MIGONGANO YA KIFIKRA: Kujinyonga - "Ajinyonga Kwa Udanganyifu Katika Mitihani "

--Je, kujinyonga baada ya kughafirika ki aibu ni kitu cha kutetea?!
--Je, huyu kijana amekufa kishujaa au kinyonge?!
--Je, kijana huyu alivyofanya ni sawa na kujitoa mhanga?!


`




Labda tuangalie makundi matatu kwanza ya watu wanaoamua kujiua;

1. Kundi la mwanzo linahusisha wanaojiua kwa sababu ya kumuumiza/kumkomoa mtu mwingine mfano mzazi wake, mpenzi'we, rafiki'ye nk kwa matarajio kitendo chake hicho 'huenda' kitamsononesha maisha yote huyo alomkusudia kwa kujilaumu na kulaumiwa na jumuia, nk.

--Je, kujinyonga baada ya kughafirika ki aibu ni kitu cha kutetea?!
Hapana, si la kutetea; ila la msingi tukumbuke kwamba mara nyingi wanaokuwa na tendency za kujidhuru, iwe kutishia kujiua, kujiunguza na sigara ama kujikata kata na visu, ama kujiua kweli, iwe kwa kusaga chupa, kujinyonga ama kunywa sumu nk, hawa wote wana hitilafu fulani katika ubongo. kwa maana nyingine ni, wenye tabia hii hurudia rudia kauli zao mpaka pale wanapotimiza azma yao hiyo. Kubwa panahitajika mental health consultancy ili kuweza kuwafariji na kuwapa nasaha za kuboresha fikra za watu wenye tendecy hizo.

2.Kundi la pili ni wale wanaoamua kujiua ama kutokana na maradhi ya muda mrefu pengine yasokuwa na tiba, (yakiwemo UKIMWI, Akili na ulemavu) , ulevi kupita kupindukia, utumiaji wa madawa ya kulevya nakadhalika, na walokumbwa na depression, kiasi kwamba hawaoni njia nyingine yeyote ya kujitoa katika matatizo hayo ila kwa njia hiyo ya mkato, na kwa kudhani hivyo wanauhakika kifo hakitaacha pengo lolote kwa jamii husika.

--Je, huyu kijana amekufa kishujaa au kinyonge?!
Kinyonge; kwa mtazamo wa 'hadithi' yenyewe,Hatuwezi jua msukumo ulompelekea kufikia uamuzi wa kutumia mlungula ili tu aweze kufaulu mtihani wake huo, kiasi kwamba hata alipokamatwa alionelea bora tu kujiua kuliko hatma ya kufutiwa mitihani yote baada ya kubainika na majibu ya mtihani.

3. Kundi jingine ni wale ambao wanaona hawana budi kujitoa mhanga kwa ajili ya watu wengine, hawa ni wale wenye mitizamo ya kidini zaidi mfano wanaopigania haki zao kwa mujibu wa itikadi zao za dini mfano; Budha's Monks, Religious Extremists, nk... na kisiasa; mfano wale wanaotetea maslahi ya kundi, nchi au sehemu fulani dhidi ya utawala wa kikandamizaji toka tabaka fulani la watawala mfano Extremists Sikhs walomuua Rajiv Gandhi, au 'Kamikaze Pilots' wakati wa vita vikuu vya dunia).

--Je, kijana huyu alivyofanya ni sawa na kujitoa mhanga?!
Hapana, sidhani kama kwa sababu tu amekamatwa na mlungula na kufukuzwa kwenye chumba cha mtihani ni sababu tosha ya kuamua kujitolea mhanga, kwani kosa linamuelekea yeye mwanafunzi.

Mchongoma, Ahsante sana kwa maelezo yako.
Lakini hapo kwenye kijani, nikichukulia mfano mwingine wa 'sects' ambao hurubuniwa au kujirubuni na hivyo wote kujiua kama vile ilivyo wahi kutokea kule Amerika na hapa Africa (Uganda na Kenya kama sikosei); hawa wote nao wana kufa kinyonge au kishujaa ukihusisha imani yao?!

SteveD.
 
QM, thanks a lot for your good shot,

However, I have another concern brought about by your very expression above. The issue of demons, don't you see that this is rather another broad subject that some of us believe in and some don't?! Or in your opinion, is this thing for really (phyiscal) or is it a mere kind of 'thought forms'?!

Personally, I somewhat believe in 'thought forms' type of demons, just like your example above in red, they are mere personifications of concepts like fear, rage, desire/lust, envy and other emotions that someone would like to cast out of themselves.

Na nikikubaliana na hiyo form ya demons, basi kama unavyosema labda huyo kijana wa Musoma alikumbwa na hii type... tatizo swali lipo pale pale, ni kufa kishujaa au kinyonge?

(naomba kuto limit aina za hiki kifo, kama kuna khali nyinginezo zaidi ya ushujaa au unyonge naomba mtu aongezee).


