Migogoro wa wakulima na wafugaji haijapata ufumbuzi

Anna Mghwira

R I P
Mar 9, 2012
206
362
Migogoro ya ardhi imekuwa tatizo la muda mrefu nchini. Migogoro ya wakulima na wafugaji imevuka hali ya kawaida ya migogoro ya ardhi, sasa ni uhasama wa kundi moja dhidi ya kundi jingine. Migogoro imepata sura mpya na hadhi mpya kwa kila kundi. Kila wakati tumesikia hatua mbalimbali zikichukuliwa na serikali kutatua tatizo bila tatizo lenyewe kwisha: Kuna nini hasa?

Historia ya ardhi za nchi zilizokaliwa kikoloni ilihitaji kubadilishwa mara moja baada ya uhuru. Kwa sababu ardhi ndiyo ilikuwa mtaji mkuu wa uchumi wa kikoloni. Baada ya uhuru, ardhi inakuwa mtaji mkuu wa nchi huru, lakini afrika tumekataa uhuru wetu huo, wa ardhi na rasilimali zetu kwa ujumla. Tumewapa ama wakoloni wale wale ama wadau wa aina yao kumiliki rasilimali zetu. Hii ni moja ya changamoto za ardhi. Ardhi inakwa ndogo kwa matumizi yetu kwa sababu tumewapa waeni urithi huu. Tunakiri bila hofu kuwa utajiri wa asili umekwa laana ya asili badala ya kuwa Baraka ya asili.
Hapa Tanzania migogoro mingi iliyopo sasa inachangiwa na sera yetu ya siasa ni kilimo ambayo ilitoa kipaumbele cha maendeleo kwa wakulima na kuwanyima heshima hiyo hiyo wafugaji. Kwa muda mrefu tumewapuuza wafugaji. Tumeshindwa kuona thamani ya mchango wao mkubwa kwa pato la taifa. Kwa sababu hiyo kuna sera za kilmo zilizopitishwa ambazo zimekuwa kichocheo cha migogoro hii.
Mgogoro wa kwanza mkubwa kati ya wafugaji na wakulima ulianza pale wafugaji wa Ki-barbaig waliponyan’ganywa eneo la zaidi ya hekta elfu 70,000 miaka ya 60. Serikali ndiyo ilichukua eneo hili na kuanzisha mashamba ya ngano ya iliyokuwa NAFCO- Shirika la Umma la Kilimo cha ngano mkoani Manyara, wilaya ya Hanan’g. Tangu eneo hilo kubwa lichukuliwe awali na kampuni ya Ki-Kanada, baadae na serikali yetu, ardhi ya wafugaji imekuwa finyu na iliyojaa migogoro.

Serikali ikitaka kumaliza migogoro hii, ianzie pale. Iangalie hitilafu zilizojitokeza, dhuluma zilizofanyika kwa wananchi, na kuharibiwa kwa mfumo wa uzalishaji wa asili na wa kisasa wa ufugaji.

Kupitia sera ya Siasa ni Kilimo, serikali imefanikiwa kuwasaidia wakulima kwa kila hali, ifanye hivyo kwa wafugaji pia. Itajua kiini cha matatizo, na njia sahihi ya kuitatua. Kinachoonekana sasa ni kama kushughulikia matawi bila kugusa mizizi.

Sera yetu ya uwekezaji, sheria na taratibu zake na utekelezaji wake nazo ni changamoto nyingine. Hizi zinahitaji mabadiliko ya kikatiba kukidhi haja na hoja zote za umiliki na matumizi ya rasilimali zote za asili. Tunahitaji kuona mizizi ya matatizo haya ikishughulikiwa, si matawi yake.
 
tanzania yangu nakulilia! usimwage damu! kuna watawala wanapenda sana kuona kila siku wanauana hawa jamii mbili halafu wanatumia siasa kuonekana wao ndo wasuluhishi!

na tatizo la pil wafugaji wana hela kupita wakulima hvyo ni rahsi hata kutoa rushwa na kupewa maeneo karibu na wakulima!

lakin pia wafugaj hawa wanataman kukaa karibu na huduma za jamii kama hospitali shule nk. hvo serikal ingejipanga upya kuwawekea miundombinu hyo huko huko porin

ni hatari sana kwa hali tuliyonayo sasa
 
Migogoro ya ardhi imekuwa tatizo la muda mrefu nchini. Migogoro ya wakulima na wafugaji imevuka hali ya kawaida ya migogoro ya ardhi, sasa ni uhasama wa kundi moja dhidi ya kundi jingine. Migogoro imepata sura mpya na hadhi mpya kwa kila kundi. Kila wakati tumesikia hatua mbalimbali zikichukuliwa na serikali kutatua tatizo bila tatizo lenyewe kwisha: Kuna nini hasa?

