hello JF,
Sijui kama hio system ipo au bado,
Leo ningependa kuwe na utaratibu wa kuwapa mikataba ya miaka miwili tu walimu,
sababu,hatuwezi kuwaweka walimu wale wale sehemu moja,alafu tukategemea matokeo tofauti,
Kwa mfano,Dar na Mtwara,shule zilikua za mwisho mwaka jana,
kama hakijabadilika kitu,
then matokeo mabaya yatakuja na mwaka huu tena ,
mtanilaumu,lakini niko upande wa wazazi wanaopoteza mamilioni ya ada,only vijana wao kupata four ama zero..............
kukiwa na walimu ambao hawako competent,hii system itawatema,sababu baada ya miaka miwili kama anaperform vibaya,haongezewi mkataba.
This also means,wale walimu wazuri tu ndio wanaajiriwa,na walimu wabovu wanakua OUT,lol
najua mtaanza mwanafunzi wanatakiwa wajisomee wenyewe,ila asikwambie mtu mwalimu akiwa mzuri,utaenjoy somo. Akiwa mbaya utachukia tu,kwa sasa hatuna option,unakaa nae hivyo hivyo.
tena kama wanafunzi wa boarding ndio kabisaa hili linawahusu.
Hahahaaaaa shule imejengwa kati kati ya mlima hadi ufike huko kuna 4km had 5 halafu kuna nyumba moja ya mwalimu mkuu na mkuu mwenyewe anaogopa kuishi maana nyumba ipo peke yake haina jirani ,
majiraji wako mbali na shule kama 2 km hivi hahaaaaa!! Watoto wanatoka km 6 hadi 8 kwenda shule wakiwa wamevalia yebo safi kabisa na kandambili zao,hizo ndizo shule za kata bwan,
Wakati huo kitabu kipo kimoja kimoja kila somo halafu cha miaka 10 iliyo pita hadi cover halionekani hahaaaaa! Hizo ndizo shule za kata bwana
Kesi ya madawati nimpongeze sana tena sana Mh! Rais magufuli maana kwa sasa madawati sio changamoto maana shule nyingi madawati yapo ila changamoto madarasa sasa aisee maana madara mengine yaligeuzwa maabara wakati wa joto la maabara enzi za Rais mstaafu Kikwete.
madawati yamepangwa hadi mlangoni hahaaa watoto lukuki darasani mwalimu hawezi kupita kuzungukia wanafunzi maana hakuna pa kupita asee!
Kwa shule za sekondari nyingi vitabu vya sayansi vipo vya kutosha kabisa ila vya masomo ya sanaaa dah!! Shida kubwa na kila shule ina kitabu chake hahahaaa huku cha nyambari nyangwine , huku cha msabaha , huku cha Oxford, kule cha TIE yaani mh!, hiki kinasema kuna sayari tisa huku kinasema nane aisee na wanafunzi wote nchini wanafanya mtihani mmoja yaani NECTA. aiseee!
Shule moja wanasoma watoto wa ukoo mzima kuna binamu hapo hapo ,dada hapo hapo , wakwe hapo hapo, wayembi hapo hapo , mashemeji hapo hapo,na ,mawifi pia, wengine wanaitana bibi hapo shuleni na wengine babu , kuna kina sanji hapo, hahahaaaaaa!!kuna watwatsi hapo hapo aiseee
Ukitokea msiba kijijini hapo karibia nusu nzima ya shule msiba una wahusu na wote wanahitajika kushiriki msibani maana aliye kufa ni ndugu wa wanafunzi wote hahahaaaaaa , aiseee
Watoto wanatoka nyumban saa11 alfajiri kwenda shule bila kula chochote wanashindishwa shuleni hadi saa 10 jioni hahahaaaaa!tena bila kula chochote , Halafu hadi kufika nyumbani saa mbili usiku ndio ale hadi cha kushindia kesho tena kisha alale ajiandae tena kesho kuamka saa 11 alfajiri kuwahi namba aiseee,
halafu tunalazimisha dv 1,2,3 kwa wingi, huu ni mzaha kabisa na hizo ndizo shule za kata zinazo milikiwa na serikali
Wakati huo serikali nayo imeingiza mihemko ya kisiasa inataka matokeo mazuri kabisa kwa gharama ndogo na naafuu kabisa hivyo ili wizara ikwepe lawama na gharama ikaleta mfumo wa maswali ya kuchagua shule za mising ili isahihishe na mashine ili kupunguza gharama za kusahihisa walimu.
