Milo mitatu kwa siku ni kwa masikini

Milo mitatu kwa siku ni kwa masikini

Nadhan mtoa hoja kaeleza vuzuri sana namna anavyoona inafaa mtu kujiwekea ratiba za milo.

Kaeleza umuhimu wa kula milo miwili badala ya mitatu na maana yake.

Sasa wewe ulitakiwa uje na maelezo yaliyojitosheleza kutetea hoja ya milo mitatu na faida zake.

Kuna mwingine atakuja na minne ama mitano nk nk.

Nadhani mtu ale kutokana na mahitaji ya mwili kwa namna ya kaz anazozifanya, kuliko kujikaririsha ratiba za vyakula ambapo vikiliwa hurundikana tu mwilini na kusababishia watu wengi madhara ya kiafya.

Suala la kipato ama umasikini tusiliweke kwenye mjadala huu.
Watanzania wengi wana utapiamlo unaotokana na ukosefu wa chakula na wala si vinginevyo.
Wachache sana wenye viriba tumbo ambao hawazidi hata asilimia 5
 
Masikini sisi ndio tunapiga milo mitatu kwa siku tena sio miatatu tu inaweza kuwa minne. Make tunapiga Chai, mchana tunapiga Chakula jioni Supu na bado tena Chakula cha usiku. Hapo katikati kabla ya saa 7 kuna mara soda, mara karanga maea matunda.

Matajir wengi wanakula milo miwili kwa siku, asubuhi na jioni basi inatosha na wana ratiba na mpangilio wa kula, sisi masikini ssala la mpangilio wa kula halipo na ndio maana tuna figire hazieleweki eleweki.

Prof Janabi akisema anakula milo miwili mimi namuelewa fika hio ni hulka ya watu wengi wenye pesa zao. Sasa masikini lazima tushangae anaweza vipi kula milo miwili kwa siku.

Kisayansi kwanza ieleweke hakuna kitu na hahisi njaa, ile ni saikolojia isha jengeka kwemye ubongo ikifika saa 7 tu unataka kula, au saa 4 chai. Ila mwili sio kwamba ubakuta umeishiwa chakula hapana ila ni uramaduni mwili umeijengea.

Watu wanao funga ndio maaana siku za mwanzo wanapata sana shida ila wakisha zoea ile hali inapotea kabisa, sasa wakina Prof Jajabi walisha jitwin, mchana hawezi hisi njaa make kamwe.
Nia ni nini haswa? Kuishi milele au? Maisha ni zawadi, ipokee kwa furaha. Unajibanaaa boda anakugonga unakufa unamuacha pita msechu na puto lake.
 
Dewji mwenye ratiba ya kwenda gym ndiyo ale milo miwili?
 
Mtoa mada nilipokuelewa sana pale uliposema njaa ni saikolojia tu.
Miye huwa nakula milo 2
Asubuhi chai kwa kitafunwa chochote, baada ya hapo mpaka usiku napata dinner na wala sijisikii njaa
 
Wewe enenda zako, ule chakula chako kwa furaha, unywe mvinyo yako kwa moyo wa kuchangamka; kwa kuwa Mungu amekwisha kuzikubali kazi zako.

8 Mavazi yako na yawe meupe sikuzote; wala kichwa chako kisikose marhamu.

9 Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote za maisha yako ya ubatili, ulizopewa chini ya jua; siku zote za ubatili wako, kwa maana huo ni sehemu yako ya maisha; na katika taabu zako ulizozitaabika chini ya jua.

10 Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.
 
Sinywi pombe...na vyuku nisile? Wee alisema nani? Tena bongo hiihii? Kufa nitakufa tu...niacheni Nile kuku, hahaaaa
 
Matajir wengi wanakula milo miwili kwa siku
Ukiwa na mavyakula mengi tu kwenye friji yamejaajaa unakua huna hamu ya kula hilo nimeshuhudia, Ila ukiwa huna ndio hivyo kulakula tu mda wote km funza
 
Pesa nitafute Mimi , misosi anipangie Prof. Uchwara ambaye ameshindwa kugundua hata dawa ya minyoo.
No.
Prof baada ashughulike kutafuta Dawa ya kifo ili watu waishie hata miaka 500 ye anahangaka na kuwaambia watu waache kulakula, hivi anajua kwamba Njombe watu wanashindia Kande wiki nzima sio kwa kupenda
 
Masikini sisi ndio tunapiga milo mitatu kwa siku tena sio miatatu tu inaweza kuwa minne. Make tunapiga Chai, mchana tunapiga Chakula jioni Supu na bado tena Chakula cha usiku. Hapo katikati kabla ya saa 7 kuna mara soda, mara karanga maea matunda.

Matajir wengi wanakula milo miwili kwa siku, asubuhi na jioni basi inatosha na wana ratiba na mpangilio wa kula, sisi masikini ssala la mpangilio wa kula halipo na ndio maana tuna figire hazieleweki eleweki.

Prof Janabi akisema anakula milo miwili mimi namuelewa fika hio ni hulka ya watu wengi wenye pesa zao. Sasa masikini lazima tushangae anaweza vipi kula milo miwili kwa siku.

Kisayansi kwanza ieleweke hakuna kitu na hahisi njaa, ile ni saikolojia isha jengeka kwemye ubongo ikifika saa 7 tu unataka kula, au saa 4 chai. Ila mwili sio kwamba ubakuta umeishiwa chakula hapana ila ni uramaduni mwili umeijengea.

Watu wanao funga ndio maaana siku za mwanzo wanapata sana shida ila wakisha zoea ile hali inapotea kabisa, sasa wakina Prof Jajabi walisha jitwin, mchana hawezi hisi njaa make kamwe.
Umeandika kimaskini, kitoto na kama mtu asiyejitambua
Kwenye bandiko lako hujasema kwanini tusile mara 3. Umetudanganya uliposema Kisayansi hakuna anayehisi njaa? Ebu tuambie njaa ni nini na prove kisayansi kwamba hakuna njaa.
 
Prof baada ashughulike kutafuta Dawa ya kifo ili watu waishie hata miaka 500 ye anahangaka na kuwaambia watu waache kulakula, hivi anajua kwamba Njombe watu wanashindia Kande wiki nzima sio kwa kupenda
Hahaaaaa sisi tunapenda bwana kwani kande ni chakula chetu cha asili.
 
Back
Top Bottom