SteveD.

Demons are frequently depicted as a spiritual force that may be conjured and insecurely controlled. To believe or not to believe the presence of demons is merely depending on how the person perceives the essence of religious beliefs.

Je hatua ya kujiyonga aliochukua kijana wetu wa Musoma ilikuwa ni ya:
A. kishujaa au kinyonge?
B. Kuwajibika au kukwepa wajibu?

Ili kuweza kupata jibu sahihi la hatua yake ya kujinyonga, inabidi kutengeneza assumptions kadhaa:
1. Alikuwa kijana mwenye uchungu wa kufika mbali kielimu
2. Jamii/familia yake ilikuwa ina mategemeo/matumaini makubwa kwake katika siku za mbeleni
3. Ukizingatia kuwa alikuwa ana umri mkubwa (21) kwa level ya kidato cha IV, lilikuwa ni jambo la aibu kubwa kukamatwa anaibia majibu.
Sasa basi, kwa kutumia assumptions hizi, utagundua kwamba uamuzi wake wa kujinyonga hauwezi kuchukuliwa kama ni wa kishujaa wala kinyonge. Hauwezi pia kuwa wa kuwajibika wala kukwepa wajibu. Kwa maoni yangu, hatua yake ya kujiua inaweza kuchukuliwa kama ya upotezaji wa imani. Baada ya tukio la kukamatwa ana desa, alipoteza imani ya kila kitu – kielimu, kimaisha, kijamii, kifamilia, etc.
 
Demons are frequently depicted as a spiritual force that may be conjured and insecurely controlled. To believe or not to believe the presence of demons is merely depending on how the person perceives the essence of religious beliefs.

Je hatua ya kujiyonga aliochukua kijana wetu wa Musoma ilikuwa ni ya:
A. kishujaa au kinyonge?
B. Kuwajibika au kukwepa wajibu?

Ili kuweza kupata jibu sahihi la hatua yake ya kujinyonga, inabidi kutengeneza assumptions kadhaa:
1. Alikuwa kijana mwenye uchungu wa kufika mbali kielimu
2. Jamii/familia yake ilikuwa ina mategemeo/matumaini makubwa kwake katika siku za mbeleni
3. Ukizingatia kuwa alikuwa ana umri mkubwa (21) kwa level ya kidato cha IV, lilikuwa ni jambo la aibu kubwa kukamatwa anaibia majibu.
Sasa basi, kwa kutumia assumptions hizi, utagundua kwamba uamuzi wake wa kujinyonga hauwezi kuchukuliwa kama ni wa kishujaa wala kinyonge. Hauwezi pia kuwa wa kuwajibika wala kukwepa wajibu. Kwa maoni yangu, hatua yake ya kujiua inaweza kuchukuliwa kama ya upotezaji wa imani. Baada ya tukio la kukamatwa ana desa, alipoteza imani ya kila kitu – kielimu, kimaisha, kijamii, kifamilia, etc
.

QM, Ahsante,
Kutokana na hilo ulilolisema katika 'blue', je, sisi aliotuacha tukiwa hai, tumchukilieje kwa kitendo chake cha 'kupoteza imani' na kujinyonga?! Nikimaanisha kuwa, hilo tukio baada ya mazingira yake katika 'green' sisi kama wanajamii hilo ni jambo la kutetea au kukemea?! QM, ndugu mchongoma kashatoa jibu lake, naomba nasaha zako kwenye hili pia kama zinaweza kutofautiana naye. Ahsante.

SteveD.
 
QM, Ahsante,
Kutokana na hilo ulilolisema katika 'blue', je, sisi aliotuacha tukiwa hai, tumchukilieje kwa kitendo chake cha 'kupoteza imani' na kujinyonga?! Nikimaanisha kuwa, hilo tukio baada ya mazingira yake katika 'green' sisi kama wanajamii hilo ni jambo la kutetea au kukemea?! QM, ndugu mchongoma kashatoa jibu lake, naomba nasaha zako kwenye hili pia kama zinaweza kutofautiana naye. Ahsante.

SteveD.

Kwanza naomba tuelewe kwamba kujiua sio sehemu ya utamaduni wetu. Na ndio maana tukisikia mtu kajiua huwa tunashtuka sana. Sasa basi, kwa dhamira yoyote ile, jamii yetu haitetei tabia ya kujikatisha maisha kwa kujiua. Kwa hiyo sisi kama wanajamii tunapaswa kulikemea. Tunatakiwa tulikemee kwa sababu ni jambo, sio tu la huzuni, bali pia la aibu kwa jamii yetu. Ndio maana mpaka leo, familia iliyopatwa na msiba wa kujiua kwa ndugu yao, huwa inaona aibu sana on top ya kuwa na huzuni kwa kupoteza ndugu yao.
 
