Misungwi wampuuza Waziri Magufuli!

engmtolera

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
5,150
1,437
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa halmashauri ya Misungwi, Waziri Magufuli hana mamlaka yoyote ya kuzuia ukusanywaji wa ushuru katika kivuko hicho, na kwamba kamwe agizo hilo hawatalitekeleza, badala yake wataendelea kutoza ushuru huo kwa ajili ya mapato ya halmashauri.

"Waziri Magufuli hana mamlaka hayo ya kutuzuia sisi tusikusanye mapato hapo Kigongo Ferri. Tulimshangaa sana alipotoa agizo lake hilo kwetu.

"Yeye anasimamia sheria, halafu anakuwa wa kwanza kuvunja sheria. Sisi siyo mbumbumbu, ndiyo maana nasema Misungwi tutaendelea kukusanya ushuru Kigongo Ferri, bila kuogopa agizo la Magufuli", alisema mwenyekiti Porcarp kwa kujiamini mbele ya Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Xavier Tilweselekwa.

Sasa nani mwenye mamlaka hayo? ama kunafisadi akisema huyo ndio mtamwelewa? maana hii nchi bana kila mtu anamamlaka yake,akijisikia tu anaweza hata kumwambia Mh Raisi kuwa huna mamlaka ya kutawala ndiko tunako elekea sasa hivi

CHANZO: Misungwi ‘wampuuza' Waziri Magufuli! | Fikra Pevu | Kisima cha busara!
 
Sasa nani mwenye mamlaka hayo? ama kunafisadi akisema huyo ndio mtamwelewa? maana hii nchi bana kila mtu anamamlaka yake,akijisikia tu anaweza hata kumwambia Mh Raisi kuwa huna mamlaka ya kutawala ndiko tunako elekea sasa hivi

CHANZO: Misungwi ‘wampuuza' Waziri Magufuli! | Fikra Pevu | Kisima cha busara!

Mkuu hapa kuna shida. Najua Waziri Maghufuli ndiye waziri mwenye dhamana ya vivuko vyote nchini. Lakini pia najua Halmashauri huwa zina by-laws kwa ajili ya kujikusanyia mapato na huenda inakusanya hayo mapato kwa mujibu wa sheria ndogondogo za halmashauri. Kama mwenye dhamana anasema kivuko ni moving bridge hivyo hakuna haja ya kutoza wananchi lakini inakuja Halmashauri inasema tunatoza kwa mujibu wa sheria zetu ndogondogo: Nani ni nani sasa?
 
Hao misungwi wahuni,last week nilipita pale kigongo feri akaja mtoza ushuru nikamwambia sitoi nikamuuliza yeye hajackia amri ya magufuli?ckumuona tena ila kwa kutumia side mirror nilimwona akiendelea kuwatoza wengine....WAJINGA NDIO WALIWAO!!!
 
hiyo halmashauri si itafute chanzo kingine cha mapato. Hiko kivuko sio chao wala hawachangii gharama yeyote ya kukiendesha sasa huo ushuru wanaoukusanya ni wa nini? kama sio w@z mtp
 
hiyo halmashauri si itafute chanzo kingine cha mapato. Hiko kivuko sio chao wala hawachangii gharama yeyote ya kukiendesha sasa huo ushuru wanaoukusanya ni wa nini? kama sio w@z mtp

Mkuu kivuko kina helaaaaaa! Lakini mbona Kigamboni tunatozwa au hapo Kigamboni kivuko chake siyo moving bridge?
 
Back
Top Bottom