Mikataba ya kazi za ualimu

Mikataba ya kazi za ualimu

Rebeca 83

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2016
Posts
15,475
Reaction score
33,038
hello JF,

Sijui kama hio system ipo au bado,

Leo ningependa kuwe na utaratibu wa kuwapa mikataba ya miaka miwili tu walimu,

sababu,hatuwezi kuwaweka walimu wale wale sehemu moja,alafu tukategemea matokeo tofauti,

Kwa mfano,Dar na Mtwara,shule zilikua za mwisho mwaka jana,

kama hakijabadilika kitu,

then matokeo mabaya yatakuja na mwaka huu tena ,

mtanilaumu,lakini niko upande wa wazazi wanaopoteza mamilioni ya ada,only vijana wao kupata four ama zero..............

kukiwa na walimu ambao hawako competent,hii system itawatema,sababu baada ya miaka miwili kama anaperform vibaya,haongezewi mkataba.

This also means,wale walimu wazuri tu ndio wanaajiriwa,na walimu wabovu wanakua OUT,lol

najua mtaanza mwanafunzi wanatakiwa wajisomee wenyewe,ila asikwambie mtu mwalimu akiwa mzuri,utaenjoy somo. Akiwa mbaya utachukia tu,kwa sasa hatuna option,unakaa nae hivyo hivyo.

tena kama wanafunzi wa boarding ndio kabisaa hili linawahusu.
 
Mamilioni ya ada wakati elimu ni bure.
Labda shule binafsi.

embu nihabarishe,uko Dar na Mtwara waliofeli shule zilikua binafsi au za serikali???anyhow mie nimetoa tu idea,inaweza kutumika pote-serikalini au private.
 
Kazi ya mkataba ni nzuri kila mahali, si kwa waalimu tu. Nionavyo inaongeza tija, uwajibikaji na uadilifu. Lkn km mfanyakazi anajijua kua yy ni permanent na pensionable anakua hana hofu ya kua mwadilifu, mchapakazi hodari, mwadilifu na mwenye tija. Kinyume chake atakua mvivu, mlalamishi na mkosefu wa ubunifu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kazi ya mkataba ni nzuri kila mahali, si kwa waalimu tu. Nionavyo inaongeza tija, uwajibikaji na uadilifu. Lkn km mfanyakazi anajijua kua yy ni permanent na pensionable anakua hana hofu ya kua mwadilifu, mchapakazi hodari, mwadilifu na mwenye tija. Kinyume chake atakua mvivu, mlalamishi na mkosefu wa ubunifu

Sent using Jamii Forums mobile app

well put,bravo,lol
 
Ni za serikali ndio wanafeli.
Binafsi wanafaulu.
Jibu ni moja serikali haijali walimu.

Kama ni shule za serikali,wazazi hawalipii ada,na bado watoto wanafeli,then conclusion cha bure,ghali.

Mkuu ina maana hata madaktari waache kutoa huduma bora sababu serikali haiwajali?
 
hello JF,

Sijui kama hio system ipo au bado,

Leo ningependa kuwe na utaratibu wa kuwapa mikataba ya miaka miwili tu walimu,

sababu,hatuwezi kuwaweka walimu wale wale sehemu moja,alafu tukategemea matokeo tofauti,

Kwa mfano,Dar na Mtwara,shule zilikua za mwisho mwaka jana,

kama hakijabadilika kitu,

then matokeo mabaya yatakuja na mwaka huu tena ,

mtanilaumu,lakini niko upande wa wazazi wanaopoteza mamilioni ya ada,only vijana wao kupata four ama zero..............

kukiwa na walimu ambao hawako competent,hii system itawatema,sababu baada ya miaka miwili kama anaperform vibaya,haongezewi mkataba.

This also means,wale walimu wazuri tu ndio wanaajiriwa,na walimu wabovu wanakua OUT,lol

najua mtaanza mwanafunzi wanatakiwa wajisomee wenyewe,ila asikwambie mtu mwalimu akiwa mzuri,utaenjoy somo. Akiwa mbaya utachukia tu,kwa sasa hatuna option,unakaa nae hivyo hivyo.

tena kama wanafunzi wa boarding ndio kabisaa hili linawahusu.
Wazo lako ni zuri linalenga kuleta msisimko chanya ila kuna tatizo Kubwa kwenye Elimu ya watoto Wa taiga hili .

Kwanza lazima ujue wadau Wa Elimu ya hawa watoto

1.Mzazi
2.Mtoto mwenyewe
3.Mwalimu
4.Mazingira

Mzazi ni kiungo muhimu mno kwenye kuhakikisha mtoto wake anafaulu kama familia haitoe mawazo chanya kuhusu Elimu sahau kuhusu mtoto kufaulu.

Mtoto nae ni mdau muhimu kwenye hili suala kuna watoto wapi Shule ila ni hoi bin taabani kwenye masomo yaani hawawezi tunawafosi tu na kuwapotezea muda na sisi kupoteza rasilimali yaani hata miujiza haiwezi badili hilo .Pia kuna watoto wana uwezo sana kwenye masuala ya Shule hata haihitajiki nguvu nyingi.

Mwalimu ni kiungo muhimu chenye asilimia 25 tu kwenye ufaulu Wa mtoto Mara nyingi huyu ni kumsaidia na kumuongoza mtoto aende kwenye utaratibu uliowekwa. Mara nyingi wazazi na mazingira hatuviangalii tunamlaumu mwalimu tu hata kama Mzazi amemtelekeza mwanae bado atalaumu mwalimu.

Mazingira nayo yana mchango kiasi kwenye suala hili mazingira ya Shule kwa upande mmoja na ya jamii inayozunguka eneo hili.

"Never stop learning because life never stop teaching"
 
Mbona huzungumzii watoto wasio fundishika..
Walimu mnawaonea buree kazi yao ni ngumu sn ..na inahitaji hekima..lkn kizazi hiki cha kudeka kina halibiwa majumbani kuanzia..mzazi,mtoto mwenyewe na makuzi..
 
Unaishi wapi wewe,nani amekuambia wahudumu wa afya wanatoa huduma nzuri.
(Uliwahi kusikia habari ya mtu kupiga chafya akiwa chumba cha kuhifadhia maiti).
Ukitaka huduma bora za afya nenda binafsi.

hao ambao hawa afford bei za private waende wapi?
hapa sijakuuliza unaishi wapi,have I??
nimeleta hoja,itakayowaphase out walimu wabovu automatically,
wewe leta yako itayowatema wahudumu wa afya wanaotoa huduma mbovu
 
Kwa hyo ukioa ukashindwa kubebesha mimba unavunja ndoa? Ukilima ukakosa mavuno msimu wa kwanza unaacha kulima? Elimu ni neno pana zaidi ya kufaulisha mtihani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamisha mwanao peleka private,problem solved! shule za serikali zikikosa wateja zitafungwa kwa mshahara gani wa kuwakalia wenzenu kooni hivyo?watoto wenyenye kila kukicha wanapiga walimu na kupata mimba kuna wasomaji hapo kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app

ingekua kila mtu anauwezo wa kumpeleka mtoto wake private,si angefanya hivyo?yaani wazazi wanajua kabisaa kumpleleka mtoto shule ya serikali ni janga,lakini wanajilipua hivyo hivyo,sad.
 
Uliloliandika...hujui mazingira halisi na jinsi elimu inavyotolewa haswa vijijini

mkuu mbona mnasema hivyo?
wekeni wazi,lengo la kuileta hii mada sio kuleta vijembe bali kuelimishana,kwa mfano huko kijijini ungeweka wazi ,nini changamoto mnazozipata....
 
ungeanza na wazazi ambao hawawajibiki kwa watoto ningekuelewa, ukosefu wa ajira utakutesa sana
 
Back
Top Bottom