Kwanza naomba tuelewe kwamba kujiua sio sehemu ya utamaduni wetu. Na ndio maana tukisikia mtu kajiua huwa tunashtuka sana. Sasa basi, kwa dhamira yoyote ile, jamii yetu haitetei tabia ya kujikatisha maisha kwa kujiua. Kwa hiyo sisi kama wanajamii tunapaswa kulikemea. Tunatakiwa tulikemee kwa sababu ni jambo, sio tu la huzuni, bali pia la aibu kwa jamii yetu. Ndio maana mpaka leo, familia iliyopatwa na msiba wa kujiua kwa ndugu yao, huwa inaona aibu sana on top ya kuwa na huzuni kwa kupoteza ndugu yao.

QM, kweli ni hivyo?... maana hapo awali nimesha muuliza Gaijin kuhusu historia inayomhusu mtemi Mkwawa (kama sijakosea) na kujiua kwake ili asikamatwe na Wajerumani akiwa hai... ninavyokumbuka vitabu hivyo vinasema hilo lilikuwa jambo la kishujaa... Mheshimiwa, naomba nasaha zako kwenye hili. Ahsante.

SteveD.
 
Kwa mujibu wa sheria za nchi zetu (mimi sio mwanasheria kitaaluma), kujiua ama kujaribu kujiua ni sawa kabisa na kuua, na iwapo ulijaribu kujiua na ukafeli jaribio lako, sirikali huwa inakuchukulia hatua kali za kinidhamu.
Wanasheria mtusaidie, kwa nini mtu aadhibiwe kwa kujitoa uhai wake?
 
Kijana Dar ajimaliza kutokana na ugumu wa maisha

2007-11-09 18:04:46
Na Kiyao Hoza, Jijini


Mwanaume mmoja mkazi wa Jijini Dar es Salaama amejinyonga kutokana na ugumu wa maisha.

Kamanda wa mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Jamal Rwambow amesema kijana huyo Lameck Msadawa, 22, alijinyonga jana majira ya saa 5:00 asubuhi, nyumbani kwake huko Kimara King`ong`o.

Kamanda Rwambow amesema kijana huyo alijinyonga kwa kutumia shuka alilolitundika juu ya paa la bafuni kwake.

Akasema kijana huyo aliacha ujumbe mfupi uliosema `Nimeamua kujinyonga kwa sababu ya ugumu wa maisha. Wazazi na marafiki zangu wapewe taarifa hizi`.

Amesema maiti ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya Taifa Muhimbili

Chanzo: Alasiri, 9/11/2007

Hii kadhia ya watu kujitoa uhai inazidi kushika kasi kila uchao. Jamani tuendelee kuangalia namna ya kutatua tatizo hili linaloonekana kuwa sugu.
Nadhani huduma ya ushauri nasaha kwa wale wasio na ajira au wanaoishi katika mazingira magumu inafaa ianzishwe, kwani inaonekana vifo vya kujinyonga kutokana na ugumu wa maisha vinaonekana kushika kasi.
 
Mwanafunzi ajinyonga baada ya kubaini ana VVU

2007-12-13 10:51:55
Na Pendo Fundisha, PST Mbeya


Mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari Mtakatifu Agrey iliyoko Uyole, jijini Mbeya, Frank Sanga (22), amejinyonga baada ya kupima kwa hiari na kugundulika kuwa ameambukizwa virusi vya Ukimwi.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Bi. Monica Madembe alisema mwanafunzi huyo alijinyonga juzi jioni kwa kutumia kamba ya begi chumbani kwake.

Alisema kaka wa marehemu, Bw. Justine Sanga ambaye ni mfanyabiashara katika mji wa Uyole, ndiye aliyegundua kuwa mdogo wake amejinyonga baada ya kumkuta akining`inia huku kamba ya begi la shule ikiwa shingoni.

Kaimu Kamanda huyo alisema marehemu aliacha ujumbe kabla ya kujinyonga ambao ulisomeka kuwa, alifikia uamuzi huo baada ya kupima na kujikuta ana virusi vya Ukimwi.

Habari zilizoifikia ofisi ya PST kutoka kwa baadhi ya wanafunzi wenzake aliokuwa akishirikiana nao katika masomo ambao majina yao yamehifadhiwa walidai kuwa, marehemu aliguswa sana na suala la kupima kwa hiari kwani mara kwa mara alikuwa akiwapa somo na kuwaambia waende kupima.

Walisema alikuwa akitoa ushauri ambao wengi wao walijitokeza na kuunga mkono zoezi la Rais wa Jakaya Kikwete kwenda kupima afya zao bila ya kuwa na wasiwasi wowote na walikuwa tayari kupokea majibu ya aina zote mbili.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya kwa uchunguzi zaidi.

SOURCE: Nipashe
Source link: Ippmedia.

SteveD.
 
Hivi mgongano huu wa mawazo umeishia wapi haswa? SteveD upo?
 
Back
Top Bottom