Misaada ya corona yafikia bil. 6.726/-

Misaada ya corona yafikia bil. 6.726/-


MISAADA ya kusaidia Serikali kukabiliana na janga la corona imeendelea kumiminika na kufikia zaidi ya Sh. bilioni 6.726, ikiwa ni fedha taslimu na vifaa. Jana Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokea hundi ya mfano ya Sh. milioni 500 kutoka kampuni ya Export Trading Group (ETG) kwa ajili ya kukabiliana na janga hilo linaloitafuna dunia.

Waziri Mkuu alipokea msaada huo jana ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma, kutoka kwa Mkurugenzi mkazi wa ETG, Nilladri Chowdhury. Wiki iliyopita Waziri Mkuu, pia alipokea zaidi ya Sh. milioni 6.226 kutoka kwa wadau mbalimbali nchini, kwa ajili ya maji tiba na barakoa za kuwasaidia wananchi na watumishi wa afya katika kukabiliana na janga hilo.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Waziri Mkuu aliwashukuru watendaji wa kampuni ya ETG kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika mapambano dhidi ya virusi vya corona, ambapo hadi sasa kesi 49 zimeripotiwa tangu kuanza kwa ugonjwa huo nchini na wagonjwa saba wameshapona. Aliwataka wananchi wote wazidishe kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo hasa katika kipindi hiki.

“Hatua tuliyofikia hivi sasa, maambukizi yameanza kuongezeka hasa kwa Dar es Salaam na Zanzibar. Tunajua kule kuna watu wengi na shughuli zote za kiuchumi zinaanzia pale, lakini hatunabudi kufuata masharti tuliyopewa ili kuzuia ugonjwa huu usisambae,” alisema. “Serikali inatoa msisitizo kwa wananchi wazingatie maelekezo yanayotolewa kuhusu kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona ikiwamo kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka pamoja na kujiepusha na mikusanyiko isiyokuwa ya lazima.” “Muhimu zaidi sote tuendelee kumuomba Mwenyezi Mkungu ili atupunguzie makali ya ugonjwa huu,” alisisitiza.

Awali, Mwenyekiti wa Kampuni ya ETG, Mahesh Patel, Mkurugenzi Mkazi wa ETG, Nilladri Chowdhury, alisema wameamua kuchangia ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika vita ya kupambana na ugonjwa huo.

Alisema kampuni yao inashughulika na masuala ya kilimo ikiwamo kusambaza pembejeo na kuongeza thamani mazao kupitia kampuni yao ya Kapunga iliyoko Mbeya, viwanda vitatu vya kubangua korosho vilivyoko Mtwara, Newala na Tunduru na viwanda vya kusindika mbegu za mafuta.

Pia, wanatoa soko kwa wakulima kwa kununua mazao kama korosho, mbaazi, kokoa, mahindi, choroko na ufuta. Corona ilianzia kwenye mji wa Wuhan China, mwishoni mwa Disemba mwaka jana, na kwa mujibu wa kituo cha utafiti cha Chuo Kikuu cha Johns Hopkins nchini Marekani, hadi jana jumla ya watu 1,934,583 wanaugua ugonjwa huo.

Aidha, watu 120,863 wameshafariki na nchi au maeneo ya utawala yenye maambukizi ni 185, huku nchi iliyoathirika zaidi ni Marekani yenye watu 582,634 wanaougua na kati yake 23,649 wamefariki.

CHANZO: Nipashe
Wamlipe mkandarasi wa flyover ya ubungo amalize kazi haraka,tunataka kuwahi kuchapa kazi,foleni zinazingua
 

MISAADA ya kusaidia Serikali kukabiliana na janga la corona imeendelea kumiminika na kufikia zaidi ya Sh. bilioni 6.726, ikiwa ni fedha taslimu na vifaa. Jana Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokea hundi ya mfano ya Sh. milioni 500 kutoka kampuni ya Export Trading Group (ETG) kwa ajili ya kukabiliana na janga hilo linaloitafuna dunia.

Waziri Mkuu alipokea msaada huo jana ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma, kutoka kwa Mkurugenzi mkazi wa ETG, Nilladri Chowdhury. Wiki iliyopita Waziri Mkuu, pia alipokea zaidi ya Sh. milioni 6.226 kutoka kwa wadau mbalimbali nchini, kwa ajili ya maji tiba na barakoa za kuwasaidia wananchi na watumishi wa afya katika kukabiliana na janga hilo.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Waziri Mkuu aliwashukuru watendaji wa kampuni ya ETG kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika mapambano dhidi ya virusi vya corona, ambapo hadi sasa kesi 49 zimeripotiwa tangu kuanza kwa ugonjwa huo nchini na wagonjwa saba wameshapona. Aliwataka wananchi wote wazidishe kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo hasa katika kipindi hiki.

