Misaada ya corona yafikia bil. 6.726/-

Misaada ya corona yafikia bil. 6.726/-

Joined
Apr 4, 2020
Posts
16
Reaction score
7
1586932140998.png

MISAADA ya kusaidia Serikali kukabiliana na janga la corona imeendelea kumiminika na kufikia zaidi ya Sh. bilioni 6.726, ikiwa ni fedha taslimu na vifaa. Jana Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokea hundi ya mfano ya Sh. milioni 500 kutoka kampuni ya Export Trading Group (ETG) kwa ajili ya kukabiliana na janga hilo linaloitafuna dunia.

Waziri Mkuu alipokea msaada huo jana ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma, kutoka kwa Mkurugenzi mkazi wa ETG, Nilladri Chowdhury. Wiki iliyopita Waziri Mkuu, pia alipokea zaidi ya Sh. milioni 6.226 kutoka kwa wadau mbalimbali nchini, kwa ajili ya maji tiba na barakoa za kuwasaidia wananchi na watumishi wa afya katika kukabiliana na janga hilo.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Waziri Mkuu aliwashukuru watendaji wa kampuni ya ETG kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika mapambano dhidi ya virusi vya corona, ambapo hadi sasa kesi 49 zimeripotiwa tangu kuanza kwa ugonjwa huo nchini na wagonjwa saba wameshapona. Aliwataka wananchi wote wazidishe kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo hasa katika kipindi hiki.

“Hatua tuliyofikia hivi sasa, maambukizi yameanza kuongezeka hasa kwa Dar es Salaam na Zanzibar. Tunajua kule kuna watu wengi na shughuli zote za kiuchumi zinaanzia pale, lakini hatunabudi kufuata masharti tuliyopewa ili kuzuia ugonjwa huu usisambae,” alisema. “Serikali inatoa msisitizo kwa wananchi wazingatie maelekezo yanayotolewa kuhusu kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona ikiwamo kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka pamoja na kujiepusha na mikusanyiko isiyokuwa ya lazima.” “Muhimu zaidi sote tuendelee kumuomba Mwenyezi Mkungu ili atupunguzie makali ya ugonjwa huu,” alisisitiza.

Awali, Mwenyekiti wa Kampuni ya ETG, Mahesh Patel, Mkurugenzi Mkazi wa ETG, Nilladri Chowdhury, alisema wameamua kuchangia ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika vita ya kupambana na ugonjwa huo.

Alisema kampuni yao inashughulika na masuala ya kilimo ikiwamo kusambaza pembejeo na kuongeza thamani mazao kupitia kampuni yao ya Kapunga iliyoko Mbeya, viwanda vitatu vya kubangua korosho vilivyoko Mtwara, Newala na Tunduru na viwanda vya kusindika mbegu za mafuta.

Pia, wanatoa soko kwa wakulima kwa kununua mazao kama korosho, mbaazi, kokoa, mahindi, choroko na ufuta. Corona ilianzia kwenye mji wa Wuhan China, mwishoni mwa Disemba mwaka jana, na kwa mujibu wa kituo cha utafiti cha Chuo Kikuu cha Johns Hopkins nchini Marekani, hadi jana jumla ya watu 1,934,583 wanaugua ugonjwa huo.

Aidha, watu 120,863 wameshafariki na nchi au maeneo ya utawala yenye maambukizi ni 185, huku nchi iliyoathirika zaidi ni Marekani yenye watu 582,634 wanaougua na kati yake 23,649 wamefariki.

CHANZO: Nipashe
 
Wewe kweli bado mgeni wa jukwaa,ulikuwa na haraka gani ya kupost,waambie miss,warekebishe kichwa cha Habari kisomeke,YAFIKIA badala YAKIA.
 
Nashauri fedha zilizopatikana Sasa ziondolewe bank zipelekwe dar na Zanzibar kuanza kusaidia kuzuia maambukizi ya kadi na walio wagonjwa.pia kusaidia wananchi kupata missada ya kiuchumia ili kupunguza misongamano.

mfano kwa Sasa sukari imefikia TSH 3200 kwa kilo moja, ambapo wananchi wengi hawateweza kumudu gharama hizo.pia kusambaza barakoa kwa wananchi .
 
Hiyo Ni michango ambayo pesa inawekwa ktk mfuko wa maafa alafu inahamishiwa hazina kwa matumizi mengine...
Vice versa is true wanaotoa unawajua?? Kwa awamu hii kupenda sifa haiachi kumpa mtu pesa akaenda kuweka japo tu ionekane inaungwa mkono.
 
Huko marekani watu wanamwaga vyakula na maziwa kwa kuwa supply ni kubwa kuliko demand. Shule zimefungwa na events hakuna.
 

MISAADA ya kusaidia Serikali kukabiliana na janga la corona imeendelea kumiminika na kufikia zaidi ya Sh. bilioni 6.726, ikiwa ni fedha taslimu na vifaa. Jana Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokea hundi ya mfano ya Sh. milioni 500 kutoka kampuni ya Export Trading Group (ETG) kwa ajili ya kukabiliana na janga hilo linaloitafuna dunia.

Waziri Mkuu alipokea msaada huo jana ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma, kutoka kwa Mkurugenzi mkazi wa ETG, Nilladri Chowdhury. Wiki iliyopita Waziri Mkuu, pia alipokea zaidi ya Sh. milioni 6.226 kutoka kwa wadau mbalimbali nchini, kwa ajili ya maji tiba na barakoa za kuwasaidia wananchi na watumishi wa afya katika kukabiliana na janga hilo.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Waziri Mkuu aliwashukuru watendaji wa kampuni ya ETG kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika mapambano dhidi ya virusi vya corona, ambapo hadi sasa kesi 49 zimeripotiwa tangu kuanza kwa ugonjwa huo nchini na wagonjwa saba wameshapona. Aliwataka wananchi wote wazidishe kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo hasa katika kipindi hiki.

