kwenye hiki kitabu

MITANDAO YA UJASUSI DUNIANI
Ujasusi Wa Kizayuni Kutamalaki Dunia

Imeandikwa na: ‘Aabidiyn H. Kifea
Na Kupitiwa na: Muhammad Baawazir

Huda Publishers
Dar es Salaam

Chapisho La Kwanza 2006
Mitandao Ya Kijasusi
Ujasusi Wa Kizayuni Kutamalaki Dunia

Isbn 9987-441-10-6

Mtandao Wa Ujasusi Duniani - Harakati Za Kizayuni: 013 - Mifumo Mingine Ya Ujasusi Duniani: CIA, RGU, KGB | Alhidaaya.com

Mzee rekebisha kidogo. Jamaa ana kopi na ku-PASTE ..Nadhani hata jina lake umelicheki linavyooana na kazi yake hiyo. PASTER.. :D
 
hakuna kitu kibaya kama unafiki, waislamu kote duniani wanalalamika islaeli kuchukua ardhi ya wapalestina, sababu kubwa ni kuwa wapalestina ni waislamu, lakini ukija africa waarabu waivamia na kuichukua nchi ya Sudan, lakini kwa sababu waislamu ndio walioteka dunia nzima ya kiislamu ipo kimya kabisa na wanaona ni sawa tu
 
"Na wanapoambiwa msifanye uharibifu katika ardhi, husema:
Hakika sisi ndio tutengenezao.
Kwa hakika wao ndio waharibifu hawajui".
(2:11-12)

"Na Allah ndiye mlinzi wa walioamini, huwatoa kutoka katika giza na kuingiza katika nuru;
lakini wale waliokufuru viongozi wao ni matwaghuti,
huwatoa kutoka katika nuru na kuwaingiza gizani.
Hao ndo watu wa motoni humo watakaa milele".
(2:257)

"Enyi mlioamini! Kuweni wenye kusimamisha uadilifu,
mshuhudiao kwa ajili ya Allah (s.w.)..."
(4:135).
 
"Na wanapoambiwa msifanye uharibifu katika ardhi, husema:
Hakika sisi ndio tutengenezao.
Kwa hakika wao ndio waharibifu hawajui".
(2:11-12)

"Na Allah ndiye mlinzi wa walioamini, huwatoa kutoka katika giza na kuingiza katika nuru;
lakini wale waliokufuru viongozi wao ni matwaghuti,
huwatoa kutoka katika nuru na kuwaingiza gizani.
Hao ndo watu wa motoni humo watakaa milele".
(2:257)

"Enyi mlioamini! Kuweni wenye kusimamisha uadilifu,
mshuhudiao kwa ajili ya Allah (s.w.)..."
(4:135).

Ndio maana waungwana walishaliona hili, limefungwa Jukwaa la Dini mnakuja ku-pollute na huku. Wewe kama mayahudi wanakukera nenda kapambane nao huko huko ..mnatumalizia bandwidth tu hapa..
 
Enyi mlio amini! Msiseme: "Raa'ina", na semeni: "Ndhurna".
Na sikieni! Na makafiri watapata adhabu chungu.
Walio kufuru miongoni mwa watu wa Kitabu na washirikina hawapendi mteremshiwe kheri yoyote kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Na Mwenyezi Mungu humkusudia kumpa rehema yake ampendaye. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kubwa.
Ishara yoyote tunayo ifuta au tunayo isahaulisha tunailetea iliyo bora kuliko hiyo, au iliyo mfano wake. Hujui kwamba Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu?

Q 2:104-106
 
Na unapo waona, miili yao inakupendeza, na wakisema, unasikiliza usemi wao. Lakini wao ni kama magogo yaliyo egemezwa. Wao hudhania kila ukelele unao pigwa ni kwa ajili yao. Hao ni maadui; tahadhari nao. Mwenyezi Mungu awaangamizilie mbali! Vipi wanapotoka na haki...?
 
*
Idara Ya BOSS Ya Utawala Wa Makaburu

Likitoa maelezo juu ya kuundwa kwa idara ya ujasusi ya serikali ya makaburu mwezi Mei mwaka 1969, jarida la kiingereza la New Statesman liliruka na kichwa cha habari kilichosomeka “Gestapo Jipya laanzishwa Afrika Kusini”. Generali Hendrick van den Bergh, maarufu akifahamika pia kama H.J, ndiye mwasisi wa BOSS ambaye alikaririwa akidai kuwa kiuhalisia, idara hiyo haikuwa mpya bali ulikuwa ule ule mtandao wa idara ya usalama wa Taifa uliofanyiwa mabadiliko kidogo ambao awali ulikuwa ukiendeshwa kinyume cha kanuni, hivyo baadaye, kama mbinu ya kikazi, ukafanywa kuwa rasmi chini ya kibali cha Bunge kwa jina jipya la BOSS (South Africa’s Secret Police). Makao makuu ya Idara ya BOSS yalikuwa kwenye jengo moja zuri lililoitwa Concilium katikati ya Jiji la Pretoria ambako, maafisa wote waandamizi na makarani walihamia wakitokea idara ya zamani ya Usalama wa Taifa iliyoitwa, “Republican Intelligence”. Hiyo ilikuwa ofisi mpya iliyohamishiwa kila kilichohusika na usalama, yakiwemo mafaili na nyaraka zote nyeti.

Jina BOSS halikuwa limeleta tofauti yoyote ya utendaji kwa maafisa wote wa iliyokuwa idara ya usalama kwa sababu, karibu watendaji hao wote walibaki na “code” zao za awali zilizowatambulisha kama maafisa wa idara hiyo. Katika taarifa za kikazi kwa wakuu wa idara zilizokuwa chini ya jina jipya la BOSS, majasusi wote waliendelea kutumia alama “code” zao zile zile za awali, kama jasusi mmoja mkubwa ambae sasa anaishi nchini Ireland anavyofahamisha:

“Wengi wetu tulibaki na nambari zile zile za utambulisho (code numbers) tulizopewa na “Republican Intelligence”, tuliendelea kuwa chini ya utaratibu ule ule wa ukusanyaji wa habari lakini tukatakiwa kujitolea zaidi kwa kuwa kiasi cha pesa kilichotengwa kilikuwa kidogo sana, ni paundi milioni 20 tu zilizotengwa kwa ajili ya BOSS kwa mwaka ule wa kwanza”.

H.J ndiye aliyejulikana kama jasusi namba moja ambaye mitandao yote ya usalama ikiwemo ile ya jeshi pamoja na kikosi cha maji na anga, ilikuwa chini yake. H.J aliyekuwa mtu mashuhuri katika duru za ulinzi, usalama na ujasusi nchini Afrika ya Kusini, alikuwa mtumishi chini ya waziri mkuu John Voster. Umashuhuri wa H.J ulipata kutaarifiwa na baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa ambavyo vilichapisha kwa urefu wasifu wa jitu hilo la miraba minne vikimtaja kwa wasifu wa “mtu mpya katili” nchini Afrika Kusini.

Taarifa kwamba BOSS ingeundwa zilianza kufahamika kwa siri na baadhi ya waliokuwa watendaji wa ndani wa duru za usalama ambao Baba Guy na Katie, aliyemuoa mhariri wa habari za ulimbwende na mitindo, Wendy Kochman, anajitaja kuwa ni mmoja wa hao. Yeye anajitaja kama ni katika wale waliodokezwa mwanzo juu ya kuundwa kwa dubwana hilo lililoondokea kuwa la hatari sana kwa harakati za weusi nchini humo. Mume wa Wendy Kochman anabainisha kwamba:

“Nilifahamu juu ya kuundwa kwa BOSS mapema Aprili 19 mwaka 1968. Siku hiyo usiku, nilikutana kwa siri na H.J. van den Bergh chumba namba 856 au 858 katika Hoteli ya Grosvenor, London na akanidokeza kuwa walikuwa mbioni kuunda idara mpya ya ujasusi. Brigedia P.J. Tiny Venter aliyekuwa mkuu wa idara ya upelelezi ya Afrika Kusini alikuwepo kwenye mazungumzo hayo. Binafsi sikutaka awepo, nikalazimisha nisikae sana kwa kuanza kumshutumu kuwa alikuwa akivamia na kuchanganya mambo. Kwa ufundi mkubwa H.J alijaribu kuyazima majibizano yetu kwa kusema hiyo ilionesha ni kiasi gani Afrika Kusini ilipeya katika fani ya ujasusi. Hata hivyo niliendelea kumshutumu P.J. vikali nikidai alikuwa na pupa wakati akipokea taarifa za kikazi. Alikuwa mwepesi kuchukuwa hatua, huo haukuwa mwendo mzuri kwangu kwani ungesababisha nigundulike mapema hasa na watu waliokuwa karibu sana na mimi. Kuthibitisha madai yangu, nilitaja mifano ya wanahabari wawili waliokuwa mjini London, Dennis Kiley na John Goldblatt ambao wote walipokea barua kutoka serikali ya Afrika ya kusini katika kipindi cha wiki moja baada ya mimi kuwataarifa. Nikasema mtindo huu si mzuri kabisa kwa kuwa hiyo ingesababisha washuku kuwa ni mimi niliyewafitini kwasababu muda wote nimekuwa nao na walikuwa wakielezea kupinga kwao ubaguzi. H.J alimgeukia P.J. na kumwambia nilikuwa sahihi kwa hilo; P.J alionekana kutulia na baada ya muda kidogo akaondoka mle chumbani akidai alikwenda kumpigia simu rafiki yake fulani. Kuondoka kwa P.J. nilikufurahia kwa kuwa sikupenda wakati nikiwasilisha taarifa zangu kwa mkuu, mtu mwingi asikilize, na kwa kweli H.J alipendelea kunieleza masuala nyeti wakati tuko peke yetu.”

Kuhusiana na Mwanahabari Denis Kiley aliyetaarifiwa katika taarifa ya mume wa Wendy, yeye alikuwa ni mwandishi wa habari wa kwanza kupigwa faini chini ya kifungu cha kanuni ya Magereza ya mwaka 1960 ambayo ilipiga marufuku kuandika habari zilizohusu hali na wafungwa kwenye magereza. Katika habari yake, Denis Kiley aliandika juu ya kufa kwa wafungwa Waafrika kutokana na ugonjwa wa kifua kubana (pneuomonia) katika Gereza la Modder B. Sababu ya ugonjwa ilitokana na kukosekana kwa mablanketi wakati wa majira ya baridi hasa nyakati za usiku. Denis Kiley baadaye alikuwa mhariri wa gazeti la Financial Times.

Wakiwa wamebaki wawili tu katika Hoteli ya Grosvenor, H. J alimwambia asiwe anapoteza muda kupeleka taarifa Pretoria juu ya Amnesty International. Ilivyokuwa ikifahamika, Amnesty International iliundwa mwaka 1961 mjini London ikishughulika na kile kinachoitwa haki za binaadamu hasa kwa wafungwa kwenye magereza. Akijibu swali la kwa nini taarifa hizo zisitumwe Pritoria, H.J alisema, Wamarekani wanafahamu siri nyingi za Amnesty International. Wamejipenyeza barabara ndani ya shirika hilo, katika kila nchi wana mawakala wao, ni wao wanaoendesha makundi ya Amnesty International na wamekuwa wakiyatumia kwa maslahi yao.

Mume wa Wendy alipoonesha kushangazwa na hilo, H. J alitabasamu kisha alimwambia, “kama unalistaajabu hilo, basi ni vema ufahamu kuwa CIA itakuwa ya kipuuzi kabisa iwapo haitakuwa imejipenyeza katika shirika kama Amnesty International”. H. J alioongeza, “wakomunisti na wale wa mlengo wa kushoto ni watu wenye matatizo sana karibu kila nchi, na kwamba wanaharakati wao wengi wamekuwa wakikamatwa na kufungwa kila siku. Watu wa mlengo wa kushoto wangehusishwa na jambo moja kuwa wamekuwa na kawaida ya kuwaona mashujaa wale wanaokamatwa na kufungwa, hawa ndio wanaoheshimika sana miyongoni mwa makomredi”. H.J aliendelea kusema na kuongeza kwamba:

“Wamekuwa wakiwatumia watu wao wanaokamatwa na kufungwa kuchochea makundi upinzani, kila anayeachiwa hupewa heshima kubwa, na wamekuwa wakitumia vifungo katika propaganda zao za kisiasa, ndiyo sababu kwa nini CIA ilikuwa ikitumia jumuiya kama Amnesty International. Kwa kujipenyeza katika shirika hilo karibu katika kila nchi, CIA imekuwa ikivuna taarifa nyingi ambazo ni pamoja na kujua ni wepi waliokuwa wakiwazuru wafungwa wa kisiasa kwenye magereza, nani waliokuwa wakiwafadhili katika kesi zao mahakamani, nani aliokuwa akilipia rufani zao, nani waliyekuwa wakishinikiza kuachiwa kwao na nani waliokuwa wakiwasaidia kutoroka”.

Huku akitabasamu, H. J alimwambia mume wa Wendy jinsi CIA ilivyofanikiwa kueneza uvumi mkubwa pale ilipodai kuwa Amnesty International kilikuwa kitengo cha KGB kilichoundwa kuwasaidia wafungwa wa kikomunisti sehemu mbali mbali duniani ili kuikubalisha kwa watu wa mlengo wa kushoto. Ambacho mtu angejifunza kutokana na maelezo hayo ya H.J juu ya CIA na Amnesty International dhidi ya KGB na wakomunisti, ni ugunduzi wa mbinu kama hiyo iliyokuwa ikitumiwa na wataalamu wa propaganda mjini Pretoria kueneza uvumi dhidi ya taarifa za Amnesty International zilizokosoa hali mbaya ya magereza nchini Afrika Kusini. Uvumi huo mbali ya kuijenga serikali ya Afrika Kusini machoni mwa CIA ulikuwa pia ulikuwa ukiijenga serikali hiyo kwa mpiga kura ili awaone wakomunisti kama watu hatari waliokuwa tayari kuyaanika mambo ya ndani ya Afrika Kusini kupitia taarifa za Amnesty International. H. J alifafanua kwamba:

“Nilikuwa nikipokea mamia ya nyaraka za Amnesty tangu mwaka 1968 hadi mwaka 1974. Pale nilipojisikia kuifahamisha Pritoria nilifanya hivyo. Hata hivyo, baadaye nilichana nyaraka zote na kuzichoma moto. Pale ambapo sikuwa tayari kufanya hivyo, nililazimika kuzihifadhi taarifa zote muhimu katika kumbukumbu zangu za siri.”
Kwa ufupi Afrika Kusini ilikuwa na taarifa za siri za Amnesty International za sehemu mbali mbali ulimwenguni. Na ufuatao ni mfano mmoja wa maelezo yaliyopatikana kwa H.J mara tu aliporejea Afrika Kusini:

Profesa mmoja aliyeitwa Michael ‘Mike’ Pentz aliyekuwa mtaalamu wa kompyuta na aliyeanzisha shule maalumu kwa wasiokuwa wazungu mjini Cape Town, aliondoka Afrika Kusini mwaka 1974 baada ya serikali kutaka kumkamata na kumtesa akidaiwa kuunda jumuiya ya shule za usiku iliyoitwa Cape Paninsula Night Schools Association (CPNSA).

Kwa kuhudhuria darasa hizo za usiku, watu weusi (Waafrika) walikuwa wakionekana kuvunja kanuni ya maeneo ya miji ambayo iliwakataza weusi kuingia maeneo ya wazungu. Profesa Mike Pentz alikimbilia Uswisi ambako alijiunga na tawi la harakati za kupinga ubaguzi.

Idara ya BOSS ilimwambia H. J kuwa wamedokezwa kutoka chanzo cha kuaminika kwamba Profesa Mike Pentz ameomba kwenda kufundisha katika Chuo Kikuu cha Cambridge na ilishukiwa kuwa amefanya hivyo kama hatua yake ya awali kutaka kujipenyeza katika programu za utafiti wa nguvu za kinuklia unaoendeshwa na serikali ya Uingereza nchini humo. BOSS iliongeza kuwa ilikwishaiarifu idara ya usalama ya Uingereza, kwa ajili hiyo maombi ya Profesa Pentz yaliwekwa kando kwa sababu za kiusalama.

Pretoria ilitaka kufahamu kutoka H. J iwapo Profesa Pentz alikuwa na uhusiano wowote na watu waliokuwa wakipinga mfumo wa kibaguzi wa Afrika Kusini waliokimbilia nchini Uingereza kwa sababu BOSS ilikuwa na taarifa kuwa Profesa Pentz alishatembelea Cuba mwezi Januari mwaka 1968 ambako alihudhuria kongamano la utamduni, huko alijenga urafiki na Dennis Brutus na Alex La Guma, wote hao walikimbia nchi baada ya serikali kupitisha sheria ya kukifunga Chama cha Wakomunisti nchini Afrika Kusini.

Ujumbe mwingine alioupokea H. J kutoka BOSS kuhusiana na Profesa Mike Pentz ulikuwa ule wa mwezi Machi mwaka 1970. Niliambiwa kuwa Profesa Pentz kwa wakati ule alikuwa Mwadili wa Wanafunzi katika Kitivo cha Sayansi cha Chuo Kikuu Huria na alikuwa rafiki mkubwa wa Canon Collins msimamizi wa mfuko kwa ajili ya masuala ya ulinzi na misaada ya kibinadamu kwa makundi ya harakati za ukombozi.

H. J alitaarifiwa, kuwa kwa wakati fulani Profesa Pentz alikuwa akiishi nyumba moja iliyokuwa Henley lakini badaye akahamia eneo la Milton Keynes, Backinghamshire. BOSS ilimuomba H. J atafute anuani kamili ya Profesa Pentz. Hata Profesa Pentz alipokuwa Uswisi BOSS walimuomba H. J ampeleleze kwa kiasi gani alikuwa karibu na Pasta Pierre Bungener, mwanachama na mwanzilishi wa Amnesty International.

Mara nyingine, BOSS ilimtumia H. J ujumbe kama ule ukiwa na maelezo tofauti: kwamba Amnesty International ilidai kuwa isingeendelea kuwasaidia wafungwa ambao walipatikana na makosa ya kuendesha mapambano ya silaha. Pamoja na mengine, H. J alipewa ombi na BOSS, afuatilie kwa nini mzee mmoja chotara, George Peake, ambaye alihukumiwa nchini Afrika Kusini kwa kosa la kutega bomu alikuwa akiendelea kupata paundi 30 kwa mwezi kutoka Amnesty International.

Kwa ujanja mkubwa H. J aliyafanyia kazi maombi hayo ya BOSS na kufanikiwa kumuhoji “mzee chotara”, George Peake, kuhusiana na suala alilofahamishwa. George Peake alimwambia H. J kwamba alipeleka maombi yake Amnesty International kuomba msaada wa fedha kwa sababu alijiondoa katika ANC akaungana na harakati za mapambano za Chama cha Weusi kilichoitwa PAC (Pan African Congress) ambacho kifedha kilikuwa dhalili. George Peake alidai Paundi 30 alizokuwa akipokea kutoka Amnesty International kwa hakika alikuwa akilipwa na jamaa mmoja wa Amnesty International aliyeitwa Peter Benenson kutoka katika mfuko wake binafsi. Wapi BOSS lilikokuwa ikipata taarifa juu ya watu hawa, hilo lilikuwa swali ambalo majibu yake yalikuja kuwa wazi kadri H. J alivyoendelea kuletewa maagizo ya kufuatilia.
 
Ujasusi Wa BOSS Ndani Ya Amnesty


Mnamo mwezi Juni au Julai 1972 H. J alipokea telegramu kutoka BOSS iliyokuwa na ujumbe huu:

“Stephen Bubb c/o 19 Gladwin Close, Wigmore, Gillingham, Kent yumo katika wale wanaolipwa na Amnesty kama mfungwa aliyehukumiwa Pietermaritzburg, mjini Natal mnamo mwezi wa Aprili, 1972. Pesa hizo anatumiwa na kundi la Amnesty International la mjini Towns. Tafadhali peleleza na pata taarifa zaidi.”
BOSS pia lilimtumia H. J ujumbe mwingine uliodai na/ au kuwa na anuani ya kwamba:
“Stella Joyce anaaminika kuwa ni wakala wa CIA akiwa kama mmoja wa wanaharakati wa kisiasa wa Afrika Kusini waliopo mjini London. Aliacha utumishi wa Amnesty International na kujiunga na mfuko unaojulikana kama ‘Primitive People’s Fund’. Huyu ni yule Stella Sweetman, mfanyakazi wa Amnesty International ambaye sasa ameolewa na John Cavill, mwanaume wa kizungu ambaye ni mwanahabari anayeishi mjini London. Swali: Ni nani anayeeneza uvumi juu ya Stella Joyce kwamba ni wakala wa CIA? Atakuwa ni Barney Zackon, mwanaharakati kutoka Afrika Kusini ambaye sasa anaishi Mtaa wa 12 Kiddepore Gardens, London NW3. Pata taarifa zaidi juu ya uvumi huo.”

Alivyofahamu H. J, BOSS lilikuwa na uhusiano fulani na idara ya Upelelezi ya Hispania(Spanish Security Police) mwaka 1972. Mwaka huo huo H. J aliombwa kufuatilia taarifa za mwanamke huyo katika idara hiyo ya Hispania. Ujumbe alioupokea H. J ulidai wazi wazi kuwa hapakuwa na uhusiano kabisa. H. J aliambiwa kwamba chochote kilichokuwa kikiwasilishwa ilikuwa ni kwa msaada wa “jamaa zao fulani wa mjini Madrid”. Hivi ndivyo BOSS ilivyomwambia H. J.

Mapema mwaka 1972, Bibi Thelma E. H Pahahi wa Mtaa wa 4, The Graylands, High Rickleton, County Durham, alikwenda kwa jamaa wa Amnesty International kuwaarifu kuwa alikuwa mbioni kuandika makala juu ya Gereza la Segoviya. Mwezi Februari, 1972, Amnesty International mjini London ikarejeshea majibu ambayo yalisema hapakuwa na sababu ya kuandika makala juu ya Gereza hilo, na kwamba habari zinazomuhusu mfungwa aliyeko kwenye gereza hilo anayeitwa Jose Sandoval, zisichapishwe. Katika barua hiyo hiyo kwa Bibi Pehahi, Amnesty International ilieleza jambo ambalo ni muhimu kidogo kulijua juu ya habari za Madrid. Nukuu halisi ya barua hiyo ni hii hapa:
Lakini, kwa sababu ya uhusiano maalumu uliopo kati ya Amnesty International na serikali ya Hispania ambao unawaruhusu wanachama wa Amnesty International kutembelea wafungwa kwenye magereza, ni muhimu kwa hivi sasa Amnesty isielezee chochote juu ya hali za wafungwa waliopo katika magereza ya nchi hiyo na hasa kuchapisha taarifa zitakazopatikana kufuatia ziara katika magereza hayo. Tukifanya hivyo, makundi ya watu yatajenga shauku ya kutaka kujua zaidi juu ya wafungwa wanaowahusu, tuwe waangalifu, tusieleze kuwa taarifa hizo zimepatikana kufuatia ziara katika magereza hayo. Hata hivyo, tunafikiria kuchapisha taarifa nzito juu ya magereza hayo siku za usoni hasa tutakapokusanya maelezo mengi kutoka kwa ndugu, marafiki na jamaa za wafungwa hao.
BOSS ilimtaka apeleke taarifa kwa njia ya ujasusi iwapo Amnesty International ilikuwa mbioni kuchapisha taarifa hizo nzito juu ya magereza ya Hispania. Maombi haya yalimshangaza sana kwamba, iwapo BOSS ilikuwa linapokea taarifa nzito na za mara kwa mara kutoka ndani ya Amnesty International, kwa nini ilikuwa ikimtaka afuatilie wakati ikijulikana wazi kuwa hakuwa na rafiki katika Amnesty International ambaye angempatia taarifa nyeti kuhusiana na mambo inayoyashughulikia?

Mwezi Februari 1972, BOSS ilimtumia ujumbe mrefu kuhusiana na John Martinus Ferus, ambao nao ulionesha kwamba Afrika Kusini pia ilikuwa na taarifa zote muhimu na ikizijua vyema shughuli za wanachama wa Amnesty International nchini Ujerumani.
BOSS ilimwambia:
“Ferus, John Martanus, mwanaume chotara mtu mzima akifahamika pia kama “Hennie” aliyeishi Mtaa wa 14 Hamner, Worcester, Cape Province, ambaye alikuwa mwanachama wa Umoja wa Wafanyibashara (SACTU), ambaye aliwekwa kizuizini Oktoba 1, 1963 na tarehe 30, Desemba, 1963 akaachiwa kwa dhamana baada ya kuhusishwa na matukio ya hujuma dhidi ya maeneo ya serikali akiwa kama mwanachama wa ANC. Shitaka hilo lilifutwa na mahakama mwezi Januari 1964 bali aliendelea kukabiliwa na ile amri ya kupigwa marufuku kwa Chama cha Kikomunisti. Chini ya Agizo la Serikali Namba 9 Kifungu Namba 1 cha kanuni Namba 44 ya mwaka 1950 ukomunisti ulipigwa marufuku . Mwezi Aprili 1966 alikamatwa na kuteswa kwa kuvunja kanuni hiyo, maelezo zaidi juu ya suala hili ni muhimu kwa kuwa zipo taarifa kuwa yuko mbioni kuja Afrika Kusini kutembelea familia yake kupitia jamaa mmoja wa Amnesty International. Bado sheria ingalipo na ujaji wake hapa utakuwa kinyume cha kanuni hiyo. Ferus alikabiliwa na kanuni nyingine ya kuzuiliwa nyumbani kutokana na amri hiyo ya kukipiga marufuku Chama cha Kikomunisti.
Kisha BOSS ikatoa maelezo ya kina juu ya safari ya Ferus iliyoandaliwa na mwanachama huyo wa Amnesty International. Maelezo hayo yalisema:
“Taarifa tulizonazo ni kwamba Herr Claus-Rudiger von Hertzberg, mwanachama wa Amnesty International, anapanga kumtembelea Ferus. Hakuna ombi rasmi lililofanywa kabla ya kuandaa ziara hiyo, kwa hiyo tungependa kujua lini Von Hertzberg anakusudia kusafiri kuja Afrika Kusini. Chanzo chetu kisicho cha moja kwa moja ndani ya Amnesty kimetilia shaka suala hili, kwa hiyo pokea maelezo haya muhimu ambayo yatakuongoza katika upelelezi wako, maelezo haya mafupi ni kukusaidia usiende kwa wasiohusika wakati ukifanya upelelezi huo.”

Chanzo cha upelelezi wa habari juu ya kutembelewa Ferus kinasema ifuatavyo:

“Wakati fulani, shirika la Amnesty International nchini Ujerumani (Group 4) lilishughulikia suala la Ferus lakini kabla ya kwenda mbali, Von Hertzberg, aliyekuwa akilijuwa vyema suala hilo akahamia kundi la Amnesty International Namba 208 lilipo mjini Wolfhagen, hivyo akalizima kinamna suala hilo, kwa kuwa ilionekana alikuwa na ukaribu sana na jamaa huyo. Kundi namba 208 lilifungwa mwezi Novemba 1970 pale Von Hrtzberg alipohamia mjini Munich pamoja na faili la jamaa huyo. Amekuwa na mawasiliano na mama yake Ferus na amekuwa akijaribu kumuunganisha mtuhumiwa huyo na kundi la Amnesty la nchini Sweden. Von Hertzberg vile vile alipanga na jamaa yake mmoja kwenda kwa mama yake Ferus kuandaa mipango ya baada ya Ferus kuachiwa kutoka gerezani. Jamaa huyo tunamfahamu na katika ziara hiyo mjadala uliofanyika ulihusu ni namna gani atakavyotoroshwa Ferus mara baada ya kutoka gerezani”.

Hata hivyo, alipotoka gerezani Ferus alikataa kuondoka Afrika Kusini baada ya kushawishiwa na mpenzi wake mmoja. Msemaji wa kundi la Amnesty International nchini Sweden jamaa mmoja aliyeitwa Herr Stephen Rosentrom, mara kwa mara alikuwa akikutana na Von Hertzberg mjini Munich na walikuwa wakijadiliana kile ambacho BOSS wamekuwa wakikiita kama “hatua zaidi” zitakazochukuliwa kuhusiana na suala la Ferus.

Kwa mujibu wa barua iliyotumwa kwa Martin Enthoven wa Amnesty International mjini London, Februari 7, 1972 kutoka kwa Theresia Becker wa kundi la Amnesty International Namba 45 (75 Farmstrasse, Woldorf 6083, Ujerumani Magharibi), Herr Von Hertzberg na Herr Rosentrom waliendelea kulishughulikia suala la Ferus licha ya Ferus mwenyewe kutokuwa tayari kuondoka Afrika Kusini. Kwa wakati ule Von Hertzberg alisema angependa kukutana ana kwa ana na Ferus kabla ya muda mrefu kupita na angefanya hivyo wakati wa ziara yake Afrika Kusini. BOSS ilikusudia kumkamata Herr Von Hertzberg kama angalimtembelea Ferus. Hata hivyo, alifuta mpango wake huo baada ya jamaa mmoja kumuonya kuwa asijitie kitanzi mwenyewe.

Gordon anasema Mwaka 1973, BOSS ilimtumia ujumbe mwingine uliosema: Abraham, Eric Antony, mwanaume mzungu wa Afrika Kusini, mwanafunzi, umri miaka 19, alikuwa Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa Vijana uliojulikana kama National Youth Action mwaka 1971 na mwanachama wa NUSAS katika Chuo Kikuu cha Cape Town. “Kijana Tatizo” kama BOSS lilivyombabatiza, kwa wakati ule alikuwa akifanya kazi katika kundi la Amnesty International mjini London. Kwa mara ya mwisho anuani yake ilikuwa: 42 Southfield Road, Oxford, simu namba 42602; na rafiki yake huko aliitwa David King. Baada ya kupokea ujumbe huo, Gordon alimuuliza mkuu wake mjini London nini maana ya “kijana tatizo”, akajibu ulikuwa msamiati uliotumiwa na BOSS kwa vijana wote waliokuwa wakikataa kuwa wapasha habari ndumakuwili (Double Agents). Baadaye Eric Abraham alizuiliwa nyumbani wakati aliporejea Afrika Kusini. Mara kwa mara BOSS ilikuwa ikitumiwa ama ujumbe au nakala za nyaraka ambazo dhahiri zilichomolewa kutoka katika mafaili ya Amnesty International mjini London. Nyingi ya nyaraka hizo zilichomwa moto zikabaki chache. Mojawapo ni nakala halisi ya barua iliyotumwa na Bibi Tracy Ulltvei Moe kwenda kwa Bibi Jean Etsinger mjini Rio De Jeneiro Brazil, ya tarehe 11 mwezi Februari 1972. BOSS ilikuwa na kawaida ya kutuma nyaraka za Amnesty International zilizogongwa muhuri wa “siri” kila mwezi. Jasusi anayesimulia kisa hiki (Gordon) amedai kuwa nayo moja ya nakala hizo (Namba 142) ambayo imeorodhesha watendaji wote wa Amnesty International mjini London. Aidha nyaraka hiyo inaonesha mambo waliyokuwa wakiyachunguza katika nchi mbali mbali kama vile Iran, Indonesia, Sudan, Tunisia, Morocco, Ugiriki, Uturuki, Paraguay, Cuba na Ireland ya Kaskazini. Aidha, BOSS ilimjulisha juu ya watendaji wote wapya wa Amnesty International na anuani zao kamili. Bado alikuwa na orodha ya watendaji wapya wa Amnesty International wa mwaka 1970 ikiwa na majina 49. Hilo laweza kuwa jambo litakalowastaajabisha wakuu wa Amnesty International wakizingatia umakini wao kiusalama. Watashangaa ni nani aliyefichua majina ya watendaji wa shirika hilo. Hiyo ilikuwa kazi ya BOSS!

“Mwanachama wa Amnesty International Namba 233 aliorodheshwa kama Viktor Melleney mkazi wa Barabara ya 40 Grosvenor, Chiswick, mjini London W4. BOSS ilimpeleleza jamaa huyu iwapo ni yule aliyekuwa muigizaji na mtayarishaji mashuhuri wa michezo ya kuigiza Afrika Kusini, Viktor Mellene, au ni mmoja wa jamaa zake. Kwa kweli, hakuwa huyo”.

 
Boss Chanzo Cha Vurugu Za Soweto

Juni 17, 1976 saa tatu asubuhi maelfu ya wanafunzi wa Soweto walikusanyika uwanja wa shule ya Orlando kupinga ubaguzi nchini Afrika kusini. Upinzani huo ulikuja kufuatia ukaidi wa serikali ya makaburu kuitikia vilio vya wananchi. Wanafunzi walikuwa wakipinga kufundishwa masomo mbali mbali kwa lugha ya kiafrikana badala ya kizulu. Likiripoti hamasa iliyoibua vurugu kubwa, gazeti la Rand Daily Mail la liliandika:

“Walikusanyika kwa maelfu, serikali haikutaka kulimaliza suala hilo kidiplomasia, ikatuma idara yake ya kijasusi ya BOSS kunasa watu kimya kimya na vikosi vya maaskari ambao walifyatua risasi za moto kuzielekeza kwa ummti wa watu, wengi walianguka na kufa au kujeruhiwa, kwa kibri na kutokujali magari aina ya "mbogo” yalirandaranda sehemu mbali mbali mitaani”.

Ukamataji wa watu kimya kimya nyakati za usiku uliokuwa ukifanywa na BOSS na mateso dhidi ya weusi katika selo za mauwaji, hayakuzima mori wa Wananchi, maelfu waliendelea kujisanya kwa hasira za kuuliwa na kujeruhiwa. Walijibu mapigo kwa kuweka vizuizi barabarani na mitaani, kuchoma matairi na kuanzisha mapambano ya kudai haki yaliyoibua moto ambao uliilazimisha serikali ya makaburu isalimu amri mbele ya nguvu ya umma. Gazeti la Rand Mail la juni 18 liliandika kuwa kufuatia kuuliwa kwa watu wengi, wengine kadhaa kujeruhiwa, majumba ya serikali yalianza kuchomwa moto kila mahali, ilikuwa piga ni nikupige, moto na moshi mweusi ulitanda eneo lote la Soweto. Gazeti la The Times likiandika habari hiyo lilidai, vurugu ililipuka kwa mara nyingine tena usiku wa siku hiyo na kuendelea kucha kutwa kwa muda wa siku tatu walengwa wakubwa walikuwa mashushushu wa BOSS, maafisa wa serikali, familia, gari na nyumba za wakubwa”. Aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani James Kruger akikaririwa na gazeti la Rand Mail la juni 18 mwaka huo alidai hawakudhani kuwa yale yangeliweza kutokea kutokana na mbinu za hali ya juu ilizokuwa nazo idara ya ujasusi ya BOSS, hata hivyo aliwashutumu aliowaita wahochezi wachache na akajitapa kuwa vyombo vya dola vingesimama imara kukabili uasi.

Maelezo juu ya idara ya ujasusi ya BOSS ilivyosababisha vurugu la Soweto yanapatikana kwa upana zaidi katika marejeleo kadhaa ya duru za kijasusi vikiwemo vitabu vya Soweto: Life and Struggles of a South African Township kilichoandikwa na Valentin Gorodnov na Inside BOSS, South Africa’s Secret Police, kilichoandikwa na Gordon Winter, an Ex-Spy’s Dramatic and Shoking Expose.
 
Bibliografia
Adolf Kober, “Jews in the Revolution of 1848 in German, Jews Social Studies(194 .
Ali A. Mazrui, Cultural Forces in World politics, Zionism and Apartheid, James Currey Ltd London, Heinemann Educational Books Nairbi, Kenya, uk. 145-162.
Andrew Tully CIA Crest Book, 1963, uk 84 –89,
Bates, Mary Ellen: “Emerging Trends in Information Brokering Competitive Intelligence Review, vol. 8(4), 1997,
Barghoorn, Frederick, “The security police”, interest Groups in soviet politics.

Brzezinknski, Bigniew, Ideology and Power in Soviet Politics, New York, Praeger, 1962.
Buzan, B (1992), Peoples, States and Fear: An Agenda for International Security in the Post Cold war Era, 2nd edn.

CIA, America Suports the Usurpers of Palestine

Crozier Brian “European security and the soviet problem, Institute for the study of conflict, 1971.
D. MacLellan, Karl Marx: His Life and Thought, NewYork: Harper & Row, 1973), uk 3
Dulles, Allen,“The craft of Intelligence”, New York, Hepr, 1963.

Derianbin, Peter,”Watchdogs of Terror” 1972
Ethics of Spying A Reader for the Intelligence Profession:

This book provides a central reference point for ethics in the intelligence profession, vital to personal and professional development. The systemic problem inherent in a profession where truth is the goal yet deception, secrecy, and morally troubling compromises are often necessary is addressed. It offers a body of literature for building an ethical code for the intelligence professional not dependent on any particular agency, department, or even country. Providing articles and case studies of moral dilemmas and ethical codes of conduct by the various intelligence agencies, anyone involved or interested in the fields of national security, intelligence, military science, public policy, law enforcement, political science, and philosophy will benefit from this publication.
Foote, Alexander, Hand book for Spies, 1969

Fuld, Leonard, M: The New Competitor Intelligence, John Wiley & Sons New York, 1995.
Franks, Lord, Report on Offical Secrets Act. 1972.

Gordon Winter, an Ex-spy’s Dramatic and shocking Expose Inside the Boss, South Africas’s Secret Police 1981.

“Hand book of intelligence and Guerrrilla Warfare 1965.

Harun Yahya, the Global Freemasonry.

Henry Ford, Jews and the World.

Holden-Rhodes. J.F: Sharing the secrets: Open Source Intelligence, University of New Mexico Press, 1994.
John Barron, KGB, The secret work of Soviet Secret Agents.
Mendel, Ronald, L: How to conduct Investigations and Competitive Intelligence gathering, Thomas Investigation Professionals, December 1996.
Morros, Boris, My Ten Years as a Counterspay. New York, Viking, 1966.
Peacetime Strategy of Soviet Union, London
Peter Wright, Spycatcher 1951.

Peter N. Stearn: Jews and the Revolutions of 1848, uk 176-177
Report of the Royal Commission on Espionage, Common wealth of Australia.

Ramesh Thakur and Edward Newman (Ed), New Millennium New Perspectives The United Nations: Security and Governance, United Nations University Press, Tokyo, NewYork and Paris

Sydney, Gvernment Printer for New South Wales 1955.

Sammon, William, Mark Kurland, and Robert Spitalnic: Competitor Intelligence: Methods for collecting, Organizing and using Information, John Wiley & Sons, New York, 1994.
Seth, Ronald, Unmasked; “The story of soviet Espionage 1965.

Shlomo Aviner, The making of Modern Zionism: The Intellectual Origins of the Jewish state(NewYork: Basic Books, uk 30-31.

Steven M. Shaker. Mark P. Gembick: The War Room Guide to Competitive Intelligence,
Soviet Spies in the Scientific and Technical Field 1968.

Strong, Sir Kenneth, Intelligence at the Top, New York, Doubleday, 1969.
Soviet Espionage, 1953.

The Soviet Police system, 1968.

Terence Ball, Richard Dager, Political Ideologies and the Democratic Ideal, Valentin Gorodnov: Life and Struggles of a South African Township, 1988

Willie Martin, Freemasonry Explained Based upon research.
Zafar Ahmad Ansar, Jewish Conspiracy

Ahmad Husayn
Huda Publishers
Box 90399
Dar es Salaam

MWISHO
 
Back
Top Bottom