tutafikatu
JF-Expert Member
- Dec 17, 2011
- 3,241
- 4,466
Kwa kipindi kirefu Millard Ayo amekuwa akituhabarisha kwa kutupa vichwa vya magazeti ukurasa wa mbele na nyuma kila siku. Kwa bahati mbaya sana, amekuwa akiweka nembo yake ya MillardAyo.com kwa kazi za watu na pia alikuwa akikata matangazo ya biashara yaliyoko kwenye kurasa hizo, akiwa hataki kutangaza biashara za watu wakati yeye hizo kazi za watu anazifanya zake.
Wamiliki wa Magazeti ya Mwananchi yenye magazeti kama Mwananchi, The Citizen, na Mwanaspoti walimzuia kuweka nembo yake inayotangaza mtandao wake wa MillardAyo.com na pia kumzuia kufuta matangazo yao pale anapopiga picha.
Tuheshimu kazi za watu.
Magazeti anayoweka nembo
Magazeti ya Mwananchi aliyozuiwa kuweka nembo
Wamiliki wa Magazeti ya Mwananchi yenye magazeti kama Mwananchi, The Citizen, na Mwanaspoti walimzuia kuweka nembo yake inayotangaza mtandao wake wa MillardAyo.com na pia kumzuia kufuta matangazo yao pale anapopiga picha.
Tuheshimu kazi za watu.
Magazeti anayoweka nembo
Magazeti ya Mwananchi aliyozuiwa kuweka nembo