Historia ya ardhi za nchi zilizokaliwa kikoloni ilihitaji kubadilishwa mara moja baada ya uhuru. Kwa sababu ardhi ndiyo ilikuwa mtaji mkuu wa uchumi wa kikoloni. Baada ya uhuru, ardhi inakuwa mtaji mkuu wa nchi huru, lakini afrika tumekataa uhuru wetu huo, wa ardhi na rasilimali zetu kwa ujumla. Tumewapa ama wakoloni wale wale ama wadau wa aina yao kumiliki rasilimali zetu. Hii ni moja ya changamoto za ardhi. Ardhi inakwa ndogo kwa matumizi yetu kwa sababu tumewapa waeni urithi huu. Tunakiri bila hofu kuwa utajiri wa asili umekwa laana ya asili badala ya kuwa Baraka ya asili.
Hapa Tanzania migogoro mingi iliyopo sasa inachangiwa na sera yetu ya siasa ni kilimo ambayo ilitoa kipaumbele cha maendeleo kwa wakulima na kuwanyima heshima hiyo hiyo wafugaji. Kwa muda mrefu tumewapuuza wafugaji. Tumeshindwa kuona thamani ya mchango wao mkubwa kwa pato la taifa. Kwa sababu hiyo kuna sera za kilmo zilizopitishwa ambazo zimekuwa kichocheo cha migogoro hii.
Mgogoro wa kwanza mkubwa kati ya wafugaji na wakulima ulianza pale wafugaji wa Ki-barbaig waliponyan’ganywa eneo la zaidi ya hekta elfu 70,000 miaka ya 60. Serikali ndiyo ilichukua eneo hili na kuanzisha mashamba ya ngano ya iliyokuwa NAFCO- Shirika la Umma la Kilimo cha ngano mkoani Manyara, wilaya ya Hanan’g. Tangu eneo hilo kubwa lichukuliwe awali na kampuni ya Ki-Kanada, baadae na serikali yetu, ardhi ya wafugaji imekuwa finyu na iliyojaa migogoro.

Serikali ikitaka kumaliza migogoro hii, ianzie pale. Iangalie hitilafu zilizojitokeza, dhuluma zilizofanyika kwa wananchi, na kuharibiwa kwa mfumo wa uzalishaji wa asili na wa kisasa wa ufugaji.

Kupitia sera ya Siasa ni Kilimo, serikali imefanikiwa kuwasaidia wakulima kwa kila hali, ifanye hivyo kwa wafugaji pia. Itajua kiini cha matatizo, na njia sahihi ya kuitatua. Kinachoonekana sasa ni kama kushughulikia matawi bila kugusa mizizi.

Sera yetu ya uwekezaji, sheria na taratibu zake na utekelezaji wake nazo ni changamoto nyingine. Hizi zinahitaji mabadiliko ya kikatiba kukidhi haja na hoja zote za umiliki na matumizi ya rasilimali zote za asili. Tunahitaji kuona mizizi ya matatizo haya ikishughulikiwa, si matawi yake.
Mama Anna, nenda kwenye sheria, pinpoint specific kifungu baada ya kifungu katika sheria za ardhi hasa land acquisition act kifungu kipi kina madhara kwa wafugaji/wananchi kwa ujumla. Pia nenda kwenye sheria za ardhi 1999, pinpoint specific kifungu kinacholeta matatizo kirekebishwa au kifutwe kabisa/ kiongezewe kifungu kipya.
Mwisho, make ardhi a constitutional category.
ACT mnafanya nini, nyie ndio wa kuiambia serkali since you have a platform, sasa nyote ni WAOGA mko kwenye keyboard. Mama Anna, huku hakutasaidia.

Asante sana kwa wazo hili.
 
Migogoro hii ilianza tangu kipindi cha Kaini na Abeli...kwaiyo itaendelea kuwepo japo viongozi wetu wana uwezo Wa kuipoza na kupunguza makali ila kuisha kabisa sizani Kwa sababu wafugaji wetu ni watu wankuhamahama kutafuta malishi
 
Hapa Tanzania migogoro mingi iliyopo sasa inachangiwa na sera yetu ya siasa ni kilimo ambayo ilitoa kipaumbele cha maendeleo kwa wakulima na kuwanyima heshima hiyo hiyo wafugaji. Kwa muda mrefu tumewapuuza wafugaji. Tumeshindwa kuona thamani ya mchango wao mkubwa kwa pato la taifa. Kwa sababu hiyo kuna sera za kilmo zilizopitishwa ambazo zimekuwa kichocheo cha migogoro hii.
Hebu hapa tuwe wakweli! Ina maana sera hii ya kuwapa kipaumbele Wakulima na kuwaacha Wafugaji ili-apply hata kwenye maeneo ya asili ya wafugaji?!

Kwamba, kule Loliondo nako Wakulima walipewa kipaumbele cha ardhi badala ya wafugaji!

Let's be honest... migogoro mingi hivi sasa inatokea kwenye mikoa ambayo kiasili ni ya Wakulima na sio ya Wafugaji! Hii ikiwa na maana kwamba, Wafugaji hawa majority wamehamia tu kwenye hiyo mikoa baada ya kukosa malisho kwenye maeneo yao ya asili! Na miongoni mwao, wengine wanakuwa ni wapita njia... sio Wafugaji wanaoishi kwenye vijiji husika.

Sasa unataka kusema huko walikohama ni kweli Wakulima walikuwa wanapendelewa kiasi cha kuwafanya Wafugaji kuhama au ni kutokana na ufugaji holela ambao msingi wake mkuu ni kuhama hama... jambo ambalo lipo kwa karne kadhaa; iwe ni Tanzania au kokote kule kwamba; Mfugaji anayefuga kiholela huwa hatulii sehemu moja!

That's one lakini kuna tabia nyingine ya wafugaji! Katika kuhama hama huko huwa wanaswaga mifugo!

Hivi inawezekana kweli mtu unatembea na mifugo kutoka wilaya/mkoa mmoja hadi mwingine halafu usikutane na mashamba njiani?! Ni wafugaji wangapi wanaweza kusukuma mifugo mbali na mashamba eti ili mradi tu ng'ombe wasile mazao... wapo wafugaji wa aina hiyo hususani wale wanaoswaga mifugo kutoka eneo moja hadi lingine?!

Tukubali ukweli... tatizo la msingi hapa ni utamaduni wa wafugaji kuonea fahari kuwa na ng'ombe wengi... PERIOD!

Unakuwa na mamia ya ng'ombe wakati huna eneo binafsi la kulisha mifugo hiyo!

Unakuwa na mamia ya ng'ombe wakati huna uwezo wa kuwa-manage!

Tabia ama utamaduni huu wa Wafugaji unafanana kwa aina fulani na utamaduni wa watu wa pwani ambako ni ufahari kuwa na minazi mingi. Bahati mzuri, minazi haimsumbui mtu kama ilivyo kwa mifugo.

Kwahiyo, hata kama Wafugaji watachiwa nusu ya Tanzania peke yao; wasipobadilika bado migogoro itaendelea tu kuwepo!

Itaendelea kuwepo kwa sababu, hata kama wataachiwa nusu mzima ya Tanzania, ikifika kiangazi watahama kutafuta wapi kuna majani! Na huko watakoenda watakutana na mashamba!
 
serikali kushindwa kutenda maeneo kwa wafugaji ni udhaifu kwa serikali iliyopo...

waziri na wataalam wa mifugo wameshindwa kuratibu idadi ya mifugo na maeneo ambayo mifugo inapaswa kuwepo.

wafugaji wa morogoro na manyara wangeamishiwa bonde la mto rufiji karibu na hifadhi ya selous
 
serikali kushindwa kutenda maeneo kwa wafugaji ni udhaifu kwa serikali iliyopo...

waziri na wataalam wa mifugo wameshindwa kuratibu idadi ya mifugo na maeneo ambayo mifugo inapaswa kuwepo.

wafugaji wa morogoro na manyara wangeamishiwa bonde la mto rufiji karibu na hifadhi ya selous

Unataka kusema huko Bonde la Mto Rufiji hakuna Wakulima na hakuna mashamba?!
 
Shikamoo madam.
Migogoro itaishaje kama tuliwaingiza watu ofisini kwa uhodari wa kukunja ngumi na kupiga pushups?
What do you expect?
 
Hapa Tanzania migogoro mingi iliyopo sasa inachangiwa na sera yetu ya siasa ni kilimo ambayo ilitoa kipaumbele cha maendeleo kwa wakulima na kuwanyima heshima hiyo hiyo wafugaji. Kwa muda mrefu tumewapuuza wafugaji. Tumeshindwa kuona thamani ya mchango wao mkubwa kwa pato la taifa. Kwa sababu hiyo kuna sera za kilmo zilizopitishwa ambazo zimekuwa kichocheo cha migogoro hii.
Kwanza kwa kuwa umeanzisha uzi hapa, inabidi uujibu maana wanasiasa mnatabia ya kuanzisha threads na kuzikimbia.
Huoni kwamba unaonyesha kuegemea upande mmoja wa wafugaji? Kama mwanasiasa ulitakiwa kuwa on natural ground.

