I think about eternity often. I cannot fathom eternity. All I know at the moment is that we live in this universe with its laws as we know it, which incudes time. The Lord dwells in a different dimension with different laws. I cannot fathom a world with no past or future! ! !
“No eye has seen, no ear has heard, and no mind has imagined what God has prepared for those who love him.”
1cor.2.9.NLT
BTW i saw this the other day
View: https://youtu.be/-vAmjy2vVxo?si=bAlV6-GcB1elgmD1
One of my favourite Christian Apologetics,
John Lenox (Maths PhD) aliulizwa wewe jamaa mtaalam wa hesabu tena wa Oxford, unaanzaje kuamini kuwa kuna Mungu, tena Mungu mwenyewe ni Binadamu pia? Embu nielezee.
John akamwambia wewe ni mtaalam wa Fizikia embu niambie, Ufahamu (consciousness) ni nini?
Akajibiwa sijui!
John akasema OK basi energy ni nini?
Mwanafizikia akasema naweza kupima energy, naweza kuitumia....
John akamwambia hicho sicho nilichokuuliza. Energy ni nini?
Mwanafizikia akasema sijui!
John akamwambia lakini unaamini kuwa kuna energy.
Jibu ndio.
Na Unaamini kuwa kuna ufahamu (consciousness).
Ndio.
John akamwambia kwahiyo unamini vitu hivi viwili ambavyo hujui ni nini, je nikukatae kuwa ni wewe mwenye akili / mwerevu / msomi?
Mwanafizikia akasema aah usifanye hivyo.
John akasema lakini hicho ndicho ulichonifanyia ! ! ! Kama wewe hujui energy ni nini, na hakuna mwanafizikia yeyote hadi leo anayejua energy ni nini, kama bado vitu kama mwanga, gravity na ufahamu (consciousness) n.k bado ni fumbo, usishangae kuona sifa hii kwa Mungu pia.
Tena John akamuuliza kwanini unaamini vitu hivi ambavyo hata hujui ni nini?
Mwanafizikia akajiumauma.
John akamwambia si unaamini vitu hivi kwasababu dhana hizi zina maelezo yenye nguvu!
Mwanafizikia akasema ndio hivyo kabisa.
John akasema, ni kweli siwezi kuelezea jinsi gani Mungu alishuka akawa mwanadamu, lakini ndio maelezo pekee yenye nguvu yanayozingatia ushahidi uliopo! !
(not debating)