Mikopo Kausha Damu ya Kimtandao

Mikopo Kausha Damu ya Kimtandao

Songambele

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2007
Posts
4,717
Reaction score
2,594
Dunia tambara bovu na vituko haviishi na kila kukicha ni vuta nikuvute. Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na wakopeshaji wa kidigital ambao si haba wanaongezeka kila kukicha.

Mie natoleo mfano mkopo wako, hawa jamaa ni nouma sana nikiwalinganisha na wengine hawa wabunifu zaidi wameajiri wadada wachambaji, wanakupigia na maneno laini kama vile wanafanya promotion ukope sasa balaa lake siku ya marejesho wanakupigia asubuhi sana kukumbusha kulipa na wanatuma msg kukwambia mpaka saa 5 uwe umelipa, ikizidi saa tano. Mkataba wako unaonyesha tarehe ya marejesho, mie leo nilitakiwa kulipa second installment tarehe 21 July 23.

Watoto wa uswahilini waliowaajiri kudadadeki wanakupigia na kukufata inbox na michambo. Unachambwa mpaka basi naona ukipitisha tarehe lazima wakuporomeshee matusi. Na wakikupigia lazima upokee usipopokea ni michambo.

Please wenye uzoefu na kausha damu za kidigital, ebu tubadilishane uzoefu manake hii dunia ukijifungia peke yako unaweza umshindilie mtu bisu la roho ukaozee segerea. JF ndio paa la BATi na profile picture kaweka na hii ndiomsgwamenitumia mwana wa mbone
 
Dunia tambara bovu na vituko haviishi na kila kukicha ni vuta nikuvute. Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na wakopeshaji wa kidigital ambao si haba wanaongezeka kila kukicha.
Aloo,mi nilibugi nikaandika namba za watu wangu wa karibu kama wadhamini,mbona wanakiona Cha moto! Mi wakinipigia nablock muda huo huo! Walinipa mkopo maelekezo nilipe ndani ya mwezi 1 Cha ajab hata week haijaisha wanapiga sim na kutuma mameseji Yao sa kumi na Moja alfajir!

Aloo kama hauna uvumilivu unaweza kupata unapata stress na kuwajibu vibaya! Mbaya zaidi hawana kauli nzuri ni misuto na michambo tu,mi wakinipigia nkawaambia saiv Sina pesa kistaarabu tu,jibu lake sasa we kaka acha ubabaifu lipa pesa ya kampuni,ungekua huna pesa ulikopa Ili iweje? Sa kumi ikifika kama haujalipa tutakuletea barua ya wito!

Kuna lidada lingine liliwahi nidanganya lipa iyo 23k af tukupe mkopo wa 90k baada ya kulipa hakupokea Tena sim zangu,nikachukua Tena mkopo wa 29k kiasi walichotuma ni 20k riba afu 9..aloo sidhani kama nitawalipa Kwa muda ..tutasumbuana sana tu
 
Hao Ni SINGULARITY MICRO FINANCE na hao pia wananidai. TALA walinidaiii mpaka wakanyoosha mikono, nadhani wamefilisika maana mwaka na ushee sijapata simu Yao.

Branch siku hizi wamekua wajanja Sana. Huchomoki lazima ulipe na hawatumii matusi. Wako more professional sio Kama singularity walio ajiri visichana vya Mbagala. Qualification Ni matusi. Ngoja matusi yalipe madeni.
 
😂Mimi nakopa Mtandao wa Simu,mfano, Tigo au Mpesa, huko kwingine riba kubwa utajikuta umechelew kulipa au wamekukera

Unakopa hela mnakubaliana deadline tarehe 1 February,wao simu na message zinaanza tarehe 27 January 😂
 
Hao Ni SINGULARITY MICRO FINANCE na hao pia wananidai. TALA walinidaiii mpaka wakanyoosha mikono, nadhani wamefilisika maana mwaka na ushee sijapata simu Yao.

Branch siku hizi wamekua wajanja Sana. Huchomoki lazima ulipe na hawatumii matusi. Wako more professional sio Kama singularity walio ajiri visichana vya Mbagala. Qualification Ni matusi. Ngoja matusi yalipe madeni.
Branch... Nawavulia kofia wako vizuri, Salute kwao.
 
Branch unakopaje? Mbona Mimi naambiwa nisubiri siku 7
Siku hizi wamekuwa wajanja sio kama kipindi kile, sahivi ukikosea tu kidogo wanasema ombi lako limekataliwa au ndo wanakupa hizo siku, ikifika tena wanaongeza
 
Aloo,mi nilibugi nikaandika namba za watu wangu wa karibu kama wadhamini,mbona wanakiona Cha moto! Mi wakinipigia nablock muda huo huo! Walinipa mkopo maelekezo nilipe ndani ya mwezi 1 Cha ajab hata week haijaisha wanapiga sim na kutuma mameseji Yao sa kumi na Moja alfajir!

Aloo kama hauna uvumilivu unaweza kupata unapata stress na kuwajibu vibaya! Mbaya zaidi hawana kauli nzuri ni misuto na michambo tu,mi wakinipigia nkawaambia saiv Sina pesa kistaarabu tu,jibu lake sasa we kaka acha ubabaifu lipa pesa ya kampuni,ungekua huna pesa ulikopa Ili iweje? Sa kumi ikifika kama haujalipa tutakuletea barua ya wito!

Kuna lidada lingine liliwahi nidanganya lipa iyo 23k af tukupe mkopo wa 90k baada ya kulipa hakupokea Tena sim zangu,nikachukua Tena mkopo wa 29k kiasi walichotuma ni 20k riba afu 9..aloo sidhani kama nitawalipa Kwa muda ..tutasumbuana sana tu
 
Kuna jamaa yangu kawazingua,hawahawa mkopo powa na mdhamin kaniweka Mimi,anapigacmu Kuna mtu tunamdai harafu anatutukana na wewe ndio mdhan wake,nikawauliza mnataka nimdhamin?wakajibu tumeshampa ela tayri.kwanini hamkunipigia kabla ya kumpa?wananiambia cmu yangu ilikuwa haipatikani.achanani na ujinga wenu,wakanivungia kma cku mbili flani mara hawa apa Tena,kma mdhamin utawajibika kwa hili.yule dada hakuna tusi haukuwahi kuckia Toka kwangu.kwanza mipango kwa upande yangu ilijam so akawa amefika muda muafaka,baada ya hapo imefika mwezi sasa kinywa siyo kwangu Wala aliyekula ela.
 
Back
Top Bottom