Mkuu,
Mimi nilikuwepo eneo la tukio mwanzo mwisho leo pale kulikwa na mechi kwenye uwanja wa vinyago na timu 1 wapo ilikuwa ya jeshi.
So kulikuwa na wanajeshi wamevalia kiraia wakati game ikichezwa kuna polisi waliingia wamevaa kiraia na kukamata watu sasa walipiga risasi 1 na kuanza kukamata watu balaa. Na milipuko ya risasi ililindima baada ya polisi moja kumkamata MP na hapo ndipo vituko na picha ya ngumi kama za kwenye video ilitokea.
MP alitembeza kichapo kwa baadhi ya polisi waliokuwa wameshika bunduki jamaa kapigana na polisi walikuwepo defender 1 land cruser na Noah 1 wao wanampiga na vitako vya bunduki yy anapiga ngumi hatimaye alizidiwa nguvu na wananchi walikuwa wanamtetea yule mwanajeshi na baadhi ya raia wamekamatwa.
Cha kushangaza na cha hatari wakati polisi wanapiga risasi, hakuna raia aliyekuwa anakimbia hata 1 wala kuogopa zaidi ya kuwazomea na kuwazonga. Hii ni hatari sana.
Polisi ilibidi wapige risasi nyingi zaidi ili kuwatawanya raia sababu walizuia magari yasitoke na watu waliowakamata