Miss Tanzania yatia aibu Serikali na Taifa kwa ujumla

jerryempire

JF-Expert Member
Jan 4, 2017
5,128
8,648
Habari,

Katika pita pita zangu za kuanza kujichanganya na kufahamiana na watu kuna member mwenzangu humu,alinipa mwaliko pamoja na ticket ya vip kabisa kwenda kutazama shindano la miss Tanzania.

Naweza kusema hili ndio shindano langu la kwanza kwenda kuona live kutokana na mengi yaliyopitaga kuanzia 2009 kurudi nyuma kuyaona tu kupitia TV.

Hakika nilichokishuhudia kiliweza kuniumiza moyo na hata kuona aibu mbele ya mwenyeji wangu maana kwa jinsi alivyokuwa anasifia na tulichoenda kukiona humo ndani ni aibu kwa wizara ya michezo na burudani na hata kuharibu kabisa taswira ya mashindano haya kitaifa
Kwani tangu tuingie ukumbini kuanzia mishale ya saa 12 jioni mpka tunaondoka ukumbi ulikuwa na watu nusu yani viti vingi mno vilikuwa wazi kiasi cha kufanya baadhi ya watazamaji kuangalia huku wakiwa wamenyoosha miguu kwenye viti vilivyo wazi

Wito wangu kwa Serikali ni kwamba kuna baadhi ya mashindano inabidi yawe yanasimamiwa na serikali sababu impact ambayo itapatkana kupitia mashindano hayo huweza keta faida kubwa kwa serikali hasa kwenye upande wa mapato na kujitangaza hasa vivutio vyetu kupitia mamis walioshinda hasa kwenye kipengele cha kuvutia watalii na wahisani mbali mbali.

Mwisho wa siku Waziri anahojiwa badala ya kujibu wamesapoti vipi kuhusu suala hili anaanza kuongelea masuala ya ndege?
Nitoe kwa pongezi kwa mis Tanzania
Sylivia sebastian,ambae alitwaa taji hilo kwa kujinyakulia kitita cha 10m pia nitoe pongezi na pole kwa kampuni ya The look iliyoandaa shindano hilo,kwa kupata hasara kubwa ya kuwekeza kwenye shindano hilo mwisho wa siku watu hakuna,na pia pongezi za dhati kwa kuonyesha uzalendo na moyo wa dhati wa kudhamini mashindano hayo.

Wito kwa serikali yangu,hasa wizara ya utamaduni na michezo ni kuwaomba wasapoti mashindano mengine mbali ya mpira wa miguu kwani wizara hii ya michezo na utalii wakiwa wabunifu wanaweza kuwekeza kwenye michezo na kuleta impact kubwa sana katika uchumi hasa kwenye kutangaza nchi na vivutio vyake kama zifanyavyo nchi za wenzetu.
 
Hao ma miss wamejiaribia wenyewe wakishinda tunacho sikia kwao ni scandle za ngono tu siku hizi sio kama kipindi cha nyuma
 
Umenikumbusha enzi za ASPEN Miss Tanzania. Udahamini maridhawa wa sigara ya Aspen.

1566912539648.png
 
Wito wangu kwa Serikali ni kwamba kuna baadhi ya mashindano inabidi yawe yanasimamiwa na serikali sababu impact ambayo itapatkana kupitia mashindano hayo huweza keta faida kubwa kwa serikali hasa kwenye upande wa mapato na kujitangaza hasa vivutio vyetu kupitia mamis walioshinda hasa kwenye kipengele cha kuvutia watalii na wahisani mbali mbali.
Mashindano ya Miss Tanzania yana manufaa gani kwa taifa mpaka serikali igharamie mashindano hayo?\

Any way waandaji wajilaumu wenyewe kwa kushindwa kushawishi wadhamini kwa kuonyesha makampuni yatakayo dhamini shindano hili watanufaikaje nalo.
 
WAZURI WAPO MITAANI TUNAWAONA KILA SIKU KWA NINI TUHANGAIKIE WENYE WEUPE WA KICHINA
 
Watazamaji wa shindano la u-miss wakiwa wachache ukumbini nchi inapataje aibu?. Labda ungesema shindano limepungua mvuto, sio nchi kupata aibu. Utakuja kushangaa huyu miss wetu Sylvia atakuja kututoa kimasomaso watanzani na Africa. Inshu ya msingi ni miss wetu kujiandaa vizuri tu na sisi tumpigie kura za kutosha.
 
Hiyo kampuni hawajui ujanja wa wanachofanya. Basilla alipoona Zari anavutia wengi EA kuangalia ya Uganda bafala ya kujifunza akatafuta kiki kwa jambo lisilomuhusu na kuishi kushushuliwa na wengi hata kufukuza mashabiki.

Humu JF miaka yote lazima tulidhadadie.. mwaka huu nchi nzima wengi hatukujua shindano lilikuwepo hadi baada.

Wajifunze
 
Miss Tz kipindi cha kina Lundenga ilikua inafikia hatua inapata udhamini mpk wa Tsh. 1bil kutoka ma Co. Mbalimbali yaani ulifikia hatua mpk ukazidi udhamini wa ligi kuu Tanzania bara.
😂😂😂 hizo zama zitarudi tu mkuu muhimu uvumilivu.
 
Hiyo kampuni hawajui ujanja wa wanachofanya. Basilla alipoona Zari anavutia wengi EA kuangalia ya Uganda bafala ya kujifunza akatafuta kiki kwa jambo lisilomuhusu na kuishi kushushuliwa na wengi hata kufukuza mashabiki.

Humu JF miaka yote lazima tulidhadadie.. mwaka huu nchi nzima wengi hatukujua shindano lilikuwepo hadi baada.

Wajifunze

alitafutia kiki jambo gani
 
Udhamini utoke wapi? Ilihali uchumi unayumba. Hata katika soka (mchezo unaopendwa zaidi) hali ni tete. Vilabu vingi havina wadhamini.
Watu wakilalamika kuhusu uchumi wengine wanaona kama sisi tulizaliwa Kosovo sijui hatuna mapenzi na nchi yetu. Lakini ukweli ni kwanza sekta nyingi zinayumba achia mbali hali mifukoni mwa watu mitaani.
Mimi kama mdau wa soka huwa napata shida Sana kuhusu soka letu hasa wadhamini. Kwetu TZ soka linapendwa sana hiyo iko wazi naamini ni sehemu sana kwa wadhamini kuweka hela na kupata mileage kubwa. Lakini cha kushangaza hata yale makampuni makubwa nchini hayaweki pesa viwanjani. Mfano TIGO TRA (Kenya KRA wana timu kabisa premier league same as Uganda wana URA) CoCacola Pepsi TBL Twiga cement Mabenki kama NBC CRDB nk inasikitisha sana.
Ligi kuu inachezwa bila mdhamini mwaka mzima unategemea nn?
 
Back
Top Bottom