Kuna mawasiliano haya yaliyoletwa humu sasa hadi muda huu hakuna aliyetoa ufafanuzi kuhusu mipango hii hatari.Imeendelea kusambaa Facebook,Twitter na huku Jamii Forums kwa muda mrefu huku wahusika wakiwa kimya na badala yake Mwigulu Nchemba mwenye jina lilalofanana na jina la Naibu Katibu Mkuu wa CCM ambaye ni member huku amezingatia zaidi kulialia na maamuzi yaliyofanywa na kamati kuu CHADEMA dhidi ya Mhusika ambaye kwenye mawasiliano yanayoonekana hapa walipanga kumsaidia.
Pia mtu aliyetajwa kama Emmanuel Nchimbi (Jina linalofanana na Waziri wa Mambo ya Ndani) aliyeonekana akiwasiliana na huyo niliyemtaja hapo juu ameonekana akipanga kutumia vyombo vya dola kuhakikisha kumsaidia huyo aliyeadhibiwa na kamati kuu CHADEMA kwa tuhuma za uhaini .
Mara kadhaa vyombo vya dola vimetuhumiwa kutumika kisiasa na pia Mwigulu(Naibu Katibu Mkuu-CCM) amehusishwa kushirikiana na vyombo vya dola kuhujumu CHADEMA.Sasa inapotokea jina la mtu kama Waziri mwenye dhamana ya vyombo vya dola kutamba kutumia dola kisiasa kuhujumu chama cha upinzani kama inavyoonekana kwenye mawasiliano haya ni jambo la hatari linalohitaji ufafanuzi na lisilokubalika hata kidogo
Pia jina la mhusika anayetajwa kutoka CHADEMA alionyesha tabia zilizotia shaka katika sakata la kesi feki za ugaidi dhidi ya chama chake cha CHADEMA ikiwemo kuvujishwa barua za siri humu zilizokitaka chama kimtose mkurugenzi wake wa ulinzi na usalama huku akijua kuwa kama Mkurugenzi huyo angeshindwa kwenye kesi hiyo feki Chama kingehusishwa na hivyo mpango uliotangazwa na waziri mwandamizi kuwa CHADEMA kitakufa kabla ya 2015 ungetimia maana wangetaka kifutwe.Mawasiliano haya yanayoonekana hapa yanahitaji ufafanuzi maana kwa jinsi tume ya katiba ilivyohusishwa hapa ni hatari zaidi ikizingatiwa ni siku chache zilizopita tu Taifa limekumbwa na msiba katika mazingira ya kutatanisha ya kifo cha mjumbe wa tume hiyo Dr.Mvungi
Hivyo basi wahusika ni vyema wakajitokeza hadharani kuhusu hili kama nitakavyonukuu mawasiliano hayo jinsi yanavyosambaa kwenye media
Wahusika ni vyema wakatoa majibu ya hicho kilichoandikwa