Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 2,786
- 7,567
Wakuu,
Polisi na CCM mnazidi kuboronga, mmeamsha dude, hamjifunzi kila wakati mnarudia kule kule!
====
Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma linadaiwa kuwazuia viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuendelea na mikutano yao, ikiwemo mikutano ya hadhara na mkutano na waandishi wa habari uliopangwa kufanyika Alhamisi saa 5 asubuhi.
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche, amesema hayo Aprili 10, 2025, akizungumza na Jambo TV, muda mfupi baada ya kuhojiwa na polisi kutokana na wito uliowasilishwa kwa viongozi wa chama hicho kufika Kituo Kikuu cha Polisi Songea.
Akieleza hali ilivyokuwa, Heche amesema kuwa walipofika kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma (RPC), walipewa maelekezo ya kusitisha mikutano yote iliyopangwa kufanyika mkoani humo, ikiwamo mkutano na waandishi wa habari.
"Polisi walikuwa wametukamata, wametufikisha kwa RPC na wakapiga marufuku kwamba hawaruhusu mkutano wowote wala kufanya mkutano na wanahabari katika mkoa huo... wametuambia tuondoke hapa Ruvuma kwani mikutano yote imepigwa marufuku," amesema Heche.
Ameeleza kuwa walielekezwa kuwa hakuna ruhusa ya kujadili masuala yanayohusiana na kampeni ya "No Reforms No Election", na kwamba iwapo chama hicho kinataka kufanya mikutano, basi wajadili mada nyingine isiyohusiana na msimamo huo wa kisiasa.
"Nikamuuliza tuchagulie mada unayopendelea tuiwasilishe, akasema ‘hamruhusiwi kuzungumza No Reforms No Election hapa’,’’ ameongeza Heche.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Marco Chilya, alipotafutwa na Jambo TV kuhusiana na tukio hilo, amesema kuwa atatoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari muda utakapofika (Saa 7 mchana siku ya Alhamisi), na hakupenda kuzungumzia tukio hilo kwa undani kwa wakati huo.
Hata hivyo, mpaka sasa haijatolewa sababu rasmi ya kuzuia mikutano hiyo, huku Jeshi la Polisi likitarajiwa kueleza msimamo wake kuhusu sababu za usitishaji huo, hasa katika kipindi ambacho CHADEMA imezidisha kampeni ya kupinga uchaguzi mkuu ujao iwapo marekebisho ya mfumo wa uchaguzi hayatatekelezwa.
Tukio hili linatajwa kuongeza mvutano kati ya viongozi wa CHADEMA na vyombo vya dola, hasa wakati ambapo mwenyekiti wa chama hicho taifa, Tundu Lissu, naye akielezwa kukamatwa Aprili 09, 2025 mkoani humo mara baada ya mkutano wa hadhara uliohusisha kampeni ya "Tone Tone" na "No Reforms No Election".
Wachambuzi wa siasa wanatazama hatua hizi kama dalili za msuguano unaozidi kuongezeka kati ya serikali na upinzani kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025, huku wakihoji nafasi ya uhuru wa kisiasa na haki ya vyama vya siasa kufanya shughuli zao kwa mujibu wa sheria.
Polisi na CCM mnazidi kuboronga, mmeamsha dude, hamjifunzi kila wakati mnarudia kule kule!
====
Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma linadaiwa kuwazuia viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuendelea na mikutano yao, ikiwemo mikutano ya hadhara na mkutano na waandishi wa habari uliopangwa kufanyika Alhamisi saa 5 asubuhi.
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche, amesema hayo Aprili 10, 2025, akizungumza na Jambo TV, muda mfupi baada ya kuhojiwa na polisi kutokana na wito uliowasilishwa kwa viongozi wa chama hicho kufika Kituo Kikuu cha Polisi Songea.
Akieleza hali ilivyokuwa, Heche amesema kuwa walipofika kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma (RPC), walipewa maelekezo ya kusitisha mikutano yote iliyopangwa kufanyika mkoani humo, ikiwamo mkutano na waandishi wa habari.
"Polisi walikuwa wametukamata, wametufikisha kwa RPC na wakapiga marufuku kwamba hawaruhusu mkutano wowote wala kufanya mkutano na wanahabari katika mkoa huo... wametuambia tuondoke hapa Ruvuma kwani mikutano yote imepigwa marufuku," amesema Heche.
Ameeleza kuwa walielekezwa kuwa hakuna ruhusa ya kujadili masuala yanayohusiana na kampeni ya "No Reforms No Election", na kwamba iwapo chama hicho kinataka kufanya mikutano, basi wajadili mada nyingine isiyohusiana na msimamo huo wa kisiasa.
"Nikamuuliza tuchagulie mada unayopendelea tuiwasilishe, akasema ‘hamruhusiwi kuzungumza No Reforms No Election hapa’,’’ ameongeza Heche.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Marco Chilya, alipotafutwa na Jambo TV kuhusiana na tukio hilo, amesema kuwa atatoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari muda utakapofika (Saa 7 mchana siku ya Alhamisi), na hakupenda kuzungumzia tukio hilo kwa undani kwa wakati huo.
Hata hivyo, mpaka sasa haijatolewa sababu rasmi ya kuzuia mikutano hiyo, huku Jeshi la Polisi likitarajiwa kueleza msimamo wake kuhusu sababu za usitishaji huo, hasa katika kipindi ambacho CHADEMA imezidisha kampeni ya kupinga uchaguzi mkuu ujao iwapo marekebisho ya mfumo wa uchaguzi hayatatekelezwa.
Tukio hili linatajwa kuongeza mvutano kati ya viongozi wa CHADEMA na vyombo vya dola, hasa wakati ambapo mwenyekiti wa chama hicho taifa, Tundu Lissu, naye akielezwa kukamatwa Aprili 09, 2025 mkoani humo mara baada ya mkutano wa hadhara uliohusisha kampeni ya "Tone Tone" na "No Reforms No Election".
Wachambuzi wa siasa wanatazama hatua hizi kama dalili za msuguano unaozidi kuongezeka kati ya serikali na upinzani kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025, huku wakihoji nafasi ya uhuru wa kisiasa na haki ya vyama vya siasa kufanya shughuli zao kwa mujibu wa sheria.