Kifupi ni kwamba unaonyesha huelewi madhira yanayoletwa na jamii za wafugaji, hasa wamasai, maana hawajali mazao ya mkulima, yani wewe upande wao walishe mazao kwa lazima, ushawahi ona wapi huo utaratibu?
Ushawahi ona mkulima kavamia shamba la mfugaji akaanza kulima?
Kwanini ni mfugaji tu kila siku avamie shamba la mkulima?

Wafugaji wamelelewa sana, wanatenda maovu, sheria hazichukuliwa, wamevimba kichwa. Last week mkulima kapigwa mkuki mdomoni ukatokea shingoni, Morogoro tu hapo, sababu mmasai aliingiza ng'ombe kwa lazima katika shamba lake na kuanza kuharibu mazao machanga. kama ni uvumilive, wakulima wamekuwa wavumilive sana, siku wakiamka itakuwa shida.
 
Mimi mwanzoni nilijua wewe Mama una ka IQ kakubwa kakubwa kidogo hadi Zitto akakupa ugombea uraisi, kumbe hakuna kitu kabisa. Umeongelea migogoro ya ardhi ukiwa haujui kitu na bias kutokana na uzoefu wa unakotokea wewe. Migogoro mikubwa ya wakulima na wafugaji nchi hii iko Morogoro, Pwani na Dodoma ambako wamasai, wasukuma na mang'ati sio asili yao. Wehamia huko wakiwa na mifugo yao. Wewe unakurupuka hapa unasema mkulima anapendelewa
 
Yule RC wa Morogoro alietukanwa na kudhihakiwa na Faza house kuwa katumbuliwa kwa kushindwa kumaliza Mgogoro wa Wakulima na Wafugaji aombwe radhi Kama na RC wa sasa hawatatumbuliwa kwa kosa lile lile. Kumradhi Dr. Rajab Rutengwe
 
Huna hata simple logic wewe mama, umenikera sasa kwa vile mimi niliishawahi kufanya research kwenye maeneo ya mgogoro nimefika hadi kijiji cha Mvumi na Msowero Kilosa ambako wakulima kwa mamia wameishakufa kwa kuuliwa na wafugaji ambao ni wamasai na huwezi kuniambia kuwa kuna mmasai ana asili ya Mvumi, au Msovero kilosa. Mashamba ya miwa ya wakulima wa maeneo yote kuanzia kijiji cha mvomero hadi Turiani yameliwa na ng'ombe na hao wakulima wameacha kulima miwa kwa vile wafugaji wanachunga mifugo yao usiku kama wachawi. Nenda kwao umasaini hauoni ng'ombe anachungwa usiku wote wanachungwa mchana ila huku Bagamoyo, Handeni, Kilosa na Mvomero wanachunga usiku bila kusahau Kiteto. Wilaya Sugu za migogoro
 
Wewe Mama umeniboa sana leo, najiuliza kama tungekupa Ikulu hali ingekuwaje? Mkulima eneo lake ni lile lile miaka nenda rudi. Mzee Rajab wa Msowero alirithi shamba kwa baba yake zaidi ya ekari 50 miaka ya sitini, analima hapo miaka yote na amegawia wanaye na wajukuu, lakini shamba hilo hilo limesababisha apoteze wanaye na wajukuu kwa kuuwawa na wafugaji miaka 50 toka arithishwe shamba. Je lile shamba ni laana? Anajiuliza, anasema bora asingekubali lile shamba labda angebakia na wanaye na wajukuu? Lakini angewalisha nini yeye ni mkulima?
 
Suluhisho ni KILA MKULIMA ALIME KWENYE ENEO LAKE NA KILA MFUGAJI ACHUNGE MIFUGO KWENYE ENEO LAKE. Yule asiye na shamba asilime na yule asiye na eneo la kuchungia asifuge. Sio jukumu la serikali kugawia mtu eneo ya kuchunga au kulima. Kama serikali itamtafutia mfugaji eneo la kuchungia imtafutie pia na Mtanzania aliyeko Manzese Dar eneo la kujenga kibanda chake basi!!! Hakuna hicho kitu ujamaa ulienda na Nyerere biashara ya kugeuza nchi nzima malisho haikubaliki
 
katoe ushauri kwa mkuu nini kifanyike na kama mawazo yako yatakuwa na logic basi yatafanyiwa kazi na utakuwa umeisaidia sana nchi
 
Unataka kusema huko Bonde la Mto Rufiji hakuna Wakulima na hakuna mashamba?!

jiongeze kiakili...

soma maelezo yangu alafu toa na ww mapendekezo yako.

tatizo la watz tupo kukosoa hoja pasipo mapendekezo au mawazo mapya.
 
Back
Top Bottom