Mimba za utotoni ni za wazazi na serikali

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,289
12,582
Wazazi kulala chumba kimoja na watoto, watoto kulala kwa jirani, watoto kukosa mahitaji muhimu kama chakula, mavazi, nauli ya shule, chakula shuleni, mila zinazofundisha watoto mapenzi, wazazi kusafiri kwa muda mrefu. Serikali kushindwa kutoa usafiri, mabweni, chakula shuleni, kujenga uzio mashuleni. Mchanganyiko huu wa mapungufu ya wazazi na serikali unatumiwa na wanaume kupata nafasi ya kuwadanganya watoto kimapenzi kwa kigezo cha kutaka kuwatatulia watoto matatizo yao yanayowakabili kama vile ukosefu wa pahala pa kulala, mavazi, chakula, nauli, usafiri wa kwenda na kurudi shuleni, na ada. Wazazi wakali sana kwa mtoto wao anapopata alama za chini darasani, hivyo kusababisha mtoto atafute alama za juu darasani kutoka kwa wanafunzi wenzake darasani na walimu kwa gharama na mashariti yoyote. Utafiti unaonyesha kuwa ni watoto wachache saana ambao wanajiingiza kwenye mapenzi kwa mara ya kwanza kwasababu ya kutaka kujirusha/starehe tu.
 
Wazazi kulala chumba kimoja na watoto, watoto kulala kwa jirani, watoto kukosa mahitaji muhimu kama chakula, mavazi, nauli ya shule, chakula shuleni, mila zinazofundisha watoto mapenzi, wazazi kusafiri kwa muda mrefu. Serikali kushindwa kutoa usafiri, mabweni, chakula shuleni, kujenga uzio mashuleni. Mchanganyiko huu wa mapungufu ya wazazi na serikali unatumiwa na wanaume kupata nafasi ya kuwadanganya watoto kimapenzi kwa kigezo cha kuwatatulia watoto matatizo yanayowapata watoto
Hao wanaume nao si wazazi pia ama?

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Mimba za utotoni zina pande nyingi mkuu kama

Jamii
Dini
Serikali
Wazazi
Watoto wenyewe

Zitaisha kwa watajwa hapo juu kushirikiana ipasavyo



Post sent using JamiiForums mobile app
 
wafundisheni hofu ya Mungu huko ndiko salama zaidi
Katika maisha mwalimu mzuri ni hofu na maumivu. Bila hivyo vitu viwili hakuna uwajibikaji! Kwanini unawahi kazini ni kwa vile unaogopa kufukuzwa kazi na ukifukuzwa kazi maumivu yatakuwa jinsi ya kuihudumia kifedha familia yako. Kwa watoto wakijua kuwa ukifanya jigijigi unaweza pata mimba na ukipata mimba hakuna shule za serikali. Wazazi watakuwa makini kwani hawana fedha za private na watoto wataogopa na mimba za utotoni itakuwa ni historia au siyo mwalimu wangu
 
ATAKAYE PEWA MIMBA NA ANAYEPEWA MIMBA
PAMOJA NA WAZAZI AU WALEZI WA PANDE ZOTE MBILI WANATAKIWA WASHONWE JERA

TUONE KAMA TATIZO LITAENDELEA

Sent from my itel it1556 Plus using JamiiForums mobile app
 
Katika maisha mwalimu mzuri ni hofu na maumivu. Bila hivyo vitu viwili hakuna uwajibikaji! Kwanini unawahi kazini ni kwa vile unaogopa kufukuzwa kazi na ukifukuzwa kazi maumivu yatakuwa jinsi ya kuihudumia kifedha familia yako. Kwa watoto wakijua kuwa ukifanya jigijigi unaweza pata mimba na ukipata mimba hakuna shule za serikali. Wazazi watakuwa makini kwani hawana fedha za private na watoto wataogopa na mimba za utotoni itakuwa ni historia au siyo mwalimu wangu
Haiko hivyo basi, katika maisha ya binadamu mahitaji ya shule yanakuja baada ya mtoto kuhakikishiwa kwanza upatikaji wa hewa safi, maji ya kunywa, chakula, malazi, mavazi, afya njema na love. Kama mtoto akipata usumbufu kwenye kupata hewa ya oxygen, maji, chakula, malazi, mavazi na afya pamoja kupatiwa vipigo, kubezwa na kudharauriwa (maumivu) mtoto hawezi kufikiria masomo ila kupata mahitaji hayo ya lazima kwanza kwa gharama yoyote hata ikibidi kuyapata kwa kugegedwa. Sio shule tu lakini mtu hataogopa hata kupata ukimwi kama hana chakula, malazi, matibabu, na mavazi. Hata kama mchungaji au sheikh atahubiri namna gani lakini kama mtoto hapati chakula, malazi, mavazi, matibabu, upendo nyumbani, na nauli ya kwenda shule atavitafuta tu kwa mtu yeyote kwa mashariti yoyote hata kama iwe kwa kugegedwa. Ndugu yangu acha kusikiliza siasa za wanasiasa, mtoto wako atajiingiza kwenye ngono tu kutafuta chakula, malazi, mavazi, usalama, matibabu, kufaulu (heshima), na kupendwa kama wewe hutampatia mwanao vitu hivyo. Mtoto akiukosa upendo wa wazazi wake atautafuta upendo anaoukosa kutoka kwa watu wengine. fanya utafiti uone ni watoto gani wengi wanaopata ujauzito, utagundua kuwa ni watoto ambao hawapati mahitaji hayo niliyosema, utagundua pia kuwa ni watoto ambao wazazi wao wametengana, wameachana, wako bize sana na maisha, nk
 
Haiko hivyo basi, katika maisha ya binadamu mahitaji ya shule yanakuja baada ya mtoto kuhakikishiwa kwanza upatikaji wa hewa safi, maji ya kunywa, chakula, malazi, mavazi, afya njema na love. Kama mtoto akipata usumbufu kwenye kupata hewa ya oxygen, maji, chakula, malazi, mavazi na afya pamoja kupatiwa vipigo, kubezwa na kudharauriwa (maumivu) mtoto hawezi kufikiria masomo ila kupata mahitaji hayo ya lazima kwanza kwa gharama yoyote hata ikibidi kuyapata kwa kugegedwa. Sio shule tu lakini mtu hataogopa hata kupata ukimwi kama hana chakula, malazi, matibabu, na mavazi. Hata kama mchungaji au sheikh atahubiri namna gani lakini kama mtoto hapati chakula, malazi, mavazi, matibabu, upendo nyumbani, na nauli ya kwenda shule atavitafuta tu kwa mtu yeyote kwa mashariti yoyote hata kama iwe kwa kugegedwa. Ndugu yangu acha kusikiliza siasa za wanasiasa, mtoto wako atajiingiza kwenye ngono tu kutafuta chakula, malazi, mavazi, usalama, matibabu, kufaulu (heshima), na kupendwa kama wewe hutampatia mwanao vitu hivyo. Mtoto akiukosa upendo wa wazazi wake atautafuta upendo anaoukosa kutoka kwa watu wengine. fanya utafiti uone ni watoto gani wengi wanaopata ujauzito, utagundua kuwa ni watoto ambao hawapati mahitaji hayo niliyosema, utagundua pia kuwa ni watoto ambao wazazi wao wametengana, wameachana, wako bize sana na maisha, nk
Unaongea kwa hisia siyo facts! Je, unajua kuwa watoto wa walionazo ndiyo wanapata mimba mapema? Soma dhs zote utaelewa. Age at first intercourse among children from wealthy family is lower than the poor ones
 
Haiko hivyo basi, katika maisha ya binadamu mahitaji ya shule yanakuja baada ya mtoto kuhakikishiwa kwanza upatikaji wa hewa safi, maji ya kunywa, chakula, malazi, mavazi, afya njema na love. Kama mtoto akipata usumbufu kwenye kupata hewa ya oxygen, maji, chakula, malazi, mavazi na afya pamoja kupatiwa vipigo, kubezwa na kudharauriwa (maumivu) mtoto hawezi kufikiria masomo ila kupata mahitaji hayo ya lazima kwanza kwa gharama yoyote hata ikibidi kuyapata kwa kugegedwa. Sio shule tu lakini mtu hataogopa hata kupata ukimwi kama hana chakula, malazi, matibabu, na mavazi. Hata kama mchungaji au sheikh atahubiri namna gani lakini kama mtoto hapati chakula, malazi, mavazi, matibabu, upendo nyumbani, na nauli ya kwenda shule atavitafuta tu kwa mtu yeyote kwa mashariti yoyote hata kama iwe kwa kugegedwa. Ndugu yangu acha kusikiliza siasa za wanasiasa, mtoto wako atajiingiza kwenye ngono tu kutafuta chakula, malazi, mavazi, usalama, matibabu, kufaulu (heshima), na kupendwa kama wewe hutampatia mwanao vitu hivyo. Mtoto akiukosa upendo wa wazazi wake atautafuta upendo anaoukosa kutoka kwa watu wengine. fanya utafiti uone ni watoto gani wengi wanaopata ujauzito, utagundua kuwa ni watoto ambao hawapati mahitaji hayo niliyosema, utagundua pia kuwa ni watoto ambao wazazi wao wametengana, wameachana, wako bize sana na maisha, nk
Ndugu
kukosekana kwa mahitaji ya muhimu kwa mtoto hiyo pia ni sababu moja wapo.Lakini tukumbuke swala la malezi kwa watoto wetu,wazazi wengi siku hizi hatuna nafasi za kuongea na watoto wetu,hatufatilii hata mienendo yao wakitoka nyumbani kuelekea shuleni.
Jambo la msingi ni kuwajenga katika hofu ya mungu kwanza,tujenge nao urafiki,tuwape elimu ya kujitambua katika mabadiliko yao ya mwili na elimu ya afya ya uzazi.
Maana watoto wa vijijini au masikini ndio waathirika zaidi kutokana na mazingira wanayokutana nao.Wa mjini wao pia wana sababu zao lkn hawa wanathiriwa na tamaa na makundi.Pia ni watoaji wamimba wazuri tena kuna baadhi wamejiunga na family plan.

Sent from my SM-J700F using JamiiForums mobile app
 
Kuwakataza waliopata mimba wasikage tena shuleni ni sawa na kuchochea ongezeko la watoto wengi watakaotoa mimba ili kuzinusuru elimu zao, kwakuwa sababu za watoto kujiingiza kwenye vitendo vya ngono hazijatatuliwa watoto na walezi watalitatua kwa kuzitoa mimba zao ili waendelee na shule.
 
Kuwakataza waliopata mimba wasikage tena shuleni ni sawa na kuchochea ongezeko la watoto wengi watakaotoa mimba ili kuzinusuru elimu zao, kwakuwa sababu za watoto kujiingiza kwenye vitendo vya ngono hazijatatuliwa watoto na walezi watalitatua kwa kuzitoa mimba zao ili waendelee na shule.
 
Hawa wazazi wanaishi chumba kimoja na watoto, mfanye mchana watoto wakiwa shuleni
 
Back
Top Bottom