Mimi niliachwa hivi wewe uliachwa vipi?

Mimi niliachwa hivi wewe uliachwa vipi?

Ulimuacha bila kosa nini............................,
makosa alikuwa nayo, tena sio moja, nafikiri he took me for granted.
nimekaa sehemu napiga story, ktk watu wanne namjua moja tu. then wale wengine watatu ghafla wanamuongelea BF wangu kwa kumtaja jina kwamba kapata mtt na msichana mwingine, na wanatoa details zote
nilijikaza pale, baada ya hapo nikamfata, baada ya kumbana akadai ni ukweli.. so alikuwa na gals wawili at the same time. akanidanganya danganya, tukaendelea na urafiki, sikuweza kumuacha mapema (japo nia ilikuwepo) maana alining'ang'ania kila kona. Siku niliyoamua kumuacha, nilimtambulisha na mrithi wake kabisa.. hakuamini na laana nikapewa
 
mimi niko kwenye dormant relationship.. so sidhani kama huko ni kuacha ama kuachwa!
 
Kuachwa ni balaa linguine katika maisha ya mwanadamu hasa kwa wale ambao mnapendana sana. Sitapende kutoa experience yangu hapa maama mhusika ninajua ni member huku tena wa muda mrefu. Nikiandika tu hata mumewe mi member hapa atajua ninawazungumzia wao kwa kuwa walipokuwa wanaoana waliweka kila kitu wazi kwa hiyo mumewe anafahamu historia yetu. Tuliachana kwa machungu sana!!! Tulipendana sana!!! Ila hatuko maadui, tunawasiliana baada ya muda mrefu sana wa kutowasiliana. Wote tuko committed na family zetu na mke wangu anafahamu kabisa Fulani was my girlfriend. I can say we are friends na huwa kwa wakati tunawasiliana kwa simu kwa mema tu na ninashukuru kuwa sote tulikubali yaishe japo nina hakika tuliumia wote sana. Ndoa hupangwa na Mungu kama kweli unaamini na kumwomba Mungu.
 
Mara ya kwanza niliambiwa nisimjue tena na namba anafuta, hakuwa na sababu ya msingi, nikamwambia hewala mama. After three months visalamu vikaanza kwa simu sijui namba aliipata wapi tena! kaja mpaka ofisini. Nikaingia tena, sijui kama ni mzima huyu, akarudia tena, nikamwambia poa, karudi tena vile vile na visalamu. Mara ya tatu nikamwambia pole, hata hamu nae ilishaisha. Kaanza tena namwangalia tu!!! nami nilimlaani hatokuja kumpata ---- kama mimi tena!
 
Mimi niliachwa hivi...Kwanza akaanza kubafilika tabia akawa mkali ukishika simu yake hataki mwisho wa siku akabadili namba ya simu ndo ikawa ntolee nimekutana nae facebook akaniomba namba yangu mwisho wa siku anataka turudiana hebu imagine tangu abadili namba ya simu mwaka 2006 nimekutana nae 2012 anataka turudiane.sijui amegundua nini
 
kakijiwe katam haka! mi sijawai kumwacha mtu na huwa sijui nimeachwaje mana huwa nashtukia niko mikonon mwa mtu mwingne! nahis sijawai kuw na wangu zaid ya kuning'nia bila kumjua mwenye risit ya mzigo!
 
Back
Top Bottom