“Hatua tuliyofikia hivi sasa, maambukizi yameanza kuongezeka hasa kwa Dar es Salaam na Zanzibar. Tunajua kule kuna watu wengi na shughuli zote za kiuchumi zinaanzia pale, lakini hatunabudi kufuata masharti tuliyopewa ili kuzuia ugonjwa huu usisambae,” alisema. “Serikali inatoa msisitizo kwa wananchi wazingatie maelekezo yanayotolewa kuhusu kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona ikiwamo kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka pamoja na kujiepusha na mikusanyiko isiyokuwa ya lazima.” “Muhimu zaidi sote tuendelee kumuomba Mwenyezi Mkungu ili atupunguzie makali ya ugonjwa huu,” alisisitiza.

Awali, Mwenyekiti wa Kampuni ya ETG, Mahesh Patel, Mkurugenzi Mkazi wa ETG, Nilladri Chowdhury, alisema wameamua kuchangia ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika vita ya kupambana na ugonjwa huo.

Alisema kampuni yao inashughulika na masuala ya kilimo ikiwamo kusambaza pembejeo na kuongeza thamani mazao kupitia kampuni yao ya Kapunga iliyoko Mbeya, viwanda vitatu vya kubangua korosho vilivyoko Mtwara, Newala na Tunduru na viwanda vya kusindika mbegu za mafuta.

Pia, wanatoa soko kwa wakulima kwa kununua mazao kama korosho, mbaazi, kokoa, mahindi, choroko na ufuta. Corona ilianzia kwenye mji wa Wuhan China, mwishoni mwa Disemba mwaka jana, na kwa mujibu wa kituo cha utafiti cha Chuo Kikuu cha Johns Hopkins nchini Marekani, hadi jana jumla ya watu 1,934,583 wanaugua ugonjwa huo.

Aidha, watu 120,863 wameshafariki na nchi au maeneo ya utawala yenye maambukizi ni 185, huku nchi iliyoathirika zaidi ni Marekani yenye watu 582,634 wanaougua na kati yake 23,649 wamefariki.

CHANZO: Nipashe
Misaada ya shs.6.2 nakumbuka ilikuwa tarehe 8 April, kulikoni tena!
 
Utashangaaa fedha hizi zinakwenda kujenga reli

Hizi ziunganishwe na zile gratuity wanazozisubiri wabunge Dodoma zingetusukuma sana kwenye kuwasaidia wahitaji kwenye lockdown.

Bunge sitisheni vikao vyenu. Posho nazo zije huku kwenye lockdown kwa sasa.

Wabunge bila kujali vyama vyenu tutendeeni haki sisi wananchi wenu!

Kuweni na mioyo ya huruma muda unazidi kuyoyoma Corona itatumaliza.
 
Utashangaaa fedha hizi zinakwenda kujenga reli
Tutamalizia kuleta zile ndege! Na hizi fedha za emergency sidhani kama zinakuaga audited. CCM wamepatia za Uchaguzi humo humo ndio maana hawakua serious kukemea hilo Gonjwa kumbe wametega
 
Mtaani Barakoa Tsh 2000/= mihela yote hiyo yanini sasa?
 
Screenshot_20200416-172302~2.png

Kila nikiangalia hii picha naishia kuwaza kama kutakuwa na mabadiliko this time au tutaambiwa serikali haijaleta korona
 
Naona hili ni jukum la Kila mtanzania,ingependeza Kama serikali ingeweka account Kila mtanzania anaye jisikia hata akiwa 100 akachengia,kuliko sasa hivi watachangia matajiri tuu,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ni sawa na $3M ambayo inanunulia masks za mkoa wa Dar za silu moja tu!
 
Vice versa is true wanaotoa unawajua?? Kwa awamu hii kupenda sifa haiachi kumpa mtu pesa akaenda kuweka japo tu ionekane inaungwa mkono.
Ina maana hakuna watu wanaojitolea kwa ajili ya taifa lao ndo kutukuamini tu kwamba inwezekana.
 
Nashauri fedha zitumike kwa matumizi mengine, kwa mfano, miradi ya kimkakati kama SGR na Stigler gorge.
Wanaosema hizo fedha zitumike kwenye kupambana na Corona, nawashangaa kwa kweli.
Serikali ilileta Corona? Serikali ilihaidi kuleta Corona wakati wa kampeni?
Watanzania tubadilike, serikali haileti majanga. Corona ni natural disaster kama ilivyokuwa tetemeko kule Kagera.
 
Kuna mtu kashauri hizo hela za michango ya corona wapewe waathirika wenyewe wa corona.


"baba unahonga hawara elfu kumi,
watoto wanakufa na njaa nyumbani"
 
Back
Top Bottom