“Hatua tuliyofikia hivi sasa, maambukizi yameanza kuongezeka hasa kwa Dar es Salaam na Zanzibar. Tunajua kule kuna watu wengi na shughuli zote za kiuchumi zinaanzia pale, lakini hatunabudi kufuata masharti tuliyopewa ili kuzuia ugonjwa huu usisambae,” alisema. “Serikali inatoa msisitizo kwa wananchi wazingatie maelekezo yanayotolewa kuhusu kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona ikiwamo kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka pamoja na kujiepusha na mikusanyiko isiyokuwa ya lazima.” “Muhimu zaidi sote tuendelee kumuomba Mwenyezi Mkungu ili atupunguzie makali ya ugonjwa huu,” alisisitiza.

Awali, Mwenyekiti wa Kampuni ya ETG, Mahesh Patel, Mkurugenzi Mkazi wa ETG, Nilladri Chowdhury, alisema wameamua kuchangia ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika vita ya kupambana na ugonjwa huo.

Alisema kampuni yao inashughulika na masuala ya kilimo ikiwamo kusambaza pembejeo na kuongeza thamani mazao kupitia kampuni yao ya Kapunga iliyoko Mbeya, viwanda vitatu vya kubangua korosho vilivyoko Mtwara, Newala na Tunduru na viwanda vya kusindika mbegu za mafuta.

Pia, wanatoa soko kwa wakulima kwa kununua mazao kama korosho, mbaazi, kokoa, mahindi, choroko na ufuta. Corona ilianzia kwenye mji wa Wuhan China, mwishoni mwa Disemba mwaka jana, na kwa mujibu wa kituo cha utafiti cha Chuo Kikuu cha Johns Hopkins nchini Marekani, hadi jana jumla ya watu 1,934,583 wanaugua ugonjwa huo.

Aidha, watu 120,863 wameshafariki na nchi au maeneo ya utawala yenye maambukizi ni 185, huku nchi iliyoathirika zaidi ni Marekani yenye watu 582,634 wanaougua na kati yake 23,649 wamefariki.

CHANZO: Nipashe
Zitaanza kutumika lini????
 

MISAADA ya kusaidia Serikali kukabiliana na janga la corona imeendelea kumiminika na kufikia zaidi ya Sh. bilioni 6.726, ikiwa ni fedha taslimu na vifaa. Jana Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokea hundi ya mfano ya Sh. milioni 500 kutoka kampuni ya Export Trading Group (ETG) kwa ajili ya kukabiliana na janga hilo linaloitafuna dunia.

Waziri Mkuu alipokea msaada huo jana ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma, kutoka kwa Mkurugenzi mkazi wa ETG, Nilladri Chowdhury. Wiki iliyopita Waziri Mkuu, pia alipokea zaidi ya Sh. milioni 6.226 kutoka kwa wadau mbalimbali nchini, kwa ajili ya maji tiba na barakoa za kuwasaidia wananchi na watumishi wa afya katika kukabiliana na janga hilo.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Waziri Mkuu aliwashukuru watendaji wa kampuni ya ETG kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika mapambano dhidi ya virusi vya corona, ambapo hadi sasa kesi 49 zimeripotiwa tangu kuanza kwa ugonjwa huo nchini na wagonjwa saba wameshapona. Aliwataka wananchi wote wazidishe kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo hasa katika kipindi hiki.

“Hatua tuliyofikia hivi sasa, maambukizi yameanza kuongezeka hasa kwa Dar es Salaam na Zanzibar. Tunajua kule kuna watu wengi na shughuli zote za kiuchumi zinaanzia pale, lakini hatunabudi kufuata masharti tuliyopewa ili kuzuia ugonjwa huu usisambae,” alisema. “Serikali inatoa msisitizo kwa wananchi wazingatie maelekezo yanayotolewa kuhusu kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona ikiwamo kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka pamoja na kujiepusha na mikusanyiko isiyokuwa ya lazima.” “Muhimu zaidi sote tuendelee kumuomba Mwenyezi Mkungu ili atupunguzie makali ya ugonjwa huu,” alisisitiza.

Awali, Mwenyekiti wa Kampuni ya ETG, Mahesh Patel, Mkurugenzi Mkazi wa ETG, Nilladri Chowdhury, alisema wameamua kuchangia ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika vita ya kupambana na ugonjwa huo.

Alisema kampuni yao inashughulika na masuala ya kilimo ikiwamo kusambaza pembejeo na kuongeza thamani mazao kupitia kampuni yao ya Kapunga iliyoko Mbeya, viwanda vitatu vya kubangua korosho vilivyoko Mtwara, Newala na Tunduru na viwanda vya kusindika mbegu za mafuta.

Pia, wanatoa soko kwa wakulima kwa kununua mazao kama korosho, mbaazi, kokoa, mahindi, choroko na ufuta. Corona ilianzia kwenye mji wa Wuhan China, mwishoni mwa Disemba mwaka jana, na kwa mujibu wa kituo cha utafiti cha Chuo Kikuu cha Johns Hopkins nchini Marekani, hadi jana jumla ya watu 1,934,583 wanaugua ugonjwa huo.

Aidha, watu 120,863 wameshafariki na nchi au maeneo ya utawala yenye maambukizi ni 185, huku nchi iliyoathirika zaidi ni Marekani yenye watu 582,634 wanaougua na kati yake 23,649 wamefariki.

CHANZO: Nipashe
Mnatangaza fedha halafu Tanzania yote yenye watu milioni 59 kuna kakifaa kimoja tu cha kupima kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom