Mimi nimemuonea huruma huyu mama

Mimi nimemuonea huruma huyu mama

i411

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2011
Posts
906
Reaction score
297
3.JPG

Daa huyu mama na watoto wake mpaka nimeshindwa kulala lakini hii ni hali halisi katika vijiji vingi. Nguo nimpaka ccm waje kutoa za kampeni ndo watu wanapata kanga mpya na tishati na kofia. Kwaza huyo mama anaonekana bado msichana mdogo sasa anawatoto watatu. Mungu mkubwa jamani bado yupo gado na labda mwingine mwingine anakuja. Huu ni ukatili aina fulani jamani tufanyeni tuu bidii kila tuwezavyo miaka ijayo matatizo kama haya yapungue hili sio tatizo la ccm tuu jamani hawa ni wenzetu. Kwawale wanojiweza vizuri mwaweza angalau kuchimba visima kule vijijini mlipotoka kidogokidogo tukiwa na moyo wa kujitolea tutafika tuu. Mkienda kwenye kikao cha kuchangia harusi huko huko mnaweka na kamchango cha kusaidia kakijiji fulani twaweza kujikomboa.
 
kwani huyo **** anayempiga mimba hawezi kufikiria?
 
Mbona ana afadhali kidogo,wengine hata nguo tu shida.
 
Hii picha ni taswira ya kijijini kwetu kabisa. Lakini na mimi nilikulia katika mazingira kama haya! Ila mpaka leo hapajabadilika. Nitajenga kisima mwaka huu karibia na kwa bibi yangu!
 
Sera za maendeleo lazima ziwe za serikali,mwananchi,chama,mtu binafsi.huwezi kuamua kuwa na familia kubwa uwezo huna na hupangi uzazi.serikali nayo inatakiwa kuwa uwezo kuwapa wananchiwake elimu ya kutosha kupitia kodi zao.
 
Sera za maendeleo lazima ziwe za serikali,mwananchi,chama,mtu binafsi.huwezi kuamua kuwa na familia kubwa uwezo huna na hupangi uzazi.serikali nayo inatakiwa kuwa uwezo kuwapa wananchiwake elimu ya kutosha kupitia kodi zao.
hii kweli
 
Hizo hali hua zinasikitisha saaana.... But kweli Mungu ni wa ajabu...
waweza kuta yeye kazoea na anaona ni kawaida kabisa thou katika
macho yetu hali ni mbaya saana... God help us Women!!!
 
Hii picha ni taswira ya kijijini kwetu kabisa. Lakini na mimi nilikulia katika mazingira kama haya! Ila mpaka leo hapajabadilika. Nitajenga kisima mwaka huu karibia na kwa bibi yangu!
kampeni au usamaria wema?
 
<img src="http://4.bp.blogspot.com/-bqRmbZ7xO-o/Ti_nRZa8AuI/AAAAAAABq4E/uRfhPU31XDo/s1600/3.JPG" border="0" alt="" /><br />
<br />
<br />
CCM Oyeeeeeeeeeeeeeee.
Tumeahidi tumetekeleza.
Haya ndio MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA
 
kampeni au usamaria wema?
Ni usamaria kaka, Ila niliwahi kuwa na hamu ya kugombea ubunge lakni kwasasa sitaki tena labda mpaka magamba wafutike kwenye ramani ya tanzania
 
Mi hata sijamwonea huruma, mimba kazibeba mwenyewe hakubakwa,
Huenda na shule aliikimbia, hayo ndo majuto yake.
 
.......dahhh!! Ndoo kichwani, mtoto mikononi. Uchovu wake hapo siupatii picha.
 
Back
Top Bottom