Kitu ambacho hata mtoto asiye jua kusoma anaweza akaamua tu kujaza "A" maswali yote 50 kwa masomo yote na kabahatika kupata walau hata robo kama sio nusu ya maswali yote naye kuwa kwenye kundi la walio fahuru kwenda sekondari hahaaaaaa!! Ndio maana kesi ya wasio jua kusoma shule za kata haiishi aisee dah
Wakati huo pia mwalimu analazimishwa kwenda kusahihisha mitihani ya mock bila malipo na nje ya kituo chake cha kazi yaani umbali wa km zaid ya 20 kwa kuambiwa kuwa ni sehemu ya kazi yake hivyo hakuna malipo na anatumia nauli yake na gharama ya kula kwake ,kulala kwake hahaaa halafu una mtishia afanye kazi kwa ufanisi na ole akosee.dah!!
Na kama halmashauri itajitahidi sana ita mlipa pesa ya nauli tuu ambayo huwa ni flat rate bila kujali umbali wa kila mwalimu aisee!!
Wakati huo kasikia kuna watu wamekaa kikao kisicho zidi masaa matatu na kulipwa posho ya laki nne wakati huo kikao hicho kikiwa ni cha kazi vilevile kama yeye daah! aisee hii ndiyo elimu ya bongo
Nadhani nyie watoa mada muwe mnafanya kwanza tafiti kwa shule zote sio mmejifungia masaki na msasani mnaangalia shule za huko halafu mnakurupuka huku kuja kutoa ushauri wa kijinga
Wakati huo kuna wanafunzi na wana kijiji ambao kwao elimu ni kitu cha ziada hivyo wanafanya juu chini kuhakikisha wanakwamisha ikiwa ni pamoja na kuwafanyia vitimbi vya kishirikina walimu na baadhi ya wanafunzi wanao jitahid kitaaluma darasani hahaaaaa!
Mara siku ya mtihani haoni ubaoni, mara karasi halina maandishi wakati limechapishwa , mara mashetani yamepanda hahahaaaa! Oooh! Mara mwalimu anashtukia kalazwa mtoni na bukta yake yeye na mke wake na katoto kao ka miezi 7 looo! Hajakaa sawa anastukia kesho tena kaamkia makaburini dah!! Aisee Hizi ndizo shule za kata bwana ,
Kipindi cha masika shuleni hakuendeki kutokana na eneo ilipo shule si mwalimu wala mwanafunzi anaye weza kwenda shule maana shule ni kama imetupwa porini kusiko fikika kukiwa na masika maana ili ufike lazima uvuke mito na vijito hahaaaaaa , shule inafunga bila mfungo rasmi , looooo! Mvua imefunga shule yarabi! Shule za kata bwana.!
Hebu nendeni vijijini huko mkafanye tafiti acheni kujifanya washauri wa maswala ya elimu wakati mmejifungia ndani mnapigwa viyoyozi kwenye viti vya kuzunguka.
Walimu wanavumilia mengi sana na wana maumivu mengi sana mioyoni mwao ni kama samaki analia weeeeeeeeee machozi yabebwa na maji hivyo huonekana kama mda wote ana furaha na hayo ni baadhi ya mengi ambayo nimeyaona kwenye utafiti wangu juu ya maisha ya mwalimu na mazingira yake ya kazi na mengi sija yaandika maana kuna mambo mengi sana sana sana.
Na kama vile mmemjua kiongozi wenu alivyo na maamuzi ya papo kwa papo pasi na kufikiri wala kutafakari basi nanyie mnautumia vema udhaifu wake huo na mnajitahidi sana kumtumia , na kwa vile yeye ni mpenda matokeo mazuri bila kujali visaidizi vya hayo matokeo mazuri kweli mmempata.
Mimi nilijitahidi kutembelea shule nyingi za vijijini na zahanati za vijijini kama 52% ya shule zote za sekondari nchini na 12% ya shule za msingi na 68 ya zahanati maana nilikuwa na kazi maalumu aisee niliyo kutana nayo huko hadi najiuliza hivi hawa wanao panga scheme za elimu huwa wanafanyia shule zipi tafiti zaoo,? nahisi huwa wanaishia shule za dar pekee tena za mjini tuu halafu wanapanga mipango kazi ya elimu kitaifa
KWAKWELI WAPANGA MIPANGO WA ELIMU HEBU KUWENI SERIOUS BASI PANGENI MIPANGO INAYO TEKELEZEKA KWA SHULE ANGALAU ZA MAENEO YOTE WALAU HATA KWA 70% SHULE ZA MIJINI SIO CASE STUDY NZURI KUTOLEA MAAMUZI YA KITAIFA MAANA SI NYINGI KAMA ZA VIJIJINI MTAWALAUMU WALIMU BURE PAMOJA NA KWAMBA NA WAO WANA MADHAIFU YAO.