Mifuko ya PSSSF NA NSSF walipeni wastaafu mafao yao

Yaani NSSF wamepuuza kauli ya Raisi?

FAO LA kujitoa

Waziri nae kimya

Ina maana Raisi haheshimiwi au ni Kauli ya kisiasa tu?
Zile zilikuwa kauli za kisiasa tu na hazikuwa na uhalisia wowote, pamoja na wale viongozi wa vyama vya wafanyakazi kushangilia kama mazuzu. Hakuna hata siku moja utasikia kauli ya kumnufaisha mwananchi halafu ikatekelezwa mara moja, lakini ngoja itolewe kauli ya kumlemea mwananchi asubuhi inayofuata tu itaanza kutekelezwa tena kwa vitisho.
Na hapo ndo utagundua nini maana ya kuambiwa mtu ni mtawala wa wanyonge. Ni lazima watu wote wageuzwe kuwa wanyonge ili kauli mbiu hiyo ya kuongoza wanyonge itimie, huku watu wasiotafsiri hiyo kauli tata wakipiga makofi na kushangilia Mithili ya kuku walio bandani kumshangilia mchinjaji wao huku kashikilia kisu mkononi mwake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zile zilikuwa kauli za kisiasa tu na hazikuwa na uhalisia wowote, pamoja na wale viongozi wa vyama vya wafanyakazi kushangilia kama mazuzu. Hakuna hata siku moja utasikia kauli ya kumnufaisha mwananchi halafu ikatekelezwa mara moja, lakini ngoja itolewe kauli ya kumlemea mwananchi asubuhi inayofuata tu itaanza kutekelezwa tena kwa vitisho.
Na hapo ndo utagundua nini maana ya kuambiwa mtu ni mtawala wa wanyonge. Ni lazima watu wote wageuzwe kuwa wanyonge ili kauli mbiu hiyo ya kuongoza wanyonge itimie, huku watu wasiotafsiri hiyo kauli tata wakipiga makofi na kushangilia Mithili ya kuku walio bandani kumshangilia mchinjaji wao huku kashikilia kisu mkononi mwake.

Sent using Jamii Forums mobile app

TUCTA ni jipu..sasa hivi wako kimya kama vile haki ndio imepatikana....

mtu ni mtawala wa wanyonge (sio mtetezi wa wanyonge). Ni lazima watu wote wageuzwe kuwa wanyonge ili kauli mbiu hiyo ya kuongoza wanyonge itimie, huku watu wasiotafsiri hiyo kauli tata wakipiga makofi na kushangilia Mithili ya kuku walio bandani kumshangilia mchinjaji wao huku kashikilia kisu mkononi mwake.
 
Laaana kali iwaendee individual woote wa bodi za wakurugenzi wa mifuko ya LAPF, PSSF, PPF, GEPF na NSSF ambao kwa makusudi mazima walikwiba na waliiba hela za wanyonge na kutakatisha uibaji huo kwa kuanzisha miradi mikubwa ya majengo makubwa (Real Estate) ambayo hayawezi kurudisha hizo hela kwa muda mfupi. Pia laaana kali iwaendee individual wooote wa serikalini waliokopa hela kutoka mifuko ya jamii na kukataa kuzirejesha. Pia kuna wizi uliofanywa na serikali kwa watumishi wa taasisi za umma waliokuwa wanachangia mifuko mingine mbali na PPF ikawa inazipeleka PPF kwa muda wa miezi 11 kuanzia July 2011 hadi June 2012 na waathirika wa hizo hela ni wengi sana. Ukienda LAPF wanasema sio wao ni serikaki mpaka izihamishe na kuzirudisha kwa mifuko husika ya wanachama walipokuwa wanachangia. Sasa kwa vile mifuko imeunganishwa na kuwa mfuko mmoja PSSSF kwa nini wasihamishe kirahisi na kuwalipa wale walioachishwa kazi. Mlaaniwe wote na vizazi vyenu hata vizazi vya saba kwa wizi huu wa mchana kweupe ambao mliufanya mkijua madhara kwa wachangiaji pindi wakiachishwa kazi, kuacha kazi na kustaafu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom