We Know Next
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 815
- 382
wengine walimtukana Jk badala ya kujadili. kweli sio vizuri
Tutamjadili, tutamkosoa na tutasemakweli, kama hataki tumjadili aachie ofisi.Mbona watu hawanijadili mimi, yeye kautaka urais basi akubali kuwa yeye ni kioo cha jamii akicheka anajadilwa,akikohoa anajadilwa akiumwa anajadiliwa, hakuna jinsi lazima tumchane live lakini bila kumkashifu wala kumtukana. UKWELI LAZIMA USEMWE.
Rais anahusika vipi na matokeo ya mtoto wake? uzumbukuku huu.
wapendwa,
kusema ukweli, nilikuwa nataka kuanzisha thread kulaumu hili la kumhusisha binti mwanaasha na kazi ya baba yake. kwa kweli si haki na tuache tabia hii mara moja! jakaya ni jakaya na mwanaasha ni mwanaasha. mimi baba yangu aliishia darasa la pili na mimi sasa nasomea shahada ya uzamivu (PhD) ulaya, na tena sio kwa kubebwa na mtu, bali kwa kushindania na kupata moja ya scholarship adimu kabisa hapa duniani!
tujiulize, kama performance ya baba ingekuwa ina uhusiano na performance ya mtoto, kwangu ingekuwaje?
nimelazimika kulisema hili kwa sababu sioni mantiki ya kumlaumu baba mwanasha kwa matokeo yasiyo mazuri ya binti yake na ambayo naamini yamemsikitikisha pia baba yake (jakaya) tena sana. hebu tujiepushe na siasa kila wakati. tukiendelea na hii tabia, tutakuwa si tu hatumtedei haki baba yake (mzee jakaya kikwete), bali pia mwanaasha mwenyewe.
yeye si wa kwanza kupata matokeo yasiyoridhisha na wala sio wa mwisho. amepata matokeo kama mtoto mwingine yoyote na kama jamii ya wastaarabu, tulipaswa kumtia moyo mdogo wangu mwanaasha ili asikatishwe tamaa na matokeo yake na ikiwezekana tuwashauri wazazi wake kumtafutia fursa nyingine nzuri zaidi za kujiendeleza zaidi.
binafsi namjua kijana mmoja (sasa ni mwanamume wa makamo), alipata div IV form 4 na baada ya kuhangaika ku-reseat, alipata div III form 6 na sasa ninavyoandika hapa ni mmoja wa wahasibu bora kabisa duniani, akiwa amekwishafanya kazi barani ulaya, afrika na arabuni akishinda usaili shindanishi na anazo tuzo kadhaa za utendaji kazi uliotukuka.
hivyo basi wapendwa, bado mwanaasha anazo fursa za kujiendeleza na nawashauri wazazi wake wasikatishwe tamaa na matokeo hayo ya mwana wao ambayo hawakuyatarajia.
nimalizie klwa kumwambia mwanaasha (kama atanisoma hapa), asikatishwe tamaa na maneno ya watu, azungumze na wazazi wake kuona namna gani watamsaidia na asonge mbele.
pole sana baba na mama mwanaasha,
pole sana mwanaasha,
mbarikiwe sana wapendwa,
Glory to God!
Kama gadafe mwenyewe alikuwa akiwapa wananchi wake kila kitu ila bado tu walimkataa na kumtenda vibaya je huyu anaetoa majibu yanayochefua na ukimya kwa mambo nyeti ktk nchi huku utendaji wa timu yake ukiwa dhaifu na wezi wa mchana peupe pasipokuwajibishwa its so sad
Tutamjadili, tutamkosoa na tutasemakweli, kama hataki tumjadili aachie ofisi. Mbona watu hawanijadili mimi, yeye kautaka urais basi akubali kuwa yeye ni kioo cha jamii akicheka anajadiliwa, akikohoa anajadilwa akiumwa anajadiliwa, hakuna jinsi lazima tumchane live lakini bila kumkashifu wala kumtukana. UKWELI LAZIMA USEMWE.
Kwa muda mrefu mitandao ya kijamii imekuwa ikitumika kumchafua Rais JAKAYA KIKWETE kwa mambo ambayo hayahusiani kabisa na majukumu yake ya kuongoza serikali.
Yapo mambo mengi ambayo watu kupitia mitandao wamekuwa wakimchafua Rais na hapa nitatoa michango michache tu:-
1) Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ya mtoto wake aitwaye MWANAASHA KIKWETE yametumika sana kumchafua JK.
2) Thread iliyoletwa hapa JF na kichwa cha habari "Maswali mia moja kwa Rais KIKWETE" yakiwemo yaliyohoji ana wake wangapi na mengine mengi yalioonekana ni ya kumchafua Rais zaidi na hayakuwa ya kiutendaji.
Yapo mengine mengi ambayo kiukweli hata kurudia kuyaandika hapa hayafai.
Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 15/02/2012 katika ukurasa wake wa Tahariri (The Editorial page) mhariri ameandika kuhusu hili kwa kichwa cha habari "Mitandao isitumike kumchafua Rais". Amebainisha kwa uwazi na kuonya wanaomiliki mitandao hiyo wawe wanahariri na habari zinazotumwa kabla ya kuziandika katika mitandao yao.
Refference: Tanzania Daima la tarehe 15.02.2012
Kwa muda mrefu mitandao ya kijamii imekuwa ikitumika kumchafua Rais JAKAYA KIKWETE kwa mambo ambayo hayahusiani kabisa na majukumu yake ya kuongoza serikali.
Yapo mambo mengi ambayo watu kupitia mitandao wamekuwa wakimchafua Rais na hapa nitatoa michango michache tu:-
1) Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ya mtoto wake aitwaye MWANAASHA KIKWETE yametumika sana kumchafua JK.
2) Thread iliyoletwa hapa JF na kichwa cha habari "Maswali mia moja kwa Rais KIKWETE" yakiwemo yaliyohoji ana wake wangapi na mengine mengi yalioonekana ni ya kumchafua Rais zaidi na hayakuwa ya kiutendaji.
Yapo mengine mengi ambayo kiukweli hata kurudia kuyaandika hapa hayafai.
Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 15/02/2012 katika ukurasa wake wa Tahariri (The Editorial page) mhariri ameandika kuhusu hili kwa kichwa cha habari "Mitandao isitumike kumchafua Rais". Amebainisha kwa uwazi na kuonya wanaomiliki mitandao hiyo wawe wanahariri na habari zinazotumwa kabla ya kuziandika katika mitandao yao.
Refference: Tanzania Daima la tarehe 15.02.2012