Mikopo elimu ya juu: Serikali yaweka vikwazo kupunguza waombaji ili kukidhi ahadi ya 100%

Acheni serikali iwape mikopo wana science maana watu wa Arts ndo waloila hii nchi mpaka kufika hapa tulipo. Nchi imebaki kama skeleton.
 
Kuna mahali tulikosea sana katika mfumo wetu wa elimu. Inabidi tujifunze toka Ujerumani na hata Japan. Wanaweka mkazo sana kwenye Technical Colleges na sio Vyuo Vikuu. Watu wanajifunza taaluma fulani.

Tumekuwa na kasumba ya kila mtu kutaka kupata elimu ya Chuo Kikuu. Tulifika mahali tukashusha hata ufaulu ili watu wengi zaidi waende Chuo Kikuu. Tulipotoka sana, na tunahitaji kurekebisha hilo.

Mfano kwenye masomo ya uchumi na biashara, tunahitaji CBE nyingi zaidi kuliko wahatimu wa Chuo Kikuu kwenye fani hizo.
Kwanza mkuu huwezi kujifunza kupitia nchi hizo ulizotaja kwa kua tunatofautiana changamoto na mazingira

Pili kuweka kipaumbele in colleges ni nzuri lakini swali je tunataka kuwa na taifa gani?

Nadhani hatujafikia huko bado
 
Mtoa hoja usilete siasa kwenye elimu. Kuadmit watu wenye uwezo mdogo ni tatizo. Tuiamini mitihani yetu kwenye kutambua uwezo wa wanafunzi. Kama ni lazima kwenda chuo kikuu jitahidi upate alama stahili.
Kwa mwendo wa kuchukua alama E, hapo hapana. Rudia mtihani au tafuta kingine cha kufanya.
Kwani mtihani ndio kipimo cha uwezo? Hata wewe unaamini hivyo?
 
Katika uchaguzi wa mwaka Rais aliahidi kutoa mikopo kwa wanafunzi wote watakaofaulu kusoma vyuo vya Elimu ya juu. Baada ya Rais kuingia ikulu alijitahidi kutoa mikopo iliyokuwa imekwama kwa muda hivyo kuwapa wanafunzi matumaini.

Baada ya kukaa na kutengeneza budget ya mwaka wa fedha serikali imegundua kuwapa mikopo wanafunzi wote watakaofauru ni ngumu kwaani watakausha hazina yote hivyo serikali kushindwa kutekeleza ahadi nyingine hasa zile ambazo matokeo yake yanaonekana moja kwa moja kama ujenzi wa bara bara, huduma za maji na afya. Baada ya serikali kuliona hili imeamua kufanya yafuatayo:-

· Kuongeza madaraja kuingia vyuo vya elimu ya juu:- kwa sasa ili mwanafunzi aweze kwenda elimu ya juu lazima awe na alama D 2 katika mtihani wake wa kidato cha 6, ambayo ni sawa na daraja la pili. (Division two). Pia kwa wale waombaji wa Diploma lazima wawe na ufauru wa UPER SECOND 3.5 G.P.A

· Halafu ikaweka kipaumbele cha mwombaji kupata mkopo kwa wale waliosoma sayansi kidato cha 6.

Kwa vikwazo hivi serikali tayari itaweza kutoa mkopo kwa waombaji kwa asilimia 100 kwaani ni wachache sana wataoweza kupata mikopo. Nafikiri wengi waliosoma elimu ya juu wanatambua kuwa kupata alama A-D kwenye michepuo michepuo ya PCB, PCM, PGM, CBG siyo kazi nyepesi kwa shule zetu ambazo ambazo zina changamoto nyingi kama ukosefu wa maabala na upungufu wa walimu waliobobea katika masomo husika.

Pia ni ngumu kwa wanafunzi wa Diploma kufaulu kwa daraja la pili la juu yaani UPPER SECOND CLASS 3.5. mfano wanaosoma vyuo vya sayansi ya afya na sayansi nyingine km uhandisi na nk ni vigumu sana kupata alama tajwa.
kaka umemaliza chuo mwaka gani Miaka ya nyuma kujiunga UDSM LAZIMA UWE NA C,D Kwenda juu DD HULIKUWA HUCHAGULIWI;
Kama wewe ni kizazi cha walimu wa voda faster hatutakushangaa

tena tunaomba ufaulu wa C,D URUDISHWE SIO WA D,D;
Magap waliyokuwa wanaangaika kuziba kutokana na kukosa watu wenye sifa ya shazibika ; warudishe ufaulu wa C,D
 
Kuna watu wajinga sana! Mnatetea ujinga? Naamini watu waende chuo kwa vigezo hafifu. Someni, acheni uzembe. Kwanza miaka niliyosoma mimi hatukutambua E kama kigezo cha kukupeleka chuo. Vilipoongezeka vyuo binafsi ndipo na hizi E zikawa ni qualification , lakini kwa udhamini binafsi. Kisha likaletwa pendekezo la kuundwa board ya mikopo. Sisi wanafunzi wa UDSM miaka hiyo tuliipinga kwa migomo na maandamano. Tulikuwa na sababu nyingi ikiwemo hii ya kuelekea kukumbatia ujinga. Enzi hizo ulikuwa ukishachaguliwa tu chuo kikuu taayari ushapata udhamini.Hivyo ushindani ulikuwa ni alama za ufaulu.

Wanafunzi tulisoma sana miaka ya nyuma. Leo wanafunzi wamekuwa wazembe wanataka kupunguziwa alama za ufaulu. Tupa kule ******. Tunataka msome

Enzi zile km unavyosema mlisoma, nikwambie hata sasa vijana wanasoma lkn kuna tatizo kubwa sana, zamani ukisoma shule binafsi ulionekana km huna akili, shule binafsi walikuwa wanaenda walifeli kupata nafasi kwenye shule za serikali. shule za serikali zilikuwa na walimu wazuri, maabara, vitabu tulikuwa tunagawiwa bure, walimu walichunga nidhamu ya wanafunzi, kwanza hapakuwa na hizi shule zinazoitwa za kutwa maarufu kama Day. sasa ni kinyume. Tambaza sasa shule nzima ni Day, mwanafunzi wa PCM, PGM, PCB anaishi bunju, chamazi, gongo la mboto, geza ulole, kigamboni kibada na nk, anatoka nyumbani saa ngapi, anafika shule saa ngapi, akitoka shule jioni atafika nyumbani saa ngapi na aanze kujisomea akiwahi saan nyumbani atafika saa 3usiku huku mchana kutwa hajala, amechoka kwa kugombania magari, akipata atasimama masaa 3-4. akifika nyumbani apate chakula aoge, apumzike then saa 10 aanze safari ya kugombania gari, huku mwalimu wake nae akiwa katika mateso sawa, mwalimu akifanikiwa kurudi nyumbani mapema ataenda kuendesha boda boda ili apate kodi ya nyumba na ada ya watoto wake.

Kule kijini ndiyo usiseme: kijana aanasoma mbali na nyumbani shule ya kata, amepanga chumba na wenzake kijijini, anajipikia chakula, wkt mwingine anaishiwa hata hicho chakula, bado apange muda wa kwenda kutafuta kuni, achote maji na kazi nyingine za ziada. watoto wa kike wengi wameishia kupata mimba. shule za kata hazina wakimu wa masomo ya sayansi, mara nyingi wanategemea vijana wa vyuo wakifunga, shule za kata hazina maabara, hakuna sehemu ya kusoma hata hiyo tuition, vitabu hakuna. unategemea mtoto afaulu sawa na mtoto anaesoma st. Francis? FEZA, MARIAN na nk.

Enzi zako ulikuwa unakula kwa kengere, nyama mara 3 kwa wiki, wali mara 2 kwa wiki, chai saa 4 kamili wkt mwingine unapewa na mkate. vitabu ulikuwa unaenda kuazima library, wazazi wako walikuwa wanakutumia TMO kila mwezi, ulikuwa unabadili unachokitaka, kazi yako ilikuwa kusoma tu. D yako ilikuwa inaanzia 25,wkati sasa inaanzia 35.
 
Mlibebwa sana watu na E zao walikua vifua mbele chuo kikuu. Huku mtaani graduate wanashindwa hata kauandika application letter. Kuandika CV mpaka wa google
Ulivoandika tu hapa nimepata tathmini kama ungesoma ungepata daraja gani lakini sijashangaa
 
kaka umemaliza chuo mwaka gani Miaka ya nyuma kujiunga UDSM LAZIMA UWE NA C,D Kwenda juu DD HULIKUWA HUCHAGULIWI;
Kama wewe ni kizazi cha walimu wa voda faster hatutakushangaa

tena tunaomba ufaulu wa C,D URUDISHWE SIO WA D,D;
Magap waliyokuwa wanaangaika kuziba kutokana na kukosa watu wenye sifa ya shazibika ; warudishe ufaulu wa C,D

Nilimaliza siku nyingi labda kama wewe: miaka ya nyuma kulikuwa na kuchaguliwa siyo kufaulu; kuanzia secondary kutoka primary. shule za secondary na vyuo vilikuwa vichache. wengi walikuwa wanafikia vigezo lkn nafasi zilikuwa chache. mfano hata sasa course ya Medical doctror pale MUHAS kama hujafaulu kwa A,A ,A au ,B,B A au BBB huwezi kwenda, unataka kunambia ufaulu wa BCC siyo ufaulu mzuri? sababu ni kwamba nafassi ni chache japo vijana wengi wanafaulu. Mwaka jana kuna kijana wangu alimaliza KIBITI SECONDARY alifaulu kwa Div 2 comb ya PCB. Physics alipata D, Chemistry alipata B, Biology alipata B. alipenda kuwa Doctor, lkn ndoto zake zilizimwa kwani walioomba MUHAS walikuwa zaidi ya 5000 huku nafasi zikiwa 80 tu. waliofanikiwa kupata nafasi ni wale waliofaulu zaidi kwa alama AAA, ABB, BBB lakini pia waliowahi kuomba sasa kijana anasomea kufuga samaki huko SUA tena chagua la pili. Hivyo kipindi unasoma wewe wengi walikuwa wanakidhi vigezo lkn nafasi zilikuwa chache.

Chuo kikuu kilikuwa kimoja tu; UDSM, SUA ilikuwa na shule ya UDSM Huku MZUMBE ikiwa na chuo cha kuandaa wataalamu ktk fani ya uongozi-IDM Mzumbe. Institute of Developement Managment maalumu kwa kutua TECHNICIANS Educations. baada ya hapo Mzumbe ilikuwa kuwa chuo kikuu; nakumbuka mwaka 2002 kipindi hicho vijana wanaomba moja kwa moja chuo, chuo kilikuwa kina uwezo wa kudahiri wanafunzi 1200 tu lakini walioomba walikuwa zaidi ya 20,000 chuo ilibidi kiweke vigezo kuwa ili upate udahili lazima uwe una Div one. je hao wengine hawakuwa na vigezo?

Ilikuwa mwanafunzi akienda kusoma UDSM km vile amepata nafasi ya kwenda mbinguni, kwa sasa kuna vyuo vingi vinavyotoa elimu bora km ya UDSM kama siyo zaidi ya UDSM. UDSM imezidiwa na wanafunzi nasikia wengine sasa wanasimama nje wkt walimu wanafundisha, zamani ukisoma wote mlikuwa mnakaa mpaka viti vinabaki.

Nitarudi ukijibu. ....
 
Kama ni hivyo vyuo vikuu watasoma watoto waliosoma shule binafsi, kama FEZA, MARIAN, ST,ST kwani ndiyo hutoa wanafunzi kwa DIV 1-2 mara nyingi failure huwa ni div 3 tena wachache mmoja au wawili. kwa tuendelee kutengeneza matabaka, in ten years to come watoto wa maskini watakuwa hawana elimu, watoto wa wenye uwezo ndiyo watasoma university. tunajenga nchi ya namna gani? Shule Government za sasa siyo zile za miaka ile ya 90 kurudi nyuma.
Tutengeneze mazingira na kuboresha elimu katika shule za sekondari na Si kushusha viwango vya ufaulu.
 
Tutengeneze mazingira na kuboresha elimu katika shule za sekondari na Si kushusha viwango vya ufaulu.

Tuanze lini? watoto wa wakulima wataenda kuunguna na kazi ya wazazi wao st.secondary schools ndiyo watafikia vigezo vya kwenda vyuo na kupata mikopo.
 
Tuanze lini? watoto wa wakulima wataenda kuunguna na kazi ya wazazi wao st.secondary schools ndiyo watafikia vigezo vya kwenda vyuo na kupata mikopo.
Kwa bahati mbaya hawana vigezo. Hakuna namna. Hatuwezi kwenda tu kwa kuhofia matabaka. Tutaharibu zaidi. Haya mapambano yangeenda kwenye elimu bora shule za sekondari tungeweza kuona matunda yako. Ungepata fursa ya kuona elimu ilivyovurugwa, ungeshangaa. Mwanafunzi wa chuo kikuu akikuandikia paragraph unafikiria kweli ili uweze kutambua alitaka kusema nini. Tujipange.
 
Tungejua sababu za kuanzishwa kwa bodi ya mikopo ya elimu ya juu.

Aiingii akilini mwanafunzi kulipiwa 5M O and A level na mzazi wake akaweza, eti Leo hii amefaulu vizuri then alipiwe 3M na serikali wakati mzazi anaweza kumlipia!

Mna utani nyie na watoto Wa maskini, endeleeni na upuuzi Wa ubafuzi na matumizi mabaya ya madaraka
 
Kwa bahati mbaya hawana vigezo. Hakuna namna. Hatuwezi kwenda tu kwa kuhofia matabaka. Tutaharibu zaidi. Haya mapambano yangeenda kwenye elimu bora shule za sekondari tungeweza kuona matunda yako. Ungepata fursa ya kuona elimu ilivyovurugwa, ungeshangaa. Mwanafunzi wa chuo kikuu akikuandikia paragraph unafikiria kweli ili uweze kutambua alitaka kusema nini. Tujipange.

Nakubaliana na wewe lkn siamini km mwanafunzi wa chuo kushindwa au kuonyesha umahili wake tatizo ni ufaulu wake wa kidato cha 6. kuna maprofesa wengi hawakufanya vizuri secondary lkn wakaamua kurudi kujipanga upya kwa kusoma checti, diploma na sasa ni walimu wa vyuo vikuu.

Tatizo la wanafunzi wa vyuo kuwa weupe ni njia ya ufundishaji wa vyuo vikuu, Tanzania tunaangalia sana kufaulu mitihani unavyotetea badala ya practical na continuous assessment; Mwanafunzi anasoma SUA kozi ya uvuvi na ufugaji samaki/aqual culture lkn mpaka anamaliza hajawahi kufanya practical ya kuangalia hata hilo bwaha linavyochibwa, hajawahi kufika hata ferry, hajawahi hata kwenda deep sea, hajawahi hata kuona vyavu, hakuna mabwawa ya kufundishia, hakuna maabara za samaki, unategemea nini? wenzetu course work pamoja na practical work, reserch na projec zinabeba mark 70% final exams ndiyo 30 sisi huku ni kinyume.

Mwanafunzi wa degree anafanya mtihani wa multiple choice badala ya kujenga hoja kushawishi mwalimu, mwalimu kufundisha ni kama chui na simba, mwalimu analenga kukamata wanafunzi badala ya kuhakikisha wana uelewa. mwalimu anatoa quiz na test zisizo na miguu wala kichwa. wanafunzi wa vyuo vya kibango wanasomea mitihani tu. kwaani asipofanya hivyo atakosa chuo.
 
Tungejua sababu za kuanzishwa kwa bodi ya mikopo ya elimu ya juu.

Aiingii akilini mwanafunzi kulipiwa 5M O and A level na mzazi wake akaweza, eti Leo hii amefaulu vizuri then alipiwe 3M na serikali wakati mzazi anaweza kumlipia!

Mna utani nyie na watoto Wa maskini, endeleeni na upuuzi Wa ubafuzi na matumizi mabaya ya madaraka


Umekosea form 1-4 ni zaidi ya 10m. ada sasa private school ni 2,000,000/= mpaka 3,000,000/= bila matumizi mengine km madaftari, track suit za michezo, raba joz 2, mazoezi, michango ya ujenzi, nauli na nk.

St. Kayumba kutoka kule katerelo ada ya 40,000 kwa mwaka ilikuwa ni mtihani, leo hii akalipe ada ya 2,000,000/= kwa mwaka na kumpa matumizi mtoto atawezaje? hata auze mashamba yake yote, hawezi. Private ndiyo wenye Div 1-2 . Ukiona mwanafunzi maepata div 3 PCM, PCB, CBG, PGM huko kijijini huko ni genius. chuo lazime apige one.

Lakini sasa inabidi arudi kwenye kazi ya babake: MKULIMA waongeze mashaba.
 
Ndugu hakuna majibu. Usije na dhana za assignments wala field placements.
Hivi unajua kua mtihani unapima uwezo wa mwanafunzi kwa asilimia 20 tu? Kama haujui fuatilia

Pili kujua uwezo wa mtu ni sawa na kufanya research inabidi uwe na vyanzo vingi vya kukuletea data kwakua elimu yetu ni aina ya elimu inayotutengezea vyeti vya kuombea kazi basi sishangai kuona hili unalitetea

Mtu anasomea uhasibu anapelekwa field miezi mitatu kwa mwaka na kila anapoenda field anaanza kujifunza upya kama shule hakuwa akifanya kitu japo mitihani amepata A ama B+

Kwanini tusianze kubadili elimu yetu kuwa ya vitendo ili kutengeneza magwiji katika maeneo yao ya elimu?

Ndio maana leo unakuta mtu ana taaluma fulani lakini anakuja kupewa maelekezo yasio ya kitaalam na mtu mwingine anafuata hajiamini kwakua aliamini mitihani zaidi ya kujifunza
 
Back